Ukatili wa viboko umekithiri Sekondari ya Salma Kikwete

Ukatili wa viboko umekithiri Sekondari ya Salma Kikwete

HORSE POWER

JF-Expert Member
Joined
Feb 22, 2015
Posts
2,238
Reaction score
1,577
Habari wana JF.
Kwanza kabisa niharakishe kutamka hapa kwamba sipingi viboko mashuleni.Viboko 'huamsha' wazembe,halikadhalika husaidia kurekebisha nidhamu'kwa kiasi fulani'. Lakini adhabu ya viboko ina namna yake na idadi yake.Lengo la viboko ni kunyoosha na sio kukomoa.
Tatizo tulilo nalo leo ni lundo la walimu makatili mashuleni wanaonyuka fimbo watoto mashuleni utadhani wanaua nyoka.Udhalimu upo shule nyingi nchini ila 'wakubwa' wetu kama kawaida wapo kimya.
Moja ya shule inayolalamikiwa sana ni Shule ya Sekondari Salma Kikwete iliyopo Dar.Kuna binti wa rafiki yangu wa karibu ametandikwa viboko zaidi ya kumi mpaka amevimba makalio kisa hakwenda na hela ya mtihani.Malamiko ni mengi kuhusu shule hiyo na ukatili wao na hakuna hatua zinazochukuliwa.
Nataka niwakumbushe wakubwa wetu wanaozembea kwenye mambo ya hatari kama haya;ipo siku wazazi wataamua kwenda kuwashughulikia wenyewe hao makatili pale shuleni.Sasa hatutaki watu wafikie huko.DC,Mkurugenzi,Afisa Elimu,Bodi ya Shule,Mwenyekiti wa S/Mtaa na Mtendaji wake,Diwani,Mbunge na wengine;je ni kweli hamjui au hamjali?
 
kazi kweli kweli/jobtruetrue



#ponda mali kufa kwaja
 
Kwanza mtoto wa kike anachapwaje viboko vya makalio? Hilo ni kosa na udhalilishaji.

Kama wewe ni mzazi ama mdau wa elimu nenda kamweleze mkuu wa shule juu ya ukatili huo naamini ataongea na walimu wake na kuwaonya.

Ukiona hali inaendelea basi nenda kwa afisa elimu kata/mratibu elimu kata ili baadae wazazi wakiamua kwenda mahakamani basi uthibitisho utakuwa upo kwamba mlianzia ngazi ya chini pasipo msaada.

Huo ni ukatili dhidi ya watoto na ni kinyume cha sheria ya mtoto ya mwaka 2009, sheria ya elimu pamoja na muongozo wa utoaji adhabu mashuleni ya mwaka 2002.

Usipuuze ushauri huu naamini utakuwa umesaidia kudhibiti ukatili dhidi ya watoto.

Mimi huwa natembelea mashuleni kutoa elimu hii kwa walimu na mafanikio yanaonekana.
 
Mhamishe akasome Mugabe sekondari...mwenye shule ni marehemu so hakuna wa kumchapa tena!
Hivi wewe una mtoto ama hata mdogo wako anayesoma kweli?

Au umezaliwa peke yako kwenu hivyo huna huruma na ukatili dhidi ya watoto wasioweza kujitetea?

Matukio ya vifo na ulemavu wa kudumu yamekuwa yakiripotiwa ambapo hutokea mashuleni na walimu wamekuwa wakipelekwa mahakamani badala uwe mstari wa mbele kupinga ukatili wewe unajibu kama umekatwa kichwa.

Afrika maendeleo ni duni kwasababu aina ya watu kama nyinyi mpo wengi kuliko werevu.
 
Leo madogo home wameamkia viboko, yan ile ghafla tu tumemaliza ibada ya alfajir saa 11, nikaliamsha.

Watoto saa zingine bila viboko ni ngumu sana kuelewa. Hasa sisi waafrika.
Mwanangu wa form 1 alikua anafel hesabu toka aanze kidato cha kwamza january, nikachukua jukum la kumfumdisha mimi home , na kiboko pembeni, sasa hiv anapiga hesabu balaa.. ni uzembe uzembe tu

Ila kama usemavyo viboko navyo visizid sana.
 
Kama mtoto ninjeuri acha akunguntwe mboko akili zimkae sawa

Usikute kakamisi kamshikaji kake kitaa anafanya ujeuri ili arudishwe home akaulilie
 
Leo madogo home wameamkia viboko, yan ile ghafla tu tumemaliza ibada ya alfajir saa 11, nikaliamsha.

Watoto saa zingine bila viboko ni ngumu sana kuelewa. Hasa sisi waafrika.
Mwanangu wa form 1 alikua anafel hesabu toka aanze kidato cha kwamza january, nikachukua jukum la kumfumdisha mimi home , na kiboko pembeni, sasa hiv anapiga hesabu balaa.. ni uzembe uzembe tu

Ila kama usemavyo viboko navyo visizid sana.
Una malezi ya hovyo na ya kikatili sana.

Yaani ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini viboko ndiyo suluhisho la matatizo?

Wanangu sijawahi hata kumtishia kiboko achilia mbali kumchapa lakini sauti yangu tu ya upole na yenye mamlaka wakiisikia wanafanya jambo kwa usahihi na performance inaonekana.

Kuna watoto wa majirani wanachezea vipigo kutoka kwa wazazi wao lakini ndiyo wamezidi kuwa watukutu.

Wakoloni walitumia mbinu ya kuwatandika viboko watu weusi kama kuwadhalilisha halafu huko kwao wala hawawachapi watoto wao badala yake Waafrika wenye uelewa finyu wakaendeleza ukatili ulioachwa na Wakoloni. Shame on you.
 
Una malezi ya hovyo na ya kikatili sana.

Yaani ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini viboko ndiyo suluhisho la matatizo?

Wanangu sijawahi hata kumtishia kiboko achilia mbali kumchapa lakini sauti yangu tu ya upole na yenye mamlaka wakiisikia wanafanya jambo kwa usahihi na performance inaonekana.

Kuna watoto wa majirani wanachezea vipigo kutoka kwa wazazi wao lakini ndiyo wamezidi kuwa watukutu.

Wakoloni walitumia mbinu ya kuwatandika viboko watu weusi kama kuwadhalilisha halafu huko kwao wala hawawachapi watoto wao badala yake Waafrika wenye uelewa finyu wakaendeleza ukatili ulioachwa na Wakoloni. Shame on you.
Vizur sana.. sasa hao ni watoto wako chief na hongera sana kwa hilo. Usi force uniformity maana kuna factors nyiingi sanaaa kuhusu hili . Watoto wengine ni trouble some by blood. Na tunawazaa kabusa ukiwaangakia unaona huyu hiz tabia ni zangu kabisaaaa na hatabuongee vipi hii haitoki.

Mwisho kabisaa, utaonekana huna akili unapokua una judge watu straight just bcz hawafanyi unachifanya wewe, try to be brave in understanding sawa mdogo angu????
Hawa ni wanangu nimewazaa na nina uchungu nao, siwez kuua watoto niliowazaa na ninaowahangaikia, hibyo kuniita mkatili naona umenikosea sanaaaaa kias cha kufananisha malez yangu na ukoloni wa waarabu.

Nitake radhi tafadhali
 
Kuna wakuu wa shule hawayajui haya kwa sababu hamlalamiki
Nenda kwa mkuu wa shule na ukalalamike kwa mtoto kupigwa viboko 10 ni haki?
Nina uhakika lazima mwalimu atashughulikiwa
Kuna Wakurugenzi pia hawana habari wao wanafurahia matokeo mazuri tu lakini kusema la haki Kuna watoto hata wakipata 80% wanapigwa haswa

Wale wa kuandamana kwanini wasiandamane na kusema viboko basi?
Wanasiasa wanapiga kelele kwenye maslahi yao tu ikiguswa au kutafuta wapi pa kuiba ila masuala kama haya hayawahusu na ni lazima likemewe
Haki za binadamu my foot hao nao kama NGO tu
 
Kuna wakuu wa shule hawayajui haya kwa sababu hamlalamiki
Nenda kwa mkuu wa shule na ukalalamike kwa mtoto kupigwa viboko 10 ni haki?
Nina uhakika lazima mwalimu atashughulikiwa
Kuna Wakurugenzi pia hawana habari wao wanafurahia matokeo mazuri tu lakini kusema la haki Kuna watoto hata wakipata 80% wanapigwa haswa

Wale wa kuandamana kwanini wasiandamane na kusema viboko basi?
Wanasiasa wanapiga kelele kwenye maslahi yao tu ikiguswa au kutafuta wapi pa kuiba ila masuala kama haya hayawahusu na ni lazima likemewe
Haki za binadamu my foot hao nao kama NGO tu
Ni kweli ni muhim kuzingatia sheria. Na haya mambo yapo sana shule za serikali. Japo huko ndio kumejaa watoto wengi watukutu.
INgawa nasukumwa kuamini kabisaa hakuna mwalim anapenda kuchapa chapa watoto, hasa hawa waalim wa miaka ya leo, wala hawana time ya kukimbizana na viboko maana huo muda wanaona bora wachape shida za maisha yao zinazowasumbua.

NB
Fimbo muhimu
 
Kama mtoto ninjeuri acha akunguntwe mboko akili zimkae sawa

Usikute kakamisi kamshikaji kake kitaa anafanya ujeuri ili arudishwe home akaulilie
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tatizo walimu maisha magumu sana ndiyo maana hupoza machungu ya shida zao Kwa kuwachapa viboko wanafunzi
 
Una malezi ya hovyo na ya kikatili sana.

Yaani ulimwengu wa leo bado kuna watu wanaamini viboko ndiyo suluhisho la matatizo?

Wanangu sijawahi hata kumtishia kiboko achilia mbali kumchapa lakini sauti yangu tu ya upole na yenye mamlaka wakiisikia wanafanya jambo kwa usahihi na performance inaonekana.

Kuna watoto wa majirani wanachezea vipigo kutoka kwa wazazi wao lakini ndiyo wamezidi kuwa watukutu.

Wakoloni walitumia mbinu ya kuwatandika viboko watu weusi kama kuwadhalilisha halafu huko kwao wala hawawachapi watoto wao badala yake Waafrika wenye uelewa finyu wakaendeleza ukatili ulioachwa na Wakoloni. Shame on you.
Well said mkuu, hizi fikra za kikatili za kushushia watoto viboko kama mbinu ya kuwafanya wa-act kwa usahihi ni za kulaani kwa nguvu zote.
 
Hivi wewe una mtoto ama hata mdogo wako anayesoma kweli?

Au umezaliwa peke yako kwenu hivyo huna huruma na ukatili dhidi ya watoto wasioweza kujitetea?

Matukio ya vifo na ulemavu wa kudumu yamekuwa yakiripotiwa ambapo hutokea mashuleni na walimu wamekuwa wakipelekwa mahakamani badala uwe mstari wa mbele kupinga ukatili wewe unajibu kama umekatwa kichwa.

Afrika maendeleo ni duni kwasababu aina ya watu kama nyinyi mpo wengi kuliko werevu.
Una uhakika mimi ndiye mkuu wa hiyo shule?
 
Ni kweli ni muhim kuzingatia sheria. Na haya mambo yapo sana shule za serikali. Japo huko ndio kumejaa watoto wengi watukutu.
INgawa nasukumwa kuamini kabisaa hakuna mwalim anapenda kuchapa chapa watoto, hasa hawa waalim wa miaka ya leo, wala hawana time ya kukimbizana na viboko maana huo muda wanaona bora wachape shida za maisha yao zinazowasumbua.

NB
Fimbo muhimu
Sasa mnapopiga huwa mnatarajia nini kwa mtoto?
Kuna wengine wana autistic na wengi hawajui kwanini mtoto ni mtukutu kumbe mgonjwa
Wazungu hawapigi ndio wanatengeneza kila kitu

Nyie mnapiga na mtoto anaogopa hata kukuuliza kitu maana umeishamjengea hofu
 
Sasa mnapopiga huwa mnatarajia nini kwa mtoto?
Kuna wengine wana autistic na wengi hawajui kwanini mtoto ni mtukutu kumbe mgonjwa
Wazungu hawapigi ndio wanatengeneza kila kitu

Nyie mnapiga na mtoto anaogopa hata kukuuliza kitu maana umeishamjengea hofu
Haya ni ninyi mnayakuza mzee wangu baada ya kukaa sana ulaya na kuzielewa culture zao. Ila hayana ukwel hata kidogo
 
Haya ni ninyi mnayakuza mzee wangu baada ya kukaa sana ulaya na kuzielewa culture zao. Ila hayana ukwel hata kidogo
Siyakuzi hata kidogo
Huku hata mbwa hapigwi kuna watu wamesomea behavior zao na ni taaluma

Ukiruhusu kupiga fimbo tatu wao wanapiga 10
Ni kama kuwaambia watu ibeni kiasi
 
Siyakuzi hata kidogo
Huku hata mbwa hapigwi kuna watu wamesomea behavior zao na ni taaluma

Ukiruhusu kupiga fimbo tatu wao wanapiga 10
Ni kama kuwaambia watu ibeni kiasi
You understand cultural diversity, am pretty sure!!!? So this stuff huwez comment straighly kama ni wrong..

You can be legally right but morally wrong and vice versa is true.

Sheria zote zina hitaji usimamiz na ufuatiliaji.
 
Back
Top Bottom