MWAISEMBA CR
Member
- Apr 21, 2014
- 87
- 81
✳UJUMBE WA WAZI KWA MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CHADEMA, TUNDU LISSU KUELEKEA UCHAGUZI MKUU🆕
🔵From : Shujaa Charles Richard Mwaisemba (©️®️ M )
stmwaisembac@gmail.com
0712-054498/0759-420202
Kwanza kabisa nianze kwa kukupongeza sana sana niliposikia kuwa umefanya ibada ya shukurani Agosti 10,2020 katika Kanisa la mtakatifu Rita wa kashia lililopo Ikungi, Mkonoani singida kwa ajili ya Kumshukuru Mungu aliyekunusurisha na hatari ya mauti iliyotokea September 7, 2017 baada ya kushambuliwa na risasi 16 za SMG na kwa ajili ya kuwashukuru watanzania wote waliokuombea na kujitoa kwa hali na mali kwa ajili ya kunusurisha maisha yako.
Lakini jambo lililonifurahisha zaidi na kuwafurahisha Watanzania wengi, ni Roho yako ya msamaha uliyoionyesha kwa kuahidi kutokulipa kisasi mtu yeyote waliohusika na kufurahia kwa tukio hilo.Kwa Roho hiyo ya msamaha uliyoionyesha ni Roho ya Mungu kamili anayesamehe na kusahau maovu yetu ambayo itakupa kibali kikubwa hasa mbele za Mungu na Mbele za wanadamu.
Jambo la pili, nilolotamani kukuambia tunapoelekea katika uchaguzi mkuu wa 2020 ni kuepuka kushambuliia kundi lolote la watu au au taasisi zozote ambazo zinaonekana kama hazikuungi mkono au zinakupinga moja kwa moja, kumbuka nyuma ya taasisi hizo zina watu wengi nyuma yao ambao ndio wapiga kura na ambao hawapo upande wowote wa chama ila wataangalia reaction zenu juu yao na hivyo inaweza kupelekea si tu kukosa kura zao bali kukosa kibali hata kwa watu wa upande wako.
Inabidi kuwa makini sana kama si wewe basi timu kampeni zako, kuwaonya kutumia lugha za matusi au za kushambulia taasisi hizo hasa Taasisi za kidini au viongozi wa dini.Wanapowatukana au kuwashambia viongozi wa dini ujue vile vile umewashambulia waumini wao ambao hawatafurahia kuona viongozi wao wakivunjiwa heshima mbele ya jamii na hivyo inaweza kupelekea kupoteza kundi kubwa la watu ambao wangeweza kukusapoti hata kama viongozi wao wanaonekana wapo kinyume nanyi.Usishindane wala kuwajibu vibaya viongozi wa dini hilo litakupa credity kubwa katika uchaguzi huu.
Inakupasa kutumia nguvu kubwa kueleza sera na matatizo ya watu ambayo wanategemea kutatuliwa na serikali yenu ikiwa ikuchukua dola kuliko kutumia muda mwingi kujibishana na vikundi vya CCM au taasisi zinazowaunga mkono ambavyo vina lengo la kukutoa katika mstari wa kuwaelezea Ilani ya sera ya chama chenu mlichokusudia kuwafanyia watanzania.
Jambo jingine la mwisho, ninaloweza kukutia Moyo na kukuhakikishia ikiwa kweli Tume ya uchaguzi itakuwa Huru na haki na ikiwa utaplay smart kucheza na hisia za watanzania walio wengi, nafahamu unaweza kupata Ushindi tena kwa Kishindo bila shaka.
Nafahamu uwezo wako wa kujenga hoja, Uwezo wako wa kusimamia unavyoviahidi na kuvizungumza, Ujasiri wako wa kusema Ukweli bila kuwa na hofu ya chochote na nafahamu wewe ndio mtu sahihi kwa wakati huu mwenye uwezo wa kupambana na mtu aina ya Magufuli, ila fahamu Neno PASIPO YEYE(Mungu) , WEWE HUWEZI KUFANYA NENO LOLOTE(YOHANA 15:5:WARUMI 8:31), Tena fahamu BWANA ASIPOKWENDA NAWE KATIKA HATUA ZOZOTE, HUTAWEZA NA UTASHINDWA NA MAADUI ZAKO
Maana yangu ni Kwamba, Pamoja na uwezo wote ulio nao, umaarufu na ujasiri ulio nao, Pasipo kuonyesha kumtumaini Yeye Mungu katika kila jambo na kumuhofu yeye Mungu bado hatutaweza kushinda,Kumbuka ni Mungu ndiye anayempa mtu yeyote Mamlaka ya kutawala na Kumiliki (YOHANA 19:9-11)
Kumbuka watanzania, wanamtafuta Rais si tu mwenye uwezo wa kuwatoa katika ufungwa wa uhuru wao wa kujieleza,katika umsakini na ujinga na maradhi lakini zaidi sana wanatafuta Rais mwenye hofu ya Mungu ambaye ataweza kumtanguliza Mungu kwanza katika kila jambo kuliko kutumainia uwezo wake. Hivyo usipuuze ushauri au mambo yoyote yanayohusiana na Mungu kwa kufuata mfumo wa ulimwengu mzima unavyoendesha mambo yake.
Itakuwa ni jambo la ajabu sana ambalo utamsikitisha Mungu upeo, ikiwa Utapuuza Mambo ya Mungu na kuheshimu watumishi wa Mungu, Kumbuka si kwasababu wewe ni bora sana au una kitu cha ziada sana mpaka huyu Mungu asimamishe dunia kwa ajili yako kuuona MUUJIZA UNAOTEMBEA kwamba Upigwe Risasi 16 za SMG na bado uko hai, Bila shaka watanzania wamefahamu kuwa Mungu ana makusudi na wewe na nafikiri ndio Maana wengi wao wanamatumaini na wewe kuwa ndiye mtu sahihi unayeweza KULETA MABADILIKO YA KIMFUMO WALIYOKUWA WANAYAHITAJI KWA MIAKA MINGI.Ikiwa hutatambua kwanini Mungu kakuacha hai mpaka leo na kukuokoa na mauti ile basi utakuwa ni mtu wa ajabu sana kupata kutokea, ila kwa kuwa hapendi kuona yeyote anapotea bali wote wafikilie Toba hivyo naamini na hilo utalizingatia.
Mwisho kabisa nikutakie Mafanikio mema katika Kampeni mtakazozianza hivi karibuni na Mungu atakutangulia. Tunaiombea nchi yetu ipate Rais atakaweza kutupatia Katiba mpya, atakayeweza kubadilisha mifumo mibovu yote katika nchi hii,atakaweza kuruhusu uhuru wa habari na kujieleza, atakayeleta maendeleo ya watu kwanza, atakayeheshimu katiba yetu na mihimili yote, atakayeweza kusimamia rasilimali za nchi hii na Kupingana na rushwa kwa nguvu kubwa n.k.
Mungu akubariki.
🔵From : Shujaa Charles Richard Mwaisemba (©️®️ M )
stmwaisembac@gmail.com
0712-054498/0759-420202
Kwanza kabisa nianze kwa kukupongeza sana sana niliposikia kuwa umefanya ibada ya shukurani Agosti 10,2020 katika Kanisa la mtakatifu Rita wa kashia lililopo Ikungi, Mkonoani singida kwa ajili ya Kumshukuru Mungu aliyekunusurisha na hatari ya mauti iliyotokea September 7, 2017 baada ya kushambuliwa na risasi 16 za SMG na kwa ajili ya kuwashukuru watanzania wote waliokuombea na kujitoa kwa hali na mali kwa ajili ya kunusurisha maisha yako.
Lakini jambo lililonifurahisha zaidi na kuwafurahisha Watanzania wengi, ni Roho yako ya msamaha uliyoionyesha kwa kuahidi kutokulipa kisasi mtu yeyote waliohusika na kufurahia kwa tukio hilo.Kwa Roho hiyo ya msamaha uliyoionyesha ni Roho ya Mungu kamili anayesamehe na kusahau maovu yetu ambayo itakupa kibali kikubwa hasa mbele za Mungu na Mbele za wanadamu.
Jambo la pili, nilolotamani kukuambia tunapoelekea katika uchaguzi mkuu wa 2020 ni kuepuka kushambuliia kundi lolote la watu au au taasisi zozote ambazo zinaonekana kama hazikuungi mkono au zinakupinga moja kwa moja, kumbuka nyuma ya taasisi hizo zina watu wengi nyuma yao ambao ndio wapiga kura na ambao hawapo upande wowote wa chama ila wataangalia reaction zenu juu yao na hivyo inaweza kupelekea si tu kukosa kura zao bali kukosa kibali hata kwa watu wa upande wako.
Inabidi kuwa makini sana kama si wewe basi timu kampeni zako, kuwaonya kutumia lugha za matusi au za kushambulia taasisi hizo hasa Taasisi za kidini au viongozi wa dini.Wanapowatukana au kuwashambia viongozi wa dini ujue vile vile umewashambulia waumini wao ambao hawatafurahia kuona viongozi wao wakivunjiwa heshima mbele ya jamii na hivyo inaweza kupelekea kupoteza kundi kubwa la watu ambao wangeweza kukusapoti hata kama viongozi wao wanaonekana wapo kinyume nanyi.Usishindane wala kuwajibu vibaya viongozi wa dini hilo litakupa credity kubwa katika uchaguzi huu.
Inakupasa kutumia nguvu kubwa kueleza sera na matatizo ya watu ambayo wanategemea kutatuliwa na serikali yenu ikiwa ikuchukua dola kuliko kutumia muda mwingi kujibishana na vikundi vya CCM au taasisi zinazowaunga mkono ambavyo vina lengo la kukutoa katika mstari wa kuwaelezea Ilani ya sera ya chama chenu mlichokusudia kuwafanyia watanzania.
Jambo jingine la mwisho, ninaloweza kukutia Moyo na kukuhakikishia ikiwa kweli Tume ya uchaguzi itakuwa Huru na haki na ikiwa utaplay smart kucheza na hisia za watanzania walio wengi, nafahamu unaweza kupata Ushindi tena kwa Kishindo bila shaka.
Nafahamu uwezo wako wa kujenga hoja, Uwezo wako wa kusimamia unavyoviahidi na kuvizungumza, Ujasiri wako wa kusema Ukweli bila kuwa na hofu ya chochote na nafahamu wewe ndio mtu sahihi kwa wakati huu mwenye uwezo wa kupambana na mtu aina ya Magufuli, ila fahamu Neno PASIPO YEYE(Mungu) , WEWE HUWEZI KUFANYA NENO LOLOTE(YOHANA 15:5:WARUMI 8:31), Tena fahamu BWANA ASIPOKWENDA NAWE KATIKA HATUA ZOZOTE, HUTAWEZA NA UTASHINDWA NA MAADUI ZAKO
Maana yangu ni Kwamba, Pamoja na uwezo wote ulio nao, umaarufu na ujasiri ulio nao, Pasipo kuonyesha kumtumaini Yeye Mungu katika kila jambo na kumuhofu yeye Mungu bado hatutaweza kushinda,Kumbuka ni Mungu ndiye anayempa mtu yeyote Mamlaka ya kutawala na Kumiliki (YOHANA 19:9-11)
Kumbuka watanzania, wanamtafuta Rais si tu mwenye uwezo wa kuwatoa katika ufungwa wa uhuru wao wa kujieleza,katika umsakini na ujinga na maradhi lakini zaidi sana wanatafuta Rais mwenye hofu ya Mungu ambaye ataweza kumtanguliza Mungu kwanza katika kila jambo kuliko kutumainia uwezo wake. Hivyo usipuuze ushauri au mambo yoyote yanayohusiana na Mungu kwa kufuata mfumo wa ulimwengu mzima unavyoendesha mambo yake.
Itakuwa ni jambo la ajabu sana ambalo utamsikitisha Mungu upeo, ikiwa Utapuuza Mambo ya Mungu na kuheshimu watumishi wa Mungu, Kumbuka si kwasababu wewe ni bora sana au una kitu cha ziada sana mpaka huyu Mungu asimamishe dunia kwa ajili yako kuuona MUUJIZA UNAOTEMBEA kwamba Upigwe Risasi 16 za SMG na bado uko hai, Bila shaka watanzania wamefahamu kuwa Mungu ana makusudi na wewe na nafikiri ndio Maana wengi wao wanamatumaini na wewe kuwa ndiye mtu sahihi unayeweza KULETA MABADILIKO YA KIMFUMO WALIYOKUWA WANAYAHITAJI KWA MIAKA MINGI.Ikiwa hutatambua kwanini Mungu kakuacha hai mpaka leo na kukuokoa na mauti ile basi utakuwa ni mtu wa ajabu sana kupata kutokea, ila kwa kuwa hapendi kuona yeyote anapotea bali wote wafikilie Toba hivyo naamini na hilo utalizingatia.
Mwisho kabisa nikutakie Mafanikio mema katika Kampeni mtakazozianza hivi karibuni na Mungu atakutangulia. Tunaiombea nchi yetu ipate Rais atakaweza kutupatia Katiba mpya, atakayeweza kubadilisha mifumo mibovu yote katika nchi hii,atakaweza kuruhusu uhuru wa habari na kujieleza, atakayeleta maendeleo ya watu kwanza, atakayeheshimu katiba yetu na mihimili yote, atakayeweza kusimamia rasilimali za nchi hii na Kupingana na rushwa kwa nguvu kubwa n.k.
Mungu akubariki.