Ujumbe kwa Anthony Lusekelo anayeamini ana tiketi ya mbinguni tayari pamoja na wanaojiita walokole

Ujumbe kwa Anthony Lusekelo anayeamini ana tiketi ya mbinguni tayari pamoja na wanaojiita walokole

Mkungunero

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2023
Posts
401
Reaction score
569
PAPA FRANCIS ALISEMA: "Fikiria mama asiye na mume anayeenda kanisani au parokiani, na kumwambia katibu: NATAKA KUBATIZA MWANANGU, na mhudumu anasema: 'Hapana, huwezi, kwa sababu hajaolewa..."

Tukumbuke kwamba. Mama huyu alikuwa na ujasiri wa kuendelea na ujauzito - na ni kitu gani kilichompata ? Na mlango umefungwa! Kwa hivyo, tukifuata njia na mtazamo huu, hatufanyi watu wa Mungu, wema.

Yesu aliumba sakramenti saba na kwa mtazamo wa aina hii tunaunda ya nane: sakramenti ya desturi za kichungaji! "YEYOTE ALIYEKARIBIA KANISA LAZIMA ATAFUTE MILANGO ILIYO WAZI NA SIO HOFU YA IMANI".

“Tunawahitaji watakatifu wasio na pazia, wasio na tona. Tunahitaji watakatifu wanaovaa jeans na sneakers.

Tunahitaji watakatifu ambao wataenda kwenye sinema, kusikiliza muziki, na kutembea na marafiki zao.

Tunawahitaji watakatifu wanaomtanguliza Mungu na walio bora katika Chuo Kikuu.

Tunahitaji watakatifu wanaopata muda wa kuomba kila siku na kujua jinsi ya kupenda usafi walioko wa kisasa, watakatifu wa karne ya ishirini na moja walio na hali ya kiroho iliyoingia katika wakati wetu.

Tunahitaji watakatifu waliojitolea kwa maskini na mabadiliko muhimu ya kijamii.

Tunahitaji watakatifu wanaoishi ulimwenguni, wanaopata utakatifu katika ulimwengu, na ambao hawaogopi kuishi ulimwenguni.

Tunahitaji watakatifu wanaokunywa coke na kula kitimoto, wanaosikiliza iPod.

Tunahitaji watakatifu wanaopenda Ekaristi na hawaoni aibu kunywa bia au kula pizza wikendi na marafiki.

Tunahitaji watakatifu wanaopenda sinema, ukumbi wa michezo, muziki, densi, michezo.

Tunahitaji watakatifu wa kijamii, wazi, wa kawaida, marafiki, wachangamfu, masahaba.

Tunawahitaji watakatifu walioko duniani na wanaoweza kuonja vitu safi na vyema vya dunia, lakini bila kuwa wa kidunia." Huyu anatakiwa kuwa sisi! 🙏❤️
 
Mungu anajua yaliyo ndani yetu.
Utakatifu ni ibada inayolenga maisha ya mtu anayependa kuwepo kwa Mungu muda wote
 
Tunahtaji watakatifu watakaocheza na kulala na makahaba kwenye madanguro na bado wakabaki na Utakatifu wao na hivyo kuwasaidia Makahaba kuokoka.

CHEZA NA BAPA WEWE!
 
Ukimuondoa huyo Lusekelo, tena afadhali umemuacha huko kwenye title, ila kwa kumuondoa huyo hii ni bonge la Message na miaka yangu yote nimekua nikiishi hii.
 
Walokole wamepotea?

Una uhakika gani kuwa wewe ambae sio mlokole ndio haukupotea?

Yani umetumia reference ya papa Francis ambae ni binadamu kama wewe kuwahukumu binadamu wenzako, au umetumia waraka wa TEC unaopingwa na watanzania kujazia jazia mada yako?
 
Back
Top Bottom