Ujio wa Tundu Lissu na matokeo ya ajabu

Ujio wa Tundu Lissu na matokeo ya ajabu

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kuna vitu vinatokea kwa namna ya kipekee na ajabu kabisa. Ujio wa Lissu kurejea nyumbani akiwa bukheri wa afya una mengi ya kusimulia

Lissu aliyeondoka mahututi hajitambui kwenye machela baada ya kunusurika kifo cha risasi 36, anarejea nchini akiwa mwenye tabasamu na matumaini mengi.

Mtuhumiwa wake kwenye shambulio husika wakati huo alikuwa mwenye mamlaka na nguvu nyingi akiivinjari nchi atakavyo huku akifanya atakayo bila kuguswa na yeyote yule.

Leo hii Lissu anaporejea nchini mtuhumiwa wake si lolote si chochote tena(labda huko mbeleni) mtuhumiwa wake sasa ni mwananchi wa kawaida kabisa mwenye msongo wa mawazo huku sintofahamu ikimtawala kuhusu future yake. Anachosubiri kwasasa ni huruma ya mkulu kama kwa bahati mbaya wakiweza kufanya figisu.

Imagine leo hii Lissu anapokaribia kabisa kurudi mwana bado angekuwa na yale maguvu yake, sipati picha ingekuwaje. Kuna maanguko huja kwa hatua. Wazungu wanasema: A day when everything went wrong. Waswahel wanasema siku imeanza vibaya, na siku ya kufa nyani miti yote huteleza.

Umeteleza wa ubunge kwenye kura za wajumbe, unaweza kuteleza kwenye uteuzi, ama kwenye viti maalum.

Mambo huja kinyume. Wakati Lissu atakapokuwa kwenye msafara wa hiari, mwana atakuwa kajificha mahali na remote mkononi akiangalia kwa uchungu live updates za mbaya wake mwenye na uso wa tabasamu kubwa.
 
Ujio wa lissu ni sawa kwa mapana yake na marefu yake kwangu naona sawa.

Mshana Jr je, umewekewa uvuli wa mauti au akili zimecheza? Ni nani aliyekudanganya kwamba wana wanadhoofika?

Nikikuamini kama msomi na mtafiti mbobevu ni wapi umefeli mtani wangu?

Weka vidhibiti mwendo my dear, mwana saa hii ndo yuko huru anatembea kama kondoo aliyelowa ili ajiokotee mawindo ya kushiba.

Wakati huu waweza kuwa nyakati mbaya kuliko zote huko mbeleni, tena aweza anza kazi ya kuuza vikombe na visahani mtaani kwako mtatia story ila siku ya tatu historia yako itakoma.

Note me.
 
Mtuhumiwa wake kwenye shambulio husika wakati huo alikuwa mwenye mamlaka na nguvu nyingi akiivinjari nchi atakavyo huku akifanya atakayo bila kuguswa na yeyote yule
Mkuu Mshana Jr , hii haijakaa vizuri kwasababu kwenye shambulio la Lissu, ukiondoa uzushi wa mitaani na ramli chonganishi, hakuna mtuhumiwa yoyote rasmi, kufuatia shambulio hilo kufanywa na watu wasiojulikana, hivyo kitendo cha wewe kusema kuna mtuhumiwa, huku sheria zetu ziko wazi kabisa, kukitokea tukio lolote la jinai, kama kuna mtu yoyote mwenye taarifa zozote za mhusika au wahusika wa tukio hilo, anapaswa kuripoti kunakohusika na sio kutegenea uzushi wa mitaani na mitandaoni, vinginevyo na mada yako hii ni ramli chonganishi!.

Kukitokea jinai yoyote, mtu yoyote mwenye taarifa kuhusu jinai hiyo kabla haijatendeka, na hakutoa taarifa au kuripoti kwa vyombo husika, kunamfanya mtu huyo kuwa ni sehemu ya jinai hiyo as an accessory before the facts.

Na akiijua baada ya kutendeka na bado ukanyamaza, anakuwa ni sehemu ya jinai hiyo as accessory after the facts!.

Don't be one, kamripoti!. Jinai haina ukomo!.

Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!

P
 
Wafipa tuna misemo yetu miwili inafanana sana

1. Time will tell
2. Time will heal all the wounds.

Sio kila mbwa Koko anayebweka mbele yako umpige kwa mawe, wengine ni wa kuwaacha tu wabweke wewe upite zako.

Ntafurahi sana iwapo Tundu Lissu atawasamehe watesi wake wote na kuuachia muda na karma viwahukumu.
 
Mkuu Mshana, hii haijakaa vizuri kwasababu kwenye shambulio la Lissu, ukiondoa uzushi wa mitaani na ramli chonganishi, hakuna mtuhumiwa yoyote rasmi, kufuatia shambulio hilo kufanywa na watu wasiojulikana, hivyo kitendo cha wewe kusema kuna mtuhumiwa, huku sheria zetu ziko wazi kabisa, kukitokea tukio lolote la jinai, kama kuna mtu yoyote mwenye taarifa zozote za mhusika au wahusika wa tukio hilo, anapaswa kuripoti kunakohusika na sio kutegenea uzushi wa mitaani na mitandaoni, vinginevyo na mada yako hii ni ramli chonganishi!.

Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!.
P
Jalada lilifungwa taarifa itapelekwa kwa nani?
 
Mkuu Mshana, hii haijakaa vizuri kwasababu kwenye shambulio la Lissu, ukiondoa uzushi wa mitaani na ramli chonganishi, hakuna mtuhumiwa yoyote rasmi, kufuatia shambulio hilo kufanywa na watu wasiojulikana, hivyo kitendo cha wewe kusema kuna mtuhumiwa, huku sheria zetu ziko wazi kabisa, kukitokea tukio lolote la jinai, kama kuna mtu yoyote mwenye taarifa zozote za mhusika au wahusika wa tukio hilo, anapaswa kuripoti kunakohusika na sio kutegenea uzushi wa mitaani na mitandaoni, vinginevyo na mada yako hii ni ramli chonganishi!.

Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!.
P
Wewe unajulikana una chuki kwa Lissu na Chadema bora ukae kimya tu.
 
Wafipa tuna misemo yetu miwili inafanana Sana.
1. Time will tell
2. Time will heal all the wounds.
Sio kila mbwa Koko anayebweka mbele yako umpige kwa mawe, wengine ni wa kuwaacha tu wabweke wewe upite zako.
Ntafurahi sana iwapo Tundu Lissu atawasamehe watesi wake wote na kuuachia muda na karma viwahukumu.
Hapana.

Jema ni kuachia mkondo wa sheria uchukue nafasi yake.

Kusamehe ni baada ya hapo. Huwezi kusamehe bila kujua unamsamehe nani aliyekukosea.
 
Wafipa tuna misemo yetu miwili inafanana Sana.
1. Time will tell
2. Time will heal all the wounds.
Sio kila mbwa Koko anayebweka mbele yako umpige kwa mawe, wengine ni wa kuwaacha tu wabweke wewe upite zako.
Ntafurahi sana iwapo Tundu Lissu atawasamehe watesi wake wote na kuuachia muda na karma viwahukumu.
Mkuu hapo Sumbawanga bei ya radi imefika sh ngapi? Nina kazi nayo
 
Mshana Jr,

Kinabii kuna kitu/mabadiliko yanakwenda tokea, wakati wa Mungu si wa binadamu, mwenge zindiko limekiukwa sababu ya corona,suspect kachezea spana, nguzo mbabe wa CCM Mungu kampenda huyu alitumia vyote nguvu na akili kuibeba CCM oyee waliobaki msamiati wa matumizi ya akili hawana kwao nguvu ndo jawabu, wakakosea kuwazoeza polisi kukamata watu hii ni mbaya sana ktk nchi watu wakishazoea kukamatwa utiisho na uoga utoweka.

Prophecies asubui kumekucha. Hakuna cha Jecha Wala Lubuva Safari hii, anga limefunguka.
 
Wafipa tuna misemo yetu miwili inafanana Sana.
1. Time will tell
2. Time will heal all the wounds.
Sio kila mbwa Koko anayebweka mbele yako umpige kwa mawe, wengine ni wa kuwaacha tu wabweke wewe upite zako.
Ntafurahi sana iwapo Tundu Lissu atawasamehe watesi wake wote na kuuachia muda na karma viwahukumu.

Matured and civilized ahangaiki na kelele za bawaba hizo zilikuwapo zitakuwepo Wala hazimnyimi usingizi. Things fall apart.
 
Mkuu Mshana, hii haijakaa vizuri kwasababu kwenye shambulio la Lissu, ukiondoa uzushi wa mitaani na ramli chonganishi, hakuna mtuhumiwa yoyote rasmi, kufuatia shambulio hilo kufanywa na watu wasiojulikana, hivyo kitendo cha wewe kusema kuna mtuhumiwa, huku sheria zetu ziko wazi kabisa, kukitokea tukio lolote la jinai, kama kuna mtu yoyote mwenye taarifa zozote za mhusika au wahusika wa tukio hilo, anapaswa kuripoti kunakohusika na sio kutegenea uzushi wa mitaani na mitandaoni, vinginevyo na mada yako hii ni ramli chonganishi!.

Tuacheni Ramli Chonganishi: Tusihukumu, Tusije Tukahukumiwa!. "Karma Ndio Pekee Hutoa Hukumu ya Haki Hapa Duniani!.
P
P nimelitumia hilo neno kwa umakini wa hali ya juu na tahadhari zote. Na sijachukua uzushi wa mitaani bali yale yaliyonenwa na mhanga mara kadha..by the way ni MTUHUMUWA sijasema MHUSIKA
 
Back
Top Bottom