UK General Election: Waingereza leo kupiga kura kumchagua Waziri Mkuu na Wabunge

UK General Election: Waingereza leo kupiga kura kumchagua Waziri Mkuu na Wabunge

Protect

Senior Member
Joined
Apr 4, 2020
Posts
103
Reaction score
362
1720163914497.png

Wananchi wa Uingereza leo wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa kuchagua Waziri Mkuu na Wabunge.

Wagombea wanaopewa nafasi kubwa ya kushinda ni Waziri Mkuu wa sasa Rishi Sunak kutoka Chama cha Conservative na Keir Starmer kutoka Chama cha Labour.

Vyombo vya habari vingi vimetabiri kuwa Chama Cha Labour na mgombea wake Keir Starmer kitashinda uchaguazi huo kwa kura nyingi.

Watu milioni 46 wanastahili kupiga kura kwenye uchaguzi huu.

Vituo vya kupiga kura vitafunguliwa saa moja asubuhi mpaka saa nne usiku.

Uchaguzi mkuu wa mwisho ulifanyika mwaka 2019 ambapo mgombea wa Chama cha Conservative, Boris Johnson alishinda uchaguzi huo.

=========

Utabiri baada ya kura kupigwa nchini Uingereza unaonesha kuwa chama cha Labour kimeibuka na ushindi wa kishindo, huku kiongozi wake, Keir Starmer akielekea kuchukuwa nafasi ya Rishi Sunak kama waziri mkuu mpya.

Matokeo yaliyopitiwa na mashirika mbalimbali ya habari yanaashiria kuwa chama cha Labour kinachofuata siasa za mrengo wa kati kushoto kimepata viti 410 kati ya 650 bungeni, huku wahafidhina wa mrengo wa kulia, Conservative, wakimudu kukusanya viti 131 tu, kiwango cha chini kabisa kwa chama hicho kwa zaidi ya miaka 100 sasa.

"Kwa kila aliyeipigia kampeni Labour kwenye uchaguzi huu, kwa kila aliyetupigia kura na kukiamini chama chetu cha Labour kilichobadilika, ahsanteni." AliandikaStarmerkwenye mitandao ya kijamii.

Naibu wake, Angela Rayner, aliliambia shirika la utangazaji la BBC kwamba wametiwa moyo sana na matokeo, lakini asingeweza kusema zaidi mpaka pale matokeo yote yawe yamekusanywa na kutangazwa rasmi.
 
Waingereza wakichagua Labour wamekwisha kwa maana Sera ya Labour ni Open borders....ni vyema wakajifunza kwa wenzao wafaransa
 
Wananchi wa Uingereza leo wanapiga kura katika uchaguzi mkuu wa kuchagua Waziri Mkuu na Wabunge.

Wagombea wanaopewa nafasi kubwa ya kushinda ni Waziri Mkuu wa sasa Rishi Sunak kutoka Chama cha Conservative na Keir Starmer kutoka Chama cha Labour.

Vyombo vya habari vingi vimetabiri kuwa Chama Cha Labour na mgombea wake Keir Starmer kitashinda uchaguazi huo kwa kura nyingi.

Watu milioni 46 wanastahili kupiga kura kwenye uchaguzi huu.

Vituo vya kupiga kura vitafunguliwa saa moja asubuhi mpaka saa nne usiku.

Uchaguzi mkuu wa mwisho ulifanyika mwaka 2019 ambapo mgombea wa Chama cha Conservative, Boris Johnson alishinda uchaguzi huo.
sunak out
 
Nchi inayoongoza duniani kwa kubadili Mawaziri Wakuu. Toka mwaka 1900 mpaka leo wameshakuwa na Mawaziri Wakuu 26!
 
Hata achaguliwe nani lakini hakuna serikali ya Uingereza inayoweza kuunga mkono ugaidi au kuunga mkono imani yoyote inayoelekea kuunga mkono ugaidi, hilo halipo na magaidi lazima wataangamizwa tu.
 
Hata achaguliwe nani lakini hakuna serikali ya Uingereza inayoweza kuunga mkono ugaidi au kuunga mkono imani yoyote inayoelekea kuunga mkono ugaidi, hilo halipo na magaidi lazima wataangamizwa tu.
Wewe nani kakuambia sisi tunawategemea uingereza sisi tunamtegemea Allah alisha wambia kwenye bahari kuna hayo, miaka 1400 ilio pita afu hawa ndio juzi wamekuja na hio research miaka 100 ya nyuma.

Quran 22.40

Or [they are] like darknesses within an unfathomable sea which is covered by waves, upon which are waves, over which are clouds - darknesses, some of them upon others. When one puts out his hand [therein], he can hardly see it. And he to whom Allāh has not granted light - for him there is no light.

Afu tumtegeme muingereza sisi Waislam, ni Waisraeli ndio wana wategemea hao sio Waislam.
 
Watanzania bwana! utapata faida gani Sunak akishindwa?

Halafu hawafahamu kuwa Sunak ni Mtanzania mwenzao :

Rishi Sunak alizaliwa tarehe 12 Mei 1980 katika Hospitali Kuu ya Southampton huko Southampton , Hampshire, kwa wazazi wa Kihindu wazaliwa wa Afrika Mashariki wenye asili ya Kihindi ya Kipunjabi, Yashvir na Usha Sunak.

Baba yake alizaliwa nchini Kenya kabla ya ukoloni mwaka wa 1949, huku mama yake akizaliwa nchini Tanzania

1720136214272.png

Sunak akipongezwa na wazazi wake mama kushoto mzaliwa wa Tanzania na baba katikati mzaliwa wa Kenya... baada ya kuteuliwa na chama chake kuwa waziri mkuu (picha maktaba)
1720136615455.png

Mamia ya diaspora ya watu kutoka Afrika ya Mashariki walijitokeza kumpongeza waziri mkuu Sunak .pamoja na wazazi wake (Picha Maktaba)
 
Halafu hawafahamu kuwa Sunak ni Mtanzania mwenzao :

Rishi Sunak alizaliwa tarehe 12 Mei 1980 katika Hospitali Kuu ya Southampton huko Southampton , Hampshire, kwa wazazi wa Kihindu wazaliwa wa Afrika Mashariki wenye asili ya Kihindi ya Kipunjabi, Yashvir na Usha Sunak.

Baba yake alizaliwa nchini Kenya kabla ya ukoloni mwaka wa 1949, huku mama yake akizaliwa nchini Tanzania

View attachment 3033922
Sunak akipongezwa na wazazi wake mama kushoto mzaliwa wa Tanzania na baba katikati mzaliwa wa Kenya... baada ya kuteuliwa na chama chake kuwa waziri mkuu (picha maktaba)
View attachment 3033925
Mamia ya diaspora ya watu kutoka Afrika ya Mashariki walijitokeza kumpongeza waziri mkuu Sunak .pamoja na wazazi wake (Picha Maktaba)
Ameshapigwa chini,,,,Ulaya sahivi nao wanafanya mapinduzi,,,,anabakia Trump tu kumtoa mzee Biden
 
Back
Top Bottom