Ukifanikiwa wafanye wengine pia wafanikiwe kupitia wewe

Ukifanikiwa wafanye wengine pia wafanikiwe kupitia wewe

Street brain

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2022
Posts
584
Reaction score
767

Jambo letu

Haitoshi tu kuwa na mafanikio makubwa bali tumia nafasi hiyo kuwasaidia wengine kufanikiwa pia. Tunaelewa ili ufanikiwe ulipita vikwazo vingi, ulishinda mengi; tumia muda huu kuwa mwalimu wetu.

Maendeleo ni kama bahari na hakuna bahari yenye kisiwa kimoja na kisiwa hakizuii kingine kuwa kisiwa. Hatua yako kubwa haiwezi kuwa ndogo kisa wengine wamepiga hatua. Wasaidie, wafanye wawe wakubwa pia, itakuletea furaha na kukuongezea heshima.
 
Uko sahihi sana, lakini lazima tuelezane njia sahihi ya kumsaidia mtu naye afanikiwe kimaisha hususani suala la kiuchumi. Kama ni Hawa vijana wa bongo naowaona akili zao,,, kama chenga hivi. Naweza kukupa mifano kadhaa 1. Nikishawahi ombwa na ndugu yangu nimsaidie ili naye atoke, nikamwambia watakaje? akanijibu fungua biashara niisimamie ili Nami nipate riziki. Nikafungua bucha nzuri tu na likapata wateja vizuri tu, kuuza kilo 70-100 ikawa kawaida kabisa na tukakubaliana faida itakayopatikana tutagawana pasupasu. Aiseee baada ya miezi kama 6 hv sikuamini kilichokuwa kinatokea. 2. Wapili tukaplani mipango na ndugu mwingine tufanye ufugaji nikamwambia sawa, coz tayari nilkuwa na shamba ikawa niliweka miundombinu tu. Basi tukaanza harakati na hata hivyo nikamwambia tutafute na fremu ya karibu ili pia wakati unasimamia ufugaji tufungue na duka ili usiwe Ido sana. Baada ya kuteleza kwa muda Mimi nanunua pumba Tani kadhaa huku mwenzangu baadhi anauza. Sasa Bora hata angeenda kufanyia maendeleo, zaidi ni kutembeza mjegeje tu kwa vibinti na wake za watu. Nikishaapa ukitaka nikusaidie nione juhudi zako na uwe na umezianza harakati Mimi nikubust lakini hivihivi tu hata mia huna pita mbali na Mimi.
 
Uko sahihi sana, lakini lazima tuelezane njia sahihi ya kumsaidia mtu naye afanikiwe kimaisha hususani suala la kiuchumi. Kama ni Hawa vijana wa bongo naowaona akili zao,,, kama chenga hivi. Naweza kukupa mifano kadhaa 1. Nikishawahi ombwa na ndugu yangu nimsaidie ili naye atoke, nikamwambia watakaje? akanijibu fungua biashara niisimamie ili Nami nipate riziki. Nikafungua bucha nzuri tu na likapata wateja vizuri tu, kuuza kilo 70-100 ikawa kawaida kabisa na tukakubaliana faida itakayopatikana tutagawana pasupasu. Aiseee baada ya miezi kama 6 hv sikuamini kilichokuwa kinatokea. 2. Wapili tukaplani mipango na ndugu mwingine tufanye ufugaji nikamwambia sawa, coz tayari nilkuwa na shamba ikawa niliweka miundombinu tu. Basi tukaanza harakati na hata hivyo nikamwambia tutafute na fremu ya karibu ili pia wakati unasimamia ufugaji tufungue na duka ili usiwe Ido sana. Baada ya kuteleza kwa muda Mimi nanunua pumba Tani kadhaa huku mwenzangu baadhi anauza. Sasa Bora hata angeenda kufanyia maendeleo, zaidi ni kutembeza mjegeje tu kwa vibinti na wake za watu. Nikishaapa ukitaka nikusaidie nione juhudi zako na uwe na umezianza harakati Mimi nikubust lakini hivihivi tu hata mia huna pita mbali na Mimi.
Ni kweli lakini mimi hawa ndugu naishi nao na ndiyo walionipa na hasira ya kupambana mpaka hapa APA nilipo kwa mfano miaka kama 25 iliyopita kuna ndugu aliniajili kwenye duka lake a jumla na rejareja but alikuwa na wafanyakazi wengine mi nilikuwa nalipwa elfu 20 kwa mwezi but wale wafanyakazi walilipwa elfu 90 kwa mwezi sasa siku moja, moja ya wale wafanyakazi akawa analalamika kuwa mshahara aongezewe daah apo nikashangaa yaani mitu analipwa 90 na analalamika duuh iliniuma sana tena siku hiyo nikaondoka zangu chuo kwa hasira nikasoma kwa mazingira magumu till now am in charge of acconntant and administration at Kilimanjaro.
But hao ndugu sina hata hamu nao tena
 
Katika maisha huwa nasema wote wanamchango katika kufanikiwa. Kwani kwa roho mbaya zao ndizo zinazotupa hasira ya kupambana. Nami wakati nimemaliza six naenda chuo kuna ndugu niliwafata wanisaidie japo hela ya kuanzia huku nasubiri mkopo weee majibu yao hatuwezi kusomesha mtoto wa mtu kwanza unaweza kufanikiwa na usije ukanisaidia . Na mtu anauwezo wake mzuri tu.

Niliumia sana siku hiyo. Lkn Mungu wa ajabu akatokea ndugu mmoja ambaye hana hata uwezo akanisapoti nikaanza chuo nilisoma kwa hasira toka naanza chuo hadi namaliza wastani wangu ulikuwa mkubwa. Nilirudi kitaaa nikaanza kupambana na ajira. Mungu athumani nikapata kazi. Nilikuja nikajikusanya nikampa yule aliyenipambania kama milioni 3 hivi za asante. Na saa hizi akipata shida au hata asiponiomba hela nikipata namtumia. Yule mwingine anaonaga hadi aibu kuniomba. Ila ilitokea siku moja aliniomba nikamwambia sina nilimpa fulani milioni 3 nikipata nitakupa akabaki ahaaaaa umempa hela zote nikamjibu ndio alipanda mbegu saa hizi ni wakati wake wa kuvuna akabaki kimya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika maisha huwa nasema wote wanamchango katika kufanikiwa. Kwani kwa roho mbaya zao ndizo zinazotupa hasira ya kupambana. Nami wakati nimemaliza six naenda chuo kuna ndugu niliwafata wanisaidie japo hela ya kuanzia huku nasubiri mkopo weee majibu yao hatuwezi kusomesha mtoto wa mtu kwanza unaweza kufanikiwa na usije ukanisaidia . Na mtu anauwezo wake mzuri tu.

Niliumia sana siku hiyo. Lkn Mungu wa ajabu akatokea ndugu mmoja ambaye hana hata uwezo akanisapoti nikaanza chuo nilisoma kwa hasira toka naanza chuo hadi namaliza wastani wangu ulikuwa mkubwa. Nilirudi kitaaa nikaanza kupambana na ajira. Mungu athumani nikapata kazi. Nilikuja nikajikusanya nikampa yule aliyenipambania kama milioni 3 hivi za asante. Na saa hizi akipata shida au hata asiponiomba hela nikipata namtumia. Yule mwingine anaonaga hadi aibu kuniomba. Ila ilitokea siku moja aliniomba nikamwambia sina nilimpa fulani milioni 3 nikipata nitakupa akabaki ahaaaaa umempa hela zote nikamjibu ndio alipanda mbegu saa hizi ni wakati wake wa kuvuna akabaki kimya.

Sent using Jamii Forums mobile app
Uko sahihi kiongozi
 

Jambo letu

Haitoshi tu kuwa na mafanikio makubwa bali tumia nafasi hiyo kuwasaidia wengine kufanikiwa pia. Tunaelewa ili ufanikiwe ulipita vikwazo vingi, ulishinda mengi; tumia muda huu kuwa mwalimu wetu.

Maendeleo ni kama bahari na hakuna bahari yenye kisiwa kimoja na kisiwa hakizuii kingine kuwa kisiwa. Hatua yako kubwa haiwezi kuwa ndogo kisa wengine wamepiga hatua. Wasaidie, wafanye wawe wakubwa pia, itakuletea furaha na kukuongezea heshima
Uko sahihi mkuu
 
Back
Top Bottom