Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ugumu uko wapi? Mbona inapotokea ajali sehemu nyingine mfano ndege tunajua ilikuwa na abiria kadhaa na wahudumu kadhaa

Hili halihitaji science yoyote. Una gari lako limebeba watu 7 hivi unahitaji sayansi gani kujua wapo 7

Huu ni uzembe tu. Taarifa za awali zingeonyesha kivuko kina watu wangapi. Hili si gumu, wagumu ni sisi Watanzania na Waafrika kila kitu ni bora liende.

Utakuwaje na chombo usichojua uwezo wake na kimebeba uwezo gani?

Huwa kinabeba kuliko idadi husika
Mfano hiko kivuko kinatakiaa kubeba 100 tu ila kutokana na wingi w watu ma muda hivyo wahusika hupakia wengi kuzidi na hakuna manifest maana sio meli ni kivuko tu
Kwa meli manifest inakuwepo
 
Kuna kitu kinaitwa immidiate situation yani hali halisi wakati wa tukio la uokoaji hivyo psychologicaly inaonekana katika sample za waliowaokoa usiku wameshafariki wakaona hakuna haja ya kusumbuka na giza huku tunatoa maiti tu.
Isingewezekana wanaookolewa wawe hai alafu wasitishe uokoaji.
Inakillah wa inaillah raajun.
 
Kuna mambo yanasikitisha

Tani 25 ni sawa na kilo 25,000. Abiria 100 katika wastani wa kilo 70 kwa abiria ni sawa na kilo 7000 sawa na tani 7. Magari 3 hayajaelezwa ni aina gani hivyo hatujui uwezo wake.
Tufanye assumption kila gari lina tani 4,magari 3 ni tani 12. Ukijumlisha 12 na 7 ni tani 19.
Haiwezekani kivuko kuwa na uwezo wa tani 25 sawa na abiria 100 na mgari 3! hesabu hazikubali

Pili, abiria wanopanda lazima wawe na ticket au wawe registered. Hadi muda kivuko kinazama taarifa za idadi ya wasafiri zingekuwa zimeshapatikana. Hakuna!, tunasubiri taarifa zipikwe!

Hili halihitaji sayansi, ni kwamba, wanaopanda wanajulikana sasa kwanini idadi isijulikane?

Tatu, Watanzania na Waafrika ni watu wa ajabu sana. Hatuwezi kufikiri mambo makubwa na muhimu kwasababu akili zetu zimeelekea katika vitu visivyo na maana.

Kila siku utasikia siasa , na siasa zenyewe ni hizi za kununua. Matumizi kwa mambo yasiyomsaidia mwananchi au kuumizana wenyewe kwa wenyewe

Nguvu kubwa zimeelekezwa kukabiliana na wanasiasa badala ya kuelekeza nguvu hizo katika kuzuia madhara kama ujazo wa ziada wa abiria, kutafuta vyanzo vya ajali na kudhibiti n.k.

Kuzama kwa MV Bukoba ilikuwa funzo kubwa, leo tungeshajua nini kimetokea na kwanini

Tungechukua tahadhari kabla kuzuia matatizo kama haya.
Eti bado hatujui hata kuchukua takwimu za wasafiri licha ya funzo la MV Bukoba!! Mungu wangu

Hatutajua watu wangapi wamefariki kwasababu hatuna utaratibu , kila kitu tunafanya kwa kubahatisha tu, pandeni hata 1000 ni kazi ya mungu. Wenye dhamana fikra zote ni siasa tu

Mag3 Pascal Mayalla JokaKuu Mwalimu
WELL SAID BROTHER![emoji115][emoji106].
TAARIFA NYETI KAMA HII HAIWEZEKANI UITOE KICHWANI. HAIINGII AKILINI ETI TANI 25 SAWA NA ABIRIA 100 NA GARI 3? KWELI? [emoji45] [emoji45] [emoji45]. NA HUYU NI MTAALAMU KWELI? [emoji45] [emoji45] [emoji45]ALIE TULOGA KAFARIKI [emoji22][emoji22][emoji22][emoji22]
 
Tutegemee mkuu wa mkoa wa mwanza kutumbuliwa kesho if not kesho kutwa
 
Ni ajabu sana kutoa taarifa kuwa haijulikani watu walikuwa wangapi

Hebu acheni kucheza na maisha ya watu jamani
 
Kwahiyo tukubaliane tu kuwa yaliyotokea ni sawa sawa, na kwamba uwezo wetu wa kufikiri umefikia kikomo.
Mbona vivuko vingine dunia hutoa taarifa hizo?
Wao wanawezaje sisi hatuwezi.

Hata boti za watalii tu wala si vivuko zina utaratibu wa kujua idadi ya abiria, sisi tunaendelea kuishi kwa njia za ramli. Akili zetu ni kupambana na mambo yasiyo na maana ndiyo maana hatuwezi kujifunza kutokana na makosa kama MV Bukoba.

Hatujajiandaa kwa majanga na hatuoneshi kujiandaa
 
Hongera CHADEMA, nimewaona mko bega kwa bega na wananchi kwenye hili janga. Naona watani zenu Ccm bado wanashangilia ushindi hewa
 
Ajali imetokea mchana. It was known Giza litaingia, so sio Giza halijaja ghafla. Why not prepare??. Taa sh ngapi??. Mbona wavuvi wanavua samaki usiku??..

Yes tutembee kifua mbele, tuko kwenye right tract.
 
Ni ajabu sana kutoa taarifa kuwa haijulikani watu walikuwa wangapi

Hebu acheni kucheza na maisha ya watu jamani
Sasa unashangaa nini kutokujua idadi ya watu .......kivuko cha hapo kigamboni geti likifunguliwa kila mtu spidi ndani ....kila mtu anawahi anapokwenda .....sawa na mwendo kasi utahesabu abiria wangapi wapo kwenye gari ..... ni ajari kivuko kime overload basi
 
Siyo kila kitu ni kulaumu tu, unakumbuka wale vijana 12 na mwalimu wao waliozingirwa na maji Thailand ilichukua muda gani kuwaokoa? Na kwa hali ilivyo humo hakuna mtu aliye hai labda kwa miujiza tu.Kwenye mafunzo ya huduma ya kwanza unashauriwa kujilinda kwanza wewe mtoa mhuduma ndiyo utoe huduma kwa mhusika.
Unakuta mtu kakatwa mapanga anavuja damu wewe kwa kujiona umepitia mafunzo ya huduma ya kwanza unamvamia tu bila hata gloves, utaenda na maji.Hapo wamesitisha zoezi kwa kuhofia maafa zaidi.


Zoezi lisitishwe kwa vile hali ya ziwa imechange. It is a shame RC kuadmit kuwa ni Giza ndio linasitisha. Hata angekaa kimya ingekuwa bora zaidi.
 
Si utani ngoja nikutajie listi

1. Kingunge alitembelewa mwishowe akavuta

2. Maria na Consolata mwishowe akavuta

3. Samuele Sita mwishowe kavuta

4. Yule aliyechora nembo ya taifa mwishowe kavuta

5. Mzee Majuto naye alivuta

6. Mzee mmoja wa CCM (jina nimelisahau) naye kavuta

7. Wengine niliowasahau nao wamevuta

Yaani hawaponi kabisa!

Duh nimeaanza kumuogopa kwa kweli ata nikiumwa nikimsikia anakuja ntakimbia na dripu zangu maana maisha matamu
Duuu wewe!
 
Hawa watu wangekuwamo wao wangesitisha uokozi kwa sababu za kisenge???.
Haya mambo yanakera kweli. Hivi kweli boti zimeshindwa kupakiza generator za nguvu kukabili hali??
 
Imenikumbusha machungu ya kupoteza ndugu wawili MV Bukoba.

Imenikumbusha Naodha Lumemweru.
 
Taarifa nilizozipata haraka sasa hivi ni kuwa watu wengi sana wanahisiwa kufa maji baada ya kivuko kubinuka juu chini, chini juu katika kisiwa cha UKALA wilayani Ukerewe.


====
Taarifa Kwa Umma Kutoka Wakala wa Ufundi na Umeme-TEMESA Kuhusu Kuzama Kwa Kivuko Cha MV.Nyerere

View attachment 872340

Kivuko cha MV Nyerere kinachofanya safari zake kati ya Bugorara na kisiwa cha Ukala katika ziwa Victoria kimezama huku taarifa za idadi ya watu waliokuwemo ndani ya kivuko hazijajulikana.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jonathan Shana amesema kivuko hicho kimezama wakati kikielekea katika Kisiwa cha Ukara. Kiliondoka saa 6 mchana na ilipofika saa nane kamili mchana kilipinduka.

Amesema bado hawajapata idadi kamili ya waliokuwemo kwenye kivuko hicho.

Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), Hassan Karonda amekiri kuzama kwa kivuko hicho na yuko njiani kulekea huko na watatoa taarifa baadaye.

Kivuko cha MV. NYERERE kilinunuliwa na kuanza kutoa huduma mwaka 2004. Kilifungwa injini mbili mpya zenye thamani ya shilingi milioni 191 JULY 2018. Kivuko cha MV. Nyerere kina uwezo wa kubeba tani 25 sawa na abiria 100 na magari 3 kwa wakati mmoja.


View attachment 872299
View attachment 872676
Wanajeshi na raia wakitoa msaada wa uokoaji​

UPDATES: 1900HRS

=> Watu watano wamekufa na wengine 32 wameokolewa mpaka sasa ila hali zao ni mbaya kufuatia ajali ya kivuko cha MV Nyerere.

=> "Mtu Hajalipwa Mshahara Halafu Anasikia Trilion 1 Imepotea Inauma" -Joseph Mkundi

Mbunge Joseph Mkundi akitahadharisha kuhusu kivuko cha MV Nyerere Apr 24, 2018

Alikuwa akichangia hoja ya bajeti ya Wizara ya Uchukuzi na Mawasiliano iliyopo chini ya Waziri wake, Profesa Makame Mbarawa.

UPDATES:
AJALI YA KIVUKO CHA MV NYERERE: WATU 44 WAMEFARIKI, ZOEZI LA UOKOAJI LASITISHWA HADI KESHO

Mbali na idadi hiyo ya waliofariki, Watu 37 wameokolewa katika ajali huku hali zao zikiwa mbaya

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongella amesema zoezi la uokoaji limesitishwa kutokana na giza kuingia
rIp
 
Dah....una fire extinguisher nyumbani?[emoji41]

hahahahaha hapo umefeli bro jikoni ziko 3, coridoni ziko 3 na sitting ziko 2, vyumba vinne kila kimoja iko moja kilo 9, na za jikoni ziko kg 9.. Nyumba nzima wanajua kutumia mpaka house girl anajua moto ukitokea nini cha kufanya...kazi kwako mkuu..

Sasa sijui ajali iliyotokea na hili la nyumbani kwangu vinauhusiano gani, usijaribu kujustify ujinga wako kwa ujinga wa mwingine tuwe serious kwa masuala nyeti kama haya..
 
Back
Top Bottom