Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #221
[SUP]MTAZAMO KUHUSU HOTUBA YA RAIS KAMA ILIVYO KATIKA BANDIKO HAPO JUU[/SUP]
Bandiko la 3
(Kifungu AI)
Rais: Hili ni jambo zito nisingeweza kukaa kimya.
Watanzania wangeshangaa nini maoni ya Rais. Mimi ndiye mlezi wa taifa.
Hoja: Tume ilitambua kuwa wewe ndiye mlezi. Ilikufuata kukutaka utoe maoni yako.
Kwa mujibu wa majibu ya Rais (Kifungu AB) mazungumzo yako na akina Warioba hayakuwa ya kina.
Hivi mlezi ambaye leo umegundua uzito wa jambo hukuwa na la kusema wakati huo?
Watanzania wasingeshangaa Rais kwanini hakutoa maoni, jibu umeshalitoa (Kifungu AC)kwamba hukutaka kuingilia mchakato na kwamba(Kifungu A D)ulikataa kutoa maoni hata pale ulipoombwa.
(Kifungu AJ)
Rais: Kwa bahati nzuri nilitoa maoni yangu mahali penyewe, ndani ya bunge la katiba.
Hoja: Mh Rais ulikiuka sheria ya katiba inayoeleza utaratibu wa kutoa maoni.
Sheria hiyo uliyosaini haina mahali inapoelekeza kuwa baadhi ya watu watatoa maoni yao nje ya yale yaliyokusanywa na rasimu.
BMLK si mahali ulipotakiwa kutoa maoni yako, nafasi hiyo uliikataa.
BMLK ni sehemu ya kueleza uzoefu wako kama Rais na kulileta taifa pamoja kwa lengo moja.
Ulichokifanya ni kuligawa taifa kuliko ilivyokuwa kabla na hata katika historia. Rais ndiye chanzo cha matusi hasa alipowadhalilisha wazee wenzake.Ile dhana ya ulezi imekosa mahali pa kusimama.
(Kifungu AK)
Rais: Nilipotoa maoni yangu sikulazimisha au kushurutisha watu wayakubali.
Hoja: Kauli ya rais ni sheria . Kwa mujibu wa katiba ya leo, baada ya kura ya maoni atakayesaini katiba kuwa sheria ni Rais wa JMT. Hivyo Rais husubiri sheria ije katika dawati lake.
Katika bunge la katiba, Rais alisema ''S3 zisubiri aondoke'' Hapa ndipo pa kujiuliza, je hilo halikuwa kuwashawishi wajumbe kuwa kwa hali yoyote yeye hata saini hata kama wananchi wataridhia.
Kauli ya ''S3 hadi aondoke' zilieleza na kuelekeza kuwa katiba izingatie maoni yake na si ya wananchi vinginevyo hilo hataklikubali. Mh Rais hiyo ndio kulazimisha au kushurutisha na ulikuwa mwanzo wa tatizo
Bandiko la 3
(Kifungu AI)
Rais: Hili ni jambo zito nisingeweza kukaa kimya.
Watanzania wangeshangaa nini maoni ya Rais. Mimi ndiye mlezi wa taifa.
Hoja: Tume ilitambua kuwa wewe ndiye mlezi. Ilikufuata kukutaka utoe maoni yako.
Kwa mujibu wa majibu ya Rais (Kifungu AB) mazungumzo yako na akina Warioba hayakuwa ya kina.
Hivi mlezi ambaye leo umegundua uzito wa jambo hukuwa na la kusema wakati huo?
Watanzania wasingeshangaa Rais kwanini hakutoa maoni, jibu umeshalitoa (Kifungu AC)kwamba hukutaka kuingilia mchakato na kwamba(Kifungu A D)ulikataa kutoa maoni hata pale ulipoombwa.
(Kifungu AJ)
Rais: Kwa bahati nzuri nilitoa maoni yangu mahali penyewe, ndani ya bunge la katiba.
Hoja: Mh Rais ulikiuka sheria ya katiba inayoeleza utaratibu wa kutoa maoni.
Sheria hiyo uliyosaini haina mahali inapoelekeza kuwa baadhi ya watu watatoa maoni yao nje ya yale yaliyokusanywa na rasimu.
BMLK si mahali ulipotakiwa kutoa maoni yako, nafasi hiyo uliikataa.
BMLK ni sehemu ya kueleza uzoefu wako kama Rais na kulileta taifa pamoja kwa lengo moja.
Ulichokifanya ni kuligawa taifa kuliko ilivyokuwa kabla na hata katika historia. Rais ndiye chanzo cha matusi hasa alipowadhalilisha wazee wenzake.Ile dhana ya ulezi imekosa mahali pa kusimama.
(Kifungu AK)
Rais: Nilipotoa maoni yangu sikulazimisha au kushurutisha watu wayakubali.
Hoja: Kauli ya rais ni sheria . Kwa mujibu wa katiba ya leo, baada ya kura ya maoni atakayesaini katiba kuwa sheria ni Rais wa JMT. Hivyo Rais husubiri sheria ije katika dawati lake.
Katika bunge la katiba, Rais alisema ''S3 zisubiri aondoke'' Hapa ndipo pa kujiuliza, je hilo halikuwa kuwashawishi wajumbe kuwa kwa hali yoyote yeye hata saini hata kama wananchi wataridhia.
Kauli ya ''S3 hadi aondoke' zilieleza na kuelekeza kuwa katiba izingatie maoni yake na si ya wananchi vinginevyo hilo hataklikubali. Mh Rais hiyo ndio kulazimisha au kushurutisha na ulikuwa mwanzo wa tatizo