Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Swala la kujirudia linaweza kujirudia ndio maana mwanzo nimesema kuwa mwenye uwezo wa kutoa atoe ila ukikuta nafsi yako haijaridhia kutoa basi basi achana nayo usitoe

Makosa ya wahusika hayawezi kufutika kwenye fikira zetu
Mkuu njia za kutoa ziko nyingi za kuwafikia walengwa directly. Hiyo acct walipaswa kuomba radhi kwanza kuhusu yale ya tetemeko kisha wafungue mpya.
Najua wapo watakao changishwa (nguvu ya kimya kimya) kama makampuni makubwa, wenye majina makubwa, wanasiasa nk
 
Unacho sema ni kweli maana kuna wakati watu watafanya kwa kuwa mkubwa amesema
 
Hiyo ndio Serikali ya 5 ni zaidi ya uijuavyo full ubabe.
 
Kwani wameomba radhi
 
Mimi waniambie kwanza ile ya kagera ilienda wapi, nikiridhika na majibu nitatoa
 
Ccm wanafiki sana. Majukwaani wanasema serikali haitopeleka maendeleo kwenye majimbo ya wapinzani. Maafa yakitokea wanaweka kambi kuwahadaa wafiwa na kueneza propaganda kwamba hawahusiki.
 
Serikali inapenda kukamua wananchi hata kwenye jambo kama hili inataka michango rambirambi za kagera nakumbuka kilichotokea
 
Nichangie kwenye akaunti ya wafiwa wenyewe au iliyo chini ya serikali ya awamu ya 5? Utani mwingine hauna maana wanafikiri tumesahau ya Kagera?
 
Mkuu mbona ZITO aliiambia ngome yake ya Mwanza waende wakasaidie,we umewaona CCM tu?
 
Ili akawawafue wafu au?

Aende kufanya nini.

Maana gharama zilizotumika kuwapeleka viongozi waliokwisha fika huko nikubwa pengine zingesaidia kununua kivuko kingine ili wasije kufwariki kwenye mitumbwi wakati huu ambao kivuko kimelala kifudifudi.

Na watu wataogopa kukipanda kwa muda hicho kivuko KILICHOUA kitakapo zinduka.
Rais magufuli anatakiwa aende eneo la tukio soon.
 
Ccm wanafiki sana. Majukwaani wanasema serikali haitopeleka maendeleo kwenye majimbo ya wapinzani. Maafa yakitokea wanaweka kambi kuwahadaa wafiwa na kueneza propaganda kwamba hawahusiki.
Si bora hao mbowe kaweka kambi kinondoni badala ya ukara. Hii ajali ingekuwa ugweno ungeona anavyohangaika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…