Ukabila Ikulu, Ujenzi, Mambo ya nje, Mipango, TRA, BoT + Ofisi nyeti za serikali



Niliwahi kwenda kuulizia kazi ktk ofisi moja mjini aeusha, nilishangaa mkuu wa ofisi akaniuliza 'wani wewe ni mhaya', nikamwambia hapana akasema basi kama sio mhaya ondoka tu ndugu yangu. Taratiiiibu nikasepa mtoto wa kiume.......... Ni ngumu kuamini lakini hii thread ina kaukweli ambako huwezi kukatetea kwa hali historia ilivyoshape mambo. Napitapita humuhumu tu wakuuu!
 
Mkuu Ndyoko hayo maneno uliambiwa kweli ama ni katika kutaka kuonyesha wahaya ni wakabila?
 
Ndyoko,
Ili uonekana mkweli zaidi, itaje kwa jina hiyo ofisi na mhusika huyo mkuu aliekuuliza
 
Aaaah jamani ukabila wapi?? sasa tutaanza kulalamika hata mtoto wa Mnyakyusa/Mhaya/Mchaga akiwa wa kwanza darasani na somo linafundishwa na mmoja wa kabila tajwa mtasema ukabila...jamani acheni hizo huo ni USONGOMBINGOO!!!!
 
Mada hii inahitaji karesearch sio nadharia za tangu miaka 70s kila kitu kinawezekana jamani!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
TUSIRUHUSU HATA MARA MOJA KUZUNGUMZIA RANGI NA UKABILA. UHURU WETU SIO WA RANGI WALA KABILA,RAIS MSTAAFU NELSON MANDELA WA S.A ALIWAH KUSEMA "NAWACHUKIA MAKABURU WEUPE NA WEUSI" SWALA LA MSING NIKUHAKIKISHA UMOJA WETU NA UHURU NA HAKI YA ELIMU INAENDA KWA KILA MTANZANIA.

NIMEKUWA KIONGOZ NAKAMWE SIKUKUBAL UKABILA MIM NIMTANZANIA NA ASIL YANGU NI UTANZANIA NA WATOTO WANGU WATAKUWA WATANZANIA. TUSIWE WAPUMBAVU KWAKUKUBAL ONGELEA UKABILA NA UDINI HAKIKA TUTACHINJANA KAMA KUKU. MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Amen
 
Big up mkjj! Maneno ya JKN yatabaki na yataishi. Because they talk the truth. We cannot invest on tribalism. Let's be aggressive on development issues. Ukweli utabaki kuwa pale pale, wahaya, wachagga, na wanyakyusa tumesoma na tunajua thamani ya elimu na walio wengi wako tayari na hakika wanajifunga mkanda kugharamia elimu kwa watoto. Na vijana hawanapiga kitabu kwa hasira. Akina samvulachole na tuipendenchi yetu wanachokiona ni matokeo ya kusoma/shule. Bila shule unategemea upewe kazi kisa uwiano? Hapani vigezo na vigezo ni shule; vidato au madigree. Lakini akina samvulachole wanatakiwa tu kutambua kuwa jamii nyingine mi sitaki kusema makabila, watu wanaamka! Akina mama wanauza magengeni, wanauza michicha, vitumbua, karanga n.k ili kupata fedha za kugharimia elimu kwa watoto wao. Hili ndilo jambo la maana kwamba aliyekuwa amelala sasa kaamka! Samvulachole, JIULIZE, ile jamii yenu kubakilivyo tatizo ni ukabila au? Sijui kwenu kule mtafanya nini, mnapinga kila kitu! Hamataki shule, hamtaki huduma ya maji ya bomba, hamtaki vyoo vya kisasa, hamtaki barabara sasa na hapo kuna ukabila?
 
Aaaah jamani ukabila wapi?? sasa tutaanza kulalamika hata mtoto wa Mnyakyusa/Mhaya/Mchaga akiwa wa kwanza darasani na somo linafundishwa na mmoja wa kabila tajwa mtasema ukabila...jamani acheni hizo huo ni USONGOMBINGOO!!!!
embombo jilipo.
 


tujaribu kujenga hoja bila lugha ya uchochezi, na isiyo harufu ya udini.
na pia kuna tatizo gani mtu kuwa na kazi ya mhudumu wa ofisi?. we hufagii kwako?. ofisi zisingekuwa zinafanyiwa usafi pangekalika?
heshimu kazi za watu.
 
Hakuna ukabila Tanzania bali kuna fursa ambazo watu wa aina fulani huzipata kutokana na juhudi za kuzitafuta na advantagewalizopata baada ya juhusi za babu zao . Leo hii ikitangazwa kazi basi hayo makabila munayotaja yatafanya asilimia sabini ya applicant na mengine mia yaliyobaki asilimia 30. Hisitoria inasema shule wapi zilianza na wapi zilikubalika na wapi walizikataa. Kwa yule anayefikiri anaeonewa aanza sasa, nenda kijijini kwenu kaelimishe watu walo baada ya miaka hamsini kutakuwa na wasomi wengi halafu mtapendeleana.
 
Mbona hazungumzii ukabila JWTZ ambalo limejaa Wakurya?Kuzumgumzia ukabila ni UKABURU
 
Mada hii inahitaji karesearch sio nadharia za tangu miaka 70s kila kitu kinawezekana jamani!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Fanya research ndogo hii hapa na kwa siku tatu tu, nenda pale nje ya Ikulu simama kwa mbali kidogo ili Camera zao zisikunase halafu angalia wanaoingia kwa kutumia mlango mdogo wa pembeni, fanya ku-tally waliovaa kibaragashia na wasiovaa kibaragashia ktk masaa ya kazi tu na baada ya siku tatu tuletee majibu,
 
Jamani nasisi wamakonde tunataka kazi nzuri zakisomi.tumechoka kuvuna korosho na kulinda mageti ya wazungu.
 
Hakuna herufi ya V,(vyombo vinaitwa fyombo,)Wahaya (hawana' ng'ombe ,ngombe) kunyima ntu mie naona aibu somo
 
<br /> <br />
Huu ni moja ya ubaguzi usiotakiwa,kudharau kazi za wengine wakati hata ulaya na marekani kuna wafagizi,wazibua vyoo na hata wazoa taka mitaani so brother acha dharau.
 
Maelezo haya yamejitosheleza vyema ,umenifilisi naunga mkono hoja yako
 

Naungana na wewe rafiki yangu. Mtizamo wa miaka ya sabini kwamba haya makabila yameshika nyadhifa na nafasi kubwa katika maeneo mbalimbali ya kiutendaji kwa sababu wamesoma zaidi ni kutufumba macho ili kuendeleza ukabila. Watu wamesoma kutoka kila kabila, na nilichokiona ni kwamba watu wanaotoka kwenye makabila ambayo wengine wanadhani hawajaenda shule, wakisoma ni wanaelimika kweli na utendaji wao wa kazi ni smart, kwa kiwango kikubwa amini usiamini hawa ndio wenye uchungu na nchi na nakwambia ndio watakaoikomboa, hawana tabia ya wizi, udanganyifu, dhuluma na wanajaribu kufanya kazi katika misingi ya uwazi na ukweli. Greedy kwao sio kubwa ukilinganisha na makabila mengine. Kitu kizuri kinachonivutia zaidi kwa hawa watu wa makabila manyonge, hata elimu zao wanazipata kwa uaminifu - namaanisha sio watu wa kuiba mitihani, kununua vyeti au kudanganya viwango vya elimu. Mara nyingi wanapotafuta kazi hutafuta kwa haki sio kwa kutoa rushwa au kujuana, wale waliopata nafasi za kusoma ni vichwa vya kuotea mbali na uwezo wanao kweli. Kwa nini nasema hivyo? Kwa sababu watu wanaotoka hayo makabila jinsi hali ilivyokuwa ni kwamba ukifeli mtihani wa darasa la saba huwezi kusomeshwa private school kwa maana wazazi wasingeweza kumudu kutokana na kwamba hawana ajira, wanategemea labda zaidi kilimo, nyenzo duni na mvua ni za kubabaisha. Kwa hiyo unaona kwamba kuendelea sekondari ilikuwa ni lazima ufaulu kwa kiwango cha juu mno ili uweze kwenda government school. Wakati mwingine nilishuhudia wenzangu wengine waliokuwa na uwezo mzuri, lakini hali ya umaskini na kukosa mahitaji muhimu ya shule na ya kimwili iliwakatisha tamaa au iliwafanya pamoja na kujitahidi kote huko washindwe kufanya vizuri katika masomo yao. Hii jamii ya makabila yanyojiita yamesoma ambayo mie nimeyaona (ingawa sio jamii nzima) ila kwa kiwango kikubwa ni haya:

1. Kwa kuwa wakoloni walijenga shule katika mikoa yao kutokana na masilahi waliyokuwa wakiyafuata, nakubali kwamba kwa namna yoyote wangetangulia kusoma, maana kwingine watu walikuwa hawajui habari ya shule. Lakini isiwe ni kigezo mpaka sasa kwamba wao ni wamesoma ndio maana wapo wengi maofisini au serikalini au mahali pengine popote. Mfano: yaani ukute TRA au ikulu au wizara nyingine kwamba watu wa kabila fulani wao ni asilimia labda 80 halafu asilimia 20 ni makabila mengine kisa wamesoma kuliko wengine na kwenye hiyo fani ni wao tu! Nakataa. Shule zipo kila sehemu, watu wanasoma. Nimeshuhudia watu toka makabila mengine wakiburuza hadi kitaifa, wakiingia top ten, wakimaliza kwa kufaulu vizuri mno hizo fani vyuo vikuu hasa UDSM, halafu huwa wanaenda wapi kama hawawezi kupata hizo nafasi?

2. Nilishudia hili mara nyingi nilipokuwa sekondari watoto toka makabila yanayojiita yamesoma zaidi (sio wote) ila kwa asilimia kubwa wakisema kauli kama hizi: mie hata nisipopiga book utanikuta ofisi kali; yaani hata nikipata zero mambo yangu yatakuwa supa, kwanza hapa nasubiria tu muda nikakabidhiwe ofisi maana baba, mjomba, mama, shangazi etc., ni bosi sehemu, wewe ukifeli utaenda kufia kijijini kwenu, nani anakujua? Au mara wewe si unasoma sana kwa sababu umetumwa na kijiji - hapa walikuwa wakimaanisha kwamba kabila lenu halijasoma, kwa hiyo ni wewe tu ndiye uliyetumwa kuja kusoma kwa niaba ya kabila/kijiji. Kwa maana nyingine ndio mtizamo ambao mpaka sasa watu wengine wanao kwamba makabila mengine hayana wasomi! Wakati mwingine ilibidi ucheke. Hizo zilikuwa kauli za kawaida kuzisikia wakati nasoma O-level na A-level, na kweli nyingi zimetimia. Kuna marafiki zangu niliosoma nao, unakuta labda hakufaulu vizuri, sasa baada ya kuachana sekondari kila mtu anaelekea anakojua, then baada ya miaka mnakutana unamwuuliza ndugu yangu uko wapi siku hizi? Anakutajia ofisi kubwa, lakini ukimwuuliza rafiki yangu hivi tangu tulipoachana sekondari ulienda wapi? Hapo atakupa maelezo yasiyojitosheleza, kwa maana hiyo, hapa katikati hutajua kama alisoma au alifanyaje, kwani hata akikueleza utaona kwamba hiyo CV yake isingeweza kumpeleka mahali alipo.

3. Jambo la tatu ni sumu mbaya mno kwao, nchi na kwa ujumla katika utendaji wao. Nimeshuhudia mimi mwenyewe misimu ya kuendea kufanya mitihani ya Taifa, O-level na A-level jinsi watoto wa ama wakubwa au toka makabila yaliyosoma wakihaha kutafuta mitihani. Mara nyingi nillisikia wanafunzi wenzangu wakisema (wale niliokuwa karibu nao zaidi) nimesikia fulani katumiwa paper ya namba, phy, chem toka Dar sijui na nani yake, wameisolve jana usiku mjini au mahali pengine popote. Au wakiwa katika mood ya kujiorganize ili kujua ni namna gani wangepata paper toka kwa mwenzao yeyote ambaye ni mtoto wa mkubwa - ujue mara nyingi katika harakati kama hizi - tajiri na tajiri na maskini na maskini, wewe huwezi kujua hizo dili zao kwanza sio rafiki yao ni mtu wa dhiki tu fulltime. Kundi hili siku zote litakuwa ni kundi la dhuluma, wizi, udanganyifu na kutojiamni katika utendaji lakini likishikilia msimamo kwamba ndio limesoma zaidi.

Sasa haya kama yalikwepo na ni ya kweli, ni hatari ndio maana unaona jinsi watu wanavyoboronga kutoka ofisi ya juu kabisa serikalini mpaka chini. Wengi ni mashahidi, mitihani ambayo huwa inavuja unategemea kwamba huo mtihani anaoweza kuutoa wizarani kirahisi ni mkulima wa jembe la mkono, au mtu aliyeko TRA, ikulu au wizara nyingine yeyote? Una jibu bila shaka. Nikipata watoto nitawaambia soma kwa akili na nguvu zako zote nikiwapa kila msaada unaotakiwa lakini nitawaambia, usithubutu kudanganya kwenye mitihani, never, never and never na unapotafuta nafasi yoyote ile hakikisha umeipata kwa vigezo sahihi!

Hiyo hali ya wizi wa mitihani na kudanganya haikuishia sekondari, iliendelea mpaka vyuo vikuu. Kwa masikio na macho nimeshuhudia UDSM jinsi watu wanavyodanganya kwenye mitihani (sio wote) - walikuwa wakiita "kudesa" na ni hali ya kawaida kabisa na wengi walikuwa wakiabudu na kuisifia! Tunaelekea wapi?

Sasa niwachekeshe hapa ingawa ni jambo la kweli: Nimemaliza UDSM 2008, kuna kundi ambalo nilikuwa napenda kudiscuss nalo, halikuwa kundi la marafiki sana lakini lilikuwa kama kundi la marafiki wa kusoma pamoja. Kuna siku moja baada ya kumaliza kudiscuss somo fulani ambalo tulikuwa tunajindaa kwa ajili ya test, hao ndugu zangu wakasema sasa tuset format ya jinsi ya kukaa ili tudesane. Nikawaambia jamani kwa nini mnakuwa na mawazo kama haya? Tuna muda wa kujisomea kwa nini tusijiandae tukaenda kufanya test kihalali? Ili hali bado tuna muda? Kumbuka niliwashauri kwa upole kabisa na kwa upendo. Ndugu yangu mmojawapo akanijibu: wewe si unajifanya kichwa? Tuone sasa kama utamaliza bila kushikwa! Kushikwa/kukamtwa hapa ni aidha kufeli somo moja au zaidi, hali ikiwa mbaya unadisco! Nilimjibu kwa ujasiri kwamba, sitadesa, na nitamaliza hapa mlimani nikifaulu tu, na kabla hujamaliza chuo usipobadili hiyo tabia nitakushuhudia ukikamatwa wewe! Hakubadili tabia, aliendelea kudesa, alikamatwa akawa anaona aibu hata kuniangalia. Baadaye alinijia na kuniomba ushauri ni jinsi gani asome ili asishikwe. Kwanza kabisa nilimwambia marufuku kudesa kuanzia leo kama unataka kufaulu. Sasa tunaheshimiana sana.

Ningeweza kuongea mengi sana kuhusu waliosoma na wasiosoma lakini naona niishie hapa kwa leo. Kuna madhara makubwa sana ya kiutendaji kwa watu waliodanganya kwenye mitihani, waliopewa nafasi ambazo hata mioyo yao inawashudia kuwa hawana sifa. Haya mambo yamewafanya aidha wasijiamini, au wafanye kazi bila taaluma, au kwa kushauriwa tu na watu na kuchukua maamuzi bila ya wao kufikiria kwa makini kwa sababu huenda huo uwezo hawana kwani hawakujijenga katika misingi ya namna hiyo.
 
Maelezo haya yamejitosheleza vyema ,umenifilisi naunga mkono hoja yako

Mzee mwanakijiji na Mwakalinga. Msimtumie Nyerere kuhalalisha uovu na dhuluma. Mambo hayo aliyoongea Nyerere miaka mingi iliyopita, na kwa huo muda alikuwa sahihi tena huenda hata kwa asilimia 100.

Ni sawa ni hayo makabila ndio yaliyokuwa yamesoma kwa hisani ya ukoloni. Lakini usiichukue hiyo hoja miaka 30 au 40 iliyopita au zaidi ukatetea hali halisi tunayoiona sasa. Unanikumbusha, kuna watu walikumbwa na kashfa za wizi, dhuluma na uovu mwingine mwingi katika serikali yetu wengine walisimama kidete na kuwatetea kwamba ni wasafi lakini baadaye waliumbuka. Tanzania sasa hivi ukiwauliza viongozi wetu kuhusu nidhamu ya uongozi watakuambia wao ndio wanafanya vizuri kuliko nchi yoyote ile duniani - yaani hakuna rushwa, wizi, dhuluma na uonevu, nchi ina amani na demokrasia ya juu kabisa, yaani hayo majibu usishangae kuyasikia!

Makabila hayo yalitangulia kusoma, sikatai, yana wasomi wengi sikatai! Sasa hili la wizara fulani au taasisi fulani kabila moja tu ni asilimia 90, makabila mengine 0.1%, 0, -1 etc kwa kigezo hichohicho cha usomi, halafu mara zote tunawaona wanavurunda, ati makabila mengine sijui yanafika 150+ yasiwe kabisa hata na mtu mmoja! Hilo kama lipo nakataa, sio kigezo cha usomi tena ila ni vigezo vingine! Yaani unataka kuniambia hawa watu wanaograduate kuanzia miaka ya 1990 wote ni kutoka makabila matatu tu? Kuna thread yangu nyingine nimeiandika from experience kuhusu hoja hii, ukiisoma unaweza kuona evolution ya uovu ambao baadaye utaitandika Tanzania.

Sijui usomi nao watu wanauchukuliaje? Maana yake hasa ni nini, kwamba ulionekana ukiingia madarasani miaka fulani? Kuna uwezekano hapo ndiko tunapohitilafiana!

Potelea mbali, kama watu wa hayo makabila ni kweli wamesoma, na wameshika nyazifa kubwa kitaifa, wafanye mambo yanayotushawishi kweli ni wasomi, maana Tanzania hali yake ni mbaya kila eneo, sasa watumie usomi kuinusuru - sijui kama hilo linawezekana.

Sitegemei msomi kufanya mambo yanayoiumiza nchi yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…