Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Unaruhusiwa pia kuwatumia walengwa moja kwa moja
Acha maneno maneno kama wanawake wa vicoba
 
Kivuko kinabeba watu wangapi maiti zimefika ngapi Mungu muweza yote awaweke panapo stahili
 
haa. haa. badala ya kukusikiliza anaagizwa igp ashughulike na wenye mawazo tofauti....
 
Kile kitendo cha kusitisha uokoaji siku ile ya kwanza ILIKUWA KOSA KUBWA SANA

Nchi kukosa vifaa vya uokozi wakati wa usiku ni AIBU KUBWA

Hebu tafakali, ajali ingetokea usiku TUNGESUBIRI HADI ASUBUHI ndio uokoaji ndio uanze???
Natofautiana na wewe japo umekiri mwenyewe kwamba kulikuwa na upungufu wa vifaa.

Unaniambia vipi nizame usiku wakati hata taa hujanipa?
 
Wametutapeli vyakutoshaa Jiwe hachelewii kusema...."Kwani Nilivyokuja kuomba kura nilisema kivuko kitazama...???"
 
Mbowe ni mtu mbaya sana,watu wanalia yeye anatafuta ujiko wa kisiasa
Huyu jamaa anawapasua kichwa kwelikweli ase! Mnunueni basis kwa kutumia hike 1.5T mnayohifadhi chato.
 
Pole kwake na kwa familia za wote waliopatwa na masahibu haya.

lkn nyie mnaoandika Mungu sijui nini na nini jitafakarini sana namna mnavyomwasilisha huyo Mungu wenu ktk matukio haya.. we need to think.
 
Comrade From Sir With Love
Lawama zote LAZIMA serikali izibebe.

Kwa nini USIMAMIZI ni mbovu??

Aidha kwa nini hatuna VIFAA vya uokozi nyakati za usiku zikiwemo hizo TAA??
Swali zuri kiongozi. Lakini ziwa Victoria ni kubwa na pana.

Tatizo ninalo liona mimi ni kutokufanyiwa kazi makosa yaliyofanyika kwenye MV Bukoba.

Wenzetu wazungu, ajali ya meli au ndege inapotokea, matokeo yake sheria mpya huibuliwa ili kuzuia tatizo kama hilo.

Kwetu sisi, siasa ndiyo huchukua nafasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…