Ukigombewa ka' Mpira wa Kona utafanyaje?

Ukigombewa ka' Mpira wa Kona utafanyaje?

Ningemuonea huruma tu sababu anakimbia bahati

tena hizo bahati zilikuwa nyingi..kulia, kushoto, mbele na kule na kule...yani ungeweza toka hapo unameremeta kwa bahati...
 
si kila akukaribishae ni mtu mzuri na sio kila harusi unayopata kadi uhudhurie
 
Miaka michache iliyopita nilikuwa kwenye pita pita ya mitaa za Nairobi. kutahamani mbele yangu kushoto kuna mama mmoja akaniita. sijakaa vizuri mwingine pembeni kulia nae akaniita tena kwa nguvu 'kuja huku!'. kwanza nikapigwa na butwaa. Kulikoni? kutazama mbele pia kukawa na mama mwingine wa kisomali nae ananiita niende kwake. huku nyuma nako nikasikia naitwa na mama mwingine! Nikajua hapa nimepita kwenye mitaa nisiyoitarajia. ilibidi nitafute junction haraka na kutokomea huku nikitweta utadhani nimetoka kukimbia marathon. Mdau hususan Mwanamme mwenzangu wewe ungetii wito? kama ndio ungewatembelea wote wakukaribishao?

Wakwepe kama uwakwepavyo wapiga debe pale ubungo ukiwa unaeleke kupanda DAR EXPRESS
 
Back
Top Bottom