Ujira mdogo wa Tsh 4,600/ kutwa kwa vibarua muhimu kiwanda cha PEPSI Mbeya plant. Dkt. Tulia nakuomba tembelea Kiwandani kuna wapiga kura wako

Ujira mdogo wa Tsh 4,600/ kutwa kwa vibarua muhimu kiwanda cha PEPSI Mbeya plant. Dkt. Tulia nakuomba tembelea Kiwandani kuna wapiga kura wako

Hat-Trick

Senior Member
Joined
Jun 15, 2020
Posts
117
Reaction score
382
Kiwanda kikubwa cha uzalishaji soda za Pepsi, Seven Up, Mirinda, Mountain Dew n.k ambacho ni cha kanda ya kusini nyanda za juu SBC Mbeya Plant (Pepsi) kinaudumia takribani mikoa 3 au 4 yani Ruvuma, Iringa, Njombe na Mbeya yenyewe.

Vibarua wa kutwa wanalipwa 4,600/ kwa masaa 12 ya kazi wanaingia saa 07:00 asubuhi na kutoka saa 06:30 jioni.

Majukumu ya vibarua hawa muhimu,

1. Wanakagua na kuchambua chupa iliyotoka sokoni kama inafaa tena kutumika yani kwa walaji kabla ya kuoshwa kwenye mashine.

2. Wanazikagua na kuchambua chupa baada ya kuoshwa kwenye mashine kama zinafaa kutiwa soda tayari kwenda kwa walaji.

3. Wanakagua kila soda inayozalishwa kama ina muhuli wa TRA.

4. Wanakagua na kuchambua soda ambazo zipo tayari zinaoenda sokoni kama ni safi na salama hazina hitilafu kama vile ujazo,uchafu n.k

5. Kupanda kreti za soda kwenye pareti kwa ajili ya kuifadhiwa store.

Hayo ni majukumu muhimu zaidi kwa hawa wanaitwa vibarua wa "Production" bila uwepo wao kazi haziendi ni muhimu sana lakini maslahi yao ni madogo kwa mda wanaofanya kazi.

Wito kwa Mbunge wa jimbo la Mbeya tembelea Kiwandani ujionee wapiga kura wako kwa macho jinsi watu wanavyofanya kazi huku wakilalama si vibarua, si waajiriwa ni ujira wa chini sana hauridhishi, haukidhi kabisa tofauti kabisa viwanda vya jirani kama Cocacola na TBL.

4,600 ukiichambua inatumika hivi 2,000/ kula mchana na jioni,1,000 nauli kwenda na kurudi.
Balance Tsh.1,600/=
 
Ndivyo ilivyo,walikubaliana na ujira halafu wanalalamikia mshahara.

Hata hivyo si vibaya kwa Idara Kazi kuweka scale za mishahara viwandani.

Lakini pia kuangalia upya namna iliyo bora ya kupunguza tozo na makato makubwa kama yapo ili viwanda vidogo vidogo viweze kukua na kujenga uwezo wa kulipa wafanyakazi ipasavyo.
 
Kabla ya kuanza kazi kuna mkataba.kama ulisaini mkataba fanya kazi za watu.wewe unafikiri kwanini wanasema kazi za watu.@mitano tena.
Hakuna mkataba ukiitaji unafanya siku wiki 1 alafu unaacha hamna tatizo kila siku watu wapya wanaingia maana wanaocha ni wengi.
 
Wabaki nyumbani waone kama watazipata.Tatizo nikodi sio waajili TRA imewabana nao wanabana wanaowaweza ukiona ela haitoshi jiongeze sio kulalamika.
 
Wabaki nyumbani waone kama watazipata.Tatizo nikodi sio waajili TRA imewabana nao wanabana wanaowaweza ukiona ela haitoshi jiongeze sio kulalamika.
Ni kweli TRA inawabana tawi la mbeya tu? Wakati kampuni moja inaviwanda zaidi ya 3 Tanzania vibarua wale wale hulipwa zaidi kwa maeneo mengine.
 
Back
Top Bottom