Unaposema serikali haina lawama ya moja kwa moja huku ukidokeza ajira za kubebana sikuelewi hapo. Ni Nani aliyewaajiri hao mafundi wa kubebwa? Nadhani ni mmiliki wa meli, Nani mmiliki wa meli serikali, Then serikali haipaswi lawama. Wamiliki wa mabasi yanapopata ajali za kizembe kama hii wanashtakiwa pamoja na watumishi wao hasa pale watumishi wao wanapokuwa hawana baadhi ya sifa, lakini kwa serikali haipaswi kulaumiwa kwa mujibu wa maoni yako!! Serikali inapokea mapato ya abiria 250 kila siku kwa kivuko chenye uwezo wa kubeba abiria 100, inachekelea vinono vinavyoingia bila kujua vinatoka wapi? Yaani baba mwenye nyumba unamwachia mkeo hela ya dagaa mchana ukirudi unakuta mama kapika nyama ya kuku unakula kwa raha zote huku ukisifia ubunifu wa mkeo, kesho akifumaniwa na mume wa mtu hustahili lawama!!
Nina majonzi acha nikae kimya!