nuruyamnyonge
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 4,408
- 2,196
Ni majonzi makubwa mno, pale ninapowaona ndugu zangu wamelala wamenyamaza kimya! Walitoka Ukara kwenda hutafuta mkate wao wa kila siku na mahitaji ya watoto wa shule, safari ya kurudi ukara ikafika wakawapungia mkono ndugu zangu wa Bugorola wakiwa na matumaini na nyuso za furaha mahitaji yao yamekidhi matamanio ya mioyo yao.
Mita chache kivuko kikaanza kuonekana maeneo ya ukara hichooooo kinakaribia, watoto wakaanza kusogea karibu kuwapokea wazazi ndugu jamaa na marafiki zao, kumbe walikuwa wanakwenda kushuhudia kivuko kikiwaangamiza na kuwazamisha kabisa "wakara" dah! Nimlilie nani siku ya leo? Tangulieni mbele ya haki ndugu zangu, Mungu awape pumziko la milele msitarehe kwa amani katika nyumba yenu ya milele Amen!
Mita chache kivuko kikaanza kuonekana maeneo ya ukara hichooooo kinakaribia, watoto wakaanza kusogea karibu kuwapokea wazazi ndugu jamaa na marafiki zao, kumbe walikuwa wanakwenda kushuhudia kivuko kikiwaangamiza na kuwazamisha kabisa "wakara" dah! Nimlilie nani siku ya leo? Tangulieni mbele ya haki ndugu zangu, Mungu awape pumziko la milele msitarehe kwa amani katika nyumba yenu ya milele Amen!