Ukijiita "MNYONGE" utakuwa mnyonge mpaka kufa kwako,maneno yanaumba. Soma hapa uzinduke leo

Ukijiita "MNYONGE" utakuwa mnyonge mpaka kufa kwako,maneno yanaumba. Soma hapa uzinduke leo

Hii dunia ili uifaidi jitahidi iende unavyotaka siyo wanavyotaka watu, huwa inafika hatua nawakubali watu bandidu
Ongeza sauti hapo mkuu

Mnyonge utaambiwa brashi viatu vya shemej yako tajiri awahi kazini, mnyonge utaambiwa osha gari ya shemej yako haraka awahi kazini, mnyonge utaambiwa lisha ng'ombe za shemej yako wapate kunona vizuri, mnyonge utaambiwa osha miguu ya shemej yako,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unajitahidi kutafuta ila mambo hayaendi, mf. Mifugo inakufa kila wakati, biashara haiendi na unatumia utaalamu) utakuwa unamtegemea huyo tajiri na dhana ya unyonge inabakia kwako. Wanyonge wanajitahidi ila mambo yanashindikana. Omba Mungu unyonge usibishe hodi kwako. Muulize Mshana atakuambia kuna unyonge wa "kutengenezwa "

Sent from my TECNO-N2 using JamiiForums mobile app
 
Wewe kama ni mnyonge ni mnyonge tu hata ukijiita simba ukweli uko pale pale. Wanyonge,unyonge upo ndio maana hilo neno likawepo.
Kuna tofauti kati ya kujiita tu kama jina na kuamini,kama ukiamini na ukaishi kwa kupambana kwa bidii na ari unyonge utaisha tu
 
Kwanza kabisa natangulia kusema SIIJUI KESHO YANGU lakini siwezi kuwa mnyonge kila siku.

Watanzania tumejengewa dhana potovu sana. Hivi unajua kujiita mnyonge ni kujidhalilisha?

Kama ulikua hujui usipopata changamoto katika maisha utakuwa mjinga tu,ukiishi ukiamini"mimi ni mnyonge" utakuwa mnyonge mpaka kufa,hata ukipewa dili ya milioni 100 utaona ujinga sababu tayari una dhana ya unyonge moyoni mwako.

Jitoe kwenye unyonge leo acha mawazo ya miaka 1800s, nani asiependa maisha mazuri? Nani anapenda kuwa mnyonge kila siku?

Ikiwa watanzania wengi wataendelea kuamini wao ni wanyonge wasiojiongeza badi tuna safari ndefu sana kufikia hata Kenya tu.

Unyonge unafanya mtu anatawaliwa, anadharauliwa,anateswa na kuonewa.

Dhana ya unyonge inapaswa kufa haraka sana, mama Samia naomba uhakikishe hilo ili nchi isonge mbele haraka. Kama unakubali ni mnyonge nyosha kidole juu na unipe mwisho wa unyonge ni ni lini kwako.
Mimi sio mnyonge bali napenda utulivu kwenye kuamua na kung'amua kila jambo kwa sababu huwa na amini kwamba "STILLNESS IS KEY". I'm sign off.
 
Maccm Kazi yao ni kufanya watu wawe maskini na wasijitambue,wakishatengeneza matatizo wanachonga kinyago anajifanya mtu wa wanyonge at last wanapata uhalali wa kuendelea kuwa madarakani kupitia watu wasiojitambua.

Ndio maana utakuta hao wanaojiita wanyonge wanashangilia kulishwa propaganda huku wakiendelea kubali kuwa maskini na kutumika kama ngazi za kupandia .

Hao wanyonge utashangaa wamraminishwa na maccm kwamba ati umaskini wao unatokana na wafanyakazi au Matajiri makundi ya jamii ambayo ccm haiyataki kwa vile yanajitambua

Si ajabu wameacha kufanya Kazi zao za kinyonge wameenda kujiliza barabarani huku wanachokililia hawakielewi.
 
Maccm Kazi yao ni kufanya watu wawe maskini na wasijitambue,wakishatengeneza matatizo wanachonga kinyago anajifanya mtu wa wanyonge at last wanapata uhalali wa kuendelea kuwa madarakani kupitia watu wasiojitambua.

Ndio maana utakuta hao wanaojiita wanyonge wanashangilia kulishwa propaganda huku wakiendelea kubali kuwa maskini na kutumika kama ngazi za kupandia .

Hao wanyonge utashangaa wamraminishwa na maccm kwamba ati umaskini wao unatokana na wafanyakazi au Matajiri makundi ya jamii ambayo ccm haiyataki kwa vile yanajitambua

Si ajabu wameacha kufanya Kazi zao za kinyonge wameenda kujiliza barabarani huku wanachokililia hawakielewi.
 
Maccm Kazi yao ni kufanya watu wawe maskini na wasijitambue,wakishatengeneza matatizo wanachonga kinyago anajifanya mtu wa wanyonge at last wanapata uhalali wa kuendelea kuwa madarakani kupitia watu wasiojitambua.

Ndio maana utakuta hao wanaojiita wanyonge wanashangilia kulishwa propaganda huku wakiendelea kubali kuwa maskini na kutumika kama ngazi za kupandia .

Hao wanyonge utashangaa wamraminishwa na maccm kwamba ati umaskini wao unatokana na wafanyakazi au Matajiri makundi ya jamii ambayo ccm haiyataki kwa vile yanajitambua

Si ajabu wameacha kufanya Kazi zao za kinyonge wameenda kujiliza barabarani huku wanachokililia hawakielewi.
Asante sana, wanyonge wasipojitanbua wanatumika kama daraja. Elimu ni muhimu sana kwa jamii zote. Usione ulaya imeendelea ukajua ni miujiza ilitawaliwa na Roma miaka 2000 iliyopita walipoacha kuwa wanyonge wakapata elimu wakapambana wakawa huru.
 
Back
Top Bottom