UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

UKAWA wanavyobabaika: Historia ya 'juisi ya maembe' kujirudia?

Mkuu Nguruvi3

Hivi JK alikutana na UKAWA kwa mwamvuli wa TCD au ni kinyume chake? Kwa mtazamo wangu sioni kama alikutana na UKAWA. Japo wana-UKAWA walihudhuria mkutano ule lakini walihudhuria kwa kofia TCD na si vinginevyo. Makubaliano yoyote yale yaliofikiwa mule ndani ni baina ya JK na TCD sio UKAWA....

Labda wangeweza kususia kikao kile waiache TCD ya kina Cheyo na Mrema ndio waonane na JK peke yao ingawa bado najiuliza kama hatua hiyo ingeleta athari zipi...
Mwalimu , JK aliwakwepa UKAWA kwa trick.
Hakuwa amepanga kukutana na wapinzani, lakini pia hakuwa tayari kukutana na UKAWA kwasababu alitaka mahali pa kutokea.

Ndipo njia ya udanganyifu ikifanyika kutumia kituo cha Demokrasia ambacho mwenyekiti ni Cheyo.
Cheyo, Hamad Rashid, Mrema, Mapalala, Dovutwa n.k. wapo bungeni hna hivyo hakukuwa na issue ya kuzungumza na JK

Alichokifanya JK ni kuwaweka hao vibaraka ili watumike kama mpini.
Tuliwaonya UKAWA hapa jamvini, tukiwauliza ushirika na hao walioko bungeni umeanzaje?

Kama kawaida ya UKAWA, walidhani JK ni mwema kwao bila kujua anachezea akili zao kila siku.
Wamekwenda, vibaraka wakatumika kuwavuruga UKAWA na issue ikatoka kwa JK na kuwa ugomvi miongoni mwa TCD

Hata tangazo na debe la mazungumzo anayelisimamia ni Cheyo.
UKAWA tuliwaambia kabla ya mazungumzo hapa jamvini.
1. Hao wapinzani walioko bungeni wanakwenda kuonana na JK kwa sababu zipi?
2.Lini JK amekuwa mwema kwa UKAWA zaidi ya chama chake?
3. Kwanini bunge halisitishwi kupishamajadiliano?
4. Lini UKAWA wamefanya majadiliano na JK wakafanikiwa?
5. JK alipowavuruga wazee wa tume, lipi UKAWA walitegemea tofauti?
6. Wamejifunza nini kutokana na majadiliano ya siku za nyuma?

Maswali haya walipewa ili kuwafungua vichwa. Inashangaza wakaingia kichwa kichwa wakijua kabisa JK na serikali yake hawana nia wala kusudio la katiba mpya.

Leo Cheyo amepewa rungu anawaponda UKAWA, JK na CCM wakiwa wamejifungua kitanzi.

Hawa viongozi wa UKAWA kuna nyakati huwa najiuliza kama kweli wanajua michezo ya kisiasa.
Wamechezewa sana JK na wala hawaonekani kujifunza.

Huo ndio hasa mwanzo wa nyuzi hii inayohusu Juisi ya maembe. Wamekwenda wamekunya na nadhani walilewa.
 
Last edited by a moderator:
DURU: MAREJEO

Wanajamvi, haya ni yale tuliyoyasema tukaambiwa wazushi.
Hebu tutafakri kidogo
cc Mwalimu

JK AEDELEZA MBINU ZA KUWADAGANYA UKAWA
AWATAKA WAENDE KUJADILIANA NAYE WAKIWA NA GLASI ZA JUISI
BUNGE ALILOOMBWA LIAHIRISHWE LINAENDELEA

JK ANA LIPI IKIWA ALISHASEMA S3 ZISUBIRI AONDOKE?


Rais JK juzi amekaririwa akiwa Morogoro akiwataka Ukawa waende kujadiliana naye.

Huko nyuma, UKAWA walimuomba aende kujadiliana nao bila majibu.

Hatua hiyo ya UKAWA tuliipinga hapa duru katika msingi kuwa aliyevuruga ni JK, vipi waende kumuomba asuluhishe alichokivuruga tena akijua ni makusudi?

Hatua ya JK kuwataka UKAWA waonane naye imekuja huku bunge lilikosa mvuto na kuonekana kama mazingaombwe.

Imefika mahali mwenyekiti Sitta ameunda tume yake kuchukua maoni bila kupewa haki na sheria yoyote.
Ameshakutana na wafugaji na makundi wa wakulima wa Pamba

Vikao vya Sitta ni vya kitoto maana havina minutes na wala havitambuliki kisheria.
Ni mikutano ya chai isiyo na maana kwa kuanzia na 'tume ya sitta' pamoja na wanaoalikwa.

Anachokifanya Sitta si kuandika katiba ya wananchi, ni kutaka kuungwa mkono ili tu aonekane ameweza hata kama anajua kuweza huko ni kwa gharama kubwa ya taifa siku za mbeleni.

Samwel Sitta hajali tena usalama wa nchi hii, anachokiangalia ni masilahi yake manono yatakoanyo na vikao vinavyoendelea.

Sitta anajua wazi ndoto zake za Urais zimefikia kikomo, haaminiki na wala haitatokea, si kwa chama chake.
Anachokifanya ni kukusanya milioni takribani 150 mwisho wa kikao, huko mbele Watanzania watajua wenyewe.

Ndani ya bunge la CCM Dodoma, hali si shwari. Taarifa zisizosemwa ni kuhusu kukinzana kwa hoja hasa za muungano.

Ndani ya kamati kumekuwepo na mpasuko mkubwa, huku baadhi ya wabunge 'wakijitoa mhanga' kama Mh Ali Kesi ambaye amewaunga mkono UKAWA na tume ya Warioba kuhusu muundo.

Wimbi hilo litajitokeza wazi katika mijadala na sasa ni wazi kuwa hata ndani ya CCM-Bunge maalumu kuna mpasuko.

Kila muundo unaopendekezwa unaelekea kule kwa tume ya Warioba. Kukwepa hilo imekuwa kazi kubwa.

Ndani ya CC ya CCM wajumbe wa znz ndio wamekuwa kikwazo cha S3. Wao hawataki kusikia S3 kutokana na matatizo yao wenyewe ambapo muundo wa S2 wanauona una masilahi kwao kiuchumi, kijamii na hasa suala la mapinduzi.

Katika hali hiyo JK anajikuta akikumbana na nguvu ya umma, ndani ya CC, BMK la CCM na nguvu kubwa sana kutoka kwa makundi ya kijamii hasa wasomi wanaouona mchakato kama kituko kingine cha awamu hii.

JK anajaribu kwalaghai UKAWA ili aongee nao. Lengo ni kuwafiriji kuwa malalamiko yao yatasikilizwa.

Hiyo ndio mbinu yake, kwamba baada ya CC ya CCM kutaka mchakato uendelee, JK anataka kuwafurahisha UKAWA kwa kilemba cha UKOKA.

KWANINI UKAWA WAJIANGALIE

Juzi CC ya CCM chini ya kikwete imeamua mchakato uendelee

Ndani ya Bunge la Sitta, kanuni zimebasilishwa na sasa wanaongeza sura zile za rasimu ya mafichoni ya CCM
https://www.jamiiforums.com/great-t...-za-ccm-kuingiza-katiba-yao-ya-mafichoni.html

Katika hali hiyo UKAWA wajiulize

1. Iweje JK juzi aongoze CC kutoa msimamo wa kuendelea na siku 3 baadaye awatake UKAWA warudi katika majadiliano?
Ni majadiliano gani wakati CCM inaendelea na mipango yake tena ikiwa na tume ya Sitta ya kukutana na wafugaji/wakulima n.k.?

2. Je, UKAWA wakirudi, kanuni alizobadili Sitta zitakuwa zile zile za awali au itabidi wafuate zilizopo?
Na kama watafuata za sasa ni vipi watakwepa mkumbo wa kuchomeka vifungu vya maoni yasiyotokana na wananchi?

3. Na je, UKAWA wakirudi na Sitta kugoma kuwasikiliza, watarudi vipi kwa wananchi na kuwaeleza walisusia nini na walikubali nini na sasa wanasusia nini? Je hapo hawtaakuwa wamejichanganya na kuonekana hovyo?

Ni kwa muktadha huo, vikao vya Jaji Mutungi au JK na UKAWA ni dharau.
Haiwezekani bunge likawa linaendelea wakati kuna majadiliano.

JK alikataa kuahirishaau kuvunja bunge. Sitta kabadili kanuni na taratibu.

UKAWA lazima wawe makini, vinginevyo wanaweza kuambulia juisi za maembe kama kawaida

Tusemezane



cc MJINI CHAI
 
DURU : MAREJEO

Wanajamvi, siku za nyuma tuliyasema haya
Leo mnaona kila jambo. Tulisema wenye muungano watachoka na hizi zawadi kwa wazanzibar.
Wenye muungano ''keissy'' kawaambia wazanzibar ukweli.
Wznz wanuna kupewa vidonge, muungano ndio huoo!

Na huu ni mwanzo tu, aliyoyasema mbunge Keissy ndio yaliyomo mioyoni mwa Watanganyika.
Alisema Prof Palamagamba, Watangayika wana yao kifuani, siku yakitoka ni hatari. Je hatujaona yameanza kutoka?


cc. Nguruvi3 acha umbea wako by Kobello (alisema hayo, sijui kama si kweli kwa hali ilivyo)

TULIYOSEMWA DURU ZA SIASA YAANZA KUTIMIA

BMK-CCM KAZI KUBWA NI KUWAFURAHISHA WAZANZIBAR

HUWEZI KUFURAHISHA WZNZ UKAUDHI WENYE MUUNGANO

SASA MUUNGANO UNAKARIBIA KUVUNJIKA KAMA GLASS


Mabandiko ya duru yanayoendelea, tulisema lengo la CCM si kuandika katiba ya nchi, ni kuwafurahisha wazanzibar wakubaliane na mfumo wa S2

Rais JK ndiye aliyefungua pazia, kwa kuwapa wazanzibar kila walichodai.
Sasa wanaondoa vifungu vya katiba watakavyo, wanapewa zawadi zisizo na audit, fursa n.k

Wazanzibar wakakuvunja katiba ya nchi, hakuna wa kuwafanya lolote.
JK akawapa haki znz 1.2 Milioni,wachache kuliko wananchi wa Ubungo sauti na nguvu katika muungano.

Kwasasa wznz wana malalamiko mengine ambayo ni Rais wa znz kuwa makamu wa rais wa JMT.

Hii maana yake Rais wa JMT atakapokuwa hayupo, atakayekaimu nafasi yake ni Rais wa SMZ.

Rais wa SMZ hachaguliwi na rais yoyote wa Tanganyika.

Ni sawa na kumchukua Rais Uhuru wa Kenya kukaimu nafasi ya Urais nchi ya Tanganyika.

Hili ni kuwafariji wznz ili wakubali mfumo wa S2 ambao kimasilahi hauna tija wala faida kwa Watanganyika.

Hali hii inaleta hasira za kuwadhalililisha na kuwadharau Watanganyika katika hali isiyoweza kuvumilika.

Hakuna Mtanganyika anayeingia SMZ kwa bahati mbaya, kuchaguliwa au kuteuliwa. Leo tumefika mahali tunakabidhi nchi yetu kwa mamluki wa znz.

Zanzibar hawajitambui kama Watanzania, wapi wanaweza kuja kutawala Tanganyika?

Kinachofuata ni kukaribisha hasira zaidi, kuamsha damu zinazochemka dhidi ya uonevu huu unaofanywa na watu 1.2 ambao nusu yao wanaishi Tanganyika.

Kimsingi, watu wapato laki 4 wanaamua mustakabali wa Tanganyika ambao ni milioni 43.

Ni kwa mtazamo huu, CCM wanacheza karata ya hasara, hatari nay a kusikitisha.

Pamoja na BMK-CCM kukosa uhalali, nia ya CCM kuwadhalilisha, kuwatusi na kuwakashifu Watanganyika inaeleza sababu za msingi za Watanganyika kutetea nchi na utaifa wao.

majadiliano yanaonekana kuendeshwa kwa hila, ubabe na maguvu, CCM watambue muungano unaelekea kuvunjika muda mfupi sana ujao.

Hakuna mahali duniani dola ilishinda nguvu ya umma.

Nguvu ya Umma ya Watanganyika ni kubwa mara 30 ya wazanzibar.

Watanganyika wataingia mitaani kudai haki zao kwa nguvu.
Wazanzibar watabeba gharama nzito sana wakati unaoelekea kutimia

Watanganyika hawatavuka bahari, watawalazimisha wznz wavuke bahari kwa miguu na baiskeli.

Hali inapoelekea ni mbaya sana kwa wznz.

Zawadi wanazoahidiwa wazaznibar ni tamu kama big G, maana ipo siku zitakuwa shubiri midomoni mwao. Siku si nyingi, watazitema wakitoka mate, jasho napengine zaidi ya hayo

Hatari hii haionekani, inakuja kimya kama dhoruba. Inatisha na inasikitisha.

Tusemezane

Duru tulionya, tukaitwa wenye chuki tena kwa kingledha '' hater''
Leo wznz wameambiwa mchana, hadharani na bayana. Majibu ya hoja zako ni ngumi, hawana jibu lingine.

Huu ni mwanzo tu.
 
DURU MAREJEO

Tuliyasema tukaambiwa wapiga ramli na probability
Leo karata ya sitta kutumbukiza dini inaanza kuingia nyongo.

cc. Kuna analysts na watu wa probability- MwanaDiwani

CCM NA SAMWEL SITTA HOFU YAWATAWALA

SASA WATUMBUKIZA KARATA YA DINI

MWISHO WA KARATA HIYO YAWEZA KUTOKEA MAAFA

Hofu inazidi kwa CCM na Mwenyekiti Sitta wa BMK-CCM. Jitihada kutoa zawadi kwa wazanzibar zinakwama. Jana kamati zimeshauri kuwe na makamu wawili, Rais wa znz akiwa ni makamu pia wa JMT.

Hoja ilikumbana na hoja ya wazanzibar waliosema yaraka inayoandaliwa haitakanyaga ardhi ya Zanzibar.
Tayari makundi tuliyoeleza yanaanza kutoa makucha. Hadi Ijumaa ya wiki ijayo,uwezekano bunge la CCM likavunjika kwa wenyewe kupigana madongo.Tunasisitiza kwa vile UKAWA hawapo, vita ni ya familia.

Kutokana na hofu hiyo inayoonyesha na wajumbe wa CCM 'wakorofi''Sitta amekuja na mbinu ya kuwatumia viongozi wa dini. Viongozi wametoa tamko kama wajumbe wanaowakilisha taasisi za dini kundi 201

Kwanza, kuna tatizo la viongozi. Wamejichagua kama wakristo na Waislam, wakiacha makundi mengine yenye uwakilishi wa imani

Pili,hawawezi kutoa misimamo tofauti na ule wa taasisi zilizowatuma zenye mitazamo tofauti na yao

Viongoziwa dini wamekuja na hoja zisizoeleweka, kwa umakini unaweza kuona wameagizwa kwa 'motisha'

Tamko lao linafuatia tamko la Sitta na Nape ikiwa ni kuashiria hali ni tete na hivyo msaada wa viongozi wa kiroho unatakiwa.

Moja ya utetezi wao ni madai kuwa wao ni viongozi wa kiroho na wameapa kwa mwenyezi mungu na kwa katiba.
Wanachotaka tuamini ni kuwa, wakiwa viongozi wa dini ni watu wema na kauli zao ni njema

Duru tunajiuliza kama viongozi wa dini ni watu wema sana mbele ya mungu, iweje tunasikia makanisani wakichapana makonde kwa kutaka madaraka au kula sadaka?

Iweje tunasikia masheikh wakishikana wizi wa sadaka na misaada?

Iweje tunasikia makasisi na maustadhi wakikamatwa ugoni?

Iweje hawa viongozi hawaogopi makanisa na misikiti yao, leo watuambie mungu amehamia Dodoma mjengoni kwa Sitta na hivyo wao ni watu wema sana na tuwasikilize?

Iweje hawakutoa tamko kuhusu kuvurugwa kwa mchakato kuanzia mwanzo na kwamba haki ilikiukwa hata kwenye kanuni?

Iweje hawakukemea kitendo cha prof Ghai kupewa siku nzima ya kuzungumza na Warioba na tume yake waliozungumza na mamilioni ya Watanzania wapewe saa moja? Mbona hatukuwasikia wakikemea uhalifu huo leo wanataka tuwasikilize!!

Hawa viongozi ni sehemu ya mpango wa kisiasa. Madai yao dhidi ya UKAWA ni ya kupangwa na kutumwa.

Tatizo linalojitokeza ni kuhusu kuchanganya dini na siasa. CCM inawapa nguvu kwa mambo ya kisiasa.

Kesho zitazuka hoja zinazogusa imani,watatofautiana na haieleweki CCM watamtafuta nani asaidie kuwasuluhisha.

Hili jambo ni la hatari kwasababu nchi inapogawanyika kwa imani na kutoka katika secular state inatisha na kusikitisha.

Karata hii ya Samwel Sitta ni hatari sana kwa taifa.

CCM lazima wajiulize je, wana magari ya zimamoto ya kutosha siku moto utakapowaka?

CCM hawaoni ya jirani zetu au barani Afrika, na wanafikiria nini kuhusu mustakabali wa taifa hili.

Tusemezane
 
Last edited by a moderator:
DURU : MAREJEO

Ndugu yetu alituita ''kila mtu ni politicala analyst'' na tunajenga hoja kwa probabaility.

Well, hakuna probability tuliyokwenda nje ya ukweli. Kwasasa sisi wengine tunaangalia movie katika big screen.
Tulikuwepo wakati wana shoot, ndio maana tunamuuliza ndugu huyu,je bado anaamini katika probability za duru za siasas hapa jamvini?


Uzuri wa siasa za Tanzania, kila mtu ni political analyst!

Karibuni kwenye political ground zero ili mzionje siasa zilizo halisi na siyo hizi za kudonoa kupitia keyboard/keypad kwenye mitandao.

Kujenga hoja katika mlengo wa siasa za probability zenye matokeo ya aina mbili hakuhitaji kisima kirefu cha fikra!
 
Wana duru na jamvi,

Kwasasa uzi huu utakuwa endelevu kwa majadiliano tukifanyia rejea za kila kilichosemwa.
Tunasema kwa uhakika kabisa, kila lililosemwa, ima limetokea, linatokea au litatokea.

Hakuna mshindi wa bahati nasibu mara 20 atakayepewa benefit of doubt ya probability.

Tunafahamu si kila mmoja anapenda ukweli au kupendezwa na ukweli.
Duru hatutasita kuuleza umma nini kinatokea kwa mtazamo wetu bila kumuonea awaye au kumhurumia.

Duru hatufungamani na vyama vya siasa ispokuwa tunafungamana na UTAIFA.


Ni kwa mantiki hii, uzi utabaki kuwa rejea.

Kwasasa tunaandaa uzi mpya '' Hatima ya BMLK-CCM na Muungano

Tutajadili kwa undani
1. Hamkani si shwari kwa wazanzibar- heri nusu ya shari kuliko shari kamili
2. Jinsi wznz walivyoshindwa kujitetea hadharani
3. Uongo na madai ya wznz yalivyoyeyuka kama pande la barafu
4. Kwanini S3 ni muhimu sana kwao kuliko Tanganyika
5. Jinsi walivyotia kidonda chumvi na matokeo ya kelele zao
6. Hatima na hadhi yao ndani ya muungano
7. Anguko la znz kutoka ubabe hadi omba omba
8. Tanganyika itakvyozinduka kwa kishindo ikisaidiwa na Wazanzibar
9. Mwisho wa wznz kutoa kiongozi ndani ya JMT
10. JK anavyoisambaratisha CCM, kuwaacha wznz njia panda

Tutakuwa na mabandiko 4 mfululizo yakijadili mada hizo hapo juu.

Bandiko la kwanza litakuwa hewani Asubuhi ya alhamisi 18 204

TUSEMEZANE
 
Mwalimu , JK aliwakwepa UKAWA kwa trick.
Hakuwa amepanga kukutana na wapinzani, lakini pia hakuwa tayari kukutana na UKAWA kwasababu alitaka mahali pa kutokea.

Ndipo njia ya udanganyifu ikifanyika kutumia kituo cha Demokrasia ambacho mwenyekiti ni Cheyo.
Cheyo, Hamad Rashid, Mrema, Mapalala, Dovutwa n.k. wapo bungeni hna hivyo hakukuwa na issue ya kuzungumza na JK

Alichokifanya JK ni kuwaweka hao vibaraka ili watumike kama mpini.
Tuliwaonya UKAWA hapa jamvini, tukiwauliza ushirika na hao walioko bungeni umeanzaje?

Kama kawaida ya UKAWA, walidhani JK ni mwema kwao bila kujua anachezea akili zao kila siku.
Wamekwenda, vibaraka wakatumika kuwavuruga UKAWA na issue ikatoka kwa JK na kuwa ugomvi miongoni mwa TCD

Hata tangazo na debe la mazungumzo anayelisimamia ni Cheyo.
UKAWA tuliwaambia kabla ya mazungumzo hapa jamvini.
1. Hao wapinzani walioko bungeni wanakwenda kuonana na JK kwa sababu zipi?
2.Lini JK amekuwa mwema kwa UKAWA zaidi ya chama chake?
3. Kwanini bunge halisitishwi kupishamajadiliano?
4. Lini UKAWA wamefanya majadiliano na JK wakafanikiwa?
5. JK alipowavuruga wazee wa tume, lipi UKAWA walitegemea tofauti?
6. Wamejifunza nini kutokana na majadiliano ya siku za nyuma?

Maswali haya walipewa ili kuwafungua vichwa. Inashangaza wakaingia kichwa kichwa wakijua kabisa JK na serikali yake hawana nia wala kusudio la katiba mpya.

Leo Cheyo amepewa rungu anawaponda UKAWA, JK na CCM wakiwa wamejifungua kitanzi.

Hawa viongozi wa UKAWA kuna nyakati huwa najiuliza kama kweli wanajua michezo ya kisiasa.
Wamechezewa sana JK na wala hawaonekani kujifunza.

Huo ndio hasa mwanzo wa nyuzi hii inayohusu Juisi ya maembe. Wamekwenda wamekunya na nadhani walilewa.

Mkuu Nguruvi3 nakusoma vema katika hili...

Ndio maana nikauliza pia UKAWA walipaswa kufanya nini katika mazingira ya mtego kama haya? Obviously isingekuwa rahisi kwa wao kufikisha hoja na ajenda zao mbele ya JK wakati msemaji mkuu wa TCD ni Bwana Mapesa ambaye anahudhuria BMK. UKAWA walipaswa kususia kikao hicho na kuwaachia kina Cheyo na Mrema TCD yao?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 nakusoma vema katika hili...

Ndio maana nikauliza pia UKAWA walipaswa kufanya nini katika mazingira ya mtego kama haya? Obviously isingekuwa rahisi kwa wao kufikisha hoja na ajenda zao mbele ya JK wakati msemaji mkuu wa TCD ni Bwana Mapesa ambaye anahudhuria BMK. UKAWA walipaswa kususia kikao hicho na kuwaachia kina Cheyo na Mrema TCD yao?
UKAWA walipaswa kusema, wao wana tatizo na suala la bunge, hivyo wana haki ya kukutana na upande mwingine(ingawa hata kukutana ilikuwa wazo bovu) bila TCD.

Tuliwaonya mapema sana, haiwezekani JK aende kuongea na TCD na kudai maoni ya wananchi yaheshimiwe, halafu siku tatu baadaye aende kuwadhalilisha wazee. Haaminiki na hivyo walipaswa kulijua hilo mapema.
Pili, walipaswa kujua agenda na si kwenda kwa agenda isiyojulikani.

Hili la maandamano nalo pia tuliwasihi mapema sana. Tutaweka bandiko watu waone.
UKAWA sijui kama wanafahamu mbinu za kisiasa hata kama wanafahamu wanataka nini.
 
BAADA YA RASIMU YA CCM YA MAFICHONI

MTEGO ULIOWEKWA NA BUNGE LA SAMWEL SITTA

UKAWA WAKIBABIKA TU, WATAIPA RASIMU YA MAFICHONI UHALALI

HUKUMU YA KUBENEA NI MADA NZURI KUJADILI KULIKO RASIMU STTA


Tutajadili leo hii
 
BAADA YA RASIMU YA CCM YA MAFICHONI

MTEGO ULIOWEKWA NA BUNGE LA SAMWEL SITTA

UKAWA WAKIBABIKA TU, WATAIPA RASIMU YA MAFICHONI UHALALI

HUKUMU YA KUBENEA NI MADA NZURI KUJADILI KULIKO RASIMU STTA


Tutajadili leo hii

..hivi kwanini suala hili limegeuzwa kuwa la Ukawa peke yao?

..mimi nadhani suala hili ni LETU. yaani hapa ni suala la katiba ya WANANCHI vs katiba ya CCM.

..kama ni kubabaika ni sisi wananchi ambao tunatakiwa tusibabaika na tujue tunachukua hatua gani.

cc Mchambuzi, Nyamizi
 
Last edited by a moderator:
..hivi kwanini suala hili limegeuzwa kuwa la Ukawa peke yao?

..mimi nadhani suala hili ni LETU. yaani hapa ni suala la katiba ya WANANCHI vs katiba ya CCM.

..kama ni kubabaika ni sisi wananchi ambao tunatakiwa tusibabaika na tujue tunachukua hatua gani.

cc Mchambuzi, Nyamizi
JokaKuu,kwa mtazamo wangu si kwamba tumewaachia UKAWA isipokuwa wao wana nafasi kubwa sana japo kuzuia huu usanii unaoendelea Dodoma.Kumbuka sisi "the common wananchi"kwa sasa hatuna nafasi mpaka pale hiyo Rasimu yao watakapoileta kwetu kwa kupigiwa kura (???).
Kinachofanywa na kina Nguruvi3 Mchambuzi na wengine wengi hapa jamvini ni kujaribu kuwatahadharisha wasije wakafanya makosa yaliyowahi kufanyika huko nyuma.Kumbuka japo Mh.Rais alisema anakutana na TCD,lakini ukweli alikuwa anakutana na UKAWA (rejea uchambuzi wa Nguruvi3).Kwahiyo hawa wanabaki kuwa ni tumaini pekee tulilonalo kwa sasa.
Believe me,kuna mengi sana tunajifunza hapa ambayo na sisi kama tukiwaeleza wengine wasio na access na jamvi hili itasaidia sana wengi kuelewa kwa nini watu wanapinga uhuni unaoendelea Dodoma.
 
Last edited by a moderator:
JokaKuu,kwa mtazamo wangu si kwamba tumewaachia UKAWA isipokuwa wao wana nafasi kubwa sana japo kuzuia huu usanii unaoendelea Dodoma.Kumbuka sisi "the common wananchi"kwa sasa hatuna nafasi mpaka pale hiyo Rasimu yao watakapoileta kwetu kwa kupigiwa kura (???).
Kinachofanywa na kina Nguruvi3 Mchambuzi na wengine wengi hapa jamvini ni kujaribu kuwatahadharisha wasije wakafanya makosa yaliyowahi kufanyika huko nyuma.Kumbuka japo Mh.Rais alisema anakutana na TCD,lakini ukweli alikuwa anakutana na UKAWA (rejea uchambuzi wa Nguruvi3).Kwahiyo hawa wanabaki kuwa ni tumaini pekee tulilonalo kwa sasa.
Believe me,kuna mengi sana tunajifunza hapa ambayo na sisi kama tukiwaeleza wengine wasio na access na jamvi hili itasaidia sana wengi kuelewa kwa nini watu wanapinga uhuni unaoendelea Dodoma.
Nyamizi

Ahsante sana kwa kueleza dhana kama nilivyokuwa nimetarajia kuijibu.

Nisitize tu kuwa sisi wananchi ndio wenye mchakato, kwa bahati mbaya sauti zetu hazina platform kutokana na mfumo wa nchi.

Tulikataa mchakato kuanzia mapema, hatukusikilizwa kwasababu hatupo katika ''circle'' ya decision. Maamuzi waliyofanya UKAWA iwe kwenda kuonana na Raisau kususia bunge kwa sehemu kubwa sana ylikuwa na athari kwa matokeo yaliyopo na kwetu sote

Mfano, tunaeleza nini watarajie kwa kusoma mitazamo tofauti. Ndivyo tulivyowaambia hawakupaswa kwenda kuonana na Rais kwa kupitia TCD kwasababu huo ni mtego.
Leo bunge la sitta linaendelea kwasababu wapo akina Cheyo, Mrema na Rashid n.k kwa kigezo kuwa wapinzani wamo. Je, hao wasiofika hata 10 wana impact hiyo, vipi kama tuta ignore UKAWA?

Kwa ufupi, wao wana platform kubwa zaidi kuliko sisi, hilo linabaki kuwa ukweli.
Leo wakiamua kurudi bungeni kila kitu kinapata uhalali hata kama wananchi tutakataa

Sehemu kubwa ya dhana yaku address UKAWA Nyamizi kaifafanua vema sana.

Hilo haliondoi ukweli kuwa mchakato ni wananchi na sisi lazima tuwe mstari wa mbele. Swali ni kuwa tuna platform hasa kwa jinsi tunavyowajua Watanzania? Mfumo wetu unatupa nafasi hiyo? Tumebailika kufikia hatua hiyo?
 
JokaKuu,kwa mtazamo wangu si kwamba tumewaachia UKAWA isipokuwa wao wana nafasi kubwa sana japo kuzuia huu usanii unaoendelea Dodoma.Kumbuka sisi "the common wananchi"kwa sasa hatuna nafasi mpaka pale hiyo Rasimu yao watakapoileta kwetu kwa kupigiwa kura (???).
Kinachofanywa na kina Nguruvi3 Mchambuzi na wengine wengi hapa jamvini ni kujaribu kuwatahadharisha wasije wakafanya makosa yaliyowahi kufanyika huko nyuma.Kumbuka japo Mh.Rais alisema anakutana na TCD,lakini ukweli alikuwa anakutana na UKAWA (rejea uchambuzi wa Nguruvi3).Kwahiyo hawa wanabaki kuwa ni tumaini pekee tulilonalo kwa sasa.
Believe me,kuna mengi sana tunajifunza hapa ambayo na sisi kama tukiwaeleza wengine wasio na access na jamvi hili itasaidia sana wengi kuelewa kwa nini watu wanapinga uhuni unaoendelea Dodoma.

..kinachofanyika hapa ni kuwabeza UKAWA tu. Hebu soma kichwa cha habari cha thread hii.

..kwa mtizamo wangu UKAWA wamechukua maamuzi sahihi kwa kuzingatia mazingira wanayofanyia kazi.

..siyo kwamba UKAWA hawatimizi wajibu wao, wanatimiza. tatizo ni kwamba wale ambao UKAWA wana-deal nao hawatimizi wajibu wao.

..kama UKAWA wamekwenda Ikulu na wakakubaliana na Raisi kwamba mchakato uahirishwe, halafu Samuel Sitta, Dr.Asha Rose Migiro, AG Werema, wana-act as if nothing has happened, kwanini mnafikiri anayepaswa kubeba lawama ni UKAWA?

..halafu hivi mmeona ni sahihi kwa John Cheyo, na Fahmi Dovutwa, kutenda wanavyotenda baada ya kikao cha Ikulu? Je, ni wapi hawa wamekewa?

..binafsi nadhani tunaelekeza lawama mahali kusiko, and by doing that we are playing right into the hands za wale wasiotaka mabadiliko.

..CCM wanataka suala la katiba lionekane ni jambo la mizaha na kipuuzi. Wanataka tujadili nani alikunya juice, nani alikula pipi za ikulu, na mambo mengine kama hayo.

..kwa maoni yangu tungetumia vizuri nafasi yetu, siyo kwa kuwalaumu UKAWA, bali kuwalaumu wale wote wanaopinga mabadiliko ya katiba. tena kuna wengine[Nape Nnauye, Abdulrahman Kinana] wanakwenda kwenye mikutano ya kisiasa na kuwahadaa wananchi kwamba Katiba haina uhusiano wowote ule na maisha yao ya kila siku.


cc Nguruvi3, Pasco, Mchambuzi
 
Unapojaribu kudai haki kwa njia za kistaarabu dhidi ya mfumo kandamizi lazima ufike mahali ukubali kwamba uwezekano wa mafanikio ni mdogo....unless uamue kutumia njia nyingine ya kuingia msituni. UKAWA wamefanya sehemu yao kadiri ya uwezo wao katika mazingira haya dhidi ya mfumo usiotaka mabadiliko, mfumo unaotumia njia za ujanja, hadaa, undumilakuwili kusema neno moja leo na kesho kutenda vingine.

JK alipiga geresha tu alipoamua kuwaita TCD (sio UKAWA) ikulu na kuwakubalia kwamba mchakato usitishwe mpaka baada ya uchaguzi...Halafu upande wa pili anampa Sitta go ahead aendeleze mchakato ili rasimu ikamilike kabla ya deadline ya octoba 4.

Tukubali tu kwamba kazi iliyobaki sasa ni ya sisi wananchi na sio vyama vya upinzani au ukawa sababu wao ngwe yao wameshamaliza. Ni sisi wananchi kwa pamoja tuseme HAPANA!!
 
Wanaduru
Kwanza niwashukuru wote wanaochangia mada. Tutakosea kama hatutakubali mgongano wa mawazo.Ni jambo lenye afya kwasababu sote tunajifunza kutoka upande mwingine, tunajenga nyumba moja tukiwa na uchungu kwa yaliyotokea na yanayoendelea.

Mkuu JokaKuu ni mwanajamvi mwenye heshima sana, hakika hakuna alichokiandika kinachotia shaka zaidi ya kuongeza thamani ya michango yake mingi tunayoithamini sana na tunamuomba aendelee kutushauri, kosoa na kuelekeza.

Suala la wananchi kuwa mstari wa mbele tumelijibu,ni wajibu wetu.
Kwa mfumo wetu wananchi hawana platform na role ya UKAWA haiwezi kupuuzwa.

Leo tukiitisha mkutano, watakuja watu 4, watatu ndugu zangu na mmoja pengine JokaKuu, Nyamizi, Mwalimu au mwingine.

Tofauti nasi, UKAWA wanaweza kuita maelfu, wakasikilizwa watawala (siyo viongozi)

Role hiyo ndiyo imekuwa ikiwapeleka Ikulu kila mara, tukiwa hatuwezi kusogelea geti. Hivyo UKAWA ni sehemu muhimu sana.

Kwa wanaduru, mtakumbuka vema tulivyowashuri UKAWA kuanzia mwanzo, tukionyesha mbinu za watawala, kutoa scoop tulizobahatika kukumbana nazo.

Ni vema tukakumbuka UKAWA ni binadamu,wana mapungufu yao, kuwasema si kuwasimanga ni kuwapa nafasi ya kujitazama.
CCM ni sikio la kufa,kuwasema ni kuwaonea

Labda tutoe muhtasari wa nini tulichosema na kwanini tunasema Juisi ya maembe.

Mchakato ulipoanza, duru tulimkemea mwenyekiti wa Chadema kwa kumsifia JK kuanzisha mchakato.
Mchakato ilikuwa hoja ya wapinzani,haiwezekani JK akawa mwema asubuhi moja. Hakuna mahali ilani ya CCM au sera imezungumzia katiba, ushujaa wa kumwamini upo wapi?

1.Upinzani by then wakaenda bungeni kupinga mswada. Wakaitwa Ikulu, picha, za zikionyesha wanakunya juisi. Walipotoka wakawa kimya, ghafla tukawasikia wakisema makubaliano ambayo wanananchi hawakutufahamishwa yamekiukwa

2.Wakarudi Ikulu tena, tukiwatahadharisha kuhusu JK na undumila kuwili.
Mambo yaliyoendelea ni ya wajumbe201 wa CCM,mwiba mkali

3.Tulitahadharisha Upinzani , CCM itatumia wingi. Njia muafaka si kuficha bali kuwa na kura ya wazi. Leo Sitta anatumia kura ya siri waliyoitaka kuhadaa umma. Je, hili halikuwa kosa na hatukuwa sahihi kulieleza?

4.Tukawambia UKAWA, hakuna sababu za kuendelea na mchakato kama CCM hawataki kujadili rasimu ya Warioba. Wakakubali kuandika kanuni. Tena Walisema wananchi hawatawaelewa awakisusia BMK.
Leo wametoka baada ya kuona tulichowaambia ni ukweli.
Kuna kosa gani hapo kuwasema wametumia public trust na kudanganywa?

5.Tukawaambia kuwa majadiliano yakishindika na CCM basi wasimtegemee JK,yeye ni mwenyekiti, iweje majadiliano na CCM yashindikane kama hayana ridhaa yake? Ni kweli yakashindika umma ukiwa na subira.Tulikosea wapi kusema

6.Tukawambia waanze kuahamasisha umma kwa kutumia platform wakati Sitta anaendelea kuandika katiba yake. Wakakaa kimya upotoshaji ukiendelea.
Leo wanaandaa maandamano tuliyowaambia miezi 4 iliyopita.
Kosa letu lipo wapi?
7.Tukawaambia haiwezekani JK achague tume na kisha kuitusi katika TV na JK,akawa mwema kwao. Walikuwa wanachezwa shere kumtegemea JK,.
Leo JK yupo kimya mambo yakipelekwa kwa ujinga na upuuzi.
Kosa letu lipo wapi kuwatahadharisha?

8.Tukasema UKAWA wasimtegemee JK,alisema katiba mpya na S3 ni baada ya yeye kuondoka madarakani. Alimaanisha S2 ndizo zitadumu, leo rasimu ya Chenge na Sitta ina akisi tulichosema tena si kwa hilo bali kwa kila hatua wanayofanya sasa hivi.
Rejea nyuzi za ''kiwewe cha kuzinduka Tanganyika'' na kwanini Sitta aaminiwe.
9.Tukawaambia Sitta si mtu wa kumwamini tukiweka historia yake wazi.
UKAWA wakampa ueneyekiti.
Leo tunaona udikteta uliokubuhu.
Kosa letu lipo wapi kuwatahadharisha UKAWA?

10. Tukawamabia hawana sababu za kukutana na JK kwasababu hizi;

  1. Mara ya kwanza alikiuka makubaliano ya mswada wa sheria
  2. Akakiuka mswada wa pili uliokuwa na matatizo
  3. Akawananga tume ya maoni mbele ya umma mchana wa jua kali
  4. Akasema CCM wajiandae na S3 halafu akakana kauli bungeni
  5. Kasema S3 hadi aondoke madarakani(kumbuka ni mapendekezo ya tume)

11.UKAWA wakapuuza yote. Tukawambia hawana sababu ya kukutana na JK,mara zote kumekuwa na matokeo hasi.
Tuliwaonya kuwa JK na CCM watwatumia akina Mrema, Cheyo na Mapala kuhalalisha upinzani.
Hivyo wasikubali kukutana na JK kama TCD.
UKAWA wakapuuza, je makubaliano yao na JK leo yana maana yoyote?

12.Na ndipo sasa tulipo, tunawaambia tena kama wanataka kulisaidia taifa wakisaidiwa na wananchi, njia muafaka ni kutozungumzia rasimu ya Sitta na Chenge. Hilo ndilo lilikuwa kusudio letu kwa mada iliyoanzisha mjadala huo


Inaendelea...
 
Inaendelea..

Maana yetu ilikuwa njema kabisa ingawa inaweza kuwa na tafsiri tofauti.

Baada ya hayo machache miongoni mwa mabandiko mengi sana, tunapenda kusema heading haikuwa imedhamiria kuwadhalilisha, bali kama wake up call wakati wanakwenda kujadiliana au wanatafuta kuungwa mkono kwa masilahi mapana ya taifa.

Neno Juisi ya maembe lilikusudiwa kueleza kuwa zile picha zilizoonekana wakinywa Juisi na kundoka bila mafanikio zililenga kuwadhalilisha, kwamba hoja zao ni maji ya matunda.

Heading halina maana nyingine zaidi ya wake up call.
Hivyo hilo lisiwe na shaka, UKAWA wamejaribu kiasi chao tunawpongeza, hilo haliondoi ukweli kuwa lazima tuwaambie, tuwaelekeze,tuwashauri na tuwakemee pale wanapokwenda ndivyo sivyo.

Heading ya uzi inabaki kuwa na uzani tukijua mazungumzo juu ya glasi za juisi hayajazaa matunda tarajiwa.

Inaweza kuwa ''sensational'' baada ya kurudia, kudurusu na kutathmini, tunabaki kuamini kwa dhati heading ni sahihi kwa wakati muafaka kutoa ujumbe uliokusudiwa.

Lakini pia kwa wale wanaoona wamekuwa ''offended' tunawapa pole kwa usumbufu usiokusudiwa

Tunachoshauri ni watu kusoma contents za mada kwa kutambua heading ni neno au maneno machache, ujumbe wake unaweza kuwa na maana zaidi ya hapo.

Mwisho, tunadhani njia tunayotumia ndio sehemu ya kuunga mkono jitihada kama wananchi.

JF ndio platform yetu tusioweza kuitisha mikutano tukasikilizwa.

Swali linabaki, kama hatutatumia platform hii, tutaungaje mkono harakati kwa namna nyingine nzuri zaidi?

Je, kuunga mkono ni kushangilia tu bila kuonyesha njia au kukosoa?

Tusemezane
 
Mkuu Nguruvi3 ninashukuru kwa kutuletea muhtasari mwanana kabisa.
Ni kweli mfumo unamnyima mwananchi jukwaa sahihi la kufanya maamuzi, lakini anayelea upuuzi huu ni sisi wenyewe wananchi, aidha kwa ujinga wetu au kwa kurubuniwa na CCM au UKAWA, ndio maana tumezoea kauli za HATUWEZI, zao la unga wa ndele wa CCM na UKAWA!

Kwanini UKAWA ndio iwe platform pekee ya mwananchi, ipi ni nafasi ya mwananchi wa kawaida katika kufanya maamuzi ndani ya Ukawa? Je, inatofauti yoyote kubwa na ile ya CCM? Hata kama ipo ni ya paka mweusi na mweupe, si ya kuku na paka! Wote ni nyau tu, na wewe Mkuu Nguruvi3 ni shahidi kupitia uliyoorodhesha. Werevu mlishaonya na mkaonesha njia lakini bado wakashupaza shingo zao, je leo si kufuru kuendelea kudai sisi wananchi hatuwezi? Ni lini tulikaa kujadili letu mbali na yanayozuliwa na wanasiasa? Lini tulifikia ukomo wa tafakari yetu na kuona HAIWEZEKANI? Je, si unga wa ndele tuliolishwa na CCM na UKAWA? Nalo ndilo kaburi letu. Ni nani kasema haiwezekani kwa mwananchi kusema HAPANA ila tu kwa kupitia Ukawa au CCM?

Haya ndio madhara ya 'Top-Down Approach' haitatufikisha popote milele! Amini nakuambia Mkuu wangu, maelfu ya watu katika mikutano ya Ukawa, si kwa sababu maelfu hayo yanachakuifikishia Ukawa katika kupigania masilahi yetu, ila tu ni kwa kuwa wao ni aidha mashabiki au wanachama wa vyama husika, kinachowapeleka ni utiifu wao tu kwa hisia zao juu ya wanasiasa.

Mwanakijiji alishahoji kuwa kuna haraka gani ya kuiharakisha Katiba. Tujipange, tugeukie Bottom-Up. Ila maendeleo ni hesabu ndefu, si miujiza inayootwa mchana na wanasiasa wetu. Tukitambua hilo, nina hakika 100% Bottom-up itatufikisha mahali pazuri.
Harakati yoyote itakayoanzishwa huku waendeshaji wake wanahangaika kubaki au kuingia ikulu, ni KIINI MACHO KWA UMMA. Wanachofanya CCM na UKAWA ni mazingaumbwe!
Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,

..nakubaliana na maudhui mazima ya hoja zake, isipokuwa ktk approach unayoipendekeza.

..ninachoamini mimi ni kwamba UKAWA walipaswa ku-build a case ya kile ambacho baadaye watataka wananchi wawaunge mkono.

..lazima UKAWA wawe na ushahidi, tena usio na shaka, kwamba wamechukua hatua zote za kujaribu kutafuta maridhiano katika suala hili, ikiwemo kuzungumza na Raisi, na hayo yote yameshindikana.

cc Nyamizi, Mwalimu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Nguruvi3 ninashukuru kwa kutuletea muhtasari mwanana kabisa.
Ni kweli mfumo unamnyima mwananchi jukwaa sahihi la kufanya maamuzi, lakini anayelea upuuzi huu ni sisi wenyewe wananchi, aidha kwa ujinga wetu au kwa kurubuniwa na CCM au UKAWA, ndio maana tumezoea kauli za HATUWEZI, zao la unga wa ndele wa CCM na UKAWA!

Kwanini UKAWA ndio iwe platform pekee ya mwananchi, ipi ni nafasi ya mwananchi wa kawaida katika kufanya maamuzi ndani ya Ukawa? Je, inatofauti yoyote kubwa na ile ya CCM? Hata kama ipo ni ya paka mweusi na mweupe, si ya kuku na paka! Wote ni nyau tu, na wewe Mkuu Nguruvi3 ni shahidi kupitia uliyoorodhesha. Werevu mlishaonya na mkaonesha njia lakini bado wakashupaza shingo zao, je leo si kufuru kuendelea kudai sisi wananchi hatuwezi? Ni lini tulikaa kujadili letu mbali na yanayozuliwa na wanasiasa? Lini tulifikia ukomo wa tafakari yetu na kuona HAIWEZEKANI? Je, si unga wa ndele tuliolishwa na CCM na UKAWA? Nalo ndilo kaburi letu. Ni nani kasema haiwezekani kwa mwananchi kusema HAPANA ila tu kwa kupitia Ukawa au CCM?

Haya ndio madhara ya 'Top-Down Approach' haitatufikisha popote milele! Amini nakuambia Mkuu wangu, maelfu ya watu katika mikutano ya Ukawa, si kwa sababu maelfu hayo yanachakuifikishia Ukawa katika kupigania masilahi yetu, ila tu ni kwa kuwa wao ni aidha mashabiki au wanachama wa vyama husika, kinachowapeleka ni utiifu wao tu kwa hisia zao juu ya wanasiasa.

Mwanakijiji alishahoji kuwa kuna haraka gani ya kuiharakisha Katiba. Tujipange, tugeukie Bottom-Up. Ila maendeleo ni hesabu ndefu, si miujiza inayootwa mchana na wanasiasa wetu. Tukitambua hilo, nina hakika 100% Bottom-up itatufikisha mahali pazuri.
Harakati yoyote itakayoanzishwa huku waendeshaji wake wanahangaika kubaki au kuingia ikulu, ni KIINI MACHO KWA UMMA. Wanachofanya CCM na UKAWA ni mazingaumbwe!
Anaita sasa!
Ahsante, niseme kuwa suala la wananchi kushiriki katika maamuzi yetu ni muhimu sana.
Kwa bahati mbaya Watanzania ni watu wa ajabu sana, wanaweza kudanganywa kila siku na wala hawashtuki wala kujiuliza.

Unakutana na Mtanzania anakwenda Muhimbili Hospitali. Una msalimia, ''habari za siku, mambo?' Jibu analotoa ni ''mambo poa tu habari ni njema sana''. Utamuuliza tena mbona unaelekea Muhimbili? Jibu atakalotoa ''nina matatizo ya figo hazifanyi kazi''

Hapa ndipo utajiuliza, ile habari njema na mambo poa ilihusu nini? Mtu anaumwa figo halafu nasema mambo poa, habari njema.

Na hali hiyo inaendelea hadi mitaani, tunajua taifa lina matatizo makubwa katika utawala, uchumi, siasa na hata utamaduni.

Watu wakiulizwa wanasema ''mambo poa, mambo tambarare'' hakuna anayesimama kusema hapana! tuna tatizo.

Na viongozi wanachukua hiyo kama advantage ya kutugawa.
Ndipo wanatumia taasisi zao kama CCM

JokaKuu , wananchi wanaweza. Tuna mfano wa mswada wa kwanza kukataliwa na znz tena mbele ya Sitta ambapo kwa kiasi kikubwa sana ilibadilisha mwlekeo wa mchakato.

Tatizo letu linabaki pale pale kwamba hatujaweza kuwaamsha watu ili watambue nchi hii ni yao na wao wana upper hand.

Hilo ni tatizo kwakweli, na nadhani Jingala Falasafa ameongelea mada tuliowahi kujadili na akina @Mchambuzi na JingalaFasalafa kuwa approach yetu lazima ianze bottom up na si top dowm.

JingalaFalsafa, wananchi wanaohudhuria mikutano si wote wanajua nini kinaendelea.
Hata hivyo nguvu ya umma bado inabaki kuwa na nguvu na ndio maana CCM wanaiutumia sana.

Leo wamemaliza uhuni pale Dodoma, matarajio yao ni kutumia watu hao hao tunaosema hawajui kuhalalisha uhuni.

Hivyo katika 1000 wapo wachache watakaoelewa na hao ndio target kwa maana kuwa ipo siku minority itakuwa majority.

JokaKuu, nadhani sote tupo katika meli moja, nasi kwa upande wetu tuendelee kuwaamsha wananchi kupitia platform kama hii.

Katika kutoa elimu kwa umma, ni muhimu kueleza matatizo ya pande husika, kama ni CCM au UKAWA n.k. ili wananchi waelewe kuwa hatima yao ipo mikononi mwao. Ndio maana tumeeleza hatua tulizokuwa nazo za kutahadharisha kuhusu mchakato kuanzia mwanzo.

Katika mbandiko yetu hakuna jambo tuliloandika baada ya matokeo, yote tuliyaeleza in advance tena kukiwa na wiki kama si miezi kabla ya tatizo. UKAWA nao kama CCM anavyosema JingalaLalsafa, haionekani kama approach yao ilikuwa nzuri.

Bado kuba nafasi nzuri sana hasa baada ya CCM kufanya uhuni na kujichanganya.

Tunataka namna ya kuvunja mwiko wa CCM wa kutumia mbinu za kilaghai ili tuwe kama Zambia na Kenya, kwamba sasa wananchi wanachagua anayeafaa na si mazoea. Hapo ndipo nasema UKAWA hata kama si jawabu lakini inaweza kuwa mpini wa kuvunja uti wa mgongo wa ngamia. Na fursa hii imejitokeza tena, sijui kama wataweza ku-connect na wananchi ili kuwaondoa wahuni madarakani.

Hata hivyo tuendelee kuisadia nchi hii kwasababu sote ni wadau na waathirika wa mfumo huu uliotufikisha hapa miaka 50.
Tuendelee kuwaamsha wananchi wajitambue
 
Nguruvi3,

..mazingira ya siasa za Tanzania ni magumu kwelikweli.

..kwanza kuna uthubutu wa kikatili wa CCM.

..halafu kuna wananchi ambao wamezoea kufanyiwa ukatili na wamekubaliana na hali hiyo.

..kwa hiyo vyama vya upinzani vina kibarua kikubwa kwelikweli kupambana ktk mazingira hayo.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom