Kiongozi kumbuka tukio Kama hili lilitokea miaka nadhani 20 iliyopita, unaweza kutuambia ni hatua au tahadhari zipi zilichukuliwa kudhibiti au hata kuokoa watu kwenye janga Kama hili?!W
Ww ulitaka wafanyeje acheni malalamishi....
Carcinoma, Ndio wamesema hivyo !!??. taarifa za abiria wanaosafiri zinapaswa kubakia ofisini na sio kuenda nazo kwenye Kivuko/Meli, imekuwa hiace hiyo ya mlalahoi, hii si ni serikali kabisa ambayo mimi nilidhani inajielewa, ambayo kimsingi inapaswa kuwa na ofisi stationary, kwa hiyo na mapato yote yamezama kwenye ziwa ?.Dah hii nchi ni ngumu sana.
"Et mkata tiketi alizama kwenye maji pamoja ma mashine aliyokatia tiketi kwahio hatuwezi kujua idadi kamili iliyokuwemo kwenye kivuko"
Hapa mkuu nimekuelewa kwa herufi kubwaUwajibikaji ni enzi za Nyerere!.
Ingekuwa Nyerere yupo, hata mtu aliyeuza Nyumba za serikali kwa kuwagawia hata vimada wake, hadi kuuza nyumba za line police!, asingethubutu hata kuwaza kuchukua fomu!. Mtu amelitia taifa hasara ya kulipishwa fudia kibao kwa maamuzi tuu ya papara!.Mtu amenunua kivuko mtumba kwa mabilioni ya shilingi, halafu hakikufanya kazi!.
Kuwajibika kumekwenda na Nyerere, sasa ni zama za kupeana pole tuu!.
Poleni kwa yote!.
P.
Mkuu paschal Mayalla leo umeandika kwa mzuka wa Baba yako.Kwani hii ndio ajali ya kwanza ya uzembe hadi watu wawajibike?!. MV Bukoba aliwajibika nani?. MV Spice Island amewajibika nani?.
Kifo cha Daudi Mwangosi, amewajibika nani?!. .
Kifo cha Akwiline amewajibika nani?!
Mpaka watu wangapi wafe ndipo watu wawajibike?.
Utamaduni wa kuwajibika, umekufa na Nyerere!,
Mimi ni muhanga wa uwajibikaji, wakati wa Nyerere, baba yangu, Mzee Andrew Mayalla, ndiye alikuwa RSO wa Mwanza, kuna mahabusu wawili, Masanja Makulla Mazengenuka na Issack Mwanamkoboku, walikufa mikonani mwa polisi katika mahojiano baada ya kutuhumiwa kuhusika na mauaji ya vikogwe.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Hasssan Mwinyi alijiuzulu!,
Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mzena, alijiuzulu!,
Mkuu wa jeshi la Polisi, IGP, Pundugu alijiuzulu!.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Peter Kisumo, alijiuzulu!
RSO wa Mwanza, RPC, RSO na OCD kwanza walistaafishwa kwa manufaa ya umma, kisha wakafunguliwa mashitaka ya Kesi ya Mauaji Mwanza!.
Uwajibikaji ni enzi za Nyerere!.
Ingekuwa Nyerere yupo, hata mtu aliyeuza Nyumba za serikali kwa kuwagawia hata vimada wake, hadi kuuza nyumba za line police!, asingethubutu hata kuwaza kuchukua fomu!. Mtu amelitia taifa hasara ya kulipishwa fudia kibao kwa maamuzi tuu ya papara!.Mtu amenunua kivuko mtumba kwa mabilioni ya shilingi, halafu hakikufanya kazi!.
Kuwajibika kumekwenda na Nyerere, sasa ni zama za kupeana pole tuu!.
Poleni kwa yote!.
P.
Halihamishiki.Unahamisha goli?!!
Dhihaka gani?Achani dhihaka katika mambo ya msingi
Hilo la kukimbilia mbele ni kweli linasababisha Inbalance but lazima kuna sababu nyingine kubwa, taarifa zilizopo (japokuwa sijui kama ni za kweli) ni kwamba kulikuwa na abiria kiasi cha 400 na uwezo wa kivuko ni abiria 100, Serikali hii ambayo jeshi lake la polisi huwa linatumia Intelligensia ya hali ya juu kufanya maamuzi ya kuzuia mikutano ya wapinzani inashindwaje kuona udhaifu huu ?, hii ni serikali mzigo, wadau wanuliza hivi angekuwemo mama yake na JPM wangesitisha uokoaji jana ?Mimi pia sababu hiyo imenisikitisha sana! Lakini binafsi naamini hiyo imechangia ila si sababu kuu wasitudanganye. Chanzo kikuu aidha ni hiyo ya kuweka abiria wengi kupita uwezo wa kivuko, ama kuwe na sababu za kitaalam.
Nimekuwa nikisafiri kwa vivuko vya Nyamagana-Ukerewe mara kwa mara na mara zote huwa tunapokaribia kufika tunatoka nje na kusogea kwa mbele kwaajili ya kuwahi kushuka. Hivyo basi nina hakika hata kwenye kivuko hicho kulikuwa na utaratibu huo siku zote ila jana uzembe ulikuwepo tu.
Katika stori na hao mabaharia wa vivuko hivyo nilibaini walishaendekeza uzembe kiasi kwamba hata itokee hitilafu ya namna gani wao husema ni vigumu kuzama labda waamue wao! Kwakuwa hakuna hata ukaguzi wa maana wanaofanyiwa wamekuwa wakizidisha uzembe kila kukicha, kwa ninavyofahamu endapo isingetokea ajali jana kukiwa na watu 400+ si ajabu kesho tungesikia kivuko kimezama na watu 600+...
Kwakweli serikali haijarejesha nidhamu kazini, bali imeleta uoga uliopitiliza (nidhamu ya uoga) kwa watumishi katika baadhi tu ya kada. Kuna kada hazijawahi hata kutishiwa nyau.
Nimesoma kwa kina andiko lako Pascal Mayalla, naamini mtu yeyote aliyesoma shule na hiyo elimu ikamstaarabisha hawezi kukubaliana na hoja yako kwamba eti watu hawawajibiki kwa makosa ambayo ama ni moja kwa moja wamehusika au ni kwa migongo ya wsnawaongoza, Tumeshuhudia, akina Tibaijuka. Muhongo, Kitwanga. Nape, Nchemba, Je hao walipowajibika ilikuwa enzi ya Baba wa Taifa hili? Hasira yako hakika inatokana na ndugu yako kuwajibika ? Au inatokana na chuki yako binafsi? Binafsi nakufahamu sana pengine kuliko hata unavyojifahamu wewe. Kila Mara mandiko yako huwa ni ant system, lakini unasahau kuwa Taifa hili limekusomesha , linakupa fursa ya kujivinjari mitandaoni kwa gharama nafuu kabisa, kuwa na shukrani kwa Serikali yako. Siyo kila siku kuibeza.Kwani hii ndio ajali ya kwanza ya uzembe hadi watu wawajibike?!. MV Bukoba aliwajibika nani?. MV Spice Island amewajibika nani?.
Kifo cha Daudi Mwangosi, amewajibika nani?!. .
Kifo cha Akwiline amewajibika nani?!
Mpaka watu wangapi wafe ndipo watu wawajibike?.
Utamaduni wa kuwajibika, umekufa na Nyerere!,
Mimi ni muhanga wa uwajibikaji, wakati wa Nyerere, baba yangu, Mzee Andrew Mayalla, ndiye alikuwa RSO wa Mwanza, kuna mahabusu wawili, Masanja Makulla Mazengenuka na Issack Mwanamkoboku, walikufa mikonani mwa polisi katika mahojiano baada ya kutuhumiwa kuhusika na mauaji ya vikogwe.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Hasssan Mwinyi alijiuzulu!,
Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mzena, alijiuzulu!,
Mkuu wa jeshi la Polisi, IGP, Pundugu alijiuzulu!.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Peter Kisumo, alijiuzulu!
RSO wa Mwanza, RPC, RSO na OCD kwanza walistaafishwa kwa manufaa ya umma, kisha wakafunguliwa mashitaka ya Kesi ya Mauaji Mwanza!.
Uwajibikaji ni enzi za Nyerere!.
Ingekuwa Nyerere yupo, hata mtu aliyeuza Nyumba za serikali kwa kuwagawia hata vimada wake, hadi kuuza nyumba za line police!, asingethubutu hata kuwaza kuchukua fomu!. Mtu amelitia taifa hasara ya kulipishwa fudia kibao kwa maamuzi tuu ya papara!.Mtu amenunua kivuko mtumba kwa mabilioni ya shilingi, halafu hakikufanya kazi!.
Kuwajibika kumekwenda na Nyerere, sasa ni zama za kupeana pole tuu!.
Poleni kwa yote!.
P.
Mkuu paschal Mayalla leo umeandika kwa mzuka wa Baba yako.
Keep it up this spirit.
Sio leo, siku zote niko hivyo mimi ni mkweli daima.Mkuu paschal Mayalla leo umeandika kwa mzuka wa Baba yako.
Keep it up this spirit.