Ukiambiwa kuna viwanja vya bure uchague tu sehemu ya kujenga na kuishi kati ya Vikindu, Kibaha, Chanika na Bagamoyo, utachagua kujenga wapi?

Ukiambiwa kuna viwanja vya bure uchague tu sehemu ya kujenga na kuishi kati ya Vikindu, Kibaha, Chanika na Bagamoyo, utachagua kujenga wapi?

Kama mimi binafsi huwa napenda kulinganisha maeneo husika na kuona fursa zilizopo ili kuchagua sehemu sahihi ya kuishi.

Ni muhimu pia kuzingatia mambo kama miundombinu, huduma za umma, elimu, na fursa

Hata hivyo, naweza kukusaidia kwa kukupa taarifa kuhusu maeneo hayo ili uweze kufanya uamuzi wako mwenyewe.

1. Vikindu: Vikindu ni sehemu iliyoko katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Inapatikana umbali wa takribani kilomita 45 kutoka Dar es Salaam. Maeneo ya karibu na pwani yanaweza kuwa na vivutio vya kipekee, lakini umbali kutoka Dar es Salaam unaweza kuwa changamoto ikiwa unahitaji kufanya shughuli nyingi jijini.

2. Kibaha: Kibaha ni mji ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Ni eneo linalokaribia Dar es Salaam, umbali wa takribani kilomita 35, na inaunganishwa vizuri na barabara kuu na njia ya reli. Kuishi Kibaha kunaweza kukuruhusu kufurahia urahisi wa kufika Dar es Salaam na huduma zake, wakati ukijivunia mazingira ya mji mdogo na utulivu.

3. Chanika: Chanika ni eneo lililopo katika Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Tanzania. Ni sehemu ya mijini zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine uliyotaja. Kuishi Chanika kunaweza kukupa faida ya kuwa karibu na vituo vya biashara, huduma za umma, na miundombinu ya jiji. Hata hivyo, unaweza kukabiliwa na msongamano wa trafiki na kelele za mji mkubwa.

4. Bagamoyo: Bagamoyo ni mji wa kihistoria ulioko katika Mkoa wa Pwani, takribani kilomita 75 kaskazini mwa Dar es Salaam, Tanzania. Mji huu una historia ndefu ya biashara na utamaduni na inaonekana kama sehemu ya urithi wa dunia na UNESCO.

Kuchagua kujenga na kuishi Bagamoyo kunaweza kuwa chaguo nzuri kwa sababu ya mambo yafuatayo:

Utamaduni na Historia, Mandhari ya Pwani,
Amani na Utulivu, Karibu na Dar es Salaam
You done everything my friend
 
Nitachagua Chanika, ni mojawapo ya maeneo yanayokua sana kutokana na ongezeko kubwa la idadi ya watu na makazi, itafika kipindi Chanika ataweza kuipiku Gongo la Mboto na kuwa na huduma zote muhimu

Kwa sasa wamefika mbali sana na uwepo wa barabara ya lami mpaka huko ni jambo ambalo limesababisha kuwa sehemu potential sana, maana maendeleo ni watu
Kumbe Chanika nako kumekucha, mimi nilifikiri kumedolola kiaina.
 
Hapo kama ni fursa ya kuchagua japo viwanja viwili basi nitachagua kwanza kibaha alafu cha pili kitakuwa cha bagamoyo.

Huko chanika na vikindu yake kuna wafaa waswahili kama kina kingwendu nk.
Hapo tuseme jibu lako limeegemea zaidi Kibaha, maana mfano ni kiwanja kimoja tu.
 
Hapo tuseme jibu lako limeegemea zaidi Kibaha, maana mfano ni kiwanja kimoja tu.
Nakushauri tena.

Njoo haraka sana Bagamoyo.

Ntarudi hapa mwezi wa kumi na mbili mwaka huu kukukumbusha kwanini unapaswa uje Bagamoyo.

Wenye pua za kunusa fursa wote wanaamia Bagamoyo.

Hata hao madon wa kibaha sasa wananunua mashamba na viwanja kwa fujo sana Bagamoyo.
 
Kama mimi binafsi huwa napenda kulinganisha maeneo husika na kuona fursa zilizopo ili kuchagua sehemu sahihi ya kuishi.

Ni muhimu pia kuzingatia mambo kama miundombinu, huduma za umma, elimu, na fursa

Hata hivyo, naweza kukusaidia kwa kukupa taarifa kuhusu maeneo hayo ili uweze kufanya uamuzi wako mwenyewe.

1. Vikindu: Vikindu ni sehemu iliyoko katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Inapatikana umbali wa takribani kilomita 45 kutoka Dar es Salaam. Maeneo ya karibu na pwani yanaweza kuwa na vivutio vya kipekee, lakini umbali kutoka Dar es Salaam unaweza kuwa changamoto ikiwa unahitaji kufanya shughuli nyingi jijini.

2. Kibaha: Kibaha ni mji ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Ni eneo linalokaribia Dar es Salaam, umbali wa takribani kilomita 35, na inaunganishwa vizuri na barabara kuu na njia ya reli. Kuishi Kibaha kunaweza kukuruhusu kufurahia urahisi wa kufika Dar es Salaam na huduma zake, wakati ukijivunia mazingira ya mji mdogo na utulivu.

3. Chanika: Chanika ni eneo lililopo katika Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Tanzania. Ni sehemu ya mijini zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine uliyotaja. Kuishi Chanika kunaweza kukupa faida ya kuwa karibu na vituo vya biashara, huduma za umma, na miundombinu ya jiji. Hata hivyo, unaweza kukabiliwa na msongamano wa trafiki na kelele za mji mkubwa.

4. Bagamoyo: Bagamoyo ni mji wa kihistoria ulioko katika Mkoa wa Pwani, takribani kilomita 75 kaskazini mwa Dar es Salaam, Tanzania. Mji huu una historia ndefu ya biashara na utamaduni na inaonekana kama sehemu ya urithi wa dunia na UNESCO.

Kuchagua kujenga na kuishi Bagamoyo kunaweza kuwa chaguo nzuri kwa sababu ya mambo yafuatayo:

Utamaduni na Historia, Mandhari ya Pwani,
Amani na Utulivu, Karibu na Dar es Salaam
Hongera uko vizuri sana.
 
Mkuu kama nlivyokwambia hapo juu kuwa nasikia tu kutoka kwa watu. Mimi sio mwenyeji wa huko na wala sina ndugu maeneo hayo, hivyo badala ya kuniuliza nilitarajia ungenipa maelezo ya kutosha ili kunithibitishia kuwa yale nilioyasikia hayana ukweli wowote.

Asante sana 🙏
Kalibu sana CHANIKA kuko njema kumbuka hata makamo wa Samia kwake ni CHANIKA brother
 
Hata mimi kura yangu naipeleka Kibaha,sababu ni miundo mbinu iliyopo na itakayokuwepo,Bandari kavu ya Kwala na muunganiko utakaokuwepo na Bandari ya Bagamoyo bila kusahau uanzishwaji wa viwanda vingi ndani ya Kibaha na Bagamoyo kwa ujumla
 
Vikindu ipo kilometa 23.6 kutoka katikati ya jiji Kariakoo na sio kilometa 45 ulizosema na ushahidi wa Google map ikionesha umbali toka Vikindu hadi Kariakoo nimekuwekea hapo, Ila kwa hapo 1.Chanika na 2.Kibaha ndizo sehemu nzuri
Nimetumia neno takribani maana yake ni makadilio.

Halafu sijui kama unafahamu unaweza toka vikindu mpaka kariakoo kwa njia tofauti, je umbali wa njia zote tatu ni 23.6km mpaka kariakoo?

Mandela road to kariakoo via Nyerere road.
Kilwa road to kariakoo
Same distance?
 
Niaje waungwana,

Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.

Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini?
Chanika inakua kwa kasi sana.

Huko kwengine bado bushi.
 
Nakushauri tena.

Njoo haraka sana Bagamoyo.

Ntarudi hapa mwezi wa kumi na mbili mwaka huu kukukumbusha kwanini unapaswa uje Bagamoyo.

Wenye pua za kunusa fursa wote wanaamia Bagamoyo.

Hata hao madon wa kibaha sasa wananunua mashamba na viwanja kwa fujo sana Bagamoyo.
Asante mkuu, acha niutafakari ushauri wako na kuufanyia kazi haraka iwezekanavyo.
 
Kalibu sana CHANIKA kuko njema kumbuka hata makamo wa Samia kwake ni CHANIKA brother
Ya hilo nalifahamu mkuu. Kabla ya kuchukua uamuzi nataka kwanza nifunge safari nije mimi mwenyewe kupaona. Wanasema kusadiki kwa toma ni kujionea.

Nina binam yangu amejenga na kuhamia huko, japo mimi binafsi sijawahi kuja kumtembelea kutokana hatuna mazoea kwa sana. But nitajitahidi siku 1 nimtembelee ili nijionee mwenyewe kile ulichoandika hapa. Asante sana
 
Hata mimi kura yangu naipeleka Kibaha,sababu ni miundo mbinu iliyopo na itakayokuwepo,Bandari kavu ya Kwala na muunganiko utakaokuwepo na Bandari ya Bagamoyo bila kusahau uanzishwaji wa viwanda vingi ndani ya Kibaha na Bagamoyo kwa ujumla
Wengi wame prefer kwa Kibaha, japo Bagamoyo na Chanika nayo si haba, zina watu wengi wanaozikubali.
 
Mimi bagamoyo na ukanda wake naona kama kumekaa kushoto hivi, yaani ni kama sehemu ya wachawi wachawi hivi! Kibaha nako kumekaa kimkoani mkoani hivi!
Chanika nayo imekaa kiswahili Swahili hivi, kwa ufupi mbagara ya baadae.
Walau Vikindu naweza kuweka boma langu!
wengi hawawez kuliona hilo
 
Back
Top Bottom