Kibanga Ampiga Mkoloni
JF-Expert Member
- Aug 9, 2007
- 18,772
- 8,939
Kwa mujibu wa GAZETI LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA la Tarehe 5 Juni, 2020 SEHEMU YA TANO Ukururasa wa 15. Angalia Kiambatisho.
5.4 Uwasilishaji wa Malalamiko
Mgombea yeyote, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Serikali au chama kilichosaini Maadili ya Uchaguzi na kuweka
mgombea endapo kinaamini kwamba Maadili ya Uchaguzi yamekiukwa kitawasilisha malalamiko yake kwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi katika ngazi husika kwa maandishi.
5.5 Muda wa kuwasilisha malalamiko ya ukiukwaji wa Maadili
Malalamiko yoyote yatakayotokea yatawasilishwa kwa maandishi kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili
ya Uchaguzi ya ngazi husika ndani ya saa sabini na mbili (72) tangu kutokea kwa tukio linalolalamikiwa.
5.6 Kuitisha kikao cha Maadili ya Uchaguzi
Mwenyekiti wa Kamati husika baada ya kupokea malalamiko anatakiwa kuitisha kikao ndani ya saa arobaini
na nane (48).
5.7 Utaratibu wa kushughulikia Malalamiko
Utaratibu wa kushughulikia malalamiko dhidi ya ukiukwaji wa maadili utakuwa kama ifuatavyo-
(a) malalamiko yote yatajadiliwa na kuamuliwa katika kikao cha Kamati ya Maadili ya Uchaguzi kwenye
ngazi husika;
(b) Kamati itashughulikia malalamiko na kutoa uamuzi wake mapema iwezekanavyo;
(c) baada ya kupokea malalamiko, Kamati itamtaka anayelalamikiwa kuwasilisha utetezi wake kwa
maandishi ndani ya saa arobaini na nane (48) tangu kupokea taarifa ya malalamiko dhidi yake;
(d) katika kushughulikia malalamiko, Kamati inaweza kumuita mtu yeyote kutoa maelezo ili kusaidia
Kamati kufikia maamuzi ya haki;
(e) akidi ya kikao cha Kamati husika itakuwa zaidi ya nusu ya wajumbe wote wa Kamati;
(f) Kamati itaamua malalamiko yote ndani ya muda wa saa arobaini na nane (48) baada ya kusikiliza au
kupata maelezo ya utetezi kutoka kwa pande zote mbili ambazo ni mlalamikaji na mlalamikiwa;
(g) maamuzi yatakayofikiwa na Kamati ya Maadili ya Uchaguzi yatatekelezwa na pande zinazohusika na
maamuzi hayo;
(h) ikitokea kuna umuhimu wa kufanya maamuzi kwa kupiga kura, wawakilishi wa mlalamikaji na
mlalamikiwa wasiruhusiwe kupiga kura juu ya maamuzi hayo;
(i) malalamiko yatakayoshughulikiwa na Kamati ya Maadili ya Uchaguzi ni yale ya kipindi cha kampeni
za uchaguzi tu;
(j) malalamiko yatakayotokea siku ya upigaji kura yatashughulikiwa na msimamizi wa kituo cha kupigia
kura, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Msimamizi wa Uchaguzi au Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa
mujibu wa sheria za uchaguzi;
(k) Kamati itakuwa na mamlaka ya kuchunguza malalamiko yote yatakayowasilishwa kabla ya kufanya
maamuzi; na
(l) Kamati inaweza kuelekeza malalamiko mengine kupelekwa kwenye mamlaka husika kama itakavyoona
inafaa.
5.8 Rufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati
Upande ambao hautaridhika na uamuzi wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi una haki ya kukata rufaa kwa
taratibu zifuatazo-
(a) kama ni malalamiko yaliyoshughulikiwa katika ngazi ya kata husika, rufaa itakatwa kwenda kwa
Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili husika ndani
ya saa ishirini na nne (24) tangu uamuzi unaokatiwa rufaa ulipotolewa;
(b) uamuzi utakaotolewa na Kamati ya Jimbo utakuwa ni wa mwisho kwa malalamiko yote yaliyoanzia
ngazi ya Kata;
(c) iwapo malalamiko yaliyoshughulikiwa ni kutoka ngazi ya Jimbo, rufaa itakatwa kwenda kwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Kitaifa ndani ya saa 48 tangu uamuzi husika ulipotolewa;
(d) uamuzi wa Kamati ya Kitaifa utakuwa ni wa mwisho kwa malalamiko yote yaliyoanzia ngazi ya
Jimbo;
(e) iwapo malalamiko yaliyoshughulikiwa ni kutoka Kamati ya Kitaifa, rufaa itakatwa kwenda Kamati
ya Rufaa ndani ya saa arobaini na nane (48) baada ya uamuzi wa Kamati ya Kitaifa kutolewa;
(f) endapo kuna umuhimu wa kufanya maamuzi kwa kupiga kura, wawakilishi wa mlalamikaji na
mlalamikiwa hawataruhusiwa kupiga kura ya maamuzi; na
(g) upande usioridhika na maamuzi ya Kamati kwenye hatua ya mwisho ya rufaa husika unaweza kufungua
malalamiko ya Uchaguzi Mahakamani kwa mujibu wa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 au
Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292.
5.4 Uwasilishaji wa Malalamiko
Mgombea yeyote, Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Serikali au chama kilichosaini Maadili ya Uchaguzi na kuweka
mgombea endapo kinaamini kwamba Maadili ya Uchaguzi yamekiukwa kitawasilisha malalamiko yake kwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi katika ngazi husika kwa maandishi.
5.5 Muda wa kuwasilisha malalamiko ya ukiukwaji wa Maadili
Malalamiko yoyote yatakayotokea yatawasilishwa kwa maandishi kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili
ya Uchaguzi ya ngazi husika ndani ya saa sabini na mbili (72) tangu kutokea kwa tukio linalolalamikiwa.
5.6 Kuitisha kikao cha Maadili ya Uchaguzi
Mwenyekiti wa Kamati husika baada ya kupokea malalamiko anatakiwa kuitisha kikao ndani ya saa arobaini
na nane (48).
5.7 Utaratibu wa kushughulikia Malalamiko
Utaratibu wa kushughulikia malalamiko dhidi ya ukiukwaji wa maadili utakuwa kama ifuatavyo-
(a) malalamiko yote yatajadiliwa na kuamuliwa katika kikao cha Kamati ya Maadili ya Uchaguzi kwenye
ngazi husika;
(b) Kamati itashughulikia malalamiko na kutoa uamuzi wake mapema iwezekanavyo;
(c) baada ya kupokea malalamiko, Kamati itamtaka anayelalamikiwa kuwasilisha utetezi wake kwa
maandishi ndani ya saa arobaini na nane (48) tangu kupokea taarifa ya malalamiko dhidi yake;
(d) katika kushughulikia malalamiko, Kamati inaweza kumuita mtu yeyote kutoa maelezo ili kusaidia
Kamati kufikia maamuzi ya haki;
(e) akidi ya kikao cha Kamati husika itakuwa zaidi ya nusu ya wajumbe wote wa Kamati;
(f) Kamati itaamua malalamiko yote ndani ya muda wa saa arobaini na nane (48) baada ya kusikiliza au
kupata maelezo ya utetezi kutoka kwa pande zote mbili ambazo ni mlalamikaji na mlalamikiwa;
(g) maamuzi yatakayofikiwa na Kamati ya Maadili ya Uchaguzi yatatekelezwa na pande zinazohusika na
maamuzi hayo;
(h) ikitokea kuna umuhimu wa kufanya maamuzi kwa kupiga kura, wawakilishi wa mlalamikaji na
mlalamikiwa wasiruhusiwe kupiga kura juu ya maamuzi hayo;
(i) malalamiko yatakayoshughulikiwa na Kamati ya Maadili ya Uchaguzi ni yale ya kipindi cha kampeni
za uchaguzi tu;
(j) malalamiko yatakayotokea siku ya upigaji kura yatashughulikiwa na msimamizi wa kituo cha kupigia
kura, Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Msimamizi wa Uchaguzi au Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa
mujibu wa sheria za uchaguzi;
(k) Kamati itakuwa na mamlaka ya kuchunguza malalamiko yote yatakayowasilishwa kabla ya kufanya
maamuzi; na
(l) Kamati inaweza kuelekeza malalamiko mengine kupelekwa kwenye mamlaka husika kama itakavyoona
inafaa.
5.8 Rufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati
Upande ambao hautaridhika na uamuzi wa Kamati ya Maadili ya Uchaguzi una haki ya kukata rufaa kwa
taratibu zifuatazo-
(a) kama ni malalamiko yaliyoshughulikiwa katika ngazi ya kata husika, rufaa itakatwa kwenda kwa
Msimamizi wa Uchaguzi ngazi ya Jimbo ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili husika ndani
ya saa ishirini na nne (24) tangu uamuzi unaokatiwa rufaa ulipotolewa;
(b) uamuzi utakaotolewa na Kamati ya Jimbo utakuwa ni wa mwisho kwa malalamiko yote yaliyoanzia
ngazi ya Kata;
(c) iwapo malalamiko yaliyoshughulikiwa ni kutoka ngazi ya Jimbo, rufaa itakatwa kwenda kwa
Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili ya Kitaifa ndani ya saa 48 tangu uamuzi husika ulipotolewa;
(d) uamuzi wa Kamati ya Kitaifa utakuwa ni wa mwisho kwa malalamiko yote yaliyoanzia ngazi ya
Jimbo;
(e) iwapo malalamiko yaliyoshughulikiwa ni kutoka Kamati ya Kitaifa, rufaa itakatwa kwenda Kamati
ya Rufaa ndani ya saa arobaini na nane (48) baada ya uamuzi wa Kamati ya Kitaifa kutolewa;
(f) endapo kuna umuhimu wa kufanya maamuzi kwa kupiga kura, wawakilishi wa mlalamikaji na
mlalamikiwa hawataruhusiwa kupiga kura ya maamuzi; na
(g) upande usioridhika na maamuzi ya Kamati kwenye hatua ya mwisho ya rufaa husika unaweza kufungua
malalamiko ya Uchaguzi Mahakamani kwa mujibu wa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 au
Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Sura ya 292.