Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Maana kama Kesi ya Benny ni sawa na kumpelekea ngedere kesi ya nyani maana hata Makatibu wa Kuu wengi ukiangalia wanatoka sehemu fulani, sasa wengine wanazidiwa nguvu wanakuwa wasindikizaji tuu, na wao wakipewa vijinafasi viwili vya ndugu zao basi wenzao kumi

....to ask for datas in support of your claim!

....au umepiga blanket claim!
 
Mkoa wa Lindi ulikuwa na sekondari mbili hadi Mwinyi anaingia. jee maofisa wa Elimu wa mkoa wanatoka wapi? hawakuwa na program za kuendeleza maeneno hayo au walikuwa na mkakati wa wakoloni?


...kulikuwa hamna hata zile za wazazi na jumuiya nyingine?

...au kipindi hicho kujenga shule haikuwa deal huko?

...wabunge wa huko kazi yao ilikuwa nini?zaidi ya ile ya kuongea bungeni dodoma?

...hivi,huu ni ukabila?
 
Da ri salamu
Nafikiri kwa vyovyote vile utakuwa una aidha ndugu au rafiki anayefanya TRA, nenda kamuulize Ma- Commissioner wa azilishi walikuwa wanatoka wapi, Sanare Mku kabisa then waku wa Vitengo Income tax, Customs na Vat, Lawuo, Kitilya, Luoga.
Then Head Odf Human Resource Mama Sila, na Head wengine wa Huko huko, kama ni Finance etc.
Sasa hi ndio TRA yenyewe Head Office. Pale THB.
Baada ya Hapo ndio ushuke kwa wengineo Customs House na Income Tax.
Computer , Msemaji wa TRA etc.
 
Mzalendohalisi,
Naamini njia muafaka ni hiyo ya kuangalia jinsi tunavyoajiri kuanzia sasa hivi. Huwezi kuanza kufukuza watu kazi kwa nia ya kuleta religious/ethnic/regional balance.

Suala hili ni very sensitive na ni vizuri likafanyika kwa umakini mkubwa. Vilevile nadhani watu wana-concentrate zaidi kwenye ngazi za juu, bila kuangalia ngazi za kati na chini.

Chuma,
Mimi nadhani ni un-fair kusema viongozi hawana uchungu na barabara ya kusini. Vilevile siamini kama kuna hujuma zozote zile.

For 20 good years[wakati wa Mwinyi & Mkapa] mawaziri wa Ujenzi hawajatoka mikoa ya kaskazini. Vilevile tuwashukuru Mzee Mwinyi, na Mzee Mkapa, kwa juhudi zao kuleta ahueni ya usafiri kwa wananchi wa kusini.
 
Juzi juziSpika Sitta alisema tuache huu utaratibu wa kuchaguana baada ya kuonana ktk cocktail.
Kesho nitaiweka hiyo article hapa
 
Da ri salamu
Nafikiri kwa vyovyote vile utakuwa una aidha ndugu au rafiki anayefanya TRA, nenda kamuulize Ma- Commissioner wa azilishi walikuwa wanatoka wapi, Sanare Mku kabisa then waku wa Vitengo Income tax, Customs na Vat, Lawuo, Kitilya, Luoga.
Then Head Odf Human Resource Mama Sila, na Head wengine wa Huko huko, kama ni Finance etc.
Sasa hi ndio TRA yenyewe Head Office. Pale THB.
Baada ya Hapo ndio ushuke kwa wengineo Customs House na Income Tax.
Computer , Msemaji wa TRA etc.

...nadhani niliku-quote juu ya makatibu wakuu.

...tra inafahamika!
 
Ohhh, Joka Kuu
1. Nakupa tano- namaanisha ajira mpya- siyo kuwafukuza watu kazi. Ila tukiendelea na mfumo wa sasa- labda Bwana Yesu arudi haya matatizo ya ukabila hayatapungua
2. Je kuna mtu ana uzoefu wa karibuni namna ya kuaddress imbalances katika ajira kwa Tz licha ya Quota system wakati wa Nyerere ktk shule? Mie sijui kama kuna juhudi ya makusudi ya serikali kwa sasa!
 
Dari Salamu
Nashukuru kwa clarification , na samahani kwa kutokukuelewa kwenye hao Makatibu wa Kuu, So i will go back to my data Base nitafute hizo datA ZA mAKATIBU WA kUU
 
Hii ni Kauli ya Spika Kuhusu Uteuzi
na Mwandishi Wetu




SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta kwa mara nyingine tena wiki hii, amekata mzizi wa fitina kwa kuukosoa mfumo wa utawala nchini, akibainisha kuwapo kwa kasoro, hususan katika eneo la uteuzi, uwazi na uwajibikaji wa viongozi na watendaji.


Sitta, mwanasheria kitaaluma na mwanasiasa wa miaka mingi, aliyepata kushika nafasi mbalimbali za kitaaluma na kiteuzi, amesema pia kwamba, kasoro hizo ni kikwazo kikubwa kinachokwamisha maendeleo nchini.


Akihojiwa na kituo cha utangazaji cha Clouds FM mjini Dodoma jana asubuhi, muda mfupi kabla hajaanza kuendesha kikao cha Bunge, Sitta aliutaja ukosefu wa uwazi na uwajibikaji miongoni mwa viongozi na serikali, kuwa ni sababu nyingine kubwa zinazoikwamisha nchi kusonga mbele kwa kasi.


Akifafanua kuhusu uwazi, Sitta ambaye wiki hii alimaliza mgogoro wa chinichini kati yake na Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima (CCM) kwa staili ya aina yake, alisema kuwa idara nyingi za serikali, ama kwa mfumo wa kisera, ama kwa ukiritimba wa watu binafsi, hazipo wazi kwa wananchi kwa kiasi cha kutosha.


Alisema ukosefu huo wa uwazi umekuwa ukiwanyima wananchi fursa ya kufahamu mambo muhimu, ambayo yanaendelea ndani ya serikali na hivyo kuwafanya washindwe kuchangia mawazo yao ipasavyo.


Kuhusu uteuzi, alisema wakati umefika sasa kukaanza kuwekwa vigezo vya watu wanaostahili kushika nafasi fulani badala ya jambo hilo kufanywa kama ilivyo hivi sasa.


“Pia inafaa tuanzishe utaratibu wa kupima performance (utendaji) ya mtu, si tu kukutana katika cocktail (tafrija za jioni). Watu wanatakiwa kupimwa kwa uwajibikaji wao,” alisisitiza.


Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, rais ndiye aliye na mamlaka ya kuwateua takriban viongozi wa ngazi mbalimbali kitaifa, kiwizara, kimikoa, kiwilaya na wale wanaoongoza asasi mbalimbali nyeti za umma.


Pamoja na Sitta kuhoji mwelekeo huo, mawazo kama hayo yamewahi kuhojiwa na wasomi mbalimbali, ambao wamekuwa wakiona rais akipewa nafasi nyingi ambazo baadhi hazistahili kufanywa naye.


Sitta kwa upande wake, alisema Tanzania yenye neema, kama ilivyoahidiwa na Rais Jakaya Kikwete, inawezekana iwapo nchi itajipanga vizuri katika kutekeleza mipango ambayo nayo inapaswa kupangwa vizuri.


Ndiyo maana alisema katika kipindi cha miaka mitano atakayoliongoza Bunge, amedhamiria kufanya mabadiliko makubwa katika mhimili huo wa utawala ili kuhakikisha kuwa, unatoa mchango wake unaotakiwa katika kuleta maendeleo.


Alisema tayari mabadiliko yameshaanza kuonekana katika chombo hicho cha kutunga sheria, kwani kuna baadhi ya mambo ambayo yameanza kufanyika, ambayo yalikuwa hayafanyiki hapo kabla.


“Sasa hivi ripoti zote za kamati zinajadiliwa ndani ya Bunge. Tuna kamati 13 na jambo kama hili halijawahi kufanyika tangu tupate uhuru,” alisema Sitta na kutaja mabadiliko mengine kuwa ni kujadiliwa kwa Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) jambo ambalo halijawahi kufanyika tangu enzi Edward Sokoine alipokuwa Waziri Mkuu.


“Zipo hizi ripoti za mkaguzi, zinawasilishwa na zinajadiliwa, wabunge wanaona na kuhoji jinsi mamilioni ya fedha yalivyotumika… haya ni mabadiliko makubwa,” alisema.

Katika mabadiliko mengine makubwa, kuanzia mwaka huu, Bunge litakuwa likifanya vikao vya kuishauri serikali katika upangaji wa bajeti.


Sitta alisema kuwa, vikao vya mwaka huu vitafanyika Aprili 23 na 24 kwa lengo la kuwakilisha maoni ya wananchi kuhusu upangaji wa bajeti.


“Bunge linawakilisha wananchi, maoni tutakayoyatoa ndiyo maoni ya wananchi, huu ni utaratibu ambao unafanyika sehemu nyingi duniani, na serikali inatakiwa isikilize maoni haya, si busara kukaa na kujipangia tu bajeti,” alisema.


Alibainisha kuwa, mabadiliko hayo yote yamo ndani ya nia yake ya kulifanya Bunge la Tanzania kuwa moja kati ya mabunge bora kabisa barani Afrika atakapokamilisha kipindi chake cha miaka mitano kama Spika.


“Huwa najiwekea malengo kila ninapoenda, hapa nilishasema mara nyingi kuwa nia yangu ni kulifanya Bunge la Tanzania kuwa Bunge bora kabisa barani Afrika,” alisema.

Sitta alisema kuwa ndoto ya kuifanya Tanzania kuendelea kwa kasi inawezekana iwapo tu wananchi na viongozi wataamua kujipanga vizuri.


Akitoa mfano, alisema kuwa zipo nchi ambazo miaka michache iliyopita uchumi wake ulikuwa unalingana na Tanzania, lakini leo zipo mbali kutokana na kujipanga vema na kutekeleza yale waliyojipangia.


“Unaposikia China imeendelea wakati wanafuata Ujamaa haikuwa mchezo… kwa wale Wachina, mtu wanayembaini kuwa ni mhujumu uchumi, anapigwa risasi na si masihara hata kidogo,” alisema.


Kabla hajajitosa katika siasa za waziwazi kwa mara ya pili kupitia uchaguzi mkuu wa mwaka juzi, Sitta alikuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na chini ya uongozi wake, TIC ilipata kuwa moja ya vituo bora vya uwekezaji duniani.


Kabla ya kushika wadhifa huo TIC, Sitta alikuwa amewahi kuwa mbunge wa Urambo, nafasi iliyomwezesha kuteuliwa kushika uwaziri wakati wa Serikali ya Awamu ya Pili ya Ali Hassan Mwinyi.



DeleteReplyForwardSpamMove...
 
Huyu si ndie yule alietumia Mil 100 kujadili dakika? nae anastahili kupigwa risasi?
 
Masatu
Unajua ukitaka kujadili kitu, jadili one at a time, sasa kama ni ukabili tujadili huo ukabila/udini ingawa hili la dini ni very sensitive nchini kwetu.
Hayo Mapungufu ya Sitta na wengineo yawe kwenye title ingine
 
Masatu
Unajua ukitaka kujadili kitu, jadili one at a time, sasa kama ni ukabili tujadili huo ukabila/udini ingawa hili la dini ni very sensitive nchini kwetu.
Hayo Mapungufu ya Sitta na wengineo yawe kwenye title ingine

Lakini kwenye makala iliyobandikwa hapo juu Sitta haielezi chohcote kuhusiana na dini au ukabila.

Kwa nini ushauri wako usianze kwako mwenyewe kwa kuweka makala isiyohusiana na mjadala
 
Point yangu ilikuwa ktk mfumo wa uteuzi ambao unaleta hisia za ukabili/udini.
Eg labda wewe ni Bosi sehemu fulani uakafanya Sherehe/cocktail nyumbani kwako wakaja ndugu zako na marafiki na vobosile wengine, through mazungumzo labda kibosile mwingine akamuona ndugu yako wakaongea then akamuona anafaa for a certain post, huoni hapo kuna probability ya kucahaguliwa watu wa upande wako zaidi kuliko kwingine.
What about yule ambaye hakuja/ kualikwa kwa sababu hamjuani au sio wa upande wako, atakuwa haja onekana ,hivyo potential yake haijaonekana.
Au tuseme wewe unafanya uchaguzi kutokana na watu uliosoma nao na Bahati Mbaya/nzuri Umesomea Misheni au kule usukumani , si utaishia kuteu wa sehemu hiyo au wa dini hiyo.
Maana katika mjadala huu tunajaribu kuangalia tatizo la Ukabili na Jinsi ya kutatua.
Kama nimekosea unaweza nirekebisha

quotation from Sitta
Kuhusu uteuzi, alisema wakati umefika sasa kukaanza kuwekwa vigezo vya watu wanaostahili kushika nafasi fulani badala ya jambo hilo kufanywa kama ilivyo hivi sasa.


“Pia inafaa tuanzishe utaratibu wa kupima performance (utendaji) ya mtu, si tu kukutana katika cocktail (tafrija za jioni). Watu wanatakiwa kupimwa kwa uwajibikaji wao,” alisisitiza
 
samvulechole... hakuna hoja ambayo ni ngeni hapa.. madai ya makabila hayo kupendelewa hayakuanza leo! tangu mara tu baada ya uhuru kulikuwa na tuhuma hizo hizo.. so.. there is nothing there..! Hata hivyo hatari unayoweza kuleta siyo ukabila bali ubaguzi, kuwa kama mtu anatoka kwenye makabila hayo basi asipewe nafasi fulani kwa vile watu fulani wanadhani kuna ukabila! Nitakupa mfano, kuna wanasheria watatu wote ni maprofesa... kuna Prof. Mwakalindile (Sheria, uzoefu miaka 30), Prof. Mtimba (mmakua, uzoefu miaka 10, sheria), na Prof. Chanda (Mzigua, sheria uzoefu miaka 5). Assuming maeneo ya fani zao ni sawa, ceteris paribus Rais anataka kumteua mshauri wa kisheria.. nani apewe kwa haki? Wengi watasema prof. Mwakalindile! Sasa kwa kufanya hivyo hata hivyo kuna wanyakyusa wawili tayari hapo ikulu ambao wameshapata nafasi zao, je tumnyime Mwakalindile kwa vile itaonesha ukabila?
 
Mzee Mwanakijiji,

Maelezo yako kuhusu ukabila katika ajira ni mazuri sana. Nimefurahi kwa quotes zako za JKN kuhusu hili. Watu wengi wana mawazo potofu kuhusu ukabila na udini katika ajira. Ukweli ni huo uliouelezea kwa ufasaha. Endelea kuelimisha
 
😕 Julius Kambarage Nyerere yuko hai mpaka leo. Butiama kapumzika tu. Ukitumia hoja hizi kwa wanaoendesha ukabila unawadifit kabisa ni hoja nzito. Tukizama katika ukabila wakati hakuna practice ya ukabila JKN anasema we are stupid na kweli hebu check tunataka mzalendo mmoja achukue nafasi fulani toka kwa hawa tunaowaabudu siku hizi halafu tunasuka mpango wa kumkata mtu fulani on tribal grounds hahahaha!!!! we will be very stupid. Isipokuwa ukabila ambao unaonekana upo ni katika mambo mengi kwamba hata katika makampuni fulani atamchukua mtoto wa fulani ndugu yake kwa kuwa yuko katika nafasi ya uteuzi wa mwisho, kuhusu ikulu kuwa na ukabila hapo mimi sijui ila kwenye makampuni haya yaliyobinafsishwa hiyo iko ile mbaya.
 
Kuna kitu lazima tukumbuke, and this is very obvious...watu wenye madaraka ni wanadamu wa kawaida kabisa, wenye human weaknesses, sentiments; pia hawa wanadamu wana individual differences (wanatofautiana) na commonalities (kuna vitu wanafanana, kama individuals ama kama a-class ama kama a-group etc); Kwa maana nyingine wanavitu vyote vinavyokwenda na kuwa binadamu. Based on that, wanaweza kufanya mambo mengi sana, mabaya sana na mazuri sana, kwasababu binadamu anauwezo wa kufanya yote haya...

Udini, ukabila, undugu, secularism, professionalism, umalaya etc ni mambo yanafanyika kabisa na wanadamu. Kwahiyo tusihamaki na kusema kwa uhakika ukabila upo; ama haupo! Kila kitu kinawezekana as long as ni banadamu anajishughulisha nacho!

Kitu tunachotakiwa sisi kukiangalia kwenye public offices, ni kwa kiasi gani wenye madaraka wana uwezo wa kutumia ubinadamu wao kufanya maamuzi kwenye issues za public interest. Tukiwa tumeacha mianya mingi, kuna uwezekano kabisa wa hizi offices kuwa abused. Tumekuwa na kawaida ya ku-trust sana watendaji katika public offices, as if the moment mtu anaapishwa ana-cease kuwa binadamu; or as if kuna annointing fulani ukiingia kwenye ofisi fulani unaipata na automatically unaweka nchi na wananchi kuwa priorities zako. Ndio maana tunakuwa na ma-excuse kibao, mara rais kashauriwa vibaya, mara hakuna ushahidi wa rushwa, mara wanamsingizia fulani....hii yote ni systems zetu haziko updated kuhakikisha zinaziba mianya ya watu kutumia ubinadamu wao kufanya maamuzi, na wala haziko efficient and effective katika kulinda maslahi ya nchi na wananchi; wala haziwafanyi watu kuwa accountable kwa madhambi yao...eti mtu anaiba billions halafu adhabu a-resign...lets go beyond the obvious...naomba kuwasilisha![/COLOR][/FONT]
 
Mtalii,
1. Yaani ofsini kwangu 95% ya wafanyakazi ni Wakristo- na Chuoni tulisoma na Waislam wengi tu tena walipasi vema. As a country- if we dont take affirmative actions now to reddress imbalances in Ukabila, Dini, Mkoa- inafika mahali- ndo inatokea watu wa kabila moja zaidi ni TRA, wanajeshi- ni Mara n.k. Ila kisiasa there is a denial of the truth! This is not healthy to our country!
2. Naona viongozi pia wamefunga maskio ya mawazo mapya- MSITU MPYA NYANI WALE WALE! Nani achukue hatua wandugu?

Mzalendohalisi chukua tano,wanaobisha ndiyo hao hao wanaofaidika.Ukweli ukabila ni mbaya sana nimeona na yamenikuta!.na sasa hawa jamaa wanafanya kila njia kila post nzuri waishike wao.Sasa swala la kujiuliza je hiyo mishahara wanayolipwa ni kodi ya kabila lao tu?.Je makabila mengine waendelee kuwa maskini,kwani kufanya kazi kunaleta maendeleo katika familia husika na hatimaye mtu atokako.Hata kwa uhai wa taifa ni hatari pia,kwani wanaweza kufanya lolote kwani sysem yote yao.Tuache unafiki hebu tujifunze yanayotokea somalia na sehemu nyingine.hakuna kabila ambalo halijasoma na waache kujifanya cake!
 
Back
Top Bottom