Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Binaadam na kusahau kupo
Kuna meli iliokuwa imekula nyomi la watu na mizigo kama MV BUKOBA??
Lawama zilikua kama hizi za Mv Nyerere
Ohh!!meli/fery ilikua Over Loaded!!Ohh,hamna uboreshaji mzuri wa waokoaji.
Tena kibaya zaidi Mv Bukoba waliitoboa kwa moto wa gesi ndio ikazama kilaiiiini,,na maelf ya watu walipoteza maisha
Je kuna hatua zozote zilizochukuliwa kwa waliohusika/kusababisha hio ajali??
Cha msingi tuendelee tu kuwa wastahamilivu na tuzidi kumuomba mola wetu atuepushe na majanga haya
Mkuu samahani ,ilitobolewa akiwa anakarabati? Au makusudi?
 
Injinia mkuu wa mv nyerere bwana Augustino ameokolewa leo akiwa bado hai baada ya kujifungia katika chumba maalumu kilichomo katika kivuko hicho, mbali na kuwa hai amekutwa amejipaka oil mwili mzima...chanzo Milard Ayo, intagram pamoja na video ya mhanga huyo akishushwa hospital kwa matibabu zaidi....kwa nini alijipaka oili hata mimi sijuw.
 
Maji sio mchezo kama wenyewe wanamaji waoshinda humo kila siku yanawafanya hivyo sijui mimi ambaye hata Swimming pool naliogopa inakuwajee
Ajali ya majini hata kama unajua kuogelea unaweza kufa, maana inatokea ghafla hujajiandaa hafu wengi waliokufa watakuwa ni wale waliofunikwa na kivuko
 
Zaidi ya wananchi 500 wamekwama katika eneo la Bugolora baada ya kukosa usafiri wa kuelekea kisiwa cha Ukara kulikotokea ajali ya kuzama kwa kivuko cha MV Nyerere juzi Septemba 20, 2018.

Wananchi hao wanaoelekea kisiwani humo kutambua miili ya ndugu zao, wamekosa usafiri kutokana na kuwa na idadi kubwa ya watu wanaokwenda Ukara, wakiwemo viongozi mbalimbali wa Serikali.

Wakizungumza na MCL Digital leo Jumamosi Septemba 22, 2018 wameiomba Serikali kusaka njia mbadala ili kuwasaidia waweze kufika Ukara.

Lucas Makuna mkazi wa jijini Mwanza amesema huenda asiuone mwili wa kaka yake aliyefariki dunia katika ajali hiyo kwa kuwa muda umekwenda na inawekezana zoezi la utambuzi wa miili likawa na changamoto.

“Ninakumbuka mwaka 1996 ilipozama MV Bukoba baadhi ya watu walishindwa kuitambua miili ya jamaa zao hadi Serikali ikaamua kuwazika kwa pamoja,” amesema Makuna.

“Sikutaka hili litokee Serikali iangalie namna MV Nyehunge itafika hapa maana ipo kule Ukara pamoja na MV Clarias sasa sijajua kwanini.”

Christina Mwikwabe ambaye amekwama eneo hilo amesema aliwahi alfajiri katika eneo la Bogolora ili afike Ukara mapema kuutambua mwili wa mtoto wake lakini ameshindwa kufika.

Mariam Nguzu ambaye amekwama kuvuka amesema kivuko cha MV Nyehunge hakina mafuta tangu jana usiku.

Chanzo:Mwananchi
 
Mhuuuu.... Siku zote alikua wap mbona akuonekana....?

Au hakua kazini kuogopa ukubwa wa kesi ikabidi azamie aonekane alikuepo.....?

Ya Mungu mengi.
‪VIDEO: Fundi Mkuu wa MV Nyerere Alphonce Cherehani baada ya kuokolewa, inaelezwa alijifungia kwenye chumba toka walipozama huku mwili wake wote ukiwa umejaa oil. #MillardAyoUPDATES ‬
 
Ivi hata taa za Mchina hazikuweza kupatikana kabisa kotekote ?.
Unalalaje na kupata usingizi wakati watu wanatapatapa ili kujaribu kuokoa maisha yao na kuhitaji msaada ?
Kama kweli alitoa amri hiyo kwa kinywa chake basi ni vema akaachia ngazi.
HAFAI KUWA KIONGOZI WA WATU MILELE.
 
Walimuokoa akiwa eneo gani? Yani umbali gani kutoka kwenye eneo la ajali?
‪VIDEO: Fundi Mkuu wa MV Nyerere Alphonce Cherehani baada ya kuokolewa, inaelezwa alijifungia kwenye chumba toka walipozama huku mwili wake wote ukiwa umejaa oil. #MillardAyoUPDATES ‬
 
Mkuu samahani ,ilitobolewa akiwa anakarabati? Au makusudi?

Kwa maxudi,japo walizuiliwa na mmiliki wa feri za kamanga feri,ni mzungu anaeitwa Gej,
Alilia kwa machungu huyo mzungu walivokaidi ushauri wake,wakaanza kuipasua kwa gesi.baada ya kutoboa tu,walitoka watu kama watatu tu na ikaanza kuzama kwa speed saana
Feri za huyo mzungu ndio zilikuwa zimeipiga cheni mv bukoba ili isizidi kuzama.walivotoboa tu na jamaa akatoa minyororo yake iliokuwa inaizuia isizame
Yaani fery mbili ndio zilikua zimeizuiwa,sasa akahofu kuwa na feri zitazama baada ya mv bukoba kutobolewa na kuingiza hewa na kuzidi kuzama kwa kasi
 
Back
Top Bottom