Ukigombana na Mkeo, akaenda kwao; USIENDE wala Usimtafute

Ukigombana na Mkeo, akaenda kwao; USIENDE wala Usimtafute

Kwa huu uandishi hakuna aliepo kwenye ndoa kwa miaka 16....na Kama kweli Basi wanao wamedoda nyumbani na umeanza safari ya malezi upya [emoji38][emoji38]
Sawa
 
Funniest thing about wanawake wote wanaamini ni wazuri na wana uwezo wa kumtetemesha mtu yoyote ,kwa ulichoandika utaoa utaoa utaoa na hadi uzeeke utakuwa tyl n shahidi na mm "kutokuwa mjinga co kutokukubali kufanywa mjinga"
 
Inategemea na coincidence ya tukio na watoto nyumbani otherwise kitu ambacho siwezi kufanya ni kupiga magoti kumvisha pete, kupiga magoti kumuomba msamaha au kumuomba msamaha wife kwa ujumla wake nitazungumza maneno yore ila sio neno samahani
Neno samahani au nisamehe ni dawa na tiba kwenye mahusiano yote hapa duniani..Muungwana akikosea uomba samahani..kama unapeleka zawadi mbadala wa msamaha hiyo ni rushwa tu kumpumbaza mtu huyo asione kosa lako..
 
Funniest thing about wanawake wote wanaamini ni wazuri na wana uwezo wa kumtetemesha mtu yoyote ,kwa ulichoandika utaoa utaoa utaoa na hadi uzeeke utakuwa tyl n shahidi na mm "kutokuwa mjinga co kutokukubali kufanywa mjinga"

Mwanaume haoni shida kuoa hata mara elfu ikiwa ni Kwa sababu ya kulinda heshima yake
 
...kisha utampa barua awapelekee wazazi wake, waandikie na Fidia kadiri utakavyoona kulingana na siku alizokaa, na utoe onyo kuwa kama tabia hii itajitokeza wakati mwingine, barua hiyo itahesabika Kama sehemu ya onyo la mwisho, hivyo akirudi basi mtoto wao utampa talaka.
Ikiwa watashindwa kulipa fidia waambie asirudi wakae naye, au wanaweza kumuozesha na barua hiyo itahesabika Kama talaka kwani sababu utakuwa umeziorodhesha.
Ukiacha hiki kipengele cha FiDIA, naunga mkono mengine yote uliyoandika😊
 
Maisha yangu yote nilikataa Habar ya kutawaliwa na mtu anaeitwa mwanaume, napenda twende sawa hutaki pita na mia,
Kwani nini bwana weee
 
Kama utatumia hisia ni kweli utakutwa na hayo uliyoyasema,

Mwanaume ni AKILI.
Kabla hujaoa jifunze kuwa Mwanaume, yaani kutumia zaidi kuliko hisia. Usiitumie moyo.

Pengine hujui maana ya Mtawala ndio maana unaleta mambo ya Sonoma, aibu na kudharaulika.

Linapokuja suala la heshima lazima lipaganiwe Kwa nguvu zote pasipo kujali matokeo
Hili bandiko lako umeongea na idadi chache sana ya wanaume, ni kama vile umewapa semina, lakini ukweli ni kuwa kizazi hiki wanaume wa hivyo ni wachache. Unaoongea nao hapa ilitakiwa kile kizazi cha ukoloni ambapo mwanaume ananyanyuka anaenda kupigania taifa bila uoga,,hawa wa siku hizi chama kimoja tu wameshindwa kukitoa madarakani hata. Kwa mapanga wamebaki kulala mitandaoni
Eeh mwanaume ambae hata mke mmoja au wawili walikuwa hawatoshi hadi mke anaomba pooo kwa hiyo inabidi mume kufanya ndoa za mitala,

Unaita hawa wavaa suruali wanaume wakati ndani mwanamke analia hatoshelezwi kizazi cha mitala kwa wanawake fyuuu,

Mwanaume wa sasa hata kikombe cha chai hamalizi wakati enzi hizo mwanaume ndo ya lita 20 ya unga siku mbili Imeisha.
 
MKIGOMBANA NA MKEO, AKAENDA KWAO, USIMFUATE WALA USIMTAFUTE

Anaandika Robert Heriel.

Leo sina mengi ya kusema ndugu yenu. Nimefanya uchunguzi Kama mnavyonifahamu. Nikisemacho ni kweli tupu. Wala sisemi haya Kwa maslahi yangu, au ya mtu yeyote Yule. Nazungumza mambo ambayo ni kweli kabisa.

Na ujumbe huu usomwe na wangu wote. Mnisikie na kuyafuata ninayoyasema, Kwa maana maneno yangu yamepimwa na kuthibitika kuwa hayana madhara kwenu.

Kabla hujaoa jifunze kuwa Mwanaume. Niliwahi sema, mwanaume ni AKILI.
Kabla hujawa Baba jifunze kuwa Mtawala.
Na ili uwe Mtawala yakupasa uwe na hekima na busara. Pia uwe na maamuzi yasiyo yumba(uwe na msimamo).

Kitu kikubwa Kwa Baba ni Heshima, mwanaume Bora hulinda heshima yake kuliko kitu chochote. Yupo tayari kupoteza vyote lakini sio kupoteza heshima yake Kama Baba. Ndio maana Baba bora ni rahisi kufukuza mke na watoto pale anapoona heshima yake IPO hatarini.
Mwanaume anayepuuza heshima yake na kujali vitu vingine anapoteza sifa ya kuitwa Baba.

Mwanaume aliyeiva kamwe hawezi sumbuliwa na Mwanamke. Mwanaume ili asumbuliwe na mwanamke na hapa nazungumzia mke wake sharti aongozwe zaidi na Hisia pasipo Akili. Na siku zote mwanaume anayeongozwa na Hisia huyo sio mwanaume halisi.
Kama nilivyosema hapo juu. Mwanaume ni AKILI. Sio ajabu kwenye maandiko waliposema ishini na wake Kwa Akili.
Tafsiri yake ni kuwa pasipo akili heshima ya mwanaume ipo mashakani.

Baba ni jina kubwa. Baba hakosei. Na hapa namaanisha Baba aliyejifunza kuwa Mtawala.
Ikiwa Baba hakosei, tafsiri yake Baba haombi Msamaha.

Baba kuomba msamaha tafsiri yake hajielewi, hakujua alichokuwa anakifanya, Baba sharti awe na msimamo hata Kama wengine watamuona anakosea. Huyo ni Baba. Baba hapaswi kuwa kigeugeu.

Tuna Baba wawili, Baba WA kweli, ndiye MUNGU muumba wa mbingu na Nchi. Na yupo Baba wa uongo ndiye Ibilisi.
Ibilisi Kama Baba mpaka Leo anaamini yupo sahihi, licha ya wengi kuona alikosea. Ubaba ndio upo hivyo. Unapaswa uwe na msimamo. Ikiwa Baba unapaswa kuwa na msimamo basi yakubidi kabla yakufanya maamuzi yoyote lazima utumie akili ili ufanye uchaguzi uliosahihi kwako.

Ikiwa mwanamke ambaye ataitwa/utamuita Mkeo mkakosana, iwe Kwa sababu yoyote Ile, iwe wewe ndiye chanzo cha ugomvi au yeye ndiye chanzo cha ugomvi. Akaondoka kukimbia kwenda kwao pasipo wewe kumfukuza,
Akaenda kwao wakamlaki Kwa sababu ni mtoto wao, wakijua walimuozesha kwako,lakini wakampokea,
Kamwe usijeenda kumchukua, wala USIMTAFUTE, wala usitake Suluhu naye.

Utamhesabia siku saba za mwanzo, ikiwa hajakutafuta, utamhesabia siku Saba zingine, ikiwa hatajishusha, mhesabie siku saba zingine mpaka zifike siku 28, asipokuja achana naye kabisa wala usihesabu tena siku.


Ikiwa atarudi kabla hata ya mwezi Kuisha utampokea, kisha utampa barua awapelekee wazazi wake, waandikie na Fidia kadiri utakavyoona kulingana na siku alizokaa, na utoe onyo kuwa kama tabia hii itajitokeza wakati mwingine, barua hiyo itahesabika Kama sehemu ya onyo la mwisho, hivyo akirudi basi mtoto wao utampa talaka.
Ikiwa watashindwa kulipa fidia waambie asirudi wakae naye, au wanaweza kumuozesha na barua hiyo itahesabika Kama talaka kwani sababu utakuwa umeziorodhesha.

Mwanamke kuondoka nyumbani pasipo iidhini ya Mumewe ni kosa tosha la kumfukuzisha kwenye nyumba yako, isipokuwa Kwa sababu zinazohatarisha usalama wake kama kupigwa na mumewe ikiwa ni Wale wanaume vichwa maji. Na hapa kupigwa namaanisha kupigwa haswa sio Yale makofi mawili matatu ya kuonywa.

Mwanamke anapokimbilia kwao na akapokelewa na wewe ukaenda kumchukua ni dalili kuwa utawala wako umepinduliwa na sasa wewe mama Mtawala hauko utawalani.
Mwanamke kama itatokea akaona sababu ya kukimbia nyumbani kwako basi itampasa akimbilie kwenu, yaani Kwa Mama yako au Baba yako(akimbilie ukweni).
Hiyo ndio Heshima.

Na ndio maana ya wewe kuoa na kumuita huyo ni Mkeo. Lakini sio jitu umelioa likufanyie mapinduzi, ati uende ukalichukue kwao, hiyo kamwe haiwezi fanywa na Mwanaume aliyefunzwa akawa Mtawala Kama ilivyosilika ya mwanaume.

Mwanaume haweziitwa kikao ukweni akaenda, isipokuwa ukweni wanauwezo wa kuwasiliana na Familia ya Mkwe wao(mwanaume aliyeoa binti Yao), kisha wazazi wa mwanaume waitishe kikao, kisha upande wa kiukeni ualikwe Kama wageni na watoe malalamiko Yao.

Ikiwa utakiuka na kukaidi maneno haya basi utajikuta katika taabu ambayo hukupaswa uipitie.

Wanawake wengi ukienda kuwachukua kwao, hugeuka Mateso kwako hapo baadaye, huwa wajeuri, lazima wakupelekeshe kwani wanajua kabisa kuwa huwezi ishi pasipo wao.
Nimeshuhudia haya Kwa sehemu kubwa, nimejionea Kwa macho yangu na kuyafanyia tathmini hivyo maneno yangu yamepimwa yakathibitika.

Jifunze kukaza roho kabla ya kuitwa Baba. Jifunze kufanya maamuzi magumu kabla ya kuitwa Mume. Baba ni Cheo ambacho anastahili mtu mwenye maamuzi magumu. Ubaba Kwa sehemu hauhitaji kuwa na huruma hata kidogo.

Mwanamke akienda kwao Kama hamna hata mtoto mmoja mwambie akae huko huko asirudi. Kama mtakuwa na walau mtoto mmoja kuendelea unaweza mfanyia subra Kama nilivyoeleza hapo juu ya siku 28 yaani kabla mwezi mwingine haujaandama awe karudi, Kama hajarudi fukuza. Wala usimsikilize yeyote.

Baba hasikilizi yeyote isipokuwa akili yake na namna ya kulinda heshima yake. Hakuna cha serikali, hakuna cha mchungaji sijui Sheikhe, hakuna cha wazazi. Linapokuja suala la heshima yako kama Mwanaume usimsikilize yeyote Yule.

Usiponisikiliza;
Kila siku utaenda kujidhalilisha ukweni kuomba omba misamaha Kama Juha,
Kujiliza Liza Kama Paka ukweni ati kisa mwanamke asiyejielewa.
Mwanamke akijua kuwa akikimbia kwao utamfuta atakuwa hata kitu kidogo kakimbia kwao, sijui nini kwao,

Usihudhurie vikao ambavyo havina msingi wowote.
Mpaka wanakuozesha binti Yao waliridhishwa na kuwa wewe ndiye utakayemsimamia na kumhudumia mtoto wao.

Nafahamu kuna watu watanipinga, Hilo sitalijali na ninalitarajia.
Kuna watu watasema kuwa ninadada au nitazaa watoto wakike, Ndio ni kweli; mashemeji zangu na wakwe zangu WA baadaye utaratibu ni huo nilioutoa.

Kama nitakupa binti yangu akaleta upuuzi wa kukukimbia, Kwanza sitampokea, lakini kama atapata njia mbadala ya kwenda Kwa watu wengine. Fukuza na nitakupongeza na kukuona wewe ulistahili kumuoa mwanangu.

Lakini binti nimekupa alafu kakukimbia alafu unaleta pua yako kwangu, hakika nitakutoa nduki na panga mchana kweupe.

Be a Man not like a man.

Nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
Usiwadanganye wenzieo ohooo wengi wepesi wa kushauri wao hawafanyi hivyo
 
MKIGOMBANA NA MKEO, AKAENDA KWAO, USIMFUATE WALA USIMTAFUTE

Anaandika Robert Heriel.

Leo sina mengi ya kusema ndugu yenu. Nimefanya uchunguzi Kama mnavyonifahamu. Nikisemacho ni kweli tupu. Wala sisemi haya Kwa maslahi yangu, au ya mtu yeyote Yule. Nazungumza mambo ambayo ni kweli kabisa.

Na ujumbe huu usomwe na wangu wote. Mnisikie na kuyafuata ninayoyasema, Kwa maana maneno yangu yamepimwa na kuthibitika kuwa hayana madhara kwenu.

Kabla hujaoa jifunze kuwa Mwanaume. Niliwahi sema, mwanaume ni AKILI.
Kabla hujawa Baba jifunze kuwa Mtawala.
Na ili uwe Mtawala yakupasa uwe na hekima na busara. Pia uwe na maamuzi yasiyo yumba(uwe na msimamo).

Kitu kikubwa Kwa Baba ni Heshima, mwanaume Bora hulinda heshima yake kuliko kitu chochote. Yupo tayari kupoteza vyote lakini sio kupoteza heshima yake Kama Baba. Ndio maana Baba bora ni rahisi kufukuza mke na watoto pale anapoona heshima yake IPO hatarini.
Mwanaume anayepuuza heshima yake na kujali vitu vingine anapoteza sifa ya kuitwa Baba.

Mwanaume aliyeiva kamwe hawezi sumbuliwa na Mwanamke. Mwanaume ili asumbuliwe na mwanamke na hapa nazungumzia mke wake sharti aongozwe zaidi na Hisia pasipo Akili. Na siku zote mwanaume anayeongozwa na Hisia huyo sio mwanaume halisi.
Kama nilivyosema hapo juu. Mwanaume ni AKILI. Sio ajabu kwenye maandiko waliposema ishini na wake Kwa Akili.
Tafsiri yake ni kuwa pasipo akili heshima ya mwanaume ipo mashakani.

Baba ni jina kubwa. Baba hakosei. Na hapa namaanisha Baba aliyejifunza kuwa Mtawala.
Ikiwa Baba hakosei, tafsiri yake Baba haombi Msamaha.

Baba kuomba msamaha tafsiri yake hajielewi, hakujua alichokuwa anakifanya, Baba sharti awe na msimamo hata Kama wengine watamuona anakosea. Huyo ni Baba. Baba hapaswi kuwa kigeugeu.

Tuna Baba wawili, Baba WA kweli, ndiye MUNGU muumba wa mbingu na Nchi. Na yupo Baba wa uongo ndiye Ibilisi.
Ibilisi Kama Baba mpaka Leo anaamini yupo sahihi, licha ya wengi kuona alikosea. Ubaba ndio upo hivyo. Unapaswa uwe na msimamo. Ikiwa Baba unapaswa kuwa na msimamo basi yakubidi kabla yakufanya maamuzi yoyote lazima utumie akili ili ufanye uchaguzi uliosahihi kwako.

Ikiwa mwanamke ambaye ataitwa/utamuita Mkeo mkakosana, iwe Kwa sababu yoyote Ile, iwe wewe ndiye chanzo cha ugomvi au yeye ndiye chanzo cha ugomvi. Akaondoka kukimbia kwenda kwao pasipo wewe kumfukuza,
Akaenda kwao wakamlaki Kwa sababu ni mtoto wao, wakijua walimuozesha kwako,lakini wakampokea,
Kamwe usijeenda kumchukua, wala USIMTAFUTE, wala usitake Suluhu naye.

Utamhesabia siku saba za mwanzo, ikiwa hajakutafuta, utamhesabia siku Saba zingine, ikiwa hatajishusha, mhesabie siku saba zingine mpaka zifike siku 28, asipokuja achana naye kabisa wala usihesabu tena siku.


Ikiwa atarudi kabla hata ya mwezi Kuisha utampokea, kisha utampa barua awapelekee wazazi wake, waandikie na Fidia kadiri utakavyoona kulingana na siku alizokaa, na utoe onyo kuwa kama tabia hii itajitokeza wakati mwingine, barua hiyo itahesabika Kama sehemu ya onyo la mwisho, hivyo akirudi basi mtoto wao utampa talaka.
Ikiwa watashindwa kulipa fidia waambie asirudi wakae naye, au wanaweza kumuozesha na barua hiyo itahesabika Kama talaka kwani sababu utakuwa umeziorodhesha.

Mwanamke kuondoka nyumbani pasipo iidhini ya Mumewe ni kosa tosha la kumfukuzisha kwenye nyumba yako, isipokuwa Kwa sababu zinazohatarisha usalama wake kama kupigwa na mumewe ikiwa ni Wale wanaume vichwa maji. Na hapa kupigwa namaanisha kupigwa haswa sio Yale makofi mawili matatu ya kuonywa.

Mwanamke anapokimbilia kwao na akapokelewa na wewe ukaenda kumchukua ni dalili kuwa utawala wako umepinduliwa na sasa wewe mama Mtawala hauko utawalani.
Mwanamke kama itatokea akaona sababu ya kukimbia nyumbani kwako basi itampasa akimbilie kwenu, yaani Kwa Mama yako au Baba yako(akimbilie ukweni).
Hiyo ndio Heshima.

Na ndio maana ya wewe kuoa na kumuita huyo ni Mkeo. Lakini sio jitu umelioa likufanyie mapinduzi, ati uende ukalichukue kwao, hiyo kamwe haiwezi fanywa na Mwanaume aliyefunzwa akawa Mtawala Kama ilivyosilika ya mwanaume.

Mwanaume haweziitwa kikao ukweni akaenda, isipokuwa ukweni wanauwezo wa kuwasiliana na Familia ya Mkwe wao(mwanaume aliyeoa binti Yao), kisha wazazi wa mwanaume waitishe kikao, kisha upande wa kiukeni ualikwe Kama wageni na watoe malalamiko Yao.

Ikiwa utakiuka na kukaidi maneno haya basi utajikuta katika taabu ambayo hukupaswa uipitie.

Wanawake wengi ukienda kuwachukua kwao, hugeuka Mateso kwako hapo baadaye, huwa wajeuri, lazima wakupelekeshe kwani wanajua kabisa kuwa huwezi ishi pasipo wao.
Nimeshuhudia haya Kwa sehemu kubwa, nimejionea Kwa macho yangu na kuyafanyia tathmini hivyo maneno yangu yamepimwa yakathibitika.

Jifunze kukaza roho kabla ya kuitwa Baba. Jifunze kufanya maamuzi magumu kabla ya kuitwa Mume. Baba ni Cheo ambacho anastahili mtu mwenye maamuzi magumu. Ubaba Kwa sehemu hauhitaji kuwa na huruma hata kidogo.

Mwanamke akienda kwao Kama hamna hata mtoto mmoja mwambie akae huko huko asirudi. Kama mtakuwa na walau mtoto mmoja kuendelea unaweza mfanyia subra Kama nilivyoeleza hapo juu ya siku 28 yaani kabla mwezi mwingine haujaandama awe karudi, Kama hajarudi fukuza. Wala usimsikilize yeyote.

Baba hasikilizi yeyote isipokuwa akili yake na namna ya kulinda heshima yake. Hakuna cha serikali, hakuna cha mchungaji sijui Sheikhe, hakuna cha wazazi. Linapokuja suala la heshima yako kama Mwanaume usimsikilize yeyote Yule.

Usiponisikiliza;
Kila siku utaenda kujidhalilisha ukweni kuomba omba misamaha Kama Juha,
Kujiliza Liza Kama Paka ukweni ati kisa mwanamke asiyejielewa.
Mwanamke akijua kuwa akikimbia kwao utamfuta atakuwa hata kitu kidogo kakimbia kwao, sijui nini kwao,

Usihudhurie vikao ambavyo havina msingi wowote.
Mpaka wanakuozesha binti Yao waliridhishwa na kuwa wewe ndiye utakayemsimamia na kumhudumia mtoto wao.

Nafahamu kuna watu watanipinga, Hilo sitalijali na ninalitarajia.
Kuna watu watasema kuwa ninadada au nitazaa watoto wakike, Ndio ni kweli; mashemeji zangu na wakwe zangu WA baadaye utaratibu ni huo nilioutoa.

Kama nitakupa binti yangu akaleta upuuzi wa kukukimbia, Kwanza sitampokea, lakini kama atapata njia mbadala ya kwenda Kwa watu wengine. Fukuza na nitakupongeza na kukuona wewe ulistahili kumuoa mwanangu.

Lakini binti nimekupa alafu kakukimbia alafu unaleta pua yako kwangu, hakika nitakutoa nduki na panga mchana kweupe.

Be a Man not like a man.

Nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa Sasa Dar es salaam
😍
 
Usiwadanganye wenzieo ohooo wengi wepesi wa kushauri wao hawafanyi hivyo

Mimi nawapa Tu dondoo chache za kuwafunza adabu wanawake wasiofunzwa na wazazi wao.

Masomo yangu nayatoaga Kwa watu wote lakini lengo yashikwe na watu wachache tuu.

Furaha ni yawatu wachache siku zote
 
Hili bandiko lako umeongea na idadi chache sana ya wanaume, ni kama vile umewapa semina, lakini ukweli ni kuwa kizazi hiki wanaume wa hivyo ni wachache. Unaoongea nao hapa ilitakiwa kile kizazi cha ukoloni ambapo mwanaume ananyanyuka anaenda kupigania taifa bila uoga,,hawa wa siku hizi chama kimoja tu wameshindwa kukitoa madarakani hata. Kwa mapanga wamebaki kulala mitandaoni
Eeh mwanaume ambae hata mke mmoja au wawili walikuwa hawatoshi hadi mke anaomba pooo kwa hiyo inabidi mume kufanya ndoa za mitala,

Unaita hawa wavaa suruali wanaume wakati ndani mwanamke analia hatoshelezwi kizazi cha mitala kwa wanawake fyuuu,

Mwanaume wa sasa hata kikombe cha chai hamalizi wakati enzi hizo mwanaume ndo ya lita 20 ya unga siku mbili Imeisha.


🤣🤣🤣

Na hapa nazungumza na wanaume haswa ambao ni wachache Mno.

Kumbuka sifa kuu ya mwanaume ni AKILI, hekima, na nguvu, kisha MSIMAMO.

Sio rahisi Kwa mwanamke akikikutana na Mwanaume halisi kuleta upumbavu, hakuna mwanamke atakayekubali kumpoteza mwanaume mwenye sifa nilizozitaja.

Wanawake wa siku hizi wanaona rahisi kuachana na wala hawaoni tatizo Kwa sababu ya madhaifu ya kimsingi ya Vijana wa siku hizi.
Mwanamke ataumia kidogo alafu atasahau lakini kama angekutana na Mwanaume halisi, mwanamke kamwe hawezi kubali kuachwa alafu ati mwanamke mwingine achukue nafasi yake ajipatie furaha kwa huyo mwanaume aliyemuacha.

Siku hizi wanaume ndio wanateseka kwenye mahusiano kutokana na kupoteza Ile sifa ya Uanaume.
 
Hiyo heshima inapelekwa wap?

Heshima ya mwanaume ndio maisha yake na Ulinzi wake.

Ni Kama Mwanamke Naye anaheshima yake ambayo ni Ulinzi wake.
Mwanamke lazima alinde Utu wake Kwa kutofanya umalaya na kufunuliwa funuliwa na kila mwanaume.

Heshima ya mwanamke ukiipoteza jua umekwisha,
Kila mtu atakudharau hata wewe mwenyewe utajidharau.
Watoto utawatia uchungu na kukuona hufai kuwa mama Yao.

Ndio maana mwanamke haswa, mwanamke anayejua thamani yake kamwe hawezi kujirahisisha Kwa kutoa penzi kiholela, ni aibu Kwake na Kwa wanaomzunguka
 
Hapo umeeleweka, kiufupi ni kuwa wanaume halisi wanazidi kuisha
🤣🤣🤣

Na hapa nazungumza na wanaume haswa ambao ni wachache Mno.

Kumbuka sifa kuu ya mwanaume ni AKILI, hekima, na nguvu, kisha MSIMAMO.

Sio rahisi Kwa mwanamke akikikutana na Mwanaume halisi kuleta upumbavu, hakuna mwanamke atakayekubali kumpoteza mwanaume mwenye sifa nilizozitaja.

Wanawake wa siku hizi wanaona rahisi kuachana na wala hawaoni tatizo Kwa sababu ya madhaifu ya kimsingi ya Vijana wa siku hizi.
Mwanamke ataumia kidogo alafu atasahau lakini kama angekutana na Mwanaume halisi, mwanamke kamwe hawezi kubali kuachwa alafu ati mwanamke mwingine achukue nafasi yake ajipatie furaha kwa huyo mwanaume aliyemuacha.

Siku hizi wanaume ndio wanateseka kwenye mahusiano kutokana na kupoteza Ile sifa ya Uanaume.
 
Maisha yangu yote nilikataa Habar ya kutawaliwa na mtu anaeitwa mwanaume, napenda twende sawa hutaki pita na mia,
Kwani nini bwana weee


Ukitaka ujue athari yake, njoo pm nitakueleza kinagaubaga.

Kutawaliwa na Mwanaume ndio nature ilivyo. Utake usitake.
Sema lazima ujiulize anayekutawala ni mwanaume wa dizaini gani maana wanaume hawalingani mama mlivyo Wanawake.

Mtu anaweza kuwa Mwanaume lakini ukawa umemzidi akili na hekima, huyo hawezi kukutawala. Lakini haimaanishi usitafute mwanaume wa kukutawala mwenye vigezo unavyovitaka.

Dini zote kubwa, na hata tamaduni karibia zote Duniani zinakutaka uwe chini ya utawala wa mwanaume. Hilo sio ombi ni Lazima.

Biblia inasema hivyo, Quran nayo ni vivyo hivyo, na hata Mila zetu zinasema hivyo.
Labda wewe unambie ni kabila gani

Kutokutaka kutawaliwa ni ishara ya kiburi na jeuri Kwa nature uliyotwaliwa kwayo.
Na kikawaida nature inatabia ya kukuadhibu ukienda kinyume nayo.

Kusema huwezi kutawaliwa na Mwanaume ni Dalili kuwa umeshindwa kutambua na kuona Wanaume wenye sifa za kukutawala ambao ninauhakika wapo.

Mwisho: Usipende kushindana na nature, itakugharimu pakubwa, mbaya zaidi itagusa na watoto wako pia.
Nina ushahidi katika hili

Njoo pm nitakueleza Jambo muhimu.
 
Back
Top Bottom