Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Kwani hii ndio ajali ya kwanza ya uzembe hadi watu wawajibike?!. MV Bukoba aliwajibika nani?. MV Spice Island amewajibika nani?.
Kifo cha Daudi Mwangosi, amewajibika nani?!. .
Kifo cha Akwiline amewajibika nani?!
Mpaka watu wangapi wafe ndipo watu wawajibike?.

Utamaduni wa kuwajibika, umekufa na Nyerere!,
Mimi ni muhanga wa uwajibikaji, wakati wa Nyerere, baba yangu, Mzee Andrew Mayalla, ndiye alikuwa RSO wa Mwanza, kuna mahabusu wawili, Masanja Makulla Mazengenuka na Issack Mwanamkoboku, walikufa mikonani mwa polisi katika mahojiano baada ya kutuhumiwa kuhusika na mauaji ya vikogwe.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Ali Hasssan Mwinyi alijiuzulu!,
Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Mzena, alijiuzulu!,
Mkuu wa jeshi la Polisi, IGP, Pundugu alijiuzulu!.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza Peter Kisumo, alijiuzulu!
RSO wa Mwanza, RPC, RSO na OCD kwanza walistaafishwa kwa manufaa ya umma, kisha wakafunguliwa mashitaka ya Kesi ya Mauaji Mwanza!.

Uwajibikaji ni enzi za Nyerere!.

Ingekuwa Nyerere yupo, hata mtu aliyeuza Nyumba za serikali kwa kuwagawia hata vimada wake, hadi kuuza nyumba za line police!, asingethubutu hata kuwaza kuchukua fomu!. Mtu amelitia taifa hasara ya kulipishwa fudia kibao kwa maamuzi tuu ya papara!.Mtu amenunua kivuko mtumba kwa mabilioni ya shilingi, halafu hakikufanya kazi!.

Kuwajibika kumekwenda na Nyerere, sasa ni zama za kupeana pole tuu!.

Poleni kwa yote!.

P.


NASEMA HIVI MIMI nakuelewa sana, wewe watu wakienda kushoto kawaida unapiga kulia na sio bahati mbaya ni makusudi( ila ujumbe ni ule ule wa Kushoto.
#HAPAKAZITU
 
Yuko live.
Anasema taarifa aliyopewa ni kuwa hiyo meli inaweza beba watu 100 na tani 25. Ila ilizidisha watu.
Pia ilipakia mahindi magunia mengi na makreti ya bia na soda na vifaa vya umeme pamoja na gari/ magari.
Ilikiwa ni siku ya soko alhamis hivyo na abiria walikuwa wamebeba mizigo, hivyo ni wazi ilizidisha watu.
Pia inasemekana aliyekuwa anaendesha yawezekana sio kapteni mwenuewe, hivyo ameagiza wote wakamatwe. Pamoja na kapteni na watendaji wa kivuko wakamatwe na shughuli za upelelezi ziendelee.
Pia amemuagiza waziri mkuu kuunda tume ya uchunguzi juu ya hii ajali.
Ataka wanasiasa wasichukulie hii kitu kisiasa.
Ilibeba watu 100 wamekufa 130+????????????how
 
Maswali mengine tuwe tunajiuliza kabla ya kuuliza watu... Mbowe akiwepo huko itasaidia nini
 
Nature ya ajali ni ngumu maboya kutumika, unajua ilikuwa upside down ndani ya dakika chache, so ni tofauti na ile inazama huku iko kawaida kiasi hata muda wa kitafuta maboya ungepatikana.

Pia maboya yatakuwa 100, abiria 400+
Dah huu usafiri wa majini ni mbaya sana kama mazingira hayajawa tayari kwa uokoaji likitokea la kutokea.
 
Nilitegemea kwa wakati huu KUB Mbowe angekuwa kisiwani Ukerewe kujumuika na mbunge wa jumbo hill ambaye ni wa Chadema pamoja na timu nzima ya viongozi wa serikali na vyombo vya dola. Kwanini Mbowe kamuacha mbunge wake akiwa mpweke katika wakati huu mgumu!
Mkuu ukipata majibu unitaq na mimi
 
Cha ajabu sasa vitu ambavyo ni basic kabisa hatuwezi kufanya, kuwa hata na counterbook litakalo record details za abiria nalo limeshindikana kabisa..


Simply "Basic"
Halafu tumekuwa na past experience ya hii kitu. Tumewahi pata haya majanga.
Na sababu kama hii..

"Boti ilikuwa na zaidi ya watu 400"

3 times the number it's capable of..
 
Hoja ya kup.umbavu kabisa.

Jambo la muhimu ilikuwa kuzuia maafa.

Mbunge wa Ukerewa amelalamika sana Bungeni. Alieleza jinsi alivyohangaika na alivyoonana na viongozi mbalimbali wa serikali kuelezea hali ya hatari iliyokuwa ikiwanyemelea watumiaji wa kivuko cha Nyerere lakini serikali haikuwahi kufanya chochote.

Leo wakati watu wamekwishakufa ndiyo wanajikusanya kwenda kisiwa cha Ukara. Unafiki mkubwa! Msaidie mtu kulinda uhai wake na siyo kubeba jeneza lake
Umeshapanic!!.......Ukerewe ni jumbo linaloongozwa na mbunge wa Chadema mbona hamumpi ushirikiano. Mbona wakati Sugu anatoka jela KUB alikuwepo!
 
Mabavicha yanang'aka likitajwa jina la Mbowe, halafu yanakuwa makali hayo balaa.
Huyo mwenyekiti wenu mnamficha wa nini? Au mnaona haya vile hajafika huko pamoja na kabineti yake ndio mnatafuta pa kujificha? Oneni aibu hivyohivyo na msijifiche nyuma ya mbowe kufikisha ujumbe wenu. Pelekeni kama ulivyo na uliza kulikoni hatukuoni huku? Wajinga na waoga kuliko mbwakoko lumumba st!
 
Mpaka saiz.magufuli na serikali yake wameshindwa na aibu ya ajali hii ikae juu yao milele.Hii hata magufuli sijaona kama amefanya lolote.kwa sababu jimbo ni la upinzani jiwe hawezi kufanya chochote.siku akienda ziarani utasikia anawaambia wanaukerewe kuwa kivuko kilibinuka kwa kuwa Mbunge ni wa Chadema.Aibu ya serikali,aibu magufuli kwa siasa za majitaka.[/QUOTE
Siku hizi wana lugha rahisi kweli katika kuwa mbele kwa kila jambo "Serikali itaubeba msiba na itagharamia kila kitu." Tanzania! Tanzania! Nakupenda kwa moyo wote
 
Back
Top Bottom