Ukiachana na Jenister muhagama kuna huyu George Mkuchika

Ukiachana na Jenister muhagama kuna huyu George Mkuchika

MAKANGEMBUZI

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2020
Posts
2,670
Reaction score
7,655
Aisee tangu niko shule ya msingi Juhudi iliyopo ukonga magereza nasoma mpaka nimemaliza elimu uchwara za Bongo na kuingia mtaani hadi sasa nikiwa na miaka 27 hawa watu majina yao ni mheshimiwa waziri bla bla bla.....yani kwa lugha nyepesi wao ni mawaziri tu.

Kuna watu hapa Tanzania keki ya taifa (asali ) wanailamba sana wanaishi kama wapo peponi.

Anyway....

Naomba kujua na kuelimishwa wana nini vya maana na upekee(unique) upi haswa katika watanzania milioni 60 au wana nini cha maana kuzidi wanachama wa CCM milioni 15 na ushee kama wanavyojinadi.

Naomba kujuzwa.

NB:wale wakubwa wa JF kiumri mababu,mabibi,wababa na wamama shikamoooni.
 
Back
Top Bottom