Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Jokakuu

badala ya ku-concetrate kwenye ukabila, tuangalie na miradi ya maendeleo ya VETA. Vilevile tuangalie ufanisi wa chombo hiki; vipi kuhusu ripoti ya ukaguzi wa mahesabu yao?

Mbona unaanza kujihami hata kabla ya nondo kuwekwa chini? Hii thread ni ya ukabila ama nakosea? Makusanyo ya pesa na ufanisi sio nyenzo ya kuendekeza ukabila kama upo. Na kama upo tutaukoromea
 
Dua,
quite frankly, mara nyingine inachosa kuzungumzia watu, ni bora tukazungumzia maendeleo hata kama ni madogo.

binafsi ninapochunguza chombo kama veta/tra/jeshi/tanroad/ikulu naweka kipaumbele katika masuala ya TIJA na UFANISI. haya masuala ya kuchunguza makabila ya watu huwa siyo priority yangu hata kidogo.

veta as an institution, kwa makisio inaweza kuajiri wafanyakazi 1000[makisio]. kila mwaka vyuo vya veta vinafundisha wanafunzi 8000[makisio].

kwangu mimi, idadi ya wanafunzi wa veta, na ubora wa elimu wanayopata, ni muhimu kuliko makabila ya warasimu walioko makao makuu ya veta.

nakubaliana na wewe kwamba thread hii inahusu "ukabila." vilevile thread hii imevunja rekodi kwa muda tuliowekeza hapa. je, ukabila ndiyo the most pressing issue in tanzania? mimi nadhani yapo mambo mengine yenye umuhimu kwa taifa letu, yanayohitaji muda wetu, kuliko hii hoja ya "ukabila."
 
Joka kuu.
Kaka acha uoga. tulisema kuna ukabila kwenye taasisi mbalimbali tukaambiwa wazushi. leo unasema tu concentrate kwenye utendaji? hivi hujui kuwa Equal opportunity policy ni lazima iwe applied kila idara ya serikali au binafsi? huruhusiwe kuajiliwa kama huta apply equal opportunities policy. kwanini Veta hadi wafagiaji ni wachagga? tuambie miradi mingapi ilipelekwa moshi kabla ya hiyo mikoa unayoiita disadvantages regions kwa vile haina wachaga jikoni. ilikuwaje Morgan Manyanga akapeleka kila kitu kizuri moshi? hujui Chuo cha ufundi moshi kila mfadhili alikuwa anapelekwa huko? kuanzia Danida,Sida hadi Norad.
JOKA KUU. hapo umeweka bodi si watendaji. sisi tunataka watendaji wa VETA(HEKALU YA WACHAGGA).
FUATILIA TIMU YA MANYANGA, NA HADI SASA YA MOSHI. TUAMBIE USAWA UKO WAPI? AU NDIO MASWALA YA HISTORIA UTATUAMBIA?
VETA KUNA NUKA UKABILA. SUALA HILI ALIFIKISHIWA WAZIRI WA KAZI KAPUYA AWAMU ILIYOPITA. watu wanateseka na ukabila. kwanini Bima iliundiwa tume na TRA NA VETA kusitizamwe? JK NA SERIKALI YAKO PITIA MACHO MASUALA HAYA NI MABAYA WENZETU Rwanda, Nigeria waliyadharau leo yanawa cost sana. bora tujenge ufa kuliko ukuta.
huko Mtwara bwana JOKA KUU watendaji ni wachagga watupu ni hivyo vyuo ni boarding hivyo wachagga wanapelekwa hadi huko kujaza nafasi. kisa watendaji ni wachagga./
 
mswahili.
sina uoga wowote ule. OK, veta kumejaa wachaga kila idara. wapi kwingine kumejaa wachaga?
 
I had started thinking of this forum as a meeting of mature and balanced minds, but I am starting to have a different thinking ...

Not that such people are not around, they are aplenty everywhere. Only that they are allowed, time and again, to post their uncalled for vitriols that ought to be stopped ....

I think this forum still has some time to rescue itself from vindictive, good for nothing allegations that ought to be relegated to the gutters of Uswahili!
 
Mtukwao.
Imekuwa uswahili ? mimi naona kijana katoka ukweli na ni vizuri umujibu kwa hoja si kusema uswahili, utakuwa hutofautiani na anayesema uchaga.

Ukabila ni tatizo ambalo linahitaji solution kunyamaza si jibu la kutatua tatizo.
 
Mswahili Kata issue, JokoKuu nae baada ya kukata issue anatetea ukabila. JF ipo hapa kurekebisha mienendo ya watu, anae hamisha ajenda anataka suala hili la ukabila lisizungumzwe. Leo hii Jokakuu haoni tatizo kwasababu mfumo huu wa ukabila yeye hawezi kumkamata kisa anatoka huko. Tunachotaka wahusika wajirekebishe na Tamaa mbaya, na huko nyuma walikuwa na kisingizio kuwa watu Fulan hawajasoma, leo wapo watu wa kila mahala, lkn bado MFUMO ni uleule.
 
Mtukwao.
Imekuwa uswahili ? mimi naona kijana katoka ukweli na ni vizuri umujibu kwa hoja si kusema uswahili, utakuwa hutofautiani na anayesema uchaga.

Ukabila ni tatizo ambalo linahitaji solution kunyamaza si jibu la kutatua tatizo.

Moja, Uswahili nilivyoutumia hapa hauna maana ya Kabila, kwa sababu hata hivyo hakuna kabila hilo, ila ina maana ya tabia na mtazamo fulani ambao siyo endelevu .... Kwa maana hiyo mchaga naye anaweza kuwa na tabia hiyo, ya kiswahili ... Siyo sifa nzuri, lakini imejengeka tayari, kwamba mambo ya hovyo hovyo huitwa mambo ya kiswahili ....

Pili, mimi siamini kabisa kwamba kuna ukabila, kama upo, havijatolewa vithibitisho. Kuwepo kwa watu wa kabila moja sehemu moja, nakataa, siyo ukabila. Kama ni ukabila, basi wanaosema hivyo waondoe vipengele vyote ambavyo vinaweza kuwaweka watu hao hapo, tubaki na huo ukabila.

  • Mbona watanzania wengine wamo sana kwenye biashara, sasa sijui serikali ifanyeje kusawazisha...

  • Mbona wanasheria wengi, wenye makampuni ya sheria mengi ni watu wa kabila fulani, nani kawapendelea? Serikali inabidi isawazishe, fani hii isiwe mali ya kabila moja ....

Ukabila Haupo, Wanaosema upo, wanajijengea hoja ....
 
Majameni!

Dont u think enough is enough on this thread? We have exhausted each and every thing, arguments and counter arguments.

Cant we agreed in disagreement and move on?
 
chuma,
kama walivyoeleza wachangiaji wengine kuwepo kwa idadi kubwa ya kabila moja ktk sekta fulani siyo uthibitisho wa ukabila. ushahidi anaoleta mswahili hapa hautoshi kuthibitisha kwamba kuna ukabila ktk hizo taasisi anazozituhumu.

yuko mchangiaji aliyeleta mpaka majina ya watumishi wa baadhi ya vitengo vya TRA. ushahidi huo ulithibitisha kwamba kuna diversity nzuri tu huko TRA. majibu ya mswahili yalikuwa kwamba ameleta majina ya walinzi,wafagizi, na madereva wa TRA. leo hii mswahili anaibuka na kudai kwamba VETA kumejaa wachaga, hata wafagizi ni wa wachaga!!

mswahili huyuhuyu akadai kwamba waziri mramba amependelea jimbo lake ktk kutoa fedha za ujenzi wa barabara. uchunguzi ukabainisha kwamba Mramba siye aliyeanzisha ujenzi huo, bali waziri john magufuli.

mswahili akaibuka tena na kudai kuna mbunge amelalamikia jinsi fedha za miradi ya barabara zilivyogawiwa na Waziri Mramba. In particular, jimbo la mbunge husika lilipewa sh.billioni 1, na jimbo la Mramba lilipewa billioni 17. uchunguzi[data frm TANROADS & budget speech] ukabainisha kwamba tofauti hiyo ilitokana na ukweli kwamba barabara ya jimbo la Waziri Mramba iko ktk hatua ya ujenzi, wakati ile ya Mbunge aliyelalamika ipo ktk hatua ya fesiability study and design.

Unajua Mama Anna Abdalah mbunge wa kusini alipata kuwa waziri wa ujenzi. Katika uongozi wake barabara za Kusini zilipewa kipaumbele kuliko sehemu zingine za Tanzania. Sikusikia mtu yeyote akilalamika. Watanzania tuliolelewa katika umoja tulielewa shida ya wenzetu wa mikoa ya kusini.

yuko mchangiaji mwingine, sina uhakika kama ni mswahili, akaibuka na madai kwamba mamlaka ya elimu imejaa wachaga, na inapendelea uchagani. again, tulipoangalia bodi ya wakurugenzi, na management ya mamlaka ya elimu, tukakuta kwamba tuhuma kwamba pamejaa wachaga si za kweli. vilevile taarifa za mahesabu ya mamlaka ya elimu hazikuthibitisha upendeleo kwa shule za uchagani.

mswahili huyuhuyu alikuwa akimpamba sana Dr.Asha-Rose Migiro. Kumpamba huko inaelekea kulitokana na imani yake kwamba Mama Migiro ni mtu wa pwani/"mtoto wa mjini"/"mtoto wa kiswahili." Kwani Mama Migiro alipokwenda kijijini kwao Usangi, Kilimanjaro, na kuandaliwa sherehe ya kimila, basi mswahili akawa kama amemsusa--hatujaona akimpamba tena!!

Kurasa 118, Replies 1117, na views zaidi ya 20,500 hapa Jamboforums, zote zinalisakama kabila moja tu, WACHAGA!! Mbona Wambulu na Barabaig hawanyanyaswi kwa kudominate mbio ndefu Tanzania? Mbona hakuna anayehoji Jeshini ambako idadi kubwa ni watu wa Musoma? Mbona hakuna anayehoji kwamba matajiri wengi wa mabasi ni Wakinga?

Binafsi siamini kama Wambulu,Barabaig,Wakurya,Wakinga, wanaukabila. SIAMINI kama kuwepo kwa idadi kubwa ya makabila hayo ktk michezo, na taasisi nilizozitaja, kumetokana na UKABILA. Anayelia ukabila anajaribu kuleta majibu rahisi kwa maswali magumu.
 
Mtukwao.
Si busara kusema uswahili ni ovyo ovyo, na ujue kuna waswahili wapo.

Joka kuu.

Ukabila upo hilo halina mjadala inawezekana wewe ukawa umenufaika nao, lakini usifikie sehemu kusema kuwa haupo. likewise kama mtu akisema Tanzania mtu hawezi kula mlo wa siku moja, wewe uje kusema kuwa sio kweli kwani kwetu tunakula milo minne kwa siku inatakiwa kulitazame jambo kwa mapana yake Bima ilundwa tume kuchunguza jambo hilo vipi serikali ipoteze pesa kwa kitu kisicho kuwepo?, kulizungumza tatizo ni sehemu ya kupata suluhu,
nimefuatilia maoni ya Mswahili kwa familia ya migiro inaonekana anawajua sana, binafsi nawafamu na wana asili ya pwani -Rufiji pia, na ASHA rose amesoma shule ya msingi Mnazi Mmmoja-Dar.
inawezekana baada ya kuuupata ukatibu mkuu watu wa huko Kilimanjaro wakachangamka na kuwaacha kwenye mataa Wandengereko. hata wewe ukipata madaraka leo hii utapata ndugu wengi wapya.nitakutumia kwenye PM watu wake wengi wa Pwani wa DR.Migiro na family yao kama unataka.
 
Kimsingi tunapozungumzia ukabila tunaangalia ktk Taasis za Umma, yaani vyombo vya serikali. Hii inatoa taasis binafsi, kama leo ukiinzisha website yako ya Habaritanzania, ukawaajiri wapare wote hakuna atakaekulaumu, atakaelaumu hajui tofauti ya Mali binafsi na mali ya Umma. kama wakinga wanamilki Magari ya usafiri its fine, as long as hawafanyi hujuma kuwazuia wengine kufanya hivyo. Ikiwa wakinga watafanya hujuma ya wazi kuwazuia waluguru wasimiliki biashara hio hapo itakuwa tatizo. Kama Mswahili kaanza na Benk, TRA, na sasa yupo VETA, basi muhim aendelee au wengine pia wanaweza kumsaidia kutoa nyeti sehm zingine ambako yapo makabila. Waswahili wanamsemo wao, wanasema aisifue MVUA imemnyea...means ambae anaona uchaga au U-kilimanjaro unasemwa either yeye ni Mkilimanjaro au hajakumbwa na u-kilimanjaro.
 
Swali, kuna mtu yoyote anajua mgogoro wa KKKT, ya katibu Mwenegoha na Cleopa Msuya?kuna harufu yoyote ya huu ugonjwa unaosemwa hapa?msio na data msi-extrapolate....
 
Chuma,
tatizo ni madai ya mswahili na data anazoleta. mara nyingi ameshindwa kuleta anything credible. kitu ambacho nampongeza na kumsifia ni ku-post kwa HASIRA,JAZBA, na KUJIRUDIA-RUDIA.

kuna watu wametumbukia ktk mtego wa kumuamini mchangiaji yeyote yule ilimradi azungumze kwa HASIRA, JAZBA, na KUJIRUDIA-RUDIA.

Yapo maneno aliyoyasema mswahili ambayo yanaashiria CHUKI za kikabila. Imefikia mahali inaonekana kama vile Mswahili anapinga "wachaga" na siyo "ukabila." Hilo ni tatizo. Kitu cha kushangaza ni kwamba ni wachache sana miongoni mwetu tuliodiriki kumkemea kwa hilo.

TOFAUTI kati ya KAMPUNI BINAFSI na TAASISI YA UMMA ni suala la UMILIKI. Kwa msingi huo, kampuni binafsi zinabanwa na MAADILI YA KIJAMII kama ilivyo kwa taasisi za Umma. Ni makosa kwa taasisi yoyote, iwe ya Umma, ua Binafsi, kuendeshwa kwa misingi ya ubaguzi wa aina yoyote ile.

Hoja yako ya "U-Kilimanjaro" imeniacha hoi kidogo. Unajua hilo ni kabila aliloligundua Mswahili ili kulazimisha hoja yake hapa. Mswahili anadai kuna aliance ya Wachaga na Wapare, "U-Kilimanjaro." Mtu yeyote yule mwenye uelewa mdogo tu wa makabila hayo hawezi kuamini kuwepo kwa kitu kama "U-Kilimanjaro."

Mzee Kifimbo,
Dr.Asha-Rose Migiro amezaliwa Songea. Baba yake Mama Migiro ni mzaliwa wa Usangi, Kilimanjaro, na Mama yake ni Mndengereko. Mama Migiro amesoma Mnazi-Mmoja na Korogwe Primary, sekondari amesoma Weruweru na Korogwe Girls. Zaidi amesoma chuo kikuu DSM, na Konstanz, Ujerumani.

Naomba tukifunge hiki kipengele cha Dr.Migiro, Undengereko, na Ukilimanjaro. Tuendelee na mada kuu.
 
Joka kuu.
Asha Rose amekulia zaidi kwa mama yake na upande wa mama yake hali yao kimaisha ni nzuri sana. huko Korogwe alikwenda boarding school.
ni mtoto wa kariakoo elewa hivyo.

Chuma.

Msuya ndio chimboko la ukabila na sumu aliyoipanda ya ukabila imeligharimu sana Taifa. KKKT ni magomvi ya kikabila.
 
Mswahili,

Huu ubishi ulikuwepo siku nyingi sana. hauna mantiki hata kidogo wala ukweli zaidi ya watu kutazama hesabu ya watu. Mkoa wa Kilimanjaro unaweza kuwa na shule 10 ukatoa wanafunzi 100 na mkoa wa Mwanza una shule mbili ukatoa wanafunzi 30 bado itahesabika kwao kuwa Kilimanjaro ina... kisha kati ya hao wanafunzi 100 wa Kilimanjaro wazawa wa hapo ni robo ya hesabu kamili.
Isitoshe makabila madogo, mathlan Wakarewe ambao population yao haifiki laki 3 wakisoma 10 ni wengi kuliko wachagga 50 ktk population yao ya millioni 2.
Kwa hiyo tunaposema wachagga wengi wamesoma lazima tukubali pia Wachagga wengi hawakusoma!...wasitupe hesabu za CCM hapa, kutafuta sababu za kujiona watu keki!...

TRA kuna ukabila!!!!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…