Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Aisee...Hadi mda huu zishapatikana zaidi ya Tsh 15,000,000/=.
Na wako wana fungua akaunti maalum kwa ajili ya rambirambi.
Wamesha panga kila mfiwa na walio nusurika wata patiwa Tsh 500,000/=. Hawajasema kama wata consider idadi ya waliopoteza maisha kwa familia moja.


WATU HAWATA ACHA KUCHANGIA
Chanzo TBC1
 
Mleta mada ukiwa kwenye magazeti kule utauza sana maana unajua kuipamba heading ikavutia wasomaji....By the way Mh Mbunge kaongea kauli ambayo imebalance pande zote bila kutoa shutuma kwa yeyote yule.....Poleni kwa mliokutwa na hilo janga
 
Tatizi sio ubovu wa kivuko ni uzidishaji wa mizigo na abiria wakuwajibishwa wasimamizi
 
cha msingi ni kwamba
KIVUKO CHA POMBE kimeua, alikinunua mwaka 2004 akiwa waziri wa miundo mbinu, tukumbuke pia pombe alinunua kivuko kingine kibovu cha MV DAR ES SALAAM..
pia pombe kajenga hosteli mbovu za mlimani..
roho za watanzania zinatolewa kafara na huyu mwanasiasa..
 
Mbunge wa Ukerewe Joseph Mkundi ni msaliti.

Amesema kuwa Kivuko hicho kilifanyiwa ukarabati miezi miwili iliyopita, hivyo kilikuwa sawa na kilikuwa mbioni kubadilishiwa ratiba ikiwemo kuongeza idadi ya safari ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa eneo hilo.

Aidha, amesema kuwa yeye mwenyewe ni miongoni wa watu waliopoteza ndugu katika ajali hiyo ambapo amedai kuwa takribani ndugu zake watatu wamefariki kwenye ajali hiyo.
 
Hapa tuna zungumzia "Uzembe" wa Serikali katika kusimamia Sheria ,Serikali imezembea Raia wake wame fariki for no good reson na mbaya zaidi ktk Uokozi ndio wame jivua Nguo kabisa.

Huyu Mungu tuna msingizia mengi sana mpaka yalio ndani ya Uwezo wetu.
 
So!!
Kama alisema kuhusu hayo yakatekelezwa....alitakiwa kuweka na tahadhari ya taa eeh!!!?
 
Sehemu zenye vivuko vikubwa kama pale Mwanza-Geita, Posta - kigamboni, hivi kuna rescue team zenye kukidhi idadi ya watu wanaosafiri kwenye hivi vivuko?, hapa namaanisha rescue team yenye divers wenye vifaa vyote, na speed boats madhubuti na wenye uwezo wa kufuatilia mwenendo wa hivi vyombo muda wote.. Hii ni basic lazima tufanye ili kupunguza hatari na kuondoa kabisa.
 
Sitasahau MV bukoba iliondoka na ndugu zetu zaidi ya 800.

Mv Skagit zaidi ya 140

Mv Spice zaidi ya 200

Leo hii zaidi ya 300.
 
Sio suala la abiria kujua kuwa kivuko kina beba watu wangapi, hapo kinachoangaliwa ni uwezo wake wa kubeba ni tani ngapi!! Kama kina beba jumla ya watu 100,na tani 25 za mizigo, je kama siku hiyo kimebeba mizigo tani 10,abilia wanaweza panda hata 200,hilo ni wasimamizi wake ndio wanajua. Je wakataji tiketi wanapokata hawajui idadi inayotakiwa? Na tamesa wote wanajua kuwa huwa vinazidisha abiria kwani mapato yake ya siku c wanayaona? Dsm tu daladala ni nyingi na mtu unalazimisha kujibana humo humo wakati baada ya dk tano kuna nyingine inafika!! Sembuse usafiri wa visiwani ukiikosa leo hadi baada ya siku tatu tena?? Na kama huko ukara hi mala moja kwa wiki alhamisi tu!! Na wao tamesa wanafurahia tu kwani ni trip moja kwa wiki ila mtu wake ni nyomi ya kufa mtu!! Sema limetokea hili ndio watajifanya kuwa ni bahati mbaya!!
 
cha msingi ni kwamba
KIVUKO CHA POMBE kimeua, alikinunua mwaka 2004 akiwa waziri wa miundo mbinu, tukumbuke pia pombe alinunua kivuko kingine kibovu cha MV DAR ES SALAAM..
pia pombe kajenga hostel mbovu za mlimani..
roho za watanzania zinatolewa kafara na huyu mwanasiasa..
 
Bad news! Itakuwa kanunuliwa huyo! Anatibua agenda ya chama chake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…