Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali

I think this is one of the fastest thread on JF. What does this mean?
 
Mheshimiwa Mkjj ahsante kwa kutukumbusha, hata hivyo definition yako ya ukabila haina matatizo hata kidogo. Ila tu mimi nafikiri pengine yawezekana kabisa huko kujisikia au kuhisia kama kabila lake ni bora kuliko la wengine ndiko kunakompa mtu motisha ya kuajiri watu wa kabila lake.
 
Wanabodi,
Jamani tuwe serious kidogo na swala hili.
Siwezi kusema kuna Ukabila nchini ila nataka kuelewa ikiwa wapo watu wanaofanya mchezo huo ni hatua gani zichukuliwe?
Hii habari ya kuwa mashahidi ktk dhana ambayo hakuna kati yetu anafahamu mchezo huu unachezwa vipi ni kujidanganya!..
Huwezi kusimama hapa na kutoa mifano ya waomba kazi kama ni makabila so and so!... what if haitokei hivyo? what if kweli kuna makundi ya watu wanaokumbatia Ukabila hata ktk ajira. Hii ni right ya kila Mtanzania haiwezi kutazamwa kichinichini.
Ndio maswala ya JK kuajiri watu wake na kuwalinda wahalifu tunatafuta tena sababu za kumlinda.
Hawa watu wachache hawawakilishi kabila zima la Wachagga ila ni magugu ambayo inabidi kuyashughulikia! hakuna kutunga hadithi hapa! TRA kama kweli ajira zinatoka kwa kabila bila shaka swala hili litazamwe..
 
I think this is one of the fastest thread on JF. What does this mean?

It means it is Hot, Touchy and Delicate issue; watu wame'guswa'
Angalia vile ambavyo watu ambao ni otherwise very reasonable and humble walivyotoka kiaina kwenye hii issue!
It is also very offending when one comes up with an unsubstantiated and sweeping statement that takes on board the whole tribe indiscriminatingly. It is almost insulting. Ni kama kusema...wachagga wote ni wezi, au...wanyakyusa wote ni washirikina..au wahaya wote ni malaya..I mean, we should research, reason and make a comperative analysis before coming up with any purpoted finding. What is even more disturbing in this one is the fact that some people are deliberately refusing to see the others' point of view; whats the use of throwing out a debate/discussion if you are not prepared to hear the other side?
I think thats why some people have come up very strong about it
 
Mwendapole,
Mimi sipendi hoja zinazoongezwa ama kupanuliwa na kuwa Ukabila. Mzee Mwanakijiji kasema kweli kabisa... Tanzania hakuna Ukabila! hiyo haina ubishi na wala hatuwezi kusema hivi vidimbwi vya watu wachache ktk kabila la Wachagga wanachukua jukumu la Wachagga wote!..Siamini kuna Ukabila nchini kama definiton ya Ukabila inavyosema ama MJJ alivyotupa.
Isipokuwa kama kweli magugu haya yapo - we have to look at the problem in hand!..
Tuondokane na mawazo ya Ukabila kabisa, pengine neno lililotumika ni zito zaidi lakini hizi pockets za washirikina hawa wachache inabidi kuzitazama vizuri kuliko kulitupilia mbali swala zima kwa sababu msemaji katamka Ukabila!
 
Unaweza kukubali kuw aUKABILA hakuna kama ukikubaliana na definition ya Mwanakijiji lakini kama hukubaliani na maelezo yake basi ukabila upo tena upo kila kona ya serikali yetu tangu tulipopata Uhuru na nashangaa kuna watu wanadiriki kusema kuwa siyo kweli

Kuna mtu aligusian swala la katiba ...nadhani katiba yetu inatakiwa ifanyiwe marekebisho makubwa sana ama sivyo tunaelendelea kulea CANCER mabayo kwa kiasi kikubwa ishaenea mwili mzima wa nchi

Hutuwezi kuendelea kuishi in denial na tusidanganyane kuwa yaliyotokea RWANDA 1994 hayawezi kutokea Tanzania.
 
Kama Ukabila nilivyotoa maana haupo.. ni ukabila gani uliopo? Kwa maoni yangu na jinsi nilivyoelewa kama siyo ukabila niliouelezea ukabila uliopo Tanzania ni wa "idadi ya watu wa kabila moja mahali pamoja". Kama huu ndio tunauzungumzia, maswali yafuatayo hayana budi kujibiwa basi.

a. Je mtu kumuajiri mtu wa kabila lake ambaye ana uwezo na uzoefu wa kazi hiyo ni ukabila?

b. Je ni watu wangapi wa kabila moja wanaruhusiwa kuwepo kwenye wizara, idara, kitengo kimoja bila kuleta hisia za ukabila?

c. Je, mtu wa kabila lako ambaye hufahamiani naye akiomba kazi umnyime hata kama ana uwezo na uzoefu na ambaye vipaji vyake unaweza kuvitumia? je umuajiri hata kama tayari kuna mtu mwingine wa kabila lako hapo? Je umnyime nafasi hiyo kutokana na kabila lake na wewe mwenyewe kutojiona mbaguzi wa kikabila utawezaje kuing'ang'ania keko mkononi, wakati huo huo unataka uitafune?

d. Kwa vile inaonekana kuna watu wengi wa makabila haya matatu sehemu nyingi je tuwapunguze vipi idadi yao hata kama wana uwezo na uzoefu? Tusimamishe ajira zote zinazohusu Wahaya, Wanyakyusa, na Wachagga kwa muda (temporary freeze)? Je tuwape dili za kustaafu mapema ili nafasi ziwe wazi kwa watu wengine? Je tukianza kufanya hivyo tutakuwa tunatatua tatizo la ukabila au tunaliongeza?

e. Kama tulivyoonesha (na mifano ya Mswahili inashuhudia) tatizo kubwa katika ajira ni undugu na kufahamiana (nepotism na cronysm), je hili tutalitatua vipi ili ajira iwe on merit and merit alone?
 
Mwendapole,
Mimi sipendi hoja zinazoongezwa ama kupanuliwa na kuwa Ukabila. Mzee Mwanakijiji kasema kweli kabisa... Tanzania hakuna Ukabila! hiyo haina ubishi na wala hatuwezi kusema hivi vidimbwi vya watu wachache ktk kabila la Wachagga wanachukua jukumu la Wachagga wote!..Siamini kuna Ukabila nchini kama definiton ya Ukabila inavyosema ama MJJ alivyotupa.
Isipokuwa kama kweli magugu haya yapo - we have to look at the problem in hand!..
Tuondokane na mawazo ya Ukabila kabisa, pengine neno lililotumika ni zito zaidi lakini hizi pockets za washirikina hawa wachache inabidi kuzitazama vizuri kuliko kulitupilia mbali swala zima kwa sababu msemaji katamka Ukabila!

Now this is where the problem is: pockets za watu/viongozi ambao wanakiuka maadili yao ya kazi, na hata kukosa utu. Hili ni tatizo ambalo kama nilivyosema awali, linakuwa kwa kasi kubwa. Nina mifano mingi; na hiyo ni kuonyesha jinsi ambavyo tatizo linakua. Its time Taifa kama Taifa linaweka mkakati wa kuondoa hali hii, otherwise tutajenga taifa ambalo wafanyakazi wake ni un-qualified/unskilled/incompetent..as a result kunakuwa na irresponsibility ya hali ya juu. Wakati mwingine nashindwa kuwalaumu mashirika ya nje yanapoachisha waTZ kazi na kuanza ajira mpya kwa kuleta wa kwao; lazima tujaribu kuwaelewa; wao wamezoea watu ambao wanjituma kazini, wanapokutana na wafanyakazi ambao waliajiriwa na shemeji/mjomba/hawara, na wamezoea kuja kazini na kuondoka saa wanayotaka..they have to get rid of them..fast. Na kama waTz wanataka kuingia katika soko la ajira za Kimataifa lazima waache mtizamo wa ajira za kujuana. People should be employed on merit. Kuna tatizo kubwa la watu kuzoea favours, na viongozi/waajiri kutumia nafasi zao vibaya..wanauza ajira kwa undugu/mapenzi/woga(mtoto wa bosi fulani siwezi kumnyima, kaja ki-note)/
Hili lazima lifanyiwe kazi; na kama tunataka ku-compete na wenzetu wa EA au outside EA basi tujue mtindo huu lazima uishe; otherwise iko siku kibao kitageuka na hao walioajiriwa kwa dizaini hizo watatolewa kwa kukosa sifa na utendaji m-bovu..by then hao wazee watakuwa hawako kwenye nafasi ya kutetea, and it will be too late to catch the train..
 
Well said Mkandara...

Mtaniwia radhi nimesoma kwa haraka hapo juu; sidhani kama hii imeshachangiwa tayari na mwanabodi yoyote.

Maoni yangu ya ukabila Tz ni kama hivi: Watu wamepeana nafasi kwa sababu ya ukabila au ni kwa sababu katika mfumo fulani watu hao walitokea kuaminiana zaidi kwa vigezo vingine mbali na makabila yao kufanana. Mf walisoma wote, walikuwa majirani, walifanya kazi fulani etc.

Binadamu wote mara nyingi tunakuwa na uhuru/ furaha kiasi fulani tukijua fulani yupo pale au hapa na huyu ninamfahamu au ninafahamu familia yake au alikotoka. Sasa katika mazingira hayo ndipo anapoishia kuwa karibu zaidi na kina kina Mwakilojo, Mwasandende, Mwaikambo etc kama yeye ni wa Mbeya.

Hii ni kwa sababu nchi yetu tumeanza kuchanganyika sana miaka hii ya 90's kwenda juu huko nyuma ilikuwa vigumu kuona Mchagga akiolewa na Muhaya au Mzaramo akiolewa na Mnyakyusa. Uchumi ilikuwa mzuri wananchi wengi walikuwa katika mikoa waliyozaliwa wakifanya shughuli zao huko. Lakini kwadri uchumi ulivyoyumba huko mikoani wengi wakakimbilia mijini na huko ndiko walipopata nafasi ya kujichanganya.

Kwa sasa kujichanganya kumekuwa kwingi kiasi kwamba watoto waliozaliwa miaka ya 70's kuja mbele wengi sana wala hawajui lugha zao za asili. wanajua tuu Kiswahili na pengine English, ukiwauliza kwa nini hawajua kisambaa au kisukuma wanakuambia tumezaliwa mjini. Ni watoto hawa hawa leo haoni nongwa kuoa makabila mengine.

Kwa mtazamo wangu huo nina uhakika katika miongo 2 ijayo haya tunayoyahofia leo huko katika maofisi ya yetu yatakuwa wala hayapo. Yote yatafuata mkondo wa mabadiliko ya kiuchumi, jiografia na jamii. Wakati huo itakuwa zaidi ya nini ulichonacho kama ni mtaji, mawazo mapya, elimu yako, uzoefu katika fani fulani etc.

Alamsiki
 
Yebo yebo,
Mbali na yote haya ni uzushi kusema wakati wa Nyerere kulikuwa na Ukabila vile vile kutafuta viji sababu visivyokuwa na msingi. Haya yote yanatokana na sisi kuwa bado usingizini kiasi kwamba hata Rushwa tunapoambiwa na rais JK kuwa hata Japan, Canada na USA wana rushwa. Ni ujuha kuweka imani ya namna hiyo mbele wakati hao viongozi wa nchi hizo hawawezi kusimama na kudai nchi yao ina Rushwa kama nchini nyinginezo.. itakuwa scandal kubwa sana.
Ni hawa hawa Watanzania ambao leo tunaweka hizi sababu wakati tunalia kuajiriwa kwa wageni!... Je na wao wakituuliza kama ni kosa kumwajiri mzungu ama Mkenya mwenzake tutasema nini! Je, ni idadi gani ya wageni wanaotakiwa kuwepo kampuni moja!...
Tatizo sio kuwepo kwa Wachagga ama Wanyakyusa ktk sehemu moja ya kazi! tatizo ni kutumia kabila kama kigezo ama CV ya mtu kupata ajira!.. hakuna ushahidi wa wazi ila huwezi kunambia ati TRA zaidi ya aslimia 50 ya waajiriwa wa TRA kupitia human resources ni Wachagga kwa sababu ndio waliokwenda omba kazi na wenye qualification.
Kuamini huku ni sawa na kuamini Wakenya ndio wanaoomba kazi maofisini kuliko Watanzania hali kazi zote zinaendeshwa na Watanzania hao hao ambao wanalalamika kuhusu utoaji wa ajira. How can they complain ikiwa hawajawahi ku apply kazi hizi?
Nitakubali kama kuna kitengo cha TRA huko Kilimanjaro kuwa na Wachagga wengi kulingana na population yao huko lakini ni kujidanganya kuwa TRA ina Wachagga kwa sababu za kipuuzi ati elimu zao wakati sisi wenyewe tunakubali Wanyakyusa na Wahaya pia wamesoma, mbona wao hawapo huko TRA?.. au ukaguzi wa mahesabu na Ukusanyaji fedha sio major za Wahaya na Wanyakyusa!... mpango ule imani za Hindu.

Mwanakijiji,
Dhana unayotoa haina nguvu kabisa ikiwa leo hii mimi nitawachukua Wakerewe na kuweka visingizio kama hivyo!...na hakuna mtu anayebisha kuwepo kwa watu wa kabila moja sehemu moja ya kazi isipokuwa llazima tufahamu kuwa hata Ubaguzi wa rangi huko South na marekani walitumia sababu kama zako!...kinachotakiwa ni kulitazama swala lenyewe kama lilivyowekwa ubaoni sio kutumia dhana. South na Marekani walipowauliza waajiri wengi maneno machafu yaliwatoka! maneno kama weusi hawafanyi kazi, wazembe, hawana IQ na mengine kibao..hawa walikuwa waajiri walioyasema haya nje ya dhana ya baadhi viongozi na wananchi waliokuwa wakitetea hoja bila kuelewa undani wa issue nzima. Sisi hatujafika huko na wala tusiombee kufika huko kwa sababu ndio mwanzo tutakuja kugawanyika vibaya sana. To deny the truth bila ushahidi wakati Mswahili katupa mifano ndani ya TRA ni kukwepa ukweli.
Penye haki siku zote ukweli hujitokeza!
 
Kama Ukabila nilivyotoa maana haupo.. ni ukabila gani uliopo? Kwa maoni yangu na jinsi nilivyoelewa kama siyo ukabila niliouelezea ukabila uliopo Tanzania ni wa "idadi ya watu wa kabila moja mahali pamoja". Kama huu ndio tunauzungumzia, maswali yafuatayo hayana budi kujibiwa basi.

a. Je mtu kumuajiri mtu wa kabila lake ambaye ana uwezo na uzoefu wa kazi hiyo ni ukabila?


NO..sio ukabila.

b. Je ni watu wangapi wa kabila moja wanaruhusiwa kuwepo kwenye wizara, idara, kitengo kimoja bila kuleta hisia za ukabila?


Hakuna haja ya kuweka uwiano unaotokana na ukabila. Idara yoyote itaendelea kama kutakuwa na uwiano wa mambo haya (elimu na uzoefu). Zaidi ya mambo hayo kuna hatari ya kuharibu mambo zaidi. Chukua mfano waingereza wanavyopata shida kuweka uwiano kama huo katika jeshi la polisi kwa kutaka weusi wa wa-asia wakubaliwe kujiunga na polisi kwa wingi zaidi au kwenye na mashule ya kidini kwa kutaka wapagani nao waruhusiwe kusoma kwenye mashule ya roman catholic..!!

c. Je, mtu wa kabila lako ambaye hufahamiani naye akiomba kazi umnyime hata kama ana uwezo na uzoefu na ambaye vipaji vyake unaweza kuvitumia? je umuajiri hata kama tayari kuna mtu mwingine wa kabila lako hapo? Je umnyime nafasi hiyo kutokana na kabila lake na wewe mwenyewe kutojiona mbaguzi wa kikabila utawezaje kuing'ang'ania keko mkononi, wakati huo huo unataka uitafune?


Hili kwa kweli liko wazi kila kiongozi mwenye busara zake atajua nini cha kuamua katika hili. Kwa mimi sina cha kuongeza.

d. Kwa vile inaonekana kuna watu wengi wa makabila haya matatu sehemu nyingi je tuwapunguze vipi idadi yao hata kama wana uwezo na uzoefu? Tusimamishe ajira zote zinazohusu Wahaya, Wanyakyusa, na Wachagga kwa muda (temporary freeze)? Je tuwape dili za kustaafu mapema ili nafasi ziwe wazi kwa watu wengine? Je tukianza kufanya hivyo tutakuwa tunatatua tatizo la ukabila au tunaliongeza?


Hakuna haja ya kufanya lolote, watu hao waliweza kuwa pamoja kwa sababu ya historia tunaoijua kwa enzi hizo waliweza kusoma wengi kaika mikoa yao kuliko mikoa mingine. Sio kwamba wamewekana tu kwa sababu huyu ni Kimaro na yule ni Massawe au huyu ni Mwaitobe na yule ni Mwakalobo. Mimi siamini hivyo ila, kama wapo basi utaratibu ufanywe ili kila post huko makazini iwe analysed upya. Mfano: iwapo Mr Maganga leo hii yeye ni mkurugenzi wa Wizara basi utaratibu uwekwe kwamba kuwa Mkurugenzi wa wizara kunahitaji sifa gani...labda MBA, MSc na uzoefu wa miaka 10 etc..then Mr Maganga aangaliwe kama ana sifa hizo, kama hana basi anaweza akapewa ruhusa ya kustaafu kwa hiari. Ila iwapo anazo basi aachwe aendelee na kazi yake.

e. Kama tulivyoonesha (na mifano ya Mswahili inashuhudia) tatizo kubwa katika ajira ni undugu na kufahamiana (nepotism na cronysm), je hili tutalitatua vipi ili ajira iwe on merit and merit alone?


Namna moja wapo ya kulitatua hili kwa mimi ninavyoona na wengine wanaweza kuwa na mtazamo wao tofauti; ni kufanya usaili/interview na jopo la watu wasiopungua 3 kutoka katika idara tofauti. Huku ngambo wenzetu wakita kukupa kazi wanafanya usaili na watu wa HR, Operations Manager, Timu Leader wa ile timu utakayojiunga nayo. Baadaye wote hawa wanakuwa na muda wa kutoa maoni yao kuhusu jinsi walivyokuona kwenye huo mkutano wa kazi. Sasa utakuwa eti kwa sababu Meneja wa Operation amekuona unafaa mtu wa HR anaweza kuwa na mtazamo tafauti...katika mazingira hayo itapunguza sasa kujuana na undugu.


Alamsiki
 
Mwanakijiji,
Dhana unayotoa haina nguvu kabisa ikiwa leo hii mimi nitawachukua Wakerewe na kuweka visingizio kama hivyo!...na hakuna mtu anayebisha kuwepo kwa watu wa kabila moja sehemu moja ya kazi isipokuwa llazima tufahamu kuwa hata Ubaguzi wa rangi huko South na marekani walitumia sababu kama zako!...kinachotakiwa ni kulitazama swala lenyewe kama lilivyowekwa ubaoni sio kutumia dhana. South na Marekani walipowauliza waajiri wengi maneno machafu yaliwatoka! maneno kama weusi hawafanyi kazi, wazembe, hawana IQ na mengine kibao..hawa walikuwa waajiri walioyasema haya nje ya dhana ya baadhi viongozi na wananchi waliokuwa wakitetea hoja bila kuelewa undani wa issue nzima. Sisi hatujafika huko na wala tusiombee kufika huko kwa sababu ndio mwanzo tutakuja kugawanyika vibaya sana.

Mkandara, hivi Ukabila ambao Wahaya, Wanyakyusa, na Wachagga wanadaiwa kuwa nao ni upi? Wa kuajiri watu wa makabila yao au wa kuona kuwa wao ni bora kuliko makabila mengine? Kama ni wa kuajiri watu maswali hayo niliyouliza bado yanasimama. Kama wa kujiona bora, je watu wenye maneno haya nao ni wakabila?

Nashukuru mkuu ES

Hawa watu mjini wametukuta na sasa wanataka kutufanya wajinga, mwinyi kama wewe kumbuka enzi hizo kuna timu ya mpira kama Nungu au cosmopolitan utamuona mikael kiongozi wa timu? hata Fat yetu kulikuwa na waswahili wenzetu utakutana na kina el-mamry,mnonji, abubakar mwilima, mohamed kassanda, n.k
sasa wamevamia hadi starehe zetu za mipira ndio utaona akina dismas ndumbalu wanagombea TFF. yaani wametuulia mashirika yetu ya umma na sasa hadi kwenye mipira wanatuvamia. huyu mikael anamjua mzee Tabu Mangara? shiraz shariff?

Hili suala la "sisi" na "wao" siyo ukabila ambao mwandishi anajaribu kuupiga vita? Au ukabila ni pale Mchagga, Mhaya, na Mnyakyusa anapoajiri watu wa kabila lake lakini huu wa kuona makabila mengine duni na yasiyostahili sio ukabila?

To deny the truth bila ushahidi wakati Mswahili katupa mifano ndani ya TRA ni kukwepa ukweli.
Penye haki siku zote ukweli hujitokeza!

Mkandara nimeuliza mimi mifano aliyotoa Mswahili, je ni wangapi kati yao walikuwa wanafahamiana? Je ni wangapi ambao siyo wachagga ambao wamepewa nafasi humo TRA ambao wanafahamiana na hao viongozi? Je, ni sehemu ngapi ambapo watu wanaajiriwa kwa kujuana na kufahamiana ukilinganisha na wale wanaojiriana kwa sababu ya makabila yao? Bado sijashawishika kuwa tatizo kubwa ni ukabila na siyo undugunization!
 
Yebo yebo,
Mbali na yote haya ni uzushi kusema wakati wa Nyerere kulikuwa na Ukabila vile vile kutafuta viji sababu visivyokuwa na msingi. Haya yote yanatokana na sisi kuwa bado usingizini kiasi kwamba hata Rushwa tunapoambiwa na rais JK kuwa hata Japan, Canada na USA wana rushwa. Ni ujuha kuweka imani ya namna hiyo mbele wakati hao viongozi wa nchi hizo hawawezi kusimama na kudai nchi yao ina Rushwa kama nchini nyinginezo.. itakuwa scandal kubwa sana.


Bob,

Napo sijakuelewa..tafadhali fananua kidogo uhusiano wa mfano wa rushwa na ukabila.


Ni hawa hawa Watanzania ambao leo tunaweka hizi sababu wakati tunalia kuajiriwa kwa wageni!... Je na wao wakituuliza kama ni kosa kumwajiri mzungu ama Mkenya mwenzake tutasema nini! Je, ni idadi gani ya wageni wanaotakiwa kuwepo kampuni moja!...


Hapa kwenye wageni ni upande mwingine tofauti kabisa maana hawa jamaa kwanza wanatakiwa kuomba kibali cha kufanya kazi Tz. Sasa iwapo kuna mfano wahindi 100 ambao wana elimu ya juu sana na uzoefu wa kazi za udaktari...serikali imekubali kuwapa vibali vya kufanya kazi Tanzania mimi sioni kwa nini wasipewe kazi kama watanzania wenye sifa hizo hawapo.

Dunia imebadilika leo hii sio tena wewe ni kabila, raia wa wapi au rangi yako...ni zaidi nini unacho...angalia Football ya Uingereza ilivyoawaliwa na wageni mfano mzuri timu ya Arsenal. Angalia pia USA kwenye fani ya udaktari jinsi wageni walivyoenda kwenye remote areas kuwa madaktari huko kwa sababu wazawa hawataki kukaa humo. Elimu na Uzoefu viwe vigezo vya kwanza, zaidi ya hapo ni siasa ambazo hazina nafasi katika dunia ya utandawazi.

Tatizo sio kuwepo kwa Wachagga ama Wanyakyusa ktk sehemu moja ya kazi! tatizo ni kutumia kabila kama kigezo ama CV ya mtu kupata ajira!.. hakuna ushahidi wa wazi ila huwezi kuniambia ati TRA zaidi ya aslimia 50 ya waajiriwa wa TRA kupitia human resources ni Wachagga kwa sababu ndio waliokwenda omba kazi na wenye qualification.


Ikifikia wakati idara moja ya umma kuwa na 50% ya wafanyakazi wa kabila moja basi tujijue tuko kwenye matatizo makubwa sana. Ningependa kuamini hatujafikia huo.

Kuamini huku ni sawa na kuamini Wakenya ndio wanaoomba kazi maofisini kuliko Watanzania hali kazi zote zinaendeshwa na Watanzania hao hao ambao wanalalamika kuhusu utoaji wa ajira. How can they complain ikiwa hawajawahi ku apply kazi hizi?


Mimi sitashangaa kwa watanzania kulalamika kwa hili...watanzania tuna desturi ya kulalamika. Huo ni ukweli wa wazi. Nitakupa mfano: kuna mkurugenzi mmoja alistaafu kazi, akaanza kufuatilia mafao yake...baada ya kupingwa danadana kama ilivyo desturi maofisi yetu ya serikali akaamua kwenda kuanza kulalamika. Wafanyakazi wenzake wa zamani wakabaki kumsema pembeni, "yeye si alikuwa mkurugenzi hapa mbona hakubadili hizi taratibu, leo ndio anaona taratibu ni nyingi na ndefu zisizo na maana..??!!!"

Nikija kwenye hoja yako Bob, utakubaliana na mimi kuwa asilimia kubwa sasa ya wahitimu wetu kutoka katika vyuo vyetu vya juu leo hii wanababaika kuandika Cv...?? Sasa tukija kwenye uzoefu...mfano fani ya Marketing...hebu niambie nchi yetu Tanzania miaka ya 1980 mpaka mid 1990's kulikuwa na Marketing gani. Hebu muweke mtanzania huyu na mkenya aliyesoma kwao miaka hiyo uone kama watakuwa level moja.

Haitoshi tu kusema tu kuwa tuajiri watanzania wenzetu. Ni lazima tuangalie chimbuko na mikakati ya muda mrefu ya kutafuta ufumbuzi ikiwa na pamoja kuinua elimu yetu. Kwa kiasi kikubwa kulinda masoko ya ndani kwenye dunia ya utandawazi ni vigumu sana, mtanzania ni lazima ajifue ili kushindana na mganda, mkenya n.k
 
Tanzania yetu ya leo ni ukweli usiofichika Ukabila, Udini, Kujuana na Rushwa ni moja ya vigezo vikuu vinavyohitimisha maamuzi ya upatikanaji wa ajira kutegemeana na kitengo husika unachoomba kazi then qualifications ndiyo inafuatia na utendaji ndiyo mtizamo wa mwisho kimaamuzi.
 
Katika hoja hii naomba nikubaliane na mtoa hoja pamoja na Mkandara.Hayo makabila matatu yaliyotajwa ni kweli wana idadi kubwa ya watu waliosoma lakini ni vizuri pia tuelewe kwa sasa kuwa sio wao pekee walio na Elimu.
Mwanakijiji umeeleza vizuri huko nyuma sababu zilizofanya watu wa hayo makabila kuwa na ajira zaidi serikalini,lakini usisahau kuwa nafasi walizozipata wameendelea kuzitumia vibaya katika kuajiri.Baba atapenda kuhakikisha mtoto wake anachukua nafasi yake hata kama CV yake si nzuri kuliko yako.Mambo mengi sasa Tz yanaendeshwa kimtandaotandao.Watu wa kundi fulani watapenda watu wa kundi lao ndo wafaidike na hapo ndo ukabola unapoingia.Kama ujuavyo ajira nyingi za Tanzania zinafanyika kwa kujuana na hasa sehemu zenye ulaji na mishahara mizuri(mojawapo TRA).Katika kujuana huko tukumbuke kuwa ukabila umekuwa unaingia kwa kuwa atakaye ajiriwa ni mtoto wa Dada,kaka,mjomba au baba yake tunatoka naye kijiji kimoja.Kwa sasa kuna watu toka makabila mengine waliosoma na wenye Cv nzuri tu, lakini kama huna mtu anayekujua ni vigumu kupata kazi kwenye nyingi ya taasisi.Mfano mzuri ni BP.BP imejaa wachaga kwa kuwa kule kuna ulaji saana na walioshika nafasi nyeti ni wachaga.
 
Havijafikia katika kiwango cha kuleta machafuko LAKINI VIPO Na ni Bora tukaliona hili na kulipatia ufumbuzi yakinifu kabla havijaleta madhara makumba.Tulikemee hili Lakini tusililee kwa kujidanganya kwamba halipo!
 
UK ukiomba kazi kwenye interview kuna mahali unajaza swali hili Je unamfahamu ndugu au kiongozi yeyote wa ngazi ya juu katika Shirika au Kampuni unayoomba kazi? Kama ndiyo eleza uhusiano wenu etc.

Tatizo sio walioajiriwa wafukuzwe, tunaona viongozi tena mawaziri wakiajiri ndugu wa kabila lao au mke wakati hawana ujuzi hilo ndio tatizo. Hakuna utaratibu mzuri wa kuona ukabila hautumiki katika kupeana kazi au kuchaguliwa kwenda chuo kikuu etc. Believe me watu wengi wamepita sehemu tofauti na kama kila mtu angeweka historia yake hapa kuonyesha ukabila tungekubaliana kulifanyia kazi suala hili.
 
Tatizo lipo na naona tunajidanganya kuwa hakuna tatizo na hiii ni yale yale kama ya Udini tulijidanganya weee na tulipokuja kukubali kuw akuna tatizo tayari Cancer ilikuwa ishaenea
 
Mzee Mwanakijiji,
Ikiwa utauliza maswali haya basi kumbuka maswali haya haya yametengua hata tafsiri yako ya mwanzo kuhusu Ukabila... Na kibaya zaidi ni kwamba umeuliza hata kujuana kama moja yatafsiri za Ukabila jambo ambalo sii kweli!.. Nachosema mimi ni kwamba haya yanawezekana na ndio maana wakati Ule JK akichagua viongozi waislaam nilikaa kimya kutotetea jambo bila kumtazama mhusika jinsi anavyotoa ajira zake!..Leo hii sote kwa pamoja waliokuwa wakifikiria udini na wale waliofikiria UCCM na wengine Ushikaji tulikuja gundua kuwa JK ni mbebaji mzuri wa watu wake -MTANDAO!..ambao walikuwa toka dini tofauti, sio lazima CCM na wengine sio marafiki zake bali wamo ktk kundi fulani. Lakini ukweli umebaki kuwa he does employ people from a certain group.
Sasa basi hawa jamaa wa TRA kama wanaajiri watu toka kundi fulani inabidi tulichemkie hilo swali hadi kijulikane kinachoendelea.

Yebo Yebo,
Mfano wa JK ni ktk kueleza kwamba sisi wananchi tunakubali sana kirahisi explanation mbovu na kuzipamba. Yaani wapo watu kibao wanaotumia Japan, US,UK kama kigezo cha kusema hata huko kuna Rushwa! wakakti watu hawahawa wanafahamu kwamba RUSHWA ni adui wa haki nchi zote hata hizo walizozitaja na hakuna kiongozi hata mmoja wa nchi hizo anaweza kusimama na kuhalalisha rushwa kama tunavyofanya sisi.
na hilo la Wahindi uliotolea mfano:- umesema mwenyewe kama Watanzania watakuwa hawana uwezo wa kufanya kazi hiyo!... jibu safi kabisa na hakuna aliyesema hapa kuwa kazi za TRA haziwezwi na makabila mengine!..
Kisha jamani sote tumekaa Bongo na ajira zilitolewa serikalini na mashirika hazikuwa na picha kama hii ya leo. tena wengine sisi ajira zetu zilitoka makao makuu Dar na hata hao wanaodai kuwa kwenda Chuo kikuu lazima upitie kwa mjumbe nashindwa kuelewa huo ulikuwa wakati gani! yet siwezi kupinga kama kuna watu walipitia utaratibu huo wa kuwa mwana CCM kujiunga na chuo kikuu!..
Yebo Yebo kusema kweli mimi ningekuwa mwajiri, kuandika CV sio kabisa kigezo cha kumpa mtu kazi. CV unaweza kui - download toka ktk website kibao, wala cheti cha mtu hakiwezi kuwa kivutio kikubwa cha mimi kutoa ajira. Ila cheti ni pasi ya mtu kuingia ktk ushindani kisha huko ndani watakutana na maswali yanayohusu kazi yenyewe kwa kuzingatia nani customer wangu. Bongo mnaajiri tu watu wenye CV kubwa hali watu hawa hawafahamu kabisa mbinu za kukuza biashara, communication na costomer mbovu na wajeuri ati mnachotazama ni communication ya kule mna konunua mali! Ulaya....very strange! Ulaya ndio wanatakiwa kujifunza lugha yako kwa sababu wewe ni customer wao!....not vise verse.
No wonder wahindi wanahonga sana TRA kiasi kwamba Viongozi wanahesabu millioni zilikusanywa badala ya kuhakikisha system haitoi mwanya wa kuiba. What if tanzania ilitakiwa kukusanya billioni 3 badala ya hizi tunazojivunia kutokana na kuwepo kwa system mbove ya ukusanyaji kodi?... Tunayaona kwa barricks na wachimbaji wengine kiais kwamba ukusanyaji kodi tanzania ni adhabu kwa raia na wenye biashara ndogo. Wadanganyika wanapiga makofi na kufurahia ukusanyaji wa fedha tena basi nini - local taxes na imports from small business!...
Yebo yebo,
Nitabadilisha tone hapa kidogo,
Mwinyi alipoingia madarakani aliwaahidi Wadanganyika kuwepo kwa mitumba ni dharura hadi hapo nchi itakapo wwawezesha wananchi wake kununua nguo mpya!... do you think ipo siku hiyo itatokea!... mitumba ndio imesha tia nanga tusahau uwezo wa wananchi kununua nguo mpya! the same was for dala dala!... ndio imetoka hiyo, tunakubali kirahisi sana kushindwa vitu na kumwachia Mungu.
 
Back
Top Bottom