Robot la Matope
JF-Expert Member
- Apr 10, 2015
- 8,174
- 16,794
Unavyoandika kama vile hauna ubongo!! Hivi unaishi wapi?Emergency zinatakiwa ziwe sehemu ya plan. Nataka kuagiza gari leo la $4000 ambayo ni sawa na 10m. Najua ushuru na malipo yote hadi litoke ni 10m. Hivyo nahitaji 20m kuhakikisha gari linafika.
Kabla sijaagiza hili gari lazima niwe na 20m kwenye account. Lakini pia lazima niangalie mzunguko wangu wa fedha. Je nina mzunguko wa kutosha kumili gari (Mafuta, service)? Je nina akiba ya emergency nikipata tatizo au gharama zikiongezeka. Haya yote ni muhimu kuyaangalia kwa kina kabla hujaagiza hiyo gari. So naweza kuji ongezea muda hadi nifikishe 25m kwenye account ndo niagize gari hilo.
Usalama ni mkubwa sana, moja ya masharti ya kufungua Bonded Warehous e inabidi eneo liwe limewekewa fence, CCTV camera. Na endapo itatokea wizi ukapeleka malalamiko kwa mhusika akagoma kuwajibika ukienda kuripoti Tasac/TRA hiyo Bonded Warehouse inafungiwa na mmiliki anafunguliwa Kesi ya uhujumu uchumi maana wizi umefanyika kwa bidhaa ambayo ilikuwa chini ya uangalizi.Usalama unakuaje?? Hawachelewi kukubadirishia spare parts
Unajua kitu kinaitwa Uplifting ?!!! Unaweza ukaja na mzigo wako unamenunua bei ya kishikaji huko nje jamaa wakapinga invoice yako na wakaingia kwenye vitabu vyao na kuja na bei zao Yaani unashangaa mzigo umekuwa na gharama (Kodi zaidi ya mara Kumi) bei uliyonunulia..., Nadhani wewe ni mgeni nchini.... Anyway hii ya bonded warehouse ni kutibu symptoms badala ya kutibu tatizo... Na tatizo ni Kodi za Ajabu Ajabu...Ushauri wako ni mzuri unaweza kusaidia vijana wakurupukaji kupunguza hasara.
Yaani, kwa nini uagize gari au mzigo wakati huna uhakika wa pesa ya kutolea?
Hizi ni akili za kimaskini. Mtu mwenye akili za namna hii hawezi kupata maendeleo kamwe. Ni kama wale wanao nunua magari halafu wanauza kwa bei ya hasara baada ya miezi michache. Nikutokuwa na mipango thabiti. Huu ujinga sijui utaisha lini.
Dah!! Umetisha mkuu!! TRA wanapaswa kukulipa posho kwani hii ni elimu kwa wateja wao.Usalama ni mkubwa sana, moja ya masharti ya kufungua Bonded Warehous e inabidi eneo liwe limewekewa fence, CCTV camera. Na endapo itatokea wizi ukapeleka malalamiko kwa mhusika akagoma kuwajibika ukienda kuripoti Tasac/TRA hiyo Bonded Warehouse inafungiwa na mmiliki anafunguliwa Kesi ya uhujumu uchumi maana wizi umefanyika kwa bidhaa ambayo ilikuwa chini ya uangalizi.
Pia hakuna mmiliki anayelea wizi kwenye Bonded Warehouse maana kawekeza pesa ndefu( moja ya sharti la kupewa leseni lazima uwe na mtaji usiopungua 500million) na sheria kali zinambana akifanya kosa anaingia kwenye uhujumu uchumi.
Pitia link hii ya TRA usome vigezo vya kuanzisha Custom Bonded Warehouse
Asante sana kwa andiko zuri na la kuelimisha; je mzigo unaweza kuwekwa kwenye bonded warehouse kwa muda gani. Kuna time limit?Kama umeagiza gari au bidhaa na ikawa imefika Kwenye Bandari na wakati huo pesa ya ushuru umepungukiwa,kukwama au hukuwa na taarifa sahihi za ushuru na makadirio ya kodi yamekuja zaidi ya kiwango ulichopanga njia sahihi ni kumwambia wakala wa Forodha(Clearing Agent) afanye maombi (TRA) ya kupeleka gari au mzigo kwenye Bonded Warehouse.
Bonded Warehouse ni ghala au sehemu ambayo mizigo inayosafirishwa nje au iliyotoka nje ya nchi inatunzwa inaposubiri kulipiwa ushuru.Bonded Warehouse zipo ambazo zinamilikiwa na serikali au watu binafsi zipo mikoa yenye bandari na mipakani.
Endapo umeagiza gari au bidhaa yoyote na umekwama pesa kabla au baada ya mzigo kushuka bandarini usipate pressure. Inatakiwa umwambie Clearing Agent atafute Bonded Warehouse kwa ajili ya kuweka gari au mzigo wakikubali kuna nafasi, inabidi ajaze fomu ya TRA kuomba kupeleka mzigo Bonded Warehouse baada ya kupeleka mzigo Bonded utakapo kuwa sawa utalipa kodi hata baada ya mwaka na mzigo wako utatoka.
Faida za kutumia Bonded Warehouses
1. Gharama za kutunza mzigo (storage charges) zipo Chini na zina chajiwa kwa mwezi. Mfano gari ndogo kwa mwezi bei ni usd 80, wakati bandarini kutunza kwa mwezi bei ni kubwa sana na huchajiwa kwa siku na ukubwa (CBM) unaweza ukapewa bill ya usd 1000
2.Inaondoa mzigo kuwekwa kwenye list ya overstayed good na kuja kupigwa mnada. Mzigo ukikaa sana bandarini unaingia kwenye overstayed goods na mmiliki asipo utoa unapigwa mnada. Kwenye Bonded Warehouse mzigo unaweza kutunza zaidi ya mwaka
3. Mmiliki wa mzigo ni rahisi kwenda kuangalia mzigo au gari yake ikiwa Bonded Warehouse. Gari ikiwa bandarini mmiliki hawezi kuingia kuona gari au mzigo, ila ukiweka bonded unaomba kuingia Warehouse na kuona mzigo ila huwezi kutoa. Pia akitaka auze ni rahisi kumuonyesha mteja gari au bidhaa ikiwa Bonded tofauti na ikiwa bandarini inabidi auze kwa kutumia picha za mzigo ulikopakiwa na documents za mzigo.
Bonded Warehouse ina faida kwa waagizaji wa bidhaa na magari, inaepusha mizigo kuuzwa kwa mnada. Kama ulifanikiwa kuagiza gari ya usd 3000 (CIF) bora upeleke Bonded Warehouse ukalipe usd100 per month kuliko kuiacha bandarini ukaja kupewa storage charges za usd 3500 na ushuru unakusubiri. Hapo gari inaingia kwenye mnada unaingia hasara
Hakuna time limitAsante sana kwa andiko zuri na la kuelimisha; je mzigo unaweza kuwekwa kwenye bonded warehouse kwa muda gani. Kuna time limit?
Hapana; inategemea na timing tu. Mambo mengi hubadilika na wakatiKuagiza gari na hauna hela ya kulipa hizo expenses hizo ndo tunaita harakati za pimbi
Sio kila kitu ni kukurupuka mzee, au wewe hujawahi kukumbwa na dharura?? Sio poa kabisa unaweza kulala masikini ukaamka tajiri au the vice versaUshauri wako ni mzuri unaweza kusaidia vijana wakurupukaji kupunguza hasara.
Yaani, kwa nini uagize gari au mzigo wakati huna uhakika wa pesa ya kutolea?
Hizi ni akili za kimaskini. Mtu mwenye akili za namna hii hawezi kupata maendeleo kamwe. Ni kama wale wanao nunua magari halafu wanauza kwa bei ya hasara baada ya miezi michache. Nikutokuwa na mipango thabiti. Huu ujinga sijui utaisha lini.
Sawa,Kama umeagiza gari au bidhaa na ikawa imefika Kwenye Bandari na wakati huo pesa ya ushuru umepungukiwa,kukwama au hukuwa na taarifa sahihi za ushuru na makadirio ya kodi yamekuja zaidi ya kiwango ulichopanga njia sahihi ni kumwambia wakala wa Forodha(Clearing Agent) afanye maombi (TRA) ya kupeleka gari au mzigo kwenye Bonded Warehouse.
Bonded Warehouse ni ghala au sehemu ambayo mizigo inayosafirishwa nje au iliyotoka nje ya nchi inatunzwa inaposubiri kulipiwa ushuru.Bonded Warehouse zipo ambazo zinamilikiwa na serikali au watu binafsi zipo mikoa yenye bandari na mipakani.
Endapo umeagiza gari au bidhaa yoyote na umekwama pesa kabla au baada ya mzigo kushuka bandarini usipate pressure. Inatakiwa umwambie Clearing Agent atafute Bonded Warehouse kwa ajili ya kuweka gari au mzigo wakikubali kuna nafasi, inabidi ajaze fomu ya TRA kuomba kupeleka mzigo Bonded Warehouse baada ya kupeleka mzigo Bonded utakapo kuwa sawa utalipa kodi hata baada ya mwaka na mzigo wako utatoka.
Faida za kutumia Bonded Warehouses
1. Gharama za kutunza mzigo (storage charges) zipo Chini na zina chajiwa kwa mwezi. Mfano gari ndogo kwa mwezi bei ni usd 80, wakati bandarini kutunza kwa mwezi bei ni kubwa sana na huchajiwa kwa siku na ukubwa (CBM) unaweza ukapewa bill ya usd 1000
2.Inaondoa mzigo kuwekwa kwenye list ya overstayed good na kuja kupigwa mnada. Mzigo ukikaa sana bandarini unaingia kwenye overstayed goods na mmiliki asipo utoa unapigwa mnada. Kwenye Bonded Warehouse mzigo unaweza kutunza zaidi ya mwaka
3. Mmiliki wa mzigo ni rahisi kwenda kuangalia mzigo au gari yake ikiwa Bonded Warehouse. Gari ikiwa bandarini mmiliki hawezi kuingia kuona gari au mzigo, ila ukiweka bonded unaomba kuingia Warehouse na kuona mzigo ila huwezi kutoa. Pia akitaka auze ni rahisi kumuonyesha mteja gari au bidhaa ikiwa Bonded tofauti na ikiwa bandarini inabidi auze kwa kutumia picha za mzigo ulikopakiwa na documents za mzigo.
Bonded Warehouse ina faida kwa waagizaji wa bidhaa na magari, inaepusha mizigo kuuzwa kwa mnada. Kama ulifanikiwa kuagiza gari ya usd 3000 (CIF) bora upeleke Bonded Warehouse ukalipe usd100 per month kuliko kuiacha bandarini ukaja kupewa storage charges za usd 3500 na ushuru unakusubiri. Hapo gari inaingia kwenye mnada unaingia hasara
TRA hawasumbui mkuu, ni wepesi wa wakala wako wa forodha (Clearing Agent) kujaza fomu na kuomba nafasi kwenye Bonded Warehouse unayotakaSawa,
Ila Sasa unakuta mpaka TRA wakuruhusu hilo lazima uwe uneeakatia kadhaa. Kila mtu pale anakula Kwa urefu wa kamba yake kama alivyoruhusu Maza.
Aisee,TRA hawasumbui mkuu, ni wepesi wa wakala wako wa forodha (Clearing Agent) kujaza fomu na kuomba nafasi kwenye Bonded Warehouse unayotaka
Huyo jamaa uliyemnukuu ni kiazi sana, yaani ameandika tu utafikiri Hana kichwa...Unajua kitu kinaitwa Uplifting ?!!! Unaweza ukaja na mzigo wako unamenunua bei ya kishikaji huko nje jamaa wakapinga invoice yako na wakaingia kwenye vitabu vyao na kuja na bei zao Yaani unashangaa mzigo umekuwa na gharama (Kodi zaidi ya mara Kumi) bei uliyonunulia..., Nadhani wewe ni mgeni nchini.... Anyway hii ya bonded warehouse ni kutibu symptoms badala ya kutibu tatizo... Na tatizo ni Kodi za Ajabu Ajabu...
Iwapo tunapunguza Utoaji Huduma (kubinafsisha); kwanini Kodi hazipungui? Je, tunaongeza kumbana Mwananchi ili kutoa (huduma) gani?
Kodi ni muhimu sana ili kufadhili shughuli za serikali, huduma kwa umma kama vile barabara na mashule, Usalama wa Jamii, Afya na Mengineyo. Sasa kama hata hayo kuanzia Elimu (Mikopo na Shule Binafsi); Afya tuna BIMA ya Afya na kulipia Private; Kuhakikisha wafanyakazi wanalipwa ujira stahiki...www.jamiiforums.com
Hakuna limit ya kukaa, kukataliwa hakupo labda uwe ujakamilisha vitu au mzigo ukawa na mashaka. Mzigo ukiwa Bonded bado unakuwa upo chini ya TRA kwaiyo hapo kinachofanyika ni kubadili eneo la kutunza mizigo kutoka Bandarini kwenda Bonded Warehouse ambapo gharama za kutunza mizigo (storage charges) zipo chini.Aisee,
Na huko Bonded maximum inaweza kukaa muda gani?
Je kwenye kuomba TRA naweza kukataliwa pia?