Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

Elections 2015 UKAWA na Lowassa unganeni mchukue nchi, wakati ndio huu, mkipuuzia huu ushauri basi tena!

magufuli sijamsamehe kwa mambo haya mawili 1.nyumba za serikali ambazo viwanja vyake vinathamani ya billions yeye akauza nyumba millions ,,najua wengine watasema alipata shinikizo lkn kama mtendaji mzuri angejipambanua pale
.2. Meli ya ferry bagamoyo ya masaa sita ...haya mawili sikumuelewa kabisa......
 
Baada ya CCM kumsimamisha jembe Magufuli, Lowassa ahamie UKAWA kwenda kufanya nini?!. Kama CCM ingemsimamisha Membe, hata mimi ningeuka mkono hoja!. Lowassa hili analijua wazi na ahami ng'oo!.

Pasco
ingekuwa sawa kama angeshindwa kwenye kamati kuu .lakini sio kwenye genge la kamati ya maadili .na. Kikwete ni mwenyekiti.Pasco kumbuka pia Lowasa ana siri nzito juu ya sakataa la richmond kumhusu Jk kuwasiliana na makatibu wa wizara akiwa nje ya nchi kuhusu ualali wa kuendelea na richmond .nakuwacha kuwasiliana na waziri mkuu Lowasa .Pasco nakuaminia wewe nimjuzi katika habari na uchambuzi wa siasa .sitegemei usahau hili .so njia bora ya kuficha siri nikummaliza mjua siri .ili uwe salama .unammalizia wapi adui sirini kwenye kamati ambayo wewe ndio mshika bunduki.ukimwacha aje hadharani kwenye kamati kuu itabidi ukampeni ili amalizwa .ningumu na haswa tatizo likiwa ni lako sirini.fikiria .Pasco Karibu chadema aupendezi gweji kama wewe kujidai huko Neutral .karibu m4c .nafasi ya kazi msemaje wa rais Dr Slaa .karibu
 
Ndugu Wananchi,

Mimi kama mdau wa siasa na mzalendo kwa nchi yangu naomba nitoe ushauri ufuatao kwa UKAWA pamoja na Lowassa. Najua kuna watu inaweza ikawa ngumu sana kuelewa point yangu, lakini wenye ufahamu na mambo ya siasa na mapinduzi wataona point yangu.

Huu ushauri wangu umezingatia hali ya uchumi wa watanzania ambayo imeendelea kuwa maskini huku viongozi wakizidi kutajirika sana (mfano familia ya Rais wa sasa). Naelewa pia kuna watu watakuja hapa na fikra ya ufisadi wa ndugu Lowassa na kwamba hafai kupokelewa UKAWA. Hivi hawa ukiwauliza waweze kuthibitisha huo ufisadi wa Lowassa wanao majibu? Na je ni nani ndai ya CCM ambaye ni msafi?

Je huyu Magufuli ni msafi kiasi gani? Ni kwa vipi tumesahau juzi taarifa za CAG jinsi alivyolidanganya Bunge na upotevu wa billions zaidi ya 500? na je si ni huyu huyu Magufuli ndiye aliyehusika kwenye sakata la uuzaji wa nyumba za serikali? akimuuzia girlfriend wake na kaka yake ambao hawakuwa watumishi wa serikali kinyume cha utaratibu?

Nauliza tena, je ni nani MSAFI ndani ya CCM? Jibu ni HAKUNA MSAFI CCM. Na kwa wale wanaotegemea kuona mabadiliko yoyote hasa ya kiuchumi chini ya kiongozi yeyote ndani ya CCM hao wanajidanganya. Kwa CCM hata uwe msafi kiasi gani ukishaingia utakuwa unafanya matakwa ya CCM ya kulindana hasa ya kulinda wenye pesa na si kwa ajili ya wananchi.

Kwa hakika CCM haipo kwa ajili ya wananchi, kwani chini ya CCM tangu Uhuru, hakika hatujapata nafuu yoyote japo tuna rasilimali nyingi kama madini, maziwa , mafuta na gesi sasa. Naomba wananchi wenzangu mfungue macho na kuona jinsi muswada wa gesi na mafuta ulivyopitishwa juzi kwa hati ya dharura ili kulinda maslahi ya watu na si wananchi.

Ni wakat sasa wananchi wajue kwamba ADUI yao mkubwa ni CCM na mfumo wake na si watu, kwani watu hata wawe wazuri kiasi gani, lkn akishaingia ndani ya CCM, huyo mtu kwisha habari yake.

Baada ya huo utangulizi, sasa naomba niongelee kilichonisukuma mimi kuchukua muda kuandika thread hii. Awali ya yote naomba niseme kwamba mimi sina chama lakini ni mwenyeji wa Kanda ya Ziwa. Na kwasababu natoka eneo moja na Magufuli, wengi wangetarajia mimi pia niwe kati ya watu wanaofurahia uteuzi wake.

Naomba niseme kwamba, kwanza Magufuli ni mtendaji mzuri pamoja na kwamba ana udhaifu wake lakini kwa ccm yeye kidogo ana nafuu. Hatahivyo, pamoja na utendaji wake kuwa na unafuu, lakini HATALETA MABADILIKO yoyote, kwani akishaingia kwenye uongozi, yeye naye ataishia kufanya kama chama kinavyohitaji.

Na kwa msingi huo, mabadiliko ya maana katika nyanja zote yataletwa na chama mbadala na si ndani ya CCM.

Hivyo basi, Ombi langu kwa UKAWA ni kwamba wampokee Lowassa kupitia CHADEMA na Lowassa apewe nafasi ya kugombea Urais kupitia UKAWA. Naomba nirudie tena, Lowassa apewe nafasi ya kugombea URAIS. Hii ndio njia pekee ya kuitoa CCM na kuleta mfumo mpya utakaoleta mabadiliko hapa Tanzania.

UKAWA, kama kuna mtu mwenye value added kwenye mchakato wa kumtoa mkoloni mweusi madarakani ni Edward Lowassa, na wakati ndio huu na mkiacha tu hii nafasi, basi mtaendelea kuwa wapinzani miaka nenda rudi na mbaya zaidi hata wabunge watapunguakwa kasi sana mwaka huu. Hakuna mtu yeyote anayeweza leta thamani kwenye UKAWA na kuipa Ushindi toka CCM mbali na Lowassa pekee.

Faida ni kwamba CHADEMA tayari kina msingi nchi nzima na wafuasi wengi sana. Lowassa naye ana back up ya watu wengi sana na hata baadhi ya viongozi wa CCM katika ngazi zote watakuja naye. Naomba ieleweke kwamba Lowassa anapoingia CHADEMA atakuta mfumo ambao nao uko tayari, kwahiyo atafanya kazi ndani ya huo mfumo, na hivzo mambo ya CCM hatakuwa na impact kwenye mfumo atakaoukuta CHADEMA na UKAWA.

Na ukizingatia mfumo wa CHADEMA unavyojali wananchi, hivyo watanzania tutafaidika sana hasa kiuchumi. Lowassa akiwa mgombea Urais wa UKAWA atasaidia sana hata majimbo mengi ya ubunge kwa Wana UKAWA.

Mapendekezo yangu kwa wagombea wa UKAWA ni huu hapa:

1. Lowassa agombee urais kupitia CHADEMA.

2. Prof. Lipumba agombee Umakamu wa Urais.

3. Dr. Slaa akagombee ubunge ili aje awe waziri mkuu.

NB1: Naomba ieleweke kwamba mpaka sasa majimbo ya CHADEMA hasa za maeneo wanakokaa wasukuma (Kanada ya Ziwa) kwa kiasi kikubwa yatarudi CCM kwasababu ya Magufuli kuwa msukuma. Asiyetaka kukubaliana na mimi asubiri October. Na kura za urais vivyo hivyo. Na kwa msingi huo, ni lazima CHADEMA na UKAWA wawe na target ya kura za nyanda za juu kusini, kusini, kati na kaskazini. Na watu wa kusaidia UKAWA kukusanya kura za kutosha katika maeneo hayo ni Lowassa (Kaskazini, Kusini, kati, na nyanda za juu kusini) na Lipumba hasa kanda za magharibi na Kusini.

Najua kuna watu watakuja na hoja hapa ya Muungano kuhusu nafasi ya urais na makamu wake. Hapa UKAWA walenge kuondoa mfumo wa CCM na hivyo wanatakiwa watu wenye ngu (influencial people). Na kwa kuzingatia hilo, kwa CUF ukiondoa Lipumba anakuja Hamad amabye anagombea Zanzibar. Na kwasababu hiyo, wana-UKAWA wa Zanzibar wakubali tu wagombea wote watokee Bara, kwani matunda ya mfumo wa UKAWA utawafaidisha wananchi wote.

NB2: Lowassa atasaidia pia urais wa Seif Hamad kwa upande wa Zanzibar, kwani kuna wtu kule ambao hawajakubaliana na maamuzi ya CCM ya kuwaondoa akina Bilal. Na pia Lowassa na Karume ni kitu kimoja.

Naomba nimalizie kwa kusema kwamba hii ndio nafasi pekee ya CCM kuondolewa madarakani. Na njia pekee ni kupitia kwa Lowassa na UKAWA. Chadema na UKawa kubalini huu ushauri na hakika watanzania tuko nyuma yenu, kwani tunaamini kwamba uchumi wa Tanzania utabailika kwa mfumo ulio nje ya CCM na CHADEMA na UKAWA wanaweza kutumia nafasi hii sasa ya kumkubali Lowassa ili tupate mabadiliko.

UKAWA mnatakiwa kuwa makini, acheneni na propaganda za watu wengi hapa JF na mkubaliane na hali halisi. Wakati ndio huu na mkiuachia basi watanzania wasahau mabadiliko kwa kipindi kirefu sana.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA.

Ahsanteni.
Ni mimi Mpenda nchi.

Kuna tem Lowassa mzalendo?
 
ni ushauri mzuri huenda wenye tafiti ila wengi watacomment bila fafiti.ni mawazo mazuri na huenda bado mpinzani wa kweli atatoka ccm na huenda likatimia la baba wa taifa
 
Ndugu Wananchi,

Mimi kama mdau wa siasa na mzalendo kwa nchi yangu naomba nitoe ushauri ufuatao kwa UKAWA pamoja na Lowassa. Najua kuna watu inaweza ikawa ngumu sana kuelewa point yangu, lakini wenye ufahamu na mambo ya siasa na mapinduzi wataona point yangu.

Huu ushauri wangu umezingatia hali ya uchumi wa watanzania ambayo imeendelea kuwa maskini huku viongozi wakizidi kutajirika sana (mfano familia ya Rais wa sasa). Naelewa pia kuna watu watakuja hapa na fikra ya ufisadi wa ndugu Lowassa na kwamba hafai kupokelewa UKAWA. Hivi hawa ukiwauliza waweze kuthibitisha huo ufisadi wa Lowassa wanao majibu? Na je ni nani ndai ya CCM ambaye ni msafi?

Je huyu Magufuli ni msafi kiasi gani? Ni kwa vipi tumesahau juzi taarifa za CAG jinsi alivyolidanganya Bunge na upotevu wa billions zaidi ya 500? na je si ni huyu huyu Magufuli ndiye aliyehusika kwenye sakata la uuzaji wa nyumba za serikali? akimuuzia girlfriend wake na kaka yake ambao hawakuwa watumishi wa serikali kinyume cha utaratibu?

Nauliza tena, je ni nani MSAFI ndani ya CCM? Jibu ni HAKUNA MSAFI CCM. Na kwa wale wanaotegemea kuona mabadiliko yoyote hasa ya kiuchumi chini ya kiongozi yeyote ndani ya CCM hao wanajidanganya. Kwa CCM hata uwe msafi kiasi gani ukishaingia utakuwa unafanya matakwa ya CCM ya kulindana hasa ya kulinda wenye pesa na si kwa ajili ya wananchi.

Kwa hakika CCM haipo kwa ajili ya wananchi, kwani chini ya CCM tangu Uhuru, hakika hatujapata nafuu yoyote japo tuna rasilimali nyingi kama madini, maziwa , mafuta na gesi sasa. Naomba wananchi wenzangu mfungue macho na kuona jinsi muswada wa gesi na mafuta ulivyopitishwa juzi kwa hati ya dharura ili kulinda maslahi ya watu na si wananchi.

Ni wakat sasa wananchi wajue kwamba ADUI yao mkubwa ni CCM na mfumo wake na si watu, kwani watu hata wawe wazuri kiasi gani, lkn akishaingia ndani ya CCM, huyo mtu kwisha habari yake.

Baada ya huo utangulizi, sasa naomba niongelee kilichonisukuma mimi kuchukua muda kuandika thread hii. Awali ya yote naomba niseme kwamba mimi sina chama lakini ni mwenyeji wa Kanda ya Ziwa. Na kwasababu natoka eneo moja na Magufuli, wengi wangetarajia mimi pia niwe kati ya watu wanaofurahia uteuzi wake.

Naomba niseme kwamba, kwanza Magufuli ni mtendaji mzuri pamoja na kwamba ana udhaifu wake lakini kwa ccm yeye kidogo ana nafuu. Hatahivyo, pamoja na utendaji wake kuwa na unafuu, lakini HATALETA MABADILIKO yoyote, kwani akishaingia kwenye uongozi, yeye naye ataishia kufanya kama chama kinavyohitaji.

Na kwa msingi huo, mabadiliko ya maana katika nyanja zote yataletwa na chama mbadala na si ndani ya CCM.

Hivyo basi, Ombi langu kwa UKAWA ni kwamba wampokee Lowassa kupitia CHADEMA na Lowassa apewe nafasi ya kugombea Urais kupitia UKAWA. Naomba nirudie tena, Lowassa apewe nafasi ya kugombea URAIS. Hii ndio njia pekee ya kuitoa CCM na kuleta mfumo mpya utakaoleta mabadiliko hapa Tanzania.

UKAWA, kama kuna mtu mwenye value added kwenye mchakato wa kumtoa mkoloni mweusi madarakani ni Edward Lowassa, na wakati ndio huu na mkiacha tu hii nafasi, basi mtaendelea kuwa wapinzani miaka nenda rudi na mbaya zaidi hata wabunge watapunguakwa kasi sana mwaka huu. Hakuna mtu yeyote anayeweza leta thamani kwenye UKAWA na kuipa Ushindi toka CCM mbali na Lowassa pekee.

Faida ni kwamba CHADEMA tayari kina msingi nchi nzima na wafuasi wengi sana. Lowassa naye ana back up ya watu wengi sana na hata baadhi ya viongozi wa CCM katika ngazi zote watakuja naye. Naomba ieleweke kwamba Lowassa anapoingia CHADEMA atakuta mfumo ambao nao uko tayari, kwahiyo atafanya kazi ndani ya huo mfumo, na hivzo mambo ya CCM hatakuwa na impact kwenye mfumo atakaoukuta CHADEMA na UKAWA.

Na ukizingatia mfumo wa CHADEMA unavyojali wananchi, hivyo watanzania tutafaidika sana hasa kiuchumi. Lowassa akiwa mgombea Urais wa UKAWA atasaidia sana hata majimbo mengi ya ubunge kwa Wana UKAWA.

Mapendekezo yangu kwa wagombea wa UKAWA ni huu hapa:

1. Lowassa agombee urais kupitia CHADEMA.

2. Prof. Lipumba agombee Umakamu wa Urais.

3. Dr. Slaa akagombee ubunge ili aje awe waziri mkuu.

NB1: Naomba ieleweke kwamba mpaka sasa majimbo ya CHADEMA hasa za maeneo wanakokaa wasukuma (Kanada ya Ziwa) kwa kiasi kikubwa yatarudi CCM kwasababu ya Magufuli kuwa msukuma. Asiyetaka kukubaliana na mimi asubiri October. Na kura za urais vivyo hivyo. Na kwa msingi huo, ni lazima CHADEMA na UKAWA wawe na target ya kura za nyanda za juu kusini, kusini, kati na kaskazini. Na watu wa kusaidia UKAWA kukusanya kura za kutosha katika maeneo hayo ni Lowassa (Kaskazini, Kusini, kati, na nyanda za juu kusini) na Lipumba hasa kanda za magharibi na Kusini.

Najua kuna watu watakuja na hoja hapa ya Muungano kuhusu nafasi ya urais na makamu wake. Hapa UKAWA walenge kuondoa mfumo wa CCM na hivyo wanatakiwa watu wenye ngu (influencial people). Na kwa kuzingatia hilo, kwa CUF ukiondoa Lipumba anakuja Hamad amabye anagombea Zanzibar. Na kwasababu hiyo, wana-UKAWA wa Zanzibar wakubali tu wagombea wote watokee Bara, kwani matunda ya mfumo wa UKAWA utawafaidisha wananchi wote.

NB2: Lowassa atasaidia pia urais wa Seif Hamad kwa upande wa Zanzibar, kwani kuna wtu kule ambao hawajakubaliana na maamuzi ya CCM ya kuwaondoa akina Bilal. Na pia Lowassa na Karume ni kitu kimoja.

Naomba nimalizie kwa kusema kwamba hii ndio nafasi pekee ya CCM kuondolewa madarakani. Na njia pekee ni kupitia kwa Lowassa na UKAWA. Chadema na UKawa kubalini huu ushauri na hakika watanzania tuko nyuma yenu, kwani tunaamini kwamba uchumi wa Tanzania utabailika kwa mfumo ulio nje ya CCM na CHADEMA na UKAWA wanaweza kutumia nafasi hii sasa ya kumkubali Lowassa ili tupate mabadiliko.

UKAWA mnatakiwa kuwa makini, acheneni na propaganda za watu wengi hapa JF na mkubaliane na hali halisi. Wakati ndio huu na mkiuachia basi watanzania wasahau mabadiliko kwa kipindi kirefu sana.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki UKAWA.

Ahsanteni.
Ni mimi Mpenda nchi.

Mawazo yako ni mazuri,unajua watu hawajui kama tunatakiwa kuondokana na mfumo CCM na tusipochezesha akili CCM itaendelea kutawala,ni lazima viongozi wajifunze kutumia lines of weakness huku wakijitenga na tamaa na ubinafsi.
 
mtoa mada wewe ni shabiki wa team wa LOWASA amabaye ana shutuma kibao za Rushwa na kashifa ya Richmond ndiyo inayo mutafuna popote pale atakapo enda lazima gamba la richmond litaendelea kumutafuna. Lowasa hafai kuiongoza nchi hii hata kama atapitia upinzani bado hafai na UKAWA hawapaswi kumupokea na kumupa nafasi hiyo.mimi ni mwana UKAWA damu damu niliye choshwa na mfumo wa ccm kwa kila kona hata asimamishwe nabii lakini akiwa ndani ya ccm atakuwa mwinzi.

Loawasa hafai kwanza ana kashifa ya Richmond inamutafuna ambayo kashifa hiyo iliibuliwa na wapinzani ambao leo hii unamushauri Lowasa akajiunge nao wakati wapinzani kwa mda tofauti wamemutuhumu Lowasa.

Team iliyokuwa imemuzunguka Lowasa wote wale wana kashifa mbali mbali za rushwa na ufisadi na walikuwa kwa pamoja kila kona wakati anatangaza nia je akija ukawa ataasafishika vipi?

UKAWA WAKIMUPOKEA BASI WATANZANIA WATAKOSA IMANI NAO.
UKAWA ndilo tumanini jipya la watanzania kwa ajiri ya ukombozi mupya na kumuondoa madarakani mkoloni mweusi ccm, itakuwa ni aibu kwa ukawa wamuchukue Lowasa na pia apewe nafasi ya juu ya kugombea uraisi, Lowasa ni mtu ambaye anafanya kila means kuhakikisha anashinda jambo ambalo linaweza ku coast ukawa na kuwapa nafasi nzuri ccm kuweza kuwachafua ukawa kwa kumupokea fisadi aliye tukuka,
UKAWA dhamila yetu kuu ni kumutoa ccm madarakani ambapo jambo hili linaneda kutimia mwezi wa kumi, hivyo lowasa hatufai
Mkuu KILLERS KISS GUY, kwanza karibu jirani, nchi yetu yetu ni nzuri, ukiishajua tuu kuandika Kiswahili, unaandikishwa BVR. Mimi nimezipenda tuu hizi 'mu' zako!, karibu kwetu, na BVR ikipita pande zako, kajiandikishe tuu, hautashtukiwa!.

Pasco
 
Serena

Ulichoandika na kusisitiza ni kuwa:

Ikiwa UKAWA hawatompata LOWASA wasahau kushinda uchaguzi mkuu wa 2015.

Kwa maana rahisi ni kuwa umedharau kazi zilizofanywa na wapinzani hawa wa CCM. Unamaanisha miaka mitano ya kuimarisha upinzani imepotea bure.

Ngoja wenyewe waje.
 
ingekuwa sawa kama angeshindwa kwenye kamati kuu .lakini sio kwenye genge la kamati ya maadili .na. Kikwete ni mwenyekiti.Pasco kumbuka pia Lowasa ana siri nzito juu ya sakataa la richmond kumhusu Jk kuwasiliana na makatibu wa wizara akiwa nje ya nchi kuhusu ualali wa kuendelea na richmond .nakuwacha kuwasiliana na waziri mkuu Lowasa .Pasco nakuaminia wewe nimjuzi katika habari na uchambuzi wa siasa .sitegemei usahau hili .so njia bora ya kuficha siri nikummaliza mjua siri .ili uwe salama .unammalizia wapi adui sirini kwenye kamati ambayo wewe ndio mshika bunduki.ukimwacha aje hadharani kwenye kamati kuu itabidi ukampeni ili amalizwa .ningumu na haswa tatizo likiwa ni lako sirini.fikiria .Pasco Karibu chadema aupendezi gweji kama wewe kujidai huko Neutral .karibu m4c .nafasi ya kazi msemaje wa rais Dr Slaa .karibu
Mkuu morenja, kwanza asante kwa sababu usemayo ni kweli, Lowassa anaijua siri ya Richmond na mimi niliamini ndio karata yake ya mwisho ya turufu ya kuombea uteuzi, lakini kilichotokea, JK ni mafia wa ukweli, amemchinjia kule kule chini, na kumpiga dafrau kwa kumsimamishia Jembe JPM!. Nilitegemea angesimamishwa Membe, Lowassa angevuka upande wa pili, na kuichukua nchi kama ameokota!.

Asante kunikaribisha Chadema, kiukweli siasa nazipenda, ila kwa fani yangu ya habari, ninapaswa kuwa neutral wakati wote ili kuweza kupratice impartiality kwenye kutimiza majukumu yangu. Uandishi wangu ni kwa kujitolea, mimi ni mwandishi wa mitaani, nimeishakuwa kama kuku wa kienyeji, sifugiki!, ila pia namkubali sana msemaji wa rais Dr. Slaa aliyepo sasa, anajitahidi sana, ila kuna vitu vidogo vidogo tuu vya kurekebisha akiishaingia ikulu!.

Pasco.
 
hahahahahahah......
munaijua ccm ama mnaiskia tu!! yan lowasa ahamie ukawa then ashinde?! ccm na ufisad wao wote lkn wamemkataa lowasa.......kwa kifup hashind na lowasa mwiz zaid ya ccm
 
Lowasa na UKAWA ni two immiscible solvents..Hawakai pamoja..Mmoja ni very polar na mwingine ni non polar

Lowasa ili ayeyuke kwenye UKAWA inabidi aloose polarity yake kwa kuitisha press na kueleza kinagaubaga nani mwenye Richmond na mchakato mzima ulivyokuwa.Aeleze ni deal ngapi amepiga akiwa serikalini na awataje wenzake na mbinu wanazozitumia.

Awataje wanasiasa walio nyuma ya wauza unga,wawindaji wa tembo,wauaji wa albino etc.Ataje mbinu wanazotumia CCM kuiba kura...Yani aseme kila kitu kwa ukweli wake ili waTZ waujue ukweli wa viongozi wao

Then aombe radhi kwa waTZ na kwa Mungu wake maana ufisadi walioufanya una uhusiano wa moja kwa moja/usio wa moja kwa moja na baadhi ya vifo vya watu hapa nchini na hapo ndio 'like will dissolve like'

Bila kufanya hivyo..UKAWA itakayompokea ijiandae kuanguka vibaya

A big concept...!!! naamini mpango huo ukijulikana CCM watamuua
 
Serena

Ulichoandika na kusisitiza ni kuwa:

Ikiwa UKAWA hawatompata LOWASA wasahau kushinda uchaguzi mkuu wa 2015.

Kwa maana rahisi ni kuwa umedharau kazi zilizofanywa na wapinzani hawa wa CCM. Unamaanisha miaka mitano ya kuimarisha upinzani imepotea bure.

Ngoja wenyewe waje.

Mm nakubaliana na mawazo yako kwa asilimia mia, mbona watu wanafikiria mambo mepesi sana? Hawafikirii kwamba ufisadi wake ndo umetufikisha hapa, wao wanachofikiri ni kuiondoa ccm madarakani tu, kama ikiondolewa na mafisadi ni faida gani tutapata? kama UKAWA hawatoshi kupambana na CCM basi waendelee kuwa wapinzani, hii nchi sio ya kuchagua mtu eti kwa ajili ya kutoa chama fulani. Kama UKAWA wana mawazo hayo mgando, basi nchi haiwezi kupiga hatua kwa utaratibu huo. Hivi pesa ya Lowasa alotumia kutangaza nia Arusha na kuzunguka Tz nzima, huwezi kujiuliza kazitoa wapi? Na kabla ya hapo alianza kampeni miaka mingi tu, akipewa mwaliko makanisani& misikitini alikuwa anatoa pesa nyingi sana. lazima tutafakari sana sana, na kwa sababu anapesa nyingi sana, akipewa nafasi UKAWA zile ndoto zao za kuleta maendeleo zitapotea kabisa, wala hatokuwepo tena kiongozi wa UKAWA kukemea jambo hilo, kwa sabu UKAWA itakuwa imetekwa na kundi hilo. Mm nadhani tuendelee na viongozi wetu wa UKAWA kwa maendeleo ya wanyonge.
 
Watanzania,
Hatimaye ombi langu kama thread hii inavyosoma inaelekea kutimia muda si mrefu. Nalo ni Lowassa kuingia UKAWA na kugombea nafasi ya URAIS. Nataka niwaambie UKAWA tena, hili ni pigo kubwa sana kwa CCM na wale wote wasiopenda kuona mfumo CCM ambao ni mfumo mbaya kupita yote duniani ikiondolewa madarakani. Naomba nirudie tena, kwasasa Watanzania wanatakiwa kumtoa mdudu CCM bila kujali nani mgombea wake, kwani CCM ni mfumo usio na tiba kwa mtu anayeshinda uongozi kupitia CCM.

Na kwa wale wote mliodhani Lowassa hana impact, sasa subirini muone mwisho wake. Pia niwaombe tu muache kulalamika sasa, si mlimtema kwamba hafai, na hata wale waliokuwa upande wake wote ndani ya CCM nao wanaangushwa kwenye kura za maoni (rejea Nchimbi, Pindi Chana, n.k.) ikiwa ni maagizo toka kwa Mwenyekiti wa CCM na Wazee wa Kitengo maalumu? Sasa mnalilia nini tena, kwani Lowassa ndio huyooo?

Yaani ni raha mstareheee kila kona kwa UKAWA, ebu jaribu kufikiria, Lowassa anapiga Kampeni sehemu moja ya nchi, Dr. Slaa naye anapiga kampeni sehemu nyingine, Prof. Lipumba naye ndani ya Nyumba, Lissu kama kawaida, Mbowe naye anapiga kotekote, n.k. Naomba CCM mje hapa mniambie huu mziki wa UKAWA utatulizwa na nani????? Je Mzee Pombe Magufuli na kauli mbiu yake SITAWAANGUSHA atauwezaaa?????? Thubutu yake.

Mbarakiwe sana, kwani hatimaye naiona Tanzania mpya nje ya mdudu CCM ikizaliwa chini ya mfumo mpya unaojali maslahi ya Watanzania UKAWA.
 
magufuli sijamsamehe kwa mambo haya mawili 1.nyumba za serikali ambazo viwanja vyake vinathamani ya billions yeye akauza nyumba millions ,,najua wengine watasema alipata shinikizo lkn kama mtendaji mzuri angejipambanua pale
.2. Meli ya ferry bagamoyo ya masaa sita ...haya mawili sikumuelewa kabisa......

Magufuli hana jipya kama wenzake ndani ya CCM ndiyo maana ana kauli mbiu ya SITAWAANGUSHA, Je ni akina nani hao, kwani neno analotumia ni pana.
 
Mkuu morenja, kwanza asante kwa sababu usemayo ni kweli, Lowassa anaijua siri ya Richmond na mimi niliamini ndio karata yake ya mwisho ya turufu ya kuombea uteuzi, lakini kilichotokea, JK ni mafia wa ukweli, amemchinjia kule kule chini, na kumpiga dafrau kwa kumsimamishia Jembe JPM!. Nilitegemea angesimamishwa Membe, Lowassa angevuka upande wa pili, na kuichukua nchi kama ameokota!.

Asante kunikaribisha Chadema, kiukweli siasa nazipenda, ila kwa fani yangu ya habari, ninapaswa kuwa neutral wakati wote ili kuweza kupratice impartiality kwenye kutimiza majukumu yangu. Uandishi wangu ni kwa kujitolea, mimi ni mwandishi wa mitaani, nimeishakuwa kama kuku wa kienyeji, sifugiki!, ila pia namkubali sana msemaji wa rais Dr. Slaa aliyepo sasa, anajitahidi sana, ila kuna vitu vidogo vidogo tuu vya kurekebisha akiishaingia ikulu!.

Pasco.
Baada ya Edward Lowassa kusifiwa na rais Magufuli kuwa ni Superman, namdurufu kidogo Lowassa kwa kujikumbusha niliwahi kusema nini kuhusu mtu huyu.
P
 
Back
Top Bottom