Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

John alikuwa huku juzi juzi kuhitimisha kafara hii.Mkono wa John huu sio mtu mwingine. Hii yote ni ili aweze kufuata nyayo za Paulo na Kaguta kushikiria kiti kwa miaka mingi.
 
Kuna taa zinaitwa spotlight, kwa taa moja inaweza ika cover mita 200 mwanga kwa hiyo zingepatikana taa 3 kazi ingeendelea, ninauzoefu na hivi vitu msitetee madudu, kweru mto na kweru mkungu taa kama hizo haziwezi kukosekana, Nina uhakika kila kambi ya uvuvi hiyo taa ipo
 
Inasikitisha sana mkuu! Kila mwenye akili timamu sasa na aamini kwamba Serikali inayojipambanua kuwa ni ya wanyonge haiguswi kwa namna yoyote na unyonge wao. Nadhani hata shetani hakupata usingizi wa kutosha usiku huo, ila Serikali ya Awamu ya Tano, Serikali ya Wanyonge ililala usingizi wa pono, huku ikitarajia asubuhi ikaendelee 'kuokoa' wahanga wa ajali ambao iliamua kuwaacha jana kwa sababu ya GIZA! Na ikaamini itawakuta hai! Maajabu hayataisha duniani.
Fernando Jr, Mimi sielewi ni kitu gani kiliwashinda hawa serikali kuagiza Vivuko hata vitatu ambavyo viko jirani hapo mwanza kuja kusaidia uokoaji tangu saa nane mchana Mv Nyerere ilipozama, halafu usiku sa mbili tunaambiwa zoezi la uokoaji limesimsmishwa sababu ya giza, uzuri ni kwamba pale mahali ni karibu kabisa na nci kavu )tumeambiwa si zaidi ya mita 100, Mkuu wa mkoa na timu yake wanaamua kwenda kulala ili waje kesho yake asubuhi kuendelea na uokoaji, huo hauwezi kuitwa uokoaji bali uopoaji wa miili ya marehemu, kwani nina uhakika wengi watakuwa wameendelea kufa usiku
 
Idadi ya abiria kutojulikana ndo inanisikitisha inamaana ticket hazijulikani zilikatwa ngapi na sio za EFD kweli watu bado watakua wanapiga tu.
 
Ukiiwazia sn hii ajali kwa ujumla huwezi kujijibu vzr na hata huenda usipate mtu wa kukusaidia kupata majibu yenye msaada hadi uelewe. Taarifa za awali zinasema ni kuzidisha uwezo wake wa mizigo,huenda ika-play kwa kusogea tu karibu na ukweli lkn upande wangu nakuwa sijaridhika kabisa. Kwa tuliowahi kusafiri na ile ferry na kwa muundo wake,napata shida kuamini kwamba ikiwa kweli ilikuwa overloaded na ndiyo sabb yake kuzama,basi ingeweza kuzamia katikati ya safari yake ambako kuna mawimbi makubwa sn. Nikikadiria distance iliyopo Bugorola-Ukara ni almost 50-60km na imeenda kuzama ikiwa ishayapita mawimbi makubwa ambayo yangeweza kuidhuru mapema. Ukubwa wa mashaka yangu pia ni namna gani tukio la kuzama liliweza kutokea kwa ghafla sn ferry nzima ikawa imetumbukia na kupinduka!! Mimi niendelee kuvuta subira tu nikiwa na majonzi makubwa lkn nikitazamia taarifa ya uchunguzi itakuja na majibu yaliyo sahihi zaidi na si kuimbiana huu wimbo wa ilizidisha abiria na mizigo. Imani yangu,pamoja na hiyo bado tutapata sababu nyingine itakayosapoti hii tuliyonayo.

Mv Bukoba iliwezaje kusafiri usiku kucha tokea Bukoba ikaja kupindukia Mwanza kukiwa kushakucha? tatizo ni kujitia ujuaji kwa kila kitu, jana nilieleza humu sababu pekee ya meli kupinduka ni kukosa stability, hii husababishwa na maofisa wa meli kuzidisha mzigo, kumbuka chombo cha majini kinapoundwa huwekewa mstari wa ukomo wa mzigo ili kuwawezesha watumiaji na wakaguzi kubaini uzito stahiki kabla ya kuanza safari.


Meli inapoundwa huwekewa matanki ya maji kwa chini ili yaipe stability, kutokana na tamaa maafisa wanapoona wamezidisha mzigo na ili wasishtukiwe hupunguza maji kwenye matanki ili meli ipande juu mstari uonekane ili waruhusiwe kuondoka, kitendo hiki hupoteza stability ya meli,mzigo ukizidi tu upande mmoja meli itaoverturn sababu chini ni kwepesi kuliko juu, meli inapoondoka watu huwa wametulia sehemu zao na hivyo mzigo huwa evenly distributed, meli inapokaribia kutua nanga watu hurundikana sehemu moja hivyo meli kupinduka.
 
Fernando Jr, Mimi sielewi ni kitu gani kiliwashinda hawa serikali kuagiza Vivuko hata vitatu ambavyo viko jirani hapo mwanza kuja kusaidia uokoaji tangu saa nane mchana Mv Nyerere ilipozama, halafu usiku sa mbili tunaambiwa zoezi la uokoaji limesimsmishwa sababu ya giza, uzuri ni kwamba pale mahali ni karibu kabisa na nci kavu )tumeambiwa si zaidi ya mita 100, Mkuu wa mkoa na timu yake wanaamua kwenda kulala ili waje kesho yake asubuhi kuendelea na uokoaji, huo hauwezi kuitwa uokoaji bali uopoaji wa miili ya marehemu, kwani nina uhakika wengi watakuwa wameendelea kufa usiku
Tangu jana walivyositisha uokoaji wakasema wametoa majeruhi 37 ambao walikuwa na hali mbaya, sijui na sijasikia kama ameshapatikana majeruhi mwingine
 
Kwani hii ndio ajali ya kwanza ya uzembe hadi watu wawajibike?!. MV Bukoba aliwajibika nani?. MV Spice Island amewajibika nani?.
Kifo cha Daudi Mwangosi, amewajibika nani?!. .
Kifo cha Akwiline amewajibika nani?!
Mpaka watu wangapi wafe ndipo watu wawajibike?.

Utamaduni wa kuwajibika, umekufa na Nyerere!,
Mimi ni muhanga wa uwajibikaji, wakati wa Nyerere, baba yangu, Mzee Andrew Mayalla, ndiye alikuwa RSO wa Mwanza, kuna mahabusu wawili, Masanja Makulla Mazengenuka na Issack Mwanamkoboku, walikufa mikonani mwa polisi katika mahojiano baada ya kutuhumiwa kuhusika na mauaji ya vikogwe.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Hasssan Mwinyi alijiuzulu!,
Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mzena, alijiuzulu!,
Mkuu wa jeshi la Polisi, IGP, Pundugu alijiuzulu!.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Peter Kisumo, alijiuzulu!
RSO wa Mwanza, RPC, RSO na OCD kwanza walistaafishwa kwa manufaa ya umma, kisha wakafunguliwa mashitaka ya Kesi ya Mauaji Mwanza!.

Uwajibikaji ni enzi za Nyerere!.

Ingekuwa Nyerere yupo, hata mtu aliyeuza Nyumba za serikali kwa kuwagawia hata vimada wake, hadi kuuza nyumba za line police!, asingethubutu hata kuwaza kuchukua fomu!. Mtu amelitia taifa hasara ya kulipishwa fudia kibao kwa maamuzi tuu ya papara!.Mtu amenunua kivuko mtumba kwa mabilioni ya shilingi, halafu hakikufanya kazi!.

Kuwajibika kumekwenda na Nyerere, sasa ni zama za kupeana pole tuu!.

Poleni kwa yote!.

P.
Umeteleza kidogo mkuu muhanga alikuwa baba yako sio wewe
 
Hehima kwako mkuu.

Nilikuwa naelewa ukiniona utakuja hapa safi, sana.

Sasa bila shaka unafahamu jinsi utaratibu ulivyo wa abiria kupata nafasi ya kupanda vivuko kama hivi.

Kwanza, kulikuwa na gulio hivyo watu wengi walitaka waende gulioni.

Pili, wasimamizi wakaingiwa hamasa ya kujaza abiria hivyo initial estimate ni zaidi ya abiria 300.

Tatu, wasimamizi wa kivuko ni miongoni mwa walozama na vifaa vyote muhimu vinavyohusiana na kukata tiketi na ambao mengine vimezama majini.

Hivyo "vital evidence" imepotea lakini taarifa zinakwenda Reuters na vyombo vingine vilivyopo pale vinaelewa namna ya kupata habari kwa uhakika.

Nne, kivuko ni kizima na hakikuwa na kasoro ya kukiwezesha kuzama zaidi ya kujaza abiria wengi kupita kiasi.

Kilichobakia ni kuomba wale vijana wenye simu zao ambao walikuwa ng'ambo wakirekodi tukio.

Hivyo hapo ndo tunawaachia polisi.

..my friend, it is pre-mature kusema with confidence kuwa kivuko kimezama kwa sababu moja tu -- kuzidisha abiria na mizigo.

..unaposema wasimamizi wa kivuko wamekufa, hizo taarifa zimetoka wapi? kwa uelewa wangu kuna survivors ktk ajali hii.

..kwa msingi huo walionusurika wanatakiwa kwanza watambuliwe, wapewe ushauri nasaha, na wahojiwe kuhusu safari yao na tukio zima la ajali.

.."vital evidence" kwa upande wangu ni zaidi ya majina na idadi ya watu, na kiwango cha mizigo kwenye kivuko. "Vital evidence" nyingine ni ripoti za matengenezo na ufundi za kivuko, pamoja na mawasiliano ya waendesha kivuko siku ya tukio.
 
..mimi nadhani tumlaumu Mbunge wa Ukerewe anayetokea chama cha Chadema.

..kwanza, alipiga kura kukataa bajeti ya wizara ya uchukuzi.

..Mbunge alitegemea serekali itatoa wapi fedha za kununua au kukarabati vivuko?

..Pili Mbunge anapata milion 58 kila mwaka kwa ajili ya mfuko wa maendeleo. Angetumia fedha hizo kukarabati kivuko huenda ajali hii isingetokea.

Cc tindo

Mungu hadhihakiwi!Waliosababisha kuzama kwa kivuko Watanzania wanawajua na dunia nzima inawajua!
Mbunge wa UK kutoka CHADEMA alitimiza wajibu wake kwa KUFIKISHA BUNGENI KILIO CHA WANA UKEREWE KUWA KIVUKO HICHO HAKIKUWA SALAMA KWA WAPIGA KURA WAKE!!!MLITAKA AFANYEJE ZAIDI YA HAPO?

Tatizo ni Serikali ya Magufuli na CCM yake kupuuza HOJA ZA MBUNGE KWA VILE TU NI KUTOKA UPINZANI...!!Hivi nani asiyejua kuwa Rais Magufuli AMESHATOA MAELEKEZO YA KUTOPELEKA FEDHA KWENYE MAJIMBO YA UPINZANI???Huku ni kuwabagua Watz kwa ITIKADI ZA KISIASA AMBAYO NI DHAMBI YA UBAGUZI....!!

Baba wa Taifa aliwahi kusema,""UKIANZA DHAMBI YA UBAGUZI HUWEZI KUIACHA NI SAWA NA KULA NYAMA YA MTU...NA DHAMBI HIYO ITAWATAFUNA....NA ACHA IWATAFUNE''.
 
Unataka dunia ijue kuwa kivuko kilibeba watu 500 zaidi ya uwezo wake? Lakini pia dunia itajuaje kuwa tunaweza kuopoa miili ya marehemu kwa haraka kama hatutamaliza leo! Broh usiwe siriaz sana utakufa kwa stress, fata namna nchi inavoenda, ikienda kibwege nawewe kuwa bwege, ikishtuka nawewe shtuka.
 
Hilo la kukimbilia mbele ni kweli linasababisha Inbalance but lazima kuna sababu nyingine kubwa, taarifa zilizopo (japokuwa sijui kama ni za kweli) ni kwamba kulikuwa na abiria kiasi cha 400 na uwezo wa kivuko ni abiria 100, Serikali hii ambayo jeshi lake la polisi huwa linatumia Intelligensia ya hali ya juu kufanya maamuzi ya kuzuia mikutano ya wapinzani inashindwaje kuona udhaifu huu ?, hii ni serikali mzigo, wadau wanuliza hivi angekuwemo mama yake na JPM wangesitisha uokoaji jana ?
Imbalance ya watu ambao ni uwezo wa kivuko haiwezi kipindua... DESIGNER WANAWEKAGA NA POINT LOAD AT ONE LOCATION... Otherwise Kungekuwa na matangazo ya kutojaa sehemu moja... HUWEZI DESIGN KITU HALAFU UKATEGEMEA WATU WASIJAE SEHEMU MOJA NA HUWAAMBII... and you dont have control ya wapi wakae na wenye uzito gani...

KIFUPI ILIBEBA KULIKO UWEZO WAKE NA WENGI WAKAJAA SEHEMU MOJA...
 
Back
Top Bottom