Ujio wa Obama: Kashfa ya kupokwa ulinzi, vyombo vya habari vinavyoiona Tanzania

Ujio wa Obama: Kashfa ya kupokwa ulinzi, vyombo vya habari vinavyoiona Tanzania

Candid Scope, AshaDii Mwita Maranya na wengine,

Nafikiri mtakuwa mnafanya kosa sana kufikiri Secrety Service ya USA wametunyanyasa.

Wao kwa sasa na hasa Obama kama Rais, hawawezi kuruhusu likafanyika kosa na Obama akashambuliwa na kudhurika au kuuawa. Imeshawahi kutokea huko nyuma na hawawezi kuruhusu kitu kama hicho. Sababu kadhaa zinazosababisha hiyo hali ni kama hizi:

1. Obama hadi leo hapendwi kabisa na watu kama Donald Trump na hadi alishafikia kusema wazi ingawa alifanya kama utani kuwa "watu kama Trump walikuwa wanaombea akienda msitu wa Amazon basi apotelee huko Milele...."
Ukiacha hao, kuna wale wa WHITE POWER, KKK nk ambao walishajitangazia zamani na kujiapiza kuwa OBAMA lazima afe. Kundi hili halipo tu USA ila hadi Ulaya ambako makundi haya ya WHITE POWER, SKIN HEAD walishajitangazia na wao kama wakipata nafasi basi ni lazima Obama afe. Wengi walilaani sana mara tu ilipomshinda H. Clinton na wakaanza kuona kuwa Mjaluo anaweza kushinda. Wakasema wazi kabisa ndiyo itakuwa mwisho wa WHITE RACE.

2. Kifo cha Osama bin Laden, wafuasi wake hadi leo hawajafurahia kabisa na wanamuwinda usiku na mchana.

3. Israel hawakufurahia kushinda kwake na hasa Bibi Netanyahu ambaye aliweka vita ya wazi kabisa na Obama wakati wa kampeni na kwa bahati mbaya akashindwa. Netenyahu na hao Orthodox wenzake hawajafurahi kushinda kwake hadi leo.

4. Makundi yote ya kigaidi ambayo yamepoteza viongozi wao kwa kuuawa na Drone za USA, wanamuwinda kwa nguvu. Hapo ukiongeza na wale wa Mali na waliopigwa Libya pamoja na Ghadaffi.

Unaweza kuongeza sababu nyingi tu na utagundua kuwa Obama ni zaidi ya maadui wa J F Kennedy ambao mwisho waliweza kumuuwa. Na Usalama wa Taifa, FBI, CIA nk wanalijua hilo na hawawezi kufanya makosa.

Kuna jamaa yangu mmoja aliniambia kuwa Obama alipotembelea nchi yao huko Ulaya, basi barabara nzima ilifungwa na watu wakaondolewa siku hiyo mjini City Centre. Kwa sababu anakaa karibu na barabara inayotoka/kwenda Airport, alishangaa kuwaona Wababa na bunduki zao (Snipers) wakiwa juu ya majengo wamevalia nguo nyeusi na msafara ulivyopita, wakashuka. Pia huko Ulaya pamoja na kuwa na ulinzi wa hali ya juu sana, bado USA ilileta Walinzi 300 miezi mitatu kabla na wiki moja kabla wakaja wengine 300 na idadi kuwa hiyo ya 600 kama walivyokuja Tanzania.

Tuacheni Complex ya kudhani USA wanatudharau. Sababu kubwa ni MAADUI wa Obama na si hatuna ulinzi. Hata akienda UK au Israel, ni haohao 600 wanakwenda na mji siku hiyo unaingia kwa kibali maalumu na wanasema pia hivyohivyo na wazi kabisa kuwa kama unaweza basi safiri nje ya Mji. Na jamaa yangu anasema kweli mji ulikuwa umepungua sana watu siku hiyo.

Nakubaliana na hoja zako zenye kuakisi ukweli kutokana na dondoo ulivyozifafanua. Jambo ambalo limepitiliza mbali ya mazuri mengi uliyoyaainisha hapa ni ule mchujo wa viongozi waandamizi serikalini, maana yake hata hawa viongozi wetu wachaguliwa kuna ambao wanatiliwa shaka na usalama wa Wamarekani. Sishangai wao kuchukua jukumu la usalama wa kiongozi wao kwa 99%, lakini mchujo wa viogozi waandamizi serikalini wakiwemo mawazi hata baadhi ya makamu wa marais wetu ni jambo linaloshtua kidogo maana si la kawaida.
 
Ndugu yangu, kwa maoni yangu thread yako inadhihirisha jinsi ulivyosukumwa zaidi na dhamira za kisiasa, kiasi cha kukuacha u mtupu na kipofu kuhusu uzalendo wako.
Wenyewe wamarekani wana msemo kuwa 'where ever air force one lands, its America' wakimaanisha kuwa popote inapotua dege linalombeba Rais wa Marekani ni America.
Kwa sababu hiyo jukumu la ulinzi na usalama wa kiongozi wao na ujumbe wake linakuwa chini ya vyombo vya usalama vya marekani; iwe London, Ujerumani hata nchi ndogo km za Kiafrika. Kwa hilo hatumwi wala kuaminiwa mtu baki, na hiyo ndiyo itifaki wanayotumia, na ina gharama kubwa...SABABU!! Siasa za mabavu, uvamizi, na mauaji ya watu wasio na hatia kwa visingizio mbalimbali, zimesababisha kuibuka kwa maadui lukuki duniani. Ili kukabiliana na njama za kugeuziwa kibao, Marekani inafanya gharama kubwa kulinda wao wenyewe viongozi wake wa juu, hususan wakiwa katika ziara za nje ya nchi.

Hilo linaeleweka na hakuna siyejua kiburi cha wamarekani na wanavyojiona wanajua zaidi ya wote. Jambo moja ambalo si la kawaida ningeshukuru jaribu kulijengea utetezi kuhusu mchujo wa viogozi waandamizi serikalini. Jambo hilo halijazoeleka na halijatokea hata kwa ziara za Marais wa Marekani waliotembelea Tanzania, hali kadhalika msafara wa Obama huko West na South Afrika hakija tokea kitu kama hicho cha kuchuja viogozi waandamizi serikalini. Hapa si itikadi tunajadili yaliyojilia kwenye taifa letu la Tanzania. Unaonaje bwana KAPONGO?
 
FBI wakagua ofisi ya Kova kwa mbwa

kova.jpg


View attachment 100684
Hii habari iko kwenye magazeti, ni aibu has ukilinganisha na tambo zilizokuwa zimetolewa hapo awali

Mkuu wa ulinzi na usalama wa raia ofisi yake inakaguliwa na vikosi vya usalama vya Wamarekani hapa nchini mwentu. Marekani mbwa anapoingizwa kwenye ofisi au sehemu yo yote kwa ukaguzi maana yake ni "crime seen!" Hii imekaakaaje jamani vandugu zangu. Aibu ya mwaka.
 
Suala la kuhusu uzalendo hilo serkali ndiyo imeliharibu yenyewe kwa kutoweka mazingira sawa na haki katika kuendesha mambo yake.Kwamfano,suala la vyama vingi ni la kidemokrasia na tulilichagua wenyewe.Iweje inapokuwa wapinzani wakifanya mambo yao ,mpaka wapigwe ,wawekewe vigingi kama vile sio raia?yaani uwanyanyase watu kwa haki yao kwa sababu tu wanamtizamo tofauti na wewe, then utegemee wakuunge mkono kwenye mapungufu yako?Umoja na mshikamano unatakiwa utoke pande zote,raia kwa upande mmoja na serikali upande mwingine bila kujali ni wa upinzani au tawala.Imekua ni kawaida serikali kuwanyanyasa wapizani ,kana kwamba sio raia na hawachangii kodi ya maendeleo ya nchi hii ambayo serikali,au chama tawala kinajisifia ,wakati ni kodi zetu wenyewe.Ambazo viongozi wa nchi hii hawataki kuzilipa huku wakiendelea kujilimbikizia mali.Hivi unaweza kunijibu kwa nini viongozi nchi hii hawalipi kodi?Wakati nchi zilizoendelea sifa mojawapo ya kuwa kiongozi ni pamoja na Kulipa kodi?Kwani kodi ni tozo inayotokana na mapato halali.Hivyo linapofika suala la kodi kuanzia viongozi hadi raia ni lazima walipe kodi.Hii haipaswi kuwa na msamaha.

Kwa kifupi mazingira yaliyopo kwa sasa nchi hayaruhusu hayo unayoyataka,hayawezekani kwa sasa mpaka marekebisho ya nayopaswa yafanyike,ikiwa ni uhuru wa kujiamulia mambo yetu kama hatuvunji sheria.Ulichokua unakifanya hapa,ni kuuma na kupuliza na kujaribu kubalance maoni yako.


Mkuu suala la Ulinzi na uwepo wa raisi kwa misingi ya muda kwa sasa na miaka ya nyuma ni tofauti kabisa. US ya leo si US ya miaka 10 iliyopita. Ina maadui zaidi walio na nguvu zaidi. Hata hivyo kwa hili naomba msome hapo Sikonge kaidadafua vema - Post #.

Tukija suala la Serikali na matumizi yake ya vyombo vya dolla dhidi ya Upinzani na Wananchi thats another topic kabisa na bado sijaona inahusiana vipi na Usalama Tanzania kunyang'anywa majukumu; jambo ambalo siafiki. Waliachiwa wafanye yale yalo ndani ya uwezo wao.

Unaposema kuwa 'Uzalendo' umeharibiwa na Serikali nayo si kweli... Viongozi wa nchi wapo wangapi wenye nguvu ya kuongoza? Na wananchi wapo wangapi? Wananchi na viongozi wote si wazalendo kwa nchi yetu. Hilo ni wazi wala si siri... Kila siku tupo kulaumu Viongozi (suala ambalo halikwepeki) lakini hivi tumetafakari wale ambao ni wasomi na wanaingia katika taasisi tofauti kuwajibika nafasi yao ipo kwa kiwango kipi kwenye kuangamiza taifa?
 
Last edited by a moderator:
Naomba uangalie Diary yako kama hawa walikuja kabla au baada ya Sept 11.

AshaDii
Jaribu kurudi katika diary yako (au maktaba yako) ili ukumbuke kuwa Bush ametembelea Tanzania mwaka 2008, miaka mingi tu baada ya milipuko ya September Eleven. Aliyekuja Tanzania kabla ya milipuko hiyo ni Raisi Bill Clinton aliyekuja Tanzania mwaka 1998.

Thanks for pointing that out.. Maktaba yangu iliishia hapo. Ila nilikuwa nakumbuka kwa Hilary ni post muda huo. So hapa kilichobaki ilikuwa tu google iniokoe. Lol

CheiChei I guess you got my point. Kaka Maranya nimekusoma post yako ya awali. Nimekupata vema.
 
Vipi yule mshikaji wa matusi wa CCM alibahatika kumpa mkono OBAMA?????
 
Vipi yule mshikaji wa matusi wa CCM alibahatika kumpa mkono OBAMA?????

Makachero wanawajua fika wote walio na ndimi za moto na waliochafuka kwa damu katu hawakuruhusiwa kumkaribia Obama.
 
Back
Top Bottom