Ukimuacha Nyerere, makosa ya Marais wetu ni ya makusudi kwa manufaa ya familia zao

Yaani ndo nchi zetu za Afrika tulivyo..
..., mambo yaleyale na afadhali hata nchi kama SA wanajaribu kwa katiba yao na kuheshimu sheria zao, na jana tu tumeona yaliyofanyika kwa Jacob Zuma.... bado naona tuna safari ni ndefu...kazi iendelee.
Tanzania Marais hawawajibiki wakiwa madarakani kwakua wakimaliza muda wao haijalishi walichokifanya Bado wanabakia na heshima zao ,

Hakuna wa kuwawajibisha.
 
Jambo ambalo watu wengi hawajui ni kwamba, matatizo karibu yote ya nchi hii msingi wake uliwekwa na Nyerere. Huo ndiyo ukweli mchungu.
 
Nyerere alivyokuwa ana ongoza south south commission, alisema tatizo la south yaani "Africa" mtoto wa kiongozi

1. Anapewa mradi kwa upendeleo
2. Atalipwa pesa na kazi hatofanya hivyo huo mradi yatakuwa na tija kwa uchumi wa Nchi, lakini Asia kosa litakuwa moja tu namba moja kwamba kazi itatolewa kwa upendeleo, lakini kazi itafanyika hivyo kuwa na tija kiuchumi.

Nafikiri utakuwa umeelewa
 
Tanzania Marais hawawajibiki wakiwa madarakani kwakua wakimaliza muda wao haijalishi walichokifanya Bado wanabakia na heshima zao ,

Hakuna wa kuwawajibisha.
Hapo ndo pa kubadilisha. Haiwezekani binadamu huyuhuyu aliyezaliwa kutoka kwa Adam na Eva asiwe anategemewa kufanya makosa akiwa na nguvu kubwa kiasi hicho
 
This is not Asia bahati mbaya unless unataka kumaanisha kwamba alipewa kwa upendeleo na amefanya cha maana kitu ambacho sitakubaliana nawe and am not even ready to embark myself kwenye University work of arguments.
 
Haya yote ni matatizo ya katiba mbovu.
Katiba mpya inahitajika wakati huu kuliko wakati mwingine wowote.
 
Nyerere alijenga umoja tangu mapema kabisa. Alichofanya kilikuwa ni msingi wa utaifa wetu tukumbuke kuwa yapo mataifa ambayo hayakuanza na umoja walianza na mawazo ya kikabila na kikanda, wakavurugikiwa mapema sana.

Kiuchumi hakuwa na chaguo ilibidi awe bepari au awe mjamaa. Alifanya kazi akiwa na mazingira magumu kulinganisha na wengine waliofuatia.

Hawa waliokuja kuanzisha mitandao ndio walivuruga kila kitu, wakaleta siasa za majungu na upambe wa kujikomba.
 
Tanzania Marais hawawajibiki wakiwa madarakani kwakua wakimaliza muda wao haijalishi walichokifanya Bado wanabakia na heshima zao ,

Hakuna wa kuwawajibisha.
Ni shamba la bibi wanajichotea wao na familia zao tu huku wananchi wa kawaida wakihimizwa kuwa wazalendo na kuipenda nchi yao.
 
This is not Asia bahati mbaya unless unataka kumaanisha kwamba alipewa kwa upendeleo na amefanya cha maana kitu ambacho sitakubaliana nawe and am not even ready to embark myself kwenye University work of arguments.
So Nyerere was embarking on "university argument " akili za kuambiwa changia na zako keep it Up and keep your points to yourself if you are closed minded person.

And second point you say this is not Asia, well and good, then you should note also this is not "Europe" hence one will be wondering what is your point at all. "A kindergarten point of view" or a recent graduate who is fixed to a certain village life or what he have heard
 
Na kitakachowatesa watanzania siku zote ni hicho cha kuammini MWAMBA yeye hakuwa chanzo cha haya.
 
Mtu wa Chato huwezi kosoa mzaliwa wa Chato mwenzio kwa sababu wewe ni mojawapo ya kizazi cha nyoka mwenye sumu,katika vitu vya ovyo kabisa ni kutaka kuijenga Chato kuwa Dar wakati wananchi wakiteseka miaka mitano na robo bila ajira,mishahara kuongezewa,madaraja kazini kupandishwa,mzunguko wa pesa nchini ukiwa hafifu,uhuru wa kweli kwa Watanzania walio wengi kzorota na mateso ya kila aina,Bora hao uliowataja Watanzania walikula mema ya nchi yao kwa ujumla wao kuliko huyo unayesema alijenga Chato na kuiachia nchi umaskini wa kutupwa.
 
Nyerere hakua mzalendo kama wengi tunavyo mpamba alitambua kbs ratiba aliyo i copy nchi za koloni ni mwiba na inatoa mwanya kwa viongozi wa africa kufanya utopolo alishindwa nn kuturithisha katiba yenye kubeba maono ya tanzania tunayoitamani
 
Nyerere alifeli kwenye Mambo haya kwa mtazamo wangu .

1.Katiba Bora na Safi .

2.uchumi imara na madhubuti.

Ila alijitahidi kwenye mengi.Ndio maana anaimbwa Hadi Leo

Hawa wengine watasaulika tu maana wanajiende tu
 
Sasa kujipa tenda kuna ubaya gani kama kampuni ipo na imetimiza vigezo? Kwamba wewe usiajiriwe ofisi aliyepo baba yako kama afisa muajiri ikiwa umeomba nafasi na sifa unazo! Hebu acheni chuki za kishamba jamani
Na utakuta alitoa fursa za ajira labda iwe waajiriwa wote ni wanafamilia jambo lisilowezekana.
 
Wizi hauna manufaa hiko kiwanda cha magari hakishindani ya hyundani ya Korea wakati wote walikua sawa
 
Unaishia kusema tu inahitajika mbinu , Sasa hizo mbinu unategemea upewe na nani kama wewe mwenyewe umeshindwa kuziweka hapa?
 
JKN na JPM wapo mbaaali kabisa na hao wengine uliowataja.Hawa waliyajua mamlaka yao.Hawakuyumbishwa na kuendeshwa 'external force' kama hao wengine.Walikua wazalendo na waliumwa na umaskini wetu.Walikua na 'vision' na 'mission' ya kututoa nyikani.Hawa wengine walikua ni vibaraka wa genge la wanyang'anyi wa nje na makuwadi wao hapa nchini.Wizi,ubinafsishaji holela,upendeleo,siasa za makundi na batili nyingine nyingi ndio ilikua mtindo wa Serikali zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…