Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Kwani upinzani wamekatazwa kufika huko?
Siku hivi humu JF wengi mmekuwa majanga
 
Ivi nchi hii tumerogwa?

Inakuwaje serikali inashindwaje kuhudumia watu 200 waliofikwa na maafa mpka wachangishe watu? Tena kwa vitisho.

Nashangaa waziri wa ulinzi anadai serikali haihusiki na kuzama kwa meli ila kumbuka kuwa kivuko ni cha serikali tena kwa kusema atakaye sema serikali inahisika atakamatwa.

Ivi hela za uchaguzi zinatoka wapi ila za maafa hazipo?
Maiti moja ubani laki 5 , huku bei ya Waitara ikifika hadi mil 800 ! hii ni aibu kubwa sana !
 
Mimi nashindwa kuwaelewa. Yani vyama pinzani. Kimaendeleo vimekua adui mkubwa sana serikalini utadhani wapinzani sio watanzania. Inashangaza sana .
 
Aaaaah rafiki kwanini ulihama

Mi nipo kimachale machale tu

Miss you sana mzalendo mwenzangu[emoji23] [emoji23] [emoji23]
nina bahat mbaya mzalendo hata wale wacheza sebene walioshndkana hawanitak, nikahamia kwa wajane nikijua nitapata pumziko, wajane nao wananiambia wana watu wao.


Mungu ibariki Tanzania
 
nina bahat mbaya mzalendo hata wale wacheza sebene walioshndkana hawanitak, nikahamia kwa wajane nikijua nitapata pumziko, wajane nao wananiambia wana watu wao.


Mungu ibariki Tanzania
Ndo kusema sipati wifi loh

Una gundu mzalendo nenda kaogee maji ya bahari tu
 
Nimeandika nimefuta nimeandika nimefuta ila tusaidiane hapa ccm ukara wanafanya nini? Wameweka kambi na jezi yao ya kijani ila marufuku kwa wengine kusema juu ya msiba au kufanya lolote ni uchochezi kwa mujibu wa waziri wa mambo ya ndani.

Na marufuku kisema serikalo inahusika na kizama kwa kivuko maana serikali haihusiki na haikuwapakia hao melarehemu
Ukiamini ccm hata maiti zitakushangaa !! wamevaa hadi misale yao ile waliyomdhulumu Shigongo utadhani wako kwenye ukumbi wa Rushwa wa Chimwaga .
 
Acheni mambo ya kijinga, serikali imetangaza inagharamia mazishi. Hizi habari mmezitoa wapi nyie. Pia katika hali ya kawaida kutoa rambirambi ni kawaida hata kama ni msiba wa tajiri
 
Unaposema serikali haina lawama ya moja kwa moja huku ukidokeza ajira za kubebana sikuelewi hapo. Ni Nani aliyewaajiri hao mafundi wa kubebwa? Nadhani ni mmiliki wa meli, Nani mmiliki wa meli serikali, Then serikali haipaswi lawama. Wamiliki wa mabasi yanapopata ajali za kizembe kama hii wanashtakiwa pamoja na watumishi wao hasa pale watumishi wao wanapokuwa hawana baadhi ya sifa, lakini kwa serikali haipaswi kulaumiwa kwa mujibu wa maoni yako!! Serikali inapokea mapato ya abiria 250 kila siku kwa kivuko chenye uwezo wa kubeba abiria 100, inachekelea vinono vinavyoingia bila kujua vinatoka wapi? Yaani baba mwenye nyumba unamwachia mkeo hela ya dagaa mchana ukirudi unakuta mama kapika nyama ya kuku unakula kwa raha zote huku ukisifia ubunifu wa mkeo, kesho akifumaniwa na mume wa mtu hustahili lawama!!
Nina majonzi acha nikae kimya!
Pole sana ndugu yangu, hii janga linatia simanzi sana, nimekuw nikifuatilia kwa karibu sana. Unajua ukiinyooshea kidole serikali inakuwa vigumu kubaini tatizo! Hapa kuna watu waliopewa majukumu ya kuendesha mv nyerere ndio hawakutimiza majukumu yao na sasa yametukuta! Tukipoteza ' focus' tuanze mara serikali mara rais hatutafika kokote! Uzembe wa aina hii umekuwa ukitugharimu kila mara! Mtu leo unaomba kazi kesho hutaki kufanya kazi kwa umahiri! Hayo mapato ya watu na mizigo iliyozidi sidhani kama hata ilikuwa ikiingia serikalini zaidi ya kwenye mikono na mifuko ya mafidhuri wachache! Ikifanyika auditing ya kina huu ukweli unaweza bainika. Kila kichwa na mzigo extra ni chakula ya wahuni wachache!
Mtu anaomba na kupata tenda ya kujenga daraja anapunguza viwango na maafa yanatokea…hi ndio hali halisi..na hapa ndipo sitaacha kumtia moyo rais wetu mpendwa kwa kukemea na kushughurika na mambo kama haya ili yapungue kama sio kuisha kwa usalama wetu wote! Huwa napata shida sana watz wenzangu mnapoanza kumponda Magu!
 
Back
Top Bottom