Ujumbe kwa Hajar

Hahahaa. Ametia neno mbona.
Basi kheri,ngoja tusubiri tuone kama kura za mikononyuma zitatosha.
Ushauri,kama kura hazitatosha kutakuwa na haja ya kuitoa mikono nyuma na kuiweka mbele maana mbele ndio kunafaa, hii habari ya nyuma nyuma sidhani kama iko poa.
 
Duuh! Hii yako kali ujue mikononyuma.

Inabidi umkemee huyo shetani kwa kweli. Sababu inaweza kutokea hivyo na bado ukajikuta mwisho wa siku unamkosa Hajar halafu wakawahi wengine. Teh teh
Zamani kama unataka nyumba ya kupanga National Housing wanakwambia katafute nyumba ya NHC ambayo haina mtu halafu uiripoti kwao wakupe wewe uwe mpangaji. Sasa ilikua ukishaipata ukawafuata uwaambie nyumba iko mahali fulani haina mtu wanakushukuru kwa taarifa halafu wanakutolea orodha ya watu kibao ambao walikua katika waiting list
Acha tu unajua kumuombea mtu kifo ni zambi !!!lakini nahisi shetani ananijaribu eti natamani uanze eda ukimaliza tu niwahi
 
Hahahaaa. Huu ujumbe mikononyuma ameshaupata kwa kweli na asipouelewa basi tena. [emoji85]
 
Hahahaaa. Huu ujumbe mikononyuma ameshaupata kwa kweli na asipouelewa basi tena. [emoji85]
Mshenga kule naona alishakaa mkao wa kula, nadhani alikua na orodha ya vitu vya kumpelekea mikononyuma kama vile, mkaja wa bibi, koti la babu, mchumba ulimuonea wapi, kibwebwe cha shangazi, shanga za dada, kigodoro cha upwa na mazagazaga kibao kabda ya mahari...lakini kumbe kisicho riziki hakiliki! basi tena
 
Hahahaaa. Umeonaeee. Na alijipanga hasa sababu mpaka kufikia hatua ya kuomba ushenga sio jambo dogo.
 
Hahahaaa. Umeonaeee. Na alijipanga hasa sababu mpaka kufikia hatua ya kuomba ushenga sio jambo dogo.
Ila washenga wa Dar hua hawaaminiki aisee, kuna mmoja aliwahi kupewa ushenga si akajifanyia ushenga mwenyewe! Kwa bahati(utachagua mwenyewe hapo kama ni nzuri au mbaya) mchumba akashtuka na akawapiga chini wote akawaona wahuni, nikimkumbuka yule jamaa mshenga msambaa na lafudhi yake ilivokua akiongea hua nacheka peke yangu
 
Hahaaa! Huyo mshenga ni balaaa. Duuh.
 
Zakazaka ni noma mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…