Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Real point
 
Jina la kivuko kilichoza huko Ukara linatukumbusha muasisi wa Taifa letu ambaye alituunganisha kuwa Taifa moja la kusaidiana katika shida na Raha bila kubaguana kwa dini zetu Wala itikadi nyingine zozote zikiwemo za kisiasa.

Juzi tumepatwa na majonzi ya kuondokewa na ndugu zetu baada ya kivuko kuzama ambapo badala ya viongozi wetu kuwa kitu kimoja tulishuhudia kila mmoja kwa nafasi yake akiandika na kuongea anachojisikia katika media mbalimbali.

Tumeshuhudia Televisheni za nje zikirusha matangazo ya janga la ajali kwa muda mrefu kuliko hata Televisheni zetu ikiwemo Televisheni ya Taifa ambayo inaendeshwa kwa Kodi za wananchi. Labda niwakumbushe wamiliki wa vyombo vya habari kuwa watu hawakutaka warushe matangazo mubashara kwa lengo la kuona picha za ajali bali tulitegemea media zipaze sauti kuwaalika wadau mbalimbali wa uokozi walete ujuzi na vifaa katika kusaidia kuokoa ndugu zetu, ninyi mliona ni vyema mpige mziki na kuendelea na vipindi vyenu kwa manufaa mnayoona yanafaa.
Tumeshuhudia wanapotutoka wasannii wakubwa na viongozi wa mbalimbali mkisitisha matangazo mengine na kuomboleza kwa muda wa masaa au siku kadhaa bila hata kupewa maelekezo kutoka popote lakini kwa Mv Nyerere amkufanya hivyo....hii ni dalili ya mgawanyiko na ubaguzi ambao mwalimu aliupiga Vita.

Kilitolewa kigezo Cha Giza kusitisha uokoaji na sijaona media au KIONGOZI wa chama Tawala na serikali aliyejitokeza adharani kukemea tamko hilo lakini tumeshuhudia ajali za viongozi na wanasiasa namna zinavyoshughulikiwa..hiki kilichotokea kinatufumbua macho kuwa sisi siyo wamoja tena kwani hata viongozi wa vyama vya upinzani walikuwa na uwezo wa kwenda kuwahamasisha wananchi wakakesha wakifanya uokozi lakini nao wamebakia kwenye media kutoa matamko na kulialia bila kuchukua hatua...ubaguzi Ni dhambi kubwa.

Viongozi wa dina nao badala ya kukemea wamekuwa wanatoa kauli Tata mitandaoni bila kutoa dira na hivyo kuonyesha Kama vile wanaogopa Jambo flani japo na amini hakuna hofu kubwa kuliko hofu ya Mungu..mkiwaogopa binadamu kuliko Mungu mtaliteketeza Taifa, zungumzeni na kusimamia haki kwa Taifa Kama dini zinavyowaelekeza na siyo kuangalia binadamu anataka nini.

Ukiona Taifa limegawanyika kwenye mambo Kama haya tambua Taifa linafungua milango kwa maadui kuingia ndani kwa kupitia mianya na mgawanyiko tulioutengeneza.

Mwisho:Tunaweza kuwa na vyama vya siasa na asasi mbalimbali kwa wingi na mahitajio tunayotaka lakini hatuwezi kuwa na Tanzania zaidi ya hii tuliyonayo Sasa.

Unaweza kuhama vyama na dini utakavyo na ukaendelea kuishi huru Tanzania lakini usitegemee kuishi huru nje ya nchi yako.

Unaweza kutumia nguvu na jitihada nyingi kujenga taasisi au chombo chochote ndani ya Taifa lisilo na mgawanyiko lakini adui anaweza kubomoa taasisi na vyombo vyote pale mnaporuhusu mgawanyiko na maslahi binafsi kuwaendesha.

Pole kwa ndugu na jamaa mliofikwa na msiba.
 
HAPO WA KULAUMIWA NI @SUMATRA..Hao polisi TRA,hayo sio mamlaka yao,,kama polisi,kitengo cha Marine wao wanasubiri order tu kutoka Sumatra.
Police wanasimamia pale ..tra inajua capacity ya kivuko mana wanakatisha ticket kwann wasiseme
 
Hebu tuambie mlikuwa wangapi ndani ya Kivuko??
 
Da, watu wapo kwenye majonz wewe unaleta mambo yako ya uchama, da kuwa na huruma basi dada, chama umekikuta na utakiacha.
 
Hivi kaokolewa ? Au kaibuka mahali au katapikwa kama yona Na samaki baada ya siku tatu?

Sasa sijui inakuaje na huyu aliyesitisha zoezi la utafutaji siku ya kwanza kisa Giza na kuhitimisha hakuna atakayekuwa hai.
 

Wao wanasafiri kwa V8, wanashida gani?

Anyway huyo aliyeokolewa akiwa hai ana mengi ya kusimulia, nadhani kama kuna hukumu ya kimahakama basi huyo atazamwe kwa jicho tofauti, kifungo alichokipata kwa saa 36 kinatosha
 
Bishoo huyo.Mtoto wa waziri sehemu kubwa ya uhai wake.It was time to sleep,mum said.Lazima aondoke kulala.
 
Habari wanaJF....!!!

Kwa huzuni na majonzi[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]makubwa kupitia tukio la kitaifa la kuwapoteza ndugu zetu na majirani zetu kwa ajali ya MV Nyerere Wilayani Ukerewe.

Tuungane pamoja kuwapa faraja na kuomboleza vifo vya wenzetu waliyopoteza uhai kupitia ajali hiyo ya majini. Mpaka Sasa miilli wapatao 157 imeopolewa.
 
#ITVupdate:Mmoja wa Mainjinia wa Kivuko cha Mv.Nyerere kilichopata ajali ya kuzama ziwa Victoria ameokolewa muda mfupi uliopita akiwa hai.
Nina uchungu na hawa nyang'au Mungu ndo anajua. Juzi Mkerewe mzima kisa tu Ukuu wa Mkoa anasitisha uokoaji eti kisa Giza.? Na vimada wa Lumumba humu JF wakaja na hoja nyepesi za kipuuzi. Niliwauliza usiku ule Nani aliyewapima wahanga mle ndani ya meli na kugundua WOTE wamekufa? Haya nyie kunguni mnaoishi kwa kujipendekeza njooni tena muunge mkono kauli za Mongela!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…