Ukiagiza bidhaa au gari na ukakwama ushuru ni vyema baada ya gari kufika ukapeleka Bonded Warehouse.

Ukiagiza bidhaa au gari na ukakwama ushuru ni vyema baada ya gari kufika ukapeleka Bonded Warehouse.

Emergency zinatakiwa ziwe sehemu ya plan. Nataka kuagiza gari leo la $4000 ambayo ni sawa na 10m. Najua ushuru na malipo yote hadi litoke ni 10m. Hivyo nahitaji 20m kuhakikisha gari linafika.

Kabla sijaagiza hili gari lazima niwe na 20m kwenye account. Lakini pia lazima niangalie mzunguko wangu wa fedha. Je nina mzunguko wa kutosha kumili gari (Mafuta, service)? Je nina akiba ya emergency nikipata tatizo au gharama zikiongezeka. Haya yote ni muhimu kuyaangalia kwa kina kabla hujaagiza hiyo gari. So naweza kuji ongezea muda hadi nifikishe 25m kwenye account ndo niagize gari hilo.
Unavyoandika kama vile hauna ubongo!! Hivi unaishi wapi?
 
Usalama unakuaje?? Hawachelewi kukubadirishia spare parts
Usalama ni mkubwa sana, moja ya masharti ya kufungua Bonded Warehous e inabidi eneo liwe limewekewa fence, CCTV camera. Na endapo itatokea wizi ukapeleka malalamiko kwa mhusika akagoma kuwajibika ukienda kuripoti Tasac/TRA hiyo Bonded Warehouse inafungiwa na mmiliki anafunguliwa Kesi ya uhujumu uchumi maana wizi umefanyika kwa bidhaa ambayo ilikuwa chini ya uangalizi.

Pia hakuna mmiliki anayelea wizi kwenye Bonded Warehouse maana kawekeza pesa ndefu( moja ya sharti la kupewa leseni lazima uwe na mtaji usiopungua 500million) na sheria kali zinambana akifanya kosa anaingia kwenye uhujumu uchumi.

Pitia link hii ya TRA usome vigezo vya kuanzisha Custom Bonded Warehouse
 
Ushauri wako ni mzuri unaweza kusaidia vijana wakurupukaji kupunguza hasara.

Yaani, kwa nini uagize gari au mzigo wakati huna uhakika wa pesa ya kutolea?

Hizi ni akili za kimaskini. Mtu mwenye akili za namna hii hawezi kupata maendeleo kamwe. Ni kama wale wanao nunua magari halafu wanauza kwa bei ya hasara baada ya miezi michache. Nikutokuwa na mipango thabiti. Huu ujinga sijui utaisha lini.
Unajua kitu kinaitwa Uplifting ?!!! Unaweza ukaja na mzigo wako unamenunua bei ya kishikaji huko nje jamaa wakapinga invoice yako na wakaingia kwenye vitabu vyao na kuja na bei zao Yaani unashangaa mzigo umekuwa na gharama (Kodi zaidi ya mara Kumi) bei uliyonunulia..., Nadhani wewe ni mgeni nchini.... Anyway hii ya bonded warehouse ni kutibu symptoms badala ya kutibu tatizo... Na tatizo ni Kodi za Ajabu Ajabu...

 
Usalama ni mkubwa sana, moja ya masharti ya kufungua Bonded Warehous e inabidi eneo liwe limewekewa fence, CCTV camera. Na endapo itatokea wizi ukapeleka malalamiko kwa mhusika akagoma kuwajibika ukienda kuripoti Tasac/TRA hiyo Bonded Warehouse inafungiwa na mmiliki anafunguliwa Kesi ya uhujumu uchumi maana wizi umefanyika kwa bidhaa ambayo ilikuwa chini ya uangalizi.

Pia hakuna mmiliki anayelea wizi kwenye Bonded Warehouse maana kawekeza pesa ndefu( moja ya sharti la kupewa leseni lazima uwe na mtaji usiopungua 500million) na sheria kali zinambana akifanya kosa anaingia kwenye uhujumu uchumi.

Pitia link hii ya TRA usome vigezo vya kuanzisha Custom Bonded Warehouse
Dah!! Umetisha mkuu!! TRA wanapaswa kukulipa posho kwani hii ni elimu kwa wateja wao.
 
Kama umeagiza gari au bidhaa na ikawa imefika Kwenye Bandari na wakati huo pesa ya ushuru umepungukiwa,kukwama au hukuwa na taarifa sahihi za ushuru na makadirio ya kodi yamekuja zaidi ya kiwango ulichopanga njia sahihi ni kumwambia wakala wa Forodha(Clearing Agent) afanye maombi (TRA) ya kupeleka gari au mzigo kwenye Bonded Warehouse.

Bonded Warehouse ni ghala au sehemu ambayo mizigo inayosafirishwa nje au iliyotoka nje ya nchi inatunzwa inaposubiri kulipiwa ushuru.Bonded Warehouse zipo ambazo zinamilikiwa na serikali au watu binafsi zipo mikoa yenye bandari na mipakani.

Endapo umeagiza gari au bidhaa yoyote na umekwama pesa kabla au baada ya mzigo kushuka bandarini usipate pressure. Inatakiwa umwambie Clearing Agent atafute Bonded Warehouse kwa ajili ya kuweka gari au mzigo wakikubali kuna nafasi, inabidi ajaze fomu ya TRA kuomba kupeleka mzigo Bonded Warehouse baada ya kupeleka mzigo Bonded utakapo kuwa sawa utalipa kodi hata baada ya mwaka na mzigo wako utatoka.

Faida za kutumia Bonded Warehouses
1. Gharama za kutunza mzigo (storage charges) zipo Chini na zina chajiwa kwa mwezi. Mfano gari ndogo kwa mwezi bei ni usd 80, wakati bandarini kutunza kwa mwezi bei ni kubwa sana na huchajiwa kwa siku na ukubwa (CBM) unaweza ukapewa bill ya usd 1000

2.Inaondoa mzigo kuwekwa kwenye list ya overstayed good na kuja kupigwa mnada. Mzigo ukikaa sana bandarini unaingia kwenye overstayed goods na mmiliki asipo utoa unapigwa mnada. Kwenye Bonded Warehouse mzigo unaweza kutunza zaidi ya mwaka

3. Mmiliki wa mzigo ni rahisi kwenda kuangalia mzigo au gari yake ikiwa Bonded Warehouse. Gari ikiwa bandarini mmiliki hawezi kuingia kuona gari au mzigo, ila ukiweka bonded unaomba kuingia Warehouse na kuona mzigo ila huwezi kutoa. Pia akitaka auze ni rahisi kumuonyesha mteja gari au bidhaa ikiwa Bonded tofauti na ikiwa bandarini inabidi auze kwa kutumia picha za mzigo ulikopakiwa na documents za mzigo.

Bonded Warehouse ina faida kwa waagizaji wa bidhaa na magari, inaepusha mizigo kuuzwa kwa mnada. Kama ulifanikiwa kuagiza gari ya usd 3000 (CIF) bora upeleke Bonded Warehouse ukalipe usd100 per month kuliko kuiacha bandarini ukaja kupewa storage charges za usd 3500 na ushuru unakusubiri. Hapo gari inaingia kwenye mnada unaingia hasara
Asante sana kwa andiko zuri na la kuelimisha; je mzigo unaweza kuwekwa kwenye bonded warehouse kwa muda gani. Kuna time limit?
 
Kuagiza gari na hauna hela ya kulipa hizo expenses hizo ndo tunaita harakati za pimbi
 
Kuna bonded warehouse moja mitaa ya Akachube, ina gari zipo pale nahisi zaidi ya miaka 4 huoni hata zikisogezwa wala kufutwa vumbi...

Zile hata zikipigwa mnada si ajabu zikauzwa bei kubwa sana kufidia deni...
 
Ushauri wako ni mzuri unaweza kusaidia vijana wakurupukaji kupunguza hasara.

Yaani, kwa nini uagize gari au mzigo wakati huna uhakika wa pesa ya kutolea?

Hizi ni akili za kimaskini. Mtu mwenye akili za namna hii hawezi kupata maendeleo kamwe. Ni kama wale wanao nunua magari halafu wanauza kwa bei ya hasara baada ya miezi michache. Nikutokuwa na mipango thabiti. Huu ujinga sijui utaisha lini.
Sio kila kitu ni kukurupuka mzee, au wewe hujawahi kukumbwa na dharura?? Sio poa kabisa unaweza kulala masikini ukaamka tajiri au the vice versa

Jana ulikuwa na milioni 100 ya kucheba after days ukajikuta hauna hata 10 na deni la negative 30+ huko

Dharura inaweza kukuchachafya ukaona dunia chungu ilhali kila siku ulikuwa unapanda juu ya meza na kurusha maburungutu kwa kadamnasi
 
Kama umeagiza gari au bidhaa na ikawa imefika Kwenye Bandari na wakati huo pesa ya ushuru umepungukiwa,kukwama au hukuwa na taarifa sahihi za ushuru na makadirio ya kodi yamekuja zaidi ya kiwango ulichopanga njia sahihi ni kumwambia wakala wa Forodha(Clearing Agent) afanye maombi (TRA) ya kupeleka gari au mzigo kwenye Bonded Warehouse.

Bonded Warehouse ni ghala au sehemu ambayo mizigo inayosafirishwa nje au iliyotoka nje ya nchi inatunzwa inaposubiri kulipiwa ushuru.Bonded Warehouse zipo ambazo zinamilikiwa na serikali au watu binafsi zipo mikoa yenye bandari na mipakani.

Endapo umeagiza gari au bidhaa yoyote na umekwama pesa kabla au baada ya mzigo kushuka bandarini usipate pressure. Inatakiwa umwambie Clearing Agent atafute Bonded Warehouse kwa ajili ya kuweka gari au mzigo wakikubali kuna nafasi, inabidi ajaze fomu ya TRA kuomba kupeleka mzigo Bonded Warehouse baada ya kupeleka mzigo Bonded utakapo kuwa sawa utalipa kodi hata baada ya mwaka na mzigo wako utatoka.

Faida za kutumia Bonded Warehouses
1. Gharama za kutunza mzigo (storage charges) zipo Chini na zina chajiwa kwa mwezi. Mfano gari ndogo kwa mwezi bei ni usd 80, wakati bandarini kutunza kwa mwezi bei ni kubwa sana na huchajiwa kwa siku na ukubwa (CBM) unaweza ukapewa bill ya usd 1000

2.Inaondoa mzigo kuwekwa kwenye list ya overstayed good na kuja kupigwa mnada. Mzigo ukikaa sana bandarini unaingia kwenye overstayed goods na mmiliki asipo utoa unapigwa mnada. Kwenye Bonded Warehouse mzigo unaweza kutunza zaidi ya mwaka

3. Mmiliki wa mzigo ni rahisi kwenda kuangalia mzigo au gari yake ikiwa Bonded Warehouse. Gari ikiwa bandarini mmiliki hawezi kuingia kuona gari au mzigo, ila ukiweka bonded unaomba kuingia Warehouse na kuona mzigo ila huwezi kutoa. Pia akitaka auze ni rahisi kumuonyesha mteja gari au bidhaa ikiwa Bonded tofauti na ikiwa bandarini inabidi auze kwa kutumia picha za mzigo ulikopakiwa na documents za mzigo.

Bonded Warehouse ina faida kwa waagizaji wa bidhaa na magari, inaepusha mizigo kuuzwa kwa mnada. Kama ulifanikiwa kuagiza gari ya usd 3000 (CIF) bora upeleke Bonded Warehouse ukalipe usd100 per month kuliko kuiacha bandarini ukaja kupewa storage charges za usd 3500 na ushuru unakusubiri. Hapo gari inaingia kwenye mnada unaingia hasara
Sawa,
Ila Sasa unakuta mpaka TRA wakuruhusu hilo lazima uwe uneeakatia kadhaa. Kila mtu pale anakula Kwa urefu wa kamba yake kama alivyoruhusu Maza.
 
Sawa,
Ila Sasa unakuta mpaka TRA wakuruhusu hilo lazima uwe uneeakatia kadhaa. Kila mtu pale anakula Kwa urefu wa kamba yake kama alivyoruhusu Maza.
TRA hawasumbui mkuu, ni wepesi wa wakala wako wa forodha (Clearing Agent) kujaza fomu na kuomba nafasi kwenye Bonded Warehouse unayotaka
 
TRA hawasumbui mkuu, ni wepesi wa wakala wako wa forodha (Clearing Agent) kujaza fomu na kuomba nafasi kwenye Bonded Warehouse unayotaka
Aisee,
Na huko Bonded maximum inaweza kukaa muda gani?
Je kwenye kuomba TRA naweza kukataliwa pia?
 
Unajua kitu kinaitwa Uplifting ?!!! Unaweza ukaja na mzigo wako unamenunua bei ya kishikaji huko nje jamaa wakapinga invoice yako na wakaingia kwenye vitabu vyao na kuja na bei zao Yaani unashangaa mzigo umekuwa na gharama (Kodi zaidi ya mara Kumi) bei uliyonunulia..., Nadhani wewe ni mgeni nchini.... Anyway hii ya bonded warehouse ni kutibu symptoms badala ya kutibu tatizo... Na tatizo ni Kodi za Ajabu Ajabu...

Huyo jamaa uliyemnukuu ni kiazi sana, yaani ameandika tu utafikiri Hana kichwa...

Bandiko lake limejikita kuwalaumu vijana ambao ni wahanga wa mfumo mbovu wa Kodi pasipo hata kuangalia chanzo Cha wao kuonekana kama wamekurupuka.

SI ajabu huyo utakuta ni Mmoja ya wafanyakazi wanaohusika na mambo ya forodha huko bandarini na ni mnufaika WA mfumo kandamizi WA Kodi.
 
Aisee,
Na huko Bonded maximum inaweza kukaa muda gani?
Je kwenye kuomba TRA naweza kukataliwa pia?
Hakuna limit ya kukaa, kukataliwa hakupo labda uwe ujakamilisha vitu au mzigo ukawa na mashaka. Mzigo ukiwa Bonded bado unakuwa upo chini ya TRA kwaiyo hapo kinachofanyika ni kubadili eneo la kutunza mizigo kutoka Bandarini kwenda Bonded Warehouse ambapo gharama za kutunza mizigo (storage charges) zipo chini.

Kwenye kila Bonded Warehouse kuna ofisi rasmi za TRA.
 
Back
Top Bottom