Ukimpa mtu dili la milioni hizi, kamisheni yako unataka iwe ngapi

Airmanula

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
3,527
Reaction score
5,762
Wakuu, poleni na msiba wa kitaifa uliotukumba, pia tunashukuru Mungu Mheshimiwa Lissu amerejea nchini mwake salama akiwa hai.

Tukiachana na hayo, embu tupeane ushauri hapa, kua ukimpa mtu dili la milioni tuseme 10 au 15.

Kamisheni ambayo ni itakupendeza utataka iwe kiasi gani?

Asanteni.
 
Tujue kwanza dili ni halali au haramu? kama dili li halali basi lazima ufanye cost benefit analysis (Faida na hasara)

na kama dili ni haramu hakikisha other party anaridhika kwa utakachompa kama Ganji
 
Tujue kwanza dili ni halali au haramu?? kama dili li halali basi lazima ufanye cost benefit analysis (Faida na hasara)

na kama dili ni haramu hakikisha other party anaridhika kwa utakachompa kama Ganji
dili ni halali mkuu..na hio cost benefit unaitafutaje mkuu
 
Tujue kwanza dili ni halali au haramu?? kama dili li halali basi lazima ufanye cost benefit analysis (Faida na hasara)

na kama dili ni haramu hakikisha other party anaridhika kwa utakachompa kama Ganji
BCR = Discounted value of benefits/ discounted value of costs.

nimetafuta huko mitandaoni ...labda tuombe wataalam mtufafanulie hapa mana mimi mtupu accounting/finance
 
Mzee hilo dili la milioni 15 huyo mtu anapata faida kiasi gani? Faida ndio inaamua GANJI,
 
Mara nyingi huwa ni mpaka 30% ya net profit...unaipata baada ya kutoa gharama zote pamoja na kodi. Ila itategemea ni deal la nini...kama ni deal la service na hiyo service inapaswa ikae mwaka mmoja na hilo deal likafa baada ya mwezi wa pili ..itabidi urudishe comission ya miezi kumi.
 
Fair commission ni 10% hivyo hapo ni 1m au 1.5m kama ni biashara halali.
 
Duh! 10% ya chochote kile, let's say 10% ya 1,000 ni 100! Sidhani kama kuna deal za zero profit hilo halipo!

Sent from my TECNO Camon CX using JamiiForums mobile app
Duh nimekwambia faida ya huyo mtu ni 10% kwenye hio deal ya 10m hawezi kukupa wewe 10%. Au useme 10% ya faida.
 
Kama Ni tenda au kazi za ufundi
Mpe 10% lakini unaweza kuweka ubinaadamu ukamuongeza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…