Ukienda ugenini Kuna vitoto vinapenda sana sifa

Ukienda ugenini Kuna vitoto vinapenda sana sifa

Acha makasiriko hao wanaosema sijui kumvunja mifupa ,sijui kumbinya tako wanaongea tu kunogesha story tu usiwachulie silias.

Kuhusu watoto kufanana kwa hiyo mtoto akiiba ni sawa kwa sababu watoto hawatakiwi kufanana?
Watoto wawezi kufanana lakini wanatakiwa watofautiane kwenye tabia njema na sio tabia mbovu.

Narudia tena mtoto kumparamia na kumbugudhi mtu mzima ni tabia mbovu na sio mchezo kama unavyo sema.

Binadamu yeyote anatakiwa afundishe kuwa na mipaka.
Hata ww wazazi wako wamekuzaa na kukulea lakini bado kuna mipaka ambayo huwezi kuivuka juu yao na ndio maana huwezi kuacha baba na mama yako wamelala chumbani ww ukaingia humo chumbani bila ruhusa yao.

Mtoto anatakiwa kujua kuwa tabia ya kumgasi mtu ni moja wapo ya tabia mbaya sana.

Kuhusu suala la mm kumkanya je ikiwa nitamkanya na bado asikome ni mfanyeje? maana ww umesema kumuadhibu mtoto ni ukatiri.
Wanaleta Uzungu Kwenye Malezi Ya Kiafrika Watavuna Wanachopanda.
 
Kuna kamoja mama ake aliponipa upenyo nilikaning'niniza juu huku nimeshika masikio, nilipokashusha kalitaka kupiga yowe nukakauliza nirudie Tena kalitikisa kichwa kuwa hakataki Tena Hilo zoezi [emoji41]
 
Fanya shambulizi la kimya kimya hakuna haja ya kushika fimbo.

Shika mkono vizuri kwenye msuli(hawezi kua na msuli) binya na dole gumba kwa nguvu kiasi utakutana na mfupa, kandamiza kama sekunde 10 hivi uone kama katarudia
Ha ha ha ha ha ha ha [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Fanya hivi wakati unakabeba beba kamata tako moja halafu ufanye kama unaliviringa kwenda kulia....
Kakifanya ng`a na wewe unafanya ng'a,watajua mnacheza ila lazma wakakape panado maana katalalamika siku nzima..
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Halafu huyo mtoto wala sio mtukutu ila yupo excited kumuona Anko wake ndio maana anampandia pandia kwa furaha ila kwa kua watu mmejazwa roho mbaya na ukatili hata furaha ya watoto mnaigeuza chuki,

Hii gender ya Kiume ingeteketea tu [emoji849]
Wewe nae mbona kama unajitoa ufahamu. Ina maana wewe hadi umri huo ulionao haujui tofauti ya mtoto asiye na adabu na mtoto mwenye furaha ya kuona mgeni?!

Mtoto anatakuwa kulelewa kwa mipaka. Mfano mimi huwezi kuta mtoto aliyekulia mikononi mwangu analilia simu ya mgeni wala kuigusa.

Hivi imetokea mgeni amekuja na simu yake ya gharama lets say iphone 14 pro max, halafu mtoto wako anaililia achezee gem, mara paaaah kaibamiza chini kioo kimevunjika, wewe kama mzazi utajionaje kwa mgeni?!
 
Mtoto anakutukanaje? Itakua umejiweka kihuni sana,
Mtu aliyekaa kiheshima hawezi kudharauliwa na mtoto hadi kufikia kutukanwa, duh!
Mmmmmmhmn wewe unaonekana unataka tu kubishana haujawahi kutana na watoto wenye malezi mabovu.
 
Wewe nae mbona kama unajitoa ufahamu. Ina maana wewe hadi umri huo ulionao haujui tofauti ya mtoto asiye na adabu na mtoto mwenye furaha ya kuona mgeni?!

Mtoto anatakuwa kulelewa kwa mipaka. Mfano mimi huwezi kuta mtoto aliyekulia mikononi mwangu analilia simu ya mgeni wala kuigusa.

Hivi imetokea mgeni amekuja na simu yake ya gharama lets say iphone 14 pro max, halafu mtoto wako anaililia achezee gem, mara paaaah kaibamiza chini kioo kimevunjika, wewe kama mzazi utajionaje kwa mgeni?!
Wewe mgeni kwann umpe mtoto simu? Kwani kuililia ndio kumpa?

Malezi ya mtoto ni rahisi sana tatizo mnacomplicate vitu
 
Haijulikani wazazi wengine wanaleaje watoto wao kimaadili wangali wadogo. Natoka ibadani kanisani natembea kwa miguu kuelekea nyumbani, napita mtaani njiani nakuta watoto wadogo wa chekechea wengi wanacheza pamoja michezo yao ya kitoto. Nawasalimia, watoto hamjambo? Kanaibuka katoto kamoja cha kike kanajibu salamu yangu, hatujajamba tukijamba tutakuambia. Kama mtu mzima nilighadhibika na kutaka kukaadhibu katoto hako ila mazingira hayakuruhusu kumpa kifinyo kwa kutoa jibu lile baya kama mzazi. Ingeleta taharuki mtaani kwa mtu mzima mpita njia kuadhibu mtoto wa mtu. Nichofanya ni kumkazia macho makali na kumkunjia uso kumuonesha sikufurahishwa na jibu lake, walipoona nimekaza uso watoto wote walikimbilia makwao na mimi nikaona isiwe taabu nikaachana nao na kuendelea na safari yangu. Kwa kweli kuna watoto wadogo hawana nidhamu kabisa, wazazi wao waliwazaa lakini hawawapi maadili mema kuheshimu watu wengine
 
Haijulikani wazazi wengine wanaleaje watoto wao kimaadili wangali wadogo. Natoka ibadani kanisani natembea kwa miguu kuelekea nyumbani, napita mtaani njiani nakuta watoto wadogo wa chekechea wengi wanacheza pamoja michezo yao ya kitoto. Nawasalimia, watoto hamjambo? Kanaibuka katoto kamoja cha kike kanajibu salamu yangu, hatujamba tukijamba tutakuambia. Kama mtu mzima nilighadhibika na kutaka kukaadhibu katoto hako ila mazingira hayakuruhusu kumpa kifinyo kwa kutoa jibu lile baya kama mzazi. Ingeleta taharuki mtaani kwa mtu mzima mpita njia kuadhibu mtoto wa mtu. Nichofanya ni kumkazia macho makali na kumkunjia uso kumuonesha sikufurahishwa na jibu lake, walipoona nimekaza uso watoto wote walikimbilia makwao na mimi nikaona isiwe taabu nikaachana nao na kuendelea na safari yangu. Kwa kweli kuna watoto wadogo hawana nidhamu kabisa, wazazi wao waliwazaa lakini hawawapi maadili mema kuheshimu watu wengine
Uliwaangalia kwa macho ya kigaidi wakatawanyika wenyewe. Hahaha
 
Watoto wakorofi ndio nawapenda sana, wakija kwangu nawapa upendo hadi wanabadilika na kua good kids.... ila kumbuka raha ya mtoto awe katundu tundu asipooze sana na asizidishe utundu, tutamuhisi ana tatizo la Afya ya Akili.
Mtoto habadiriki kwa upendo tu,kuna sehemu ya upendo na sehemu ya maonyo,kwa Wakristo maandiko yanasema"fimbo huondoa upumbavu moyoni mwa mtoto Mith 22:15"pia inasema usimnyime mtoto wako mapigo Mith 23:13,..kwa hiyo kumuonya mtoto kwa fimbo ni kumfanya kua mtu bora baadae tena unakua umemsaidi,katika makuzi yetu tumepigwa fimbo na walimu na wazaz,na zilitusaidia kua hapa tulipo,..kumnyima viboko mtoto jua una mharibu...moyon mwa mtoto kuna upumbavu,fimbo humfanya awe mtu bora.
 
Fanya shambulizi la kimya kimya hakuna haja ya kushika fimbo.

Shika mkono vizuri kwenye msuli(hawezi kua na msuli) binya na dole gumba kwa nguvu kiasi utakutana na mfupa, kandamiza kama sekunde 10 hivi uone kama katarudia
mweeee kuwa na huruma jaribu njia nyingine lakin sio hii hayo maumivu yake katashusha haja ndogo
 
Mwanangu wa kiume alikuwa msumbufu lakini ule usumbufu usioumiza(unaofurahisha).Mfano mgeni kaja home ataanza kumzoea ghafla hapo anaweza akaingia ndani anakuletea pipi kama itakuwepo ule hujakaa kidogo atakuja tena na soda anakwambia "uncle/aunty kunywa soda hii" mara hujakaa vizuri kaja na simu anakuonyesha game halafu anakuuliza kama kwenye simu yako lipo mara muda wa kula anamuuliza mgeni uncle mbona huli!? Kula nyama hii anaonyesha paja kubwakubwa hapo! Mgeni akiondoka anamlilia au anaficha viatu..Nilikua nachukia sana sijui wageni wangu walikuwa wananiongelea vibaya huko kwao!?
 
Mwanangu wa kiume alikuwa msumbufu lakini ule usumbufu usioumiza(unaofurahisha).Mfano mgeni kaja home ataanza kumzoea ghafla hapo anaweza akaingia ndani anakuletea pipi kama itakuwepo ule hujakaa kidogo atakuja tena na soda anakwambia "uncle/aunty kunywa soda hii" mara hujakaa vizuri kaja na simu anakuonyesha game halafu anakuuliza kama kwenye simu yako lipo mara muda wa kula anamuuliza mgeni uncle mbona huli!? Kula nyama hii anaonyesha paja kubwakubwa hapo! Mgeni akiondoka anamlilia au anaficha viatu..Nilikua nachukia sana sijui wageni wangu walikuwa wananiongelea vibaya huko kwao!?
Wageni wenye roho mbaya na makatili lazima walikua wanamuongelea mtoto vibaya (utawaona humu humu kwenye huu uzi) lakini Mtoto wako ni mzuri sana, ni mkarimu, mwenye upendo, nimempenda bure, i send my hugs to him [emoji847] hongereni pia Wazazi kwa kua na Mtoto bora.
 
Back
Top Bottom