Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Nimeacha kuendelea kunsikiliza Kangi Lugola TBC, badala ya kueleza miakkati na kuongeza nguvu za uokoaji anaanza mipasho.
Kuwa kuna watu wanasema serikali haitaweza kuokoa watu etc.

Hawa jamaa akili zao sijui zipoje
 
Hadi sasa nimekaa hapa najiuliza viongozi wa huko SUMATRA wanasubiri nini kujiuzulu au wanataka kufukuzwa ? Mambo mengine ni suala la uwajibikaji tu siyo moja kwa moja uwe na makosa au la.
 
Kwani Dar maafa hayawezi kutokea.... Akili zako haziko vizuri
Ukijitoa ufahamu unaweza jibu ivyoooo... Hayo maeneo mm nimeishiii kiufupi kuishi mijini kama Dsm kuna social security kubwa ya majanga kuliko sehemu nyengine na ndiyo mana kigamboni wamejengewa daraja.... Jaribu kusoma mchango huku ukitafakari kilichoandikwa na ndiyo kazi ya ubongo
 
Just imagine capacity yake ilikuwa watu mia, ina maana kila wakati walikuwa wakiwasilisha mauzo ya 100 lkn wanabeba zaidi ya abiria 300, hii excess ilikuwa inawakilishwa kwa nani? je, mizogo excess ilikuwa inawakilishwa kwa nani? tunapofanya uchunguzi wa hili jambo turudi juma kuuliza walianza kubeba hii excess tangu muda gani na walikuwa wanaiwakilisha kwa nani? iundwe tume kuchunguza kwanza hizi pesa zilikuwa zinaenda kwa nani, na hao watu wakamatwe na wafilisiwe. Mods msiunganishe huu uzi, tuanzie hapa kwa uchunguzi ili wale samaki wakubwa wapatikane.
 
Ipo haja kwa hapa tulipofikia ikawa ni lazima kwa kila mtu ajue kuogelea ili kupunguza vifo vya majini

Hoja nyepesi kabisa hii Mkuu na usirudie tena kuisema hapa katika ulingo huu ' tukuka ' kabisa wa ' Great Thinkers ' wa JamiiForums. Siku ukipata muda nenda pale Kunduchi Beach waulizie hawa Wavuvi wawili maarufu wa enzi hizo ambao walipewa majina ya Samaki Kulwa ( Madenge ) na Samaki Dotto ( Kudura ) kutokana na Uhodari wao wa Kuogelea na Kuyakata maji utadhani walizaliwa Baharini au wana Undugu na akina Papa na Nyangumi.

Siku moja walienda Kuvua kama kawaida yao tena wakiwa na Wavuvi wenzao ambapo huko mbele Mtumbwi wao ulipatwa na dhoruba kali kidogo kutokana na eneo waliloenda ni la Mkondo wa Nungwi kama lilivyo eneo la Pwani ya Msasani jirani na Nyumba ya Nyerere na lilipo Soko la Samaki la Msasani. Cha Kushangaza baada ya kutokea hivyo dhoruba hao akina Samaki Kulwa na Samaki Dotto pamoja na Utundu na Utaalam wao wote wa Kuogolea ila Miili yao ndiyo iliyokuwa ya Kwanza Kuopolewa huku wakiwa wameshakufa na wale ambao ndiyo walikuwa kama GENTAMYCINE ' mangumbaru ' wa Kuyakata Maji ( Kuogolea ) walijitahidi kidogo hadi wenzao wa Mtumbwi mwingine kuja Kuwaokoa ila wakiwa wameshakunywa sana Vikombe na Matumbo yameumuka.

Wewe unadhani katika hao Abiria wote waliokuwemo katika MV Nyerere kulikuwa hakuna akina Samaki Kulwa na Samaki Dotto? Tena usishangae ukasikia kwamba 95% ya waliopoteza maisha ndiyo wale ' Wajuvi / Wataalam ' wa Kuogolea na hao waliookolewa ndiyo ' Mangumbaru ' wenzangu wa Kuogelea. Kujua Kuogolea hakukupi Wewe 100% ' Guarantee ' kwamba ikitokea dhoruba Majini na Chombo ama kwenda mrama au Kuzama kabisa basi utapona. Halafu tusisahau pia kwamba Siku ikipangwa imepangwa tu.
 
Back
Top Bottom