SI KWELI Ukihisi harufu ya wali au mchele uwapo porini ni ishara kuwa Chatu yupo karibu

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Bado maelezo yako hayajibu swali husika..!!
 
Hiii imani ipo sehemu nyingi. Hata mimi mara kadhaa nimeshapita maeneo nikasikia hiyo harufu ya wali. Kwangu mimi nadhani kuna mimea/miti ambayo huwa inatoa hiyo harufu. Nakumbuka kuna mmea mmoja huwa unatoa harufu ya maziwa ya mgando.
Angalau it makes sense. Kuna yale majani ukiyafikicha yanatoa harufu ya kinyesi..!! Enzi zetu za primary school, tulikuwa tunayafikicha na kuyarushia staff room..!! au ofisi ya mwalimu mkuu kabisaaa..!!
 
Kuna mti majani yake hutoa hiyo harufu lakini haihusiani na nyoka!
 
Ni kweli...chatu anakuwa anavua ngozi yake ya nje....lakini siyo kwamba anakuwa anakuvutia
 
Kuna siku katikati mapori huko turiani na muheza nikaskia hiyo harufu nilitoka mbio balaa mpaka kijiji kingine maana nilijua tu hii balaa.
 
actually,
sio porini pekee, na sio kwa chatu pekeyake, hata nyoka wa aina nyingine, mathalani yupo ndani ya nyumba yako, akiwa amejikoboa magamba yake hunukia mithili ya mchele uliolowekwa au wali, na wakati huo hujaloweka wala kupika wali ndani kwako..

Ile harufu sio tu kwajili ya kuvutia wanyama wengine tu, bali pia ndio harufu yake baada ya kujivua gamba la zamani...

Na hiyo harufu inakujulisha au kuashiria eneo ulilopo kuna nyoka Jirani na wewe πŸ’
 
Mmmh ya kweli haya?
 
Huyo afisa pori kwa maelezo yake nae hajui. Pia kwa JF kuhitimisha kuwa sio kweli hawako sahihi. Wapo jamaa wachana mbao porini. Wanathibitisha kuwa ni nyoka huwa kavua gamba ndio unasikia hivyo.
 
Hajanishawishi kisayansi huyo mtu wa TAWA,waulizwe na watafiti wengine huyu kajibu kisiasa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…