Ruby alivyozingua faster wakamtengeneza Nandy
- Kikwete ana msemo wake kuwa ukitaka kula lazima uliwe, kibiashara tafuta tu Win-Win situation, ukitaka haki sana dunia hii hakuna utakachopata maana hata haki yenyewe ni kitu kisichokuwepo duniani
- Msimwome Diamond pale kadhalilika, katumikaa, katumiwaa - kwasasa kawa na kiburi kwasababu kashajenga Empire ambayo kimuziki haepukiki , kwahiyo hata Mamanager wake na media wanamchukulia tu kama mfanyabiashara mwenzao na siyo msanii tu. Diamond na wasanii wake hawashiriki matamasha ya Clouds, na wanaandaa ya kwao - hili Clouds hawalipendi ila ndo hivyo Diamond kashakuwa na nguvu. Hata EATV hawaelewani na WCB lakini wanapiga nyimbo zao na interviews kibishi tu maana hata EATVAwards hawakushiriki na zilikosa mvuto , so huwezi jua wafadhili Voda na Coca ambao balozi wao ni Diamond pia wanaweza kujitoa
- Na hata kama hujaridhika na umekosana na mtu usiwe mzungumzaji sana, kaa tu kimya au kataa kistaarabu - Ukiwa kidomo domo utaisoma namba