Ukiambiwa kuna viwanja vya bure uchague tu sehemu ya kujenga na kuishi kati ya Vikindu, Kibaha, Chanika na Bagamoyo, utachagua kujenga wapi?

Ukiambiwa kuna viwanja vya bure uchague tu sehemu ya kujenga na kuishi kati ya Vikindu, Kibaha, Chanika na Bagamoyo, utachagua kujenga wapi?

Mangi, huwezi kukimbia uswahili ukitaka kujenga miji ya waswahili. Sehemu yoyote iwe Pwani au Dar uswahili upo. Kila jamii Ina tabia zake uhwezi kuzkwepa. All in all sehemu yoyote Ile ndani ya Pwani au Ina thamani kuliko kishumun#du
Sijasema ukimbie maeneo ya waswahili, mimi nimesema maeneo yenye ngome za kiswahili sio za kukimbilia ovyo ovyo kwenda kujenga ili kuishi. Kwanini? Miji yenye ngome za kiswahili ina tabia ya kudumaa, kuzubaa na kubakia hivyo hivyo bila kubadilika.

Unajua maana ya ngome za waswahili?
Hayo ni maeneo yenye kuwatambulisha waswahili, kuloea, kufia, kuzikwa vizazi vyao. Haijarishi maisha yatabadilika vipi kuwazunguka au kuwakaribia, mswahili akiwa kwenye ngome yake atataka kukomaa hivyo hivyo na ukale wake, uvivu, majungu nk.
 
Vikindu ipo kilometa 23.6 kutoka katikati ya jiji Kariakoo na sio kilometa 45 ulizosema na ushahidi wa Google map ikionesha umbali toka Vikindu hadi Kariakoo nimekuwekea hapo, Ila kwa hapo 1.Chanika na 2.Kibaha ndizo sehemu nzuri
Inamaana Vikindu ni Klmr chache tu namna hii kutoka K'koo. Basi hii ilistahili kuwa ndani ya Dar es salaam kuliko Chanika.
 
Kwahiyo mkuu unaona Kibaha haikupaswa kulinganishwa na hayo maeneo mengi, inamaana hata Bagamoyo hauikubali mkuu?
makao makuu ya mkoa halaf unafananisha na vitongoj vyake kwel wametumia akili hao ? Vikindu na Bagamoyo zote zipo mkoa wa pwan ambazo zote makao makuu ni kibaha
 
Sijasema ukimbie maeneo ya waswahili, mimi nimesema maeneo yenye ngome za kiswahili sio za kukimbilia ovyo ovyo kwenda kujenga ili kuishi. Kwanini? Miji yenye ngome za kiswahili ina tabia ya kudumaa, kuzubaa na kubakia hivyo hivyo bila kubadilika.

Unajua maana ya ngome za waswahili?
Hayo ni maeneo yenye kuwatambulisha waswahili, kuloea, kufia, kuzikwa vizazi vyao. Haijarishi maisha yatabadilika vipi kuwazunguka au kuwakaribia, mswahili akiwa kwenye ngome yake atataka kukomaa hivyo hivyo na ukale wake, uvivu, majungu nk.
Ulichoandika kama kina ukweli fulani. Maana angalia Mw/nyamala, Mburahati, Kigogo, Buguruni nk hayo ni maeneo ya waswahili. Pamoja na kwamba maeneo hayo yapo katikati ya mji ambapo mtu unaweza kutembea kwa mguu kwenda K'koo, Posta nk, pia muingiliano wa watu mbali mbali kutoka maeneo tofauti ya nchi lakini maeneo yao yapo vilevile miaka nenda miaka rudi.
 
Kama mimi binafsi huwa napenda kulinganisha maeneo husika na kuona fursa zilizopo ili kuchagua sehemu sahihi ya kuishi.

Ni muhimu pia kuzingatia mambo kama miundombinu, huduma za umma, elimu, na fursa

Hata hivyo, naweza kukusaidia kwa kukupa taarifa kuhusu maeneo hayo ili uweze kufanya uamuzi wako mwenyewe.

1. Vikindu: Vikindu ni sehemu iliyoko katika Wilaya ya Mkuranga, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Inapatikana umbali wa takribani kilomita 45 kutoka Dar es Salaam. Maeneo ya karibu na pwani yanaweza kuwa na vivutio vya kipekee, lakini umbali kutoka Dar es Salaam unaweza kuwa changamoto ikiwa unahitaji kufanya shughuli nyingi jijini.

2. Kibaha: Kibaha ni mji ambao ni makao makuu ya Wilaya ya Kibaha, Mkoa wa Pwani, Tanzania. Ni eneo linalokaribia Dar es Salaam, umbali wa takribani kilomita 35, na inaunganishwa vizuri na barabara kuu na njia ya reli. Kuishi Kibaha kunaweza kukuruhusu kufurahia urahisi wa kufika Dar es Salaam na huduma zake, wakati ukijivunia mazingira ya mji mdogo na utulivu.

3. Chanika: Chanika ni eneo lililopo katika Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam, Tanzania. Ni sehemu ya mijini zaidi ikilinganishwa na maeneo mengine uliyotaja. Kuishi Chanika kunaweza kukupa faida ya kuwa karibu na vituo vya biashara, huduma za umma, na miundombinu ya jiji. Hata hivyo, unaweza kukabiliwa na msongamano wa trafiki na kelele za mji mkubwa.

4. Bagamoyo: Bagamoyo ni mji wa kihistoria ulioko katika Mkoa wa Pwani, takribani kilomita 75 kaskazini mwa Dar es Salaam, Tanzania. Mji huu una historia ndefu ya biashara na utamaduni na inaonekana kama sehemu ya urithi wa dunia na UNESCO.

Kuchagua kujenga na kuishi Bagamoyo kunaweza kuwa chaguo nzuri kwa sababu ya mambo yafuatayo:

Utamaduni na Historia, Mandhari ya Pwani,
Amani na Utulivu, Karibu na Dar es Salaam
Mkuu yaani vikindu ni mbali kuliko kibaha? Ukitokea kati kati ya Jiji , hebu nenda kafanye calculations upya aisee , unegesemea miundombinu sawa lakini c umbali mkuu
 
Niaje waungwana,

Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.

Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini?
Nani huyo anayegawa viwanjwa vya Bure ? Tupeane fursa hiyo mkuu
 
Je waweza fafanua zaidi, sababu ni nini hasa?
1. Bei ya viwanja ipo chini sana.

2. Gharama za ujenzi ni ndogo.

3. Mazingira ya kuishi na watu wa ina ile ile waliokuwa wanaishi nao Manzese, Mburahati, Kigogo nk wanasema ndege wafananao huruka pamoja.

Wengi ni wafanya biashara ndogo ndogo kama vile samaki, machungwa nk, hivyo watu wa maeneo hayo ndo wataweza kuzimudu bei za biashara zao nk.
 
1. Bei ya viwanja ipo chini sana.

2. Gharama za ujenzi ni ndogo.

3. Mazingira ya kuishi na watu wa ina ile ile waliokuwa wanaishi nao Manzese, Mburahati, Kigogo nk wanasema ndege wafananao huruka pamoja.

Wengi ni wafanya biashara ndogo ndogo kama vile samaki, machungwa nk, hivyo watu wa maeneo hayo ndo wataweza kuzimudu bei za biashara zao nk.
Du kumbe katika sehemu nilizotaja kuna maeneo uswahili ni wa kiwango cha juu namna hii.

Acha mtu asikilizie Kibaha kwanza.
 
Niaje waungwana,

Kama swali linavojieleza hapo juu, ukiambiwa uchague sehemu moja tu ya kujenga kwa ajili ya makazi kati ya Chanika, Kibaha, Vikindu na Bagamoyo ila kiwanja unapewa bure.

Ndugu muungwana hebu tuambie utachagua kujenga na kuishi wapi? Na kwanini?
Kibaha
 
Naiona Kibaha ikienda kuwa na maendeleo makubwa siku za usoni. Nimefuatilia kwa makini na kuliona hili kupitia wingi wa comment na sifa inazopewa wilaya hiyo ya mkoa wa Pwani.
Kibaha panafaa sana kwa makazi na kibiashara pameshakuwa na watu wengi sana siku hizi.
 
Back
Top Bottom