Ukiishi kwa ndugu, rafiki, jirani zingatia haya

Ukiishi kwa ndugu, rafiki, jirani zingatia haya

ERoni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
48,052
Reaction score
104,677
Ndugu zangu,

Maisha hayajawahi kuwa fair hata kidogo, coz dunia nayo haipo fair kwetu. Wapo wenzetu kwa tofauti hii ya usawa, wamezaliwa na kukuta mambo yapo vizuri kuanzia kuvaa, kula, kulala na hata mengine ambayo kwa sisi wengine tungesema ni anasa tu lakini wao wanayo na wakikuona wewe huna wanaweza kushangaa. Hawa ni aina ya watu ukimwambia "sina hata buku mfukoni hakuamini".

Sasa basi, kwenye kutafuta kuna siku lazima utatoka "kwenu" na kwenda huko kujitafutia/kujitegemea. Tuseme umeshaua college sasa inabidi kijana uchomoke kwa bimkubwa na mzee uanze kuhaso. Hapa ndipo mambo yanapobadilika, wale dunia iliyoamua kuwa fair kwao wataingia mji tofauti na kwao, watachukua self-contained room yenye sebule na jiko(wenyewe wanasema maji na umeme unajitegemea), around 250,000p/m, si wazazi wame-provide bwana, no worries hata. Huenda hata mchongo hana ila kodi ikiisha daddy atatuma nyingine tu...dunia iko fair kweli?

Kuna wale wanajiamini, wanatoka huko wanakuja town hawamjui yoyote, hawana ndugu, wapo na kianzio cha 500k maximum, hats off to them kwa kweli. Hawana connection wala mchongo, ila Mungu sio Eroni after 5yrs uliza yuko wapi and you'll be shocked. Hawa watu ni majasiri sana, imagine unaingia Dar humjui yoyote, unakutana na stand kubwa pale Louis kwa Magu...then from there unaanzia wapi.. hats off once more!!

Kuna sie waoga, tunafikia kwa kaka/dada, uncle/auntie etc. Aisee hatuna mishe ndio tunatembeza khaki zetu na kutwa tupo ajira portal. Dunia ikivyokosa adabu, unfairness ya hii dunia dhalimu, no equality wala equity, unakuta tupo kwa auntie/uncle for yrs...mambo hayaendi, hatuwezi kurudisha mpira hata kwa beki, lakini gozi limekuwa gumu halichezeki tena.

Tunaoangukia hapa tufanyeje ili tusichokwe na wenyeji wetu?(kumbuka binadamu ana tabia ya kuchoka, so tusiwalaumu sana wenyeji wetu)

1.....
2.....
3....
4....

Jadili kidogo hapo, kipindi hiki cha mpito chaweza kuwa kigumu kuliko hata hizo course works na UE.
 
Kuwa na tabia ya kuanza kujizoeza kwenda kitaa kutafuta mishe za kufanya ili siku moja moja unaleta mboga au unga ....ipo siku utaangukia mishe ya maana na ndo utakuwa mwanzo wa kutoka...Nb...usidharau KAZI YEYOTE....
 
Kuishi na watu ni kipaji,, kujifanya mjinga tu,, fanya kazi km punda,, hata ukionewa upotezee siku ukiondoka iwe ni aibu kwao,,na roho mbaya huwa tunazianzisha sie wanawake hasa kwenye misosi,, kumsimanga mtu kwa ajili ya kula ni tabia mbaya na umaskini uliopitiliza
 
Kuishi kwa ndugu, mambo ya kufanya
1. Siku zote amka mapema na ufanye shughuli za kimsaada kwenye mji huo, kwa mfano kufagia, kusafisha mabanda ya kuku n.k. wjatever it is, lakini asubuh na mapema ikukute nje.
2. Jitahidi kutoka nje na kuzunguka kitaa ukitafta mishe ndogo ndogo za kukupa vijisenti ili usipauke kisoro
3. Usiwe na mazoea yaliyopitiliza hasahasa Kwa shemeji au wifi yako. Kaa kwa step wacha kiherehere
4. Ukipata chochote huko duniani, kamwe usirudi mikono mitupu, hata ndizi za buku zinaeza sindikiza wali maharagwe hapo ndani. Always provide some input kuwapunguzia mzigo.
5. Kuwa msafi, kuwa msafi kuwa msafi!
6. Fuata sheria zao, kwa mfano kuwahi kurudi, kusali n.k. kama una sheria zako kazipeleke kwenu, hapo ni kwa watu, wacha kisebengo cha kupanga masharti.
7. Hakikisha wale watoto kina "junia" hawakuzoei, wale wana mambo ya kiwaki unaweza mkata kelebu akatema meno. Jiepushe nao
8. Beki 3 ana mbolea iliopitiliza, ukipanda mbegu nakuapia lazma izae matunda. Mkwepe!
9. Kuwa mstaarabu
 
Kuishi kwa ndugu, mambo ya kufanya
1. Siku zote amka mapema na ufanye shughuli za kimsaada kwenye mji huo, kwa mfano kufagia, kusafisha mabanda ya kuku n.k. wjatever it is, lakini asubuh na mapema ikukute nje.
2. Jitahidi kutoka nje na kuzunguka kitaa ukitafta mishe ndogo ndogo za kukupa vijisenti ili usipauke kisoro
3. Usiwe na mazoea yaliyopitiliza hasahasa Kwa shemeji au wifi yako. Kaa kwa step wacha kiherehere
4. Ukipata chochote huko duniani, kamwe usirudi mikono mitupu, hata ndizi za buku zinaeza sindikiza wali maharagwe hapo ndani. Always provide some input kuwapunguzia mzigo.
5. Kuwa msafi, kuwa msafi kuwa msafi!
6. Fuata sheria zao, kwa mfano kuwahi kurudi, kusali n.k. kama una sheria zako kazipeleke kwenu, hapo ni kwa watu, wacha kisebengo cha kupanga masharti.
7. Hakikisha wale watoto kina "junia" hawakuzoei, wale wana mambo ya kiwaki unaweza mkata kelebu akatema meno. Jiepushe nao
8. Beki 3 ana mbolea iliopitiliza, ukipanda mbegu nakuapia lazma izae matunda. Mkwepe!
9. Kuwa mstaarabu
Aisee, hapa umemaliza kila kitu yani.
 
Kuishi na watu ni kipaji,, kujifanya mjinga tu,, fanya kazi km punda,, hata ukionewa upotezee siku ukiondoka iwe ni aibu kwao,,na roho mbaya huwa tunazianzisha sie wanawake hasa kwenye misosi,, kumsimanga mtu kwa ajili ya kula ni tabia mbaya na umaskini uliopitiliza
Ni tabia mbaya sana kumsimanga mtu kwa chakula, sijui kwa nini mtu aone big deal kwenye misosi.
 
Muda wa kula usicheze mbali,siyo uitwe tu kila siku chakula tayari.
Uwe unasaidia kazi ndogondogo mfano kufagia hata uwanja,kuosha sahani au bakuli.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom