Ukimya wa Tanzania na JWTZ Kule Congo DRC si wa Kawaida – Kuna Kitu Kinachezwa?

Ukimya wa Tanzania na JWTZ Kule Congo DRC si wa Kawaida – Kuna Kitu Kinachezwa?

covid 19

JF-Expert Member
Joined
May 9, 2014
Posts
6,967
Reaction score
17,452
Kwa anayefuatilia kinachoendelea DRC, hasa katika mkoa wa Goma, atakuwa anajiuliza: Liko wapi lile jeshi jasiri la JWTZ ambalo mwaka 2012-2013 liliwafurusha waasi wa M23 na kuwafanya wasambaratike kabisa?


Kwa mshangao mkubwa, baada ya uchaguzi wa DRC na kuingia madarakani kwa Félix Tshisekedi, waasi wale wale wa M23 wameibuka tena kwa nguvu mpya, wakiwa na uwezo wa kuteka Goma na sasa wakielekea Bukavu. Inaonekana lengo lao ni kuimega DRC, lakini kosa ni la nani?


  • Je, ni Tshisekedi mwenyewe, ambaye kwa sera zake ameshindwa kuimarisha ulinzi wa nchi yake?
  • Au ni MONUSCO, ambalo lilifuta vikosi vya kulinda amani kuwa chini ya Chapter 6 badala ya Chapter 7, hivyo kulifanya JWTZ na walinda amani wengine kuwa wasio na mamlaka ya kupambana na waasi moja kwa moja?

Kwa Nini Tanzania Inaonekana Inampiga Tshisekedi Darubini?


Ukiangalia historia, Tanzania imekuwa mshirika wa karibu wa marais wawili wa DRC:


  • Laurent-Désiré Kabila, ambaye alikombolewa kwa msaada wa Tanzania.
  • Joseph Kabila, ambaye pia alifaidika na uhusiano wa karibu kati ya Tanzania na DRC.

Lakini kwa Tshisekedi, hali inaonekana tofauti. Serikali ya Tanzania inaonekana kumsaidia kwa "machale machale"—yaani, si kwa nguvu kama ilivyokuwa kwa Kabila na Kabila. Kwa nini?


  • Je, ni kwa sababu hakuwa sehemu ya mfumo wa ushawishi wa Tanzania?
  • Au ni kwa sababu alipotwaa madaraka, alikimbilia kushirikiana zaidi na Kenya badala ya Tanzania?
  • Au alidhani waasi wa M23 wangebakia kule kule Goma, bila kujua kuwa nguvu zao zinatoka Kigali na Kampala?

Tanzania inajua kinachoendelea. Watu wetu wa intelligentsia wamekusanya taarifa zote. Lakini inaonekana Tanzania imeamua kuwapotezea kwa sasa—kwa sababu nzuri tu.


Je, JWTZ Itaendelea Kukaushia au Itaingilia Kati?


Historia inaonesha kuwa Tanzania si nchi inayopenda kuona mataifa jirani yanameguka vipande vipande. Tuliwaunga mkono sana Wacongo bila masharti, tukiwapa muda wa kujijenga. Lakini wao wakaleta dharau.


Sasa swali kubwa ni: Tshisekedi atajinasua vipi?


  • Atapiga magoti kwa Tanzania na kuomba msaada?
  • Atazidi kung’ang’ania kwa Kenya na wengine, huku waasi wakiendelea kuikata DRC vipande vipande?

Muda utaamua. Lakini kwa sasa, JWTZ linaendelea na "hamsini zake", likiwa linajua vizuri kwanini halijarudi vitani kama ilivyofanya mwaka 2012-2013. Sababu tunayo, tena inajitosheleza!
 
Naweza sema katika kusoma soma juu ya huu mgogoro toka uibuke upya, wewe ndio mtu pekee umenifanya nione kitu kipya cha tofauti umekiibua kuhusi ushiriki wa Tz na JW. Umeandika kitu kipya ambacho hakijaandikwa sana kama sio kabisa humu jukwaani juu ya huu mgogoro
 
Bi Tozo hana uelewa wowote na masuala ya geo-politics, waziri wa ulinzi mwenyewe hajui lolote kuhusu masuala ya kivita ma usalama. Siku ile kathibitisha baada ya kubadili darubini mbele nyuma na nyuma mbele halafu yupo busy utasema yupo serious, sasa sijui alikuwa anaona nini, kwa maana darubini ukiigeuza pa kuangalizia unaona taswira ya kitu ipo mbali zaidi...

We imagine mtu darubini hajui kutumia, hivi atakuwa ana uelewa hata na kinachoendelea DRC?

Haya mambo yanahitaji kiongozi mwenye uelewa kwa upana kuhusu migogoro hii na historia zake, tena uelewa kwa undani zaidi, haya masuala yanahitaji intel.

Inahitajika kiongozi mwenye kujua historia za undani kuhusu majirani zake.

Mtu anasikiliza taarabu atajuaje hayo masuala?
 
Ndani ya JWTZ kiundwe kikosi kingine cha kushughulikia mambo ya Nje ya mipaka ya Nchi.

Vijana waajiriwe wakapige Kazi. Hela iletwe nchini.
Hii point kabisa ya kuinakili kwa dunia ya sasa tulipaswa kufanya hii kitu ni sehemu ya kuongez ajira pia kukuza income ya nchi wakati huohuo unalinda maslahi yako.
 
Kwa anayefuatilia kinachoendelea DRC, hasa katika mkoa wa Goma, atakuwa anajiuliza: Liko wapi lile jeshi jasiri la JWTZ ambalo mwaka 2012-2013 liliwafurusha waasi wa M23 na kuwafanya wasambaratike kabisa?


Kwa mshangao mkubwa, baada ya uchaguzi wa DRC na kuingia madarakani kwa Félix Tshisekedi, waasi wale wale wa M23 wameibuka tena kwa nguvu mpya, wakiwa na uwezo wa kuteka Goma na sasa wakielekea Bukavu. Inaonekana lengo lao ni kuimega DRC, lakini kosa ni la nani?


  • Je, ni Tshisekedi mwenyewe, ambaye kwa sera zake ameshindwa kuimarisha ulinzi wa nchi yake?
  • Au ni MONUSCO, ambalo lilifuta vikosi vya kulinda amani kuwa chini ya Chapter 6 badala ya Chapter 7, hivyo kulifanya JWTZ na walinda amani wengine kuwa wasio na mamlaka ya kupambana na waasi moja kwa moja?

Kwa Nini Tanzania Inaonekana Inampiga Tshisekedi Darubini?


Ukiangalia historia, Tanzania imekuwa mshirika wa karibu wa marais wawili wa DRC:


  • Laurent-Désiré Kabila, ambaye alikombolewa kwa msaada wa Tanzania.
  • Joseph Kabila, ambaye pia alifaidika na uhusiano wa karibu kati ya Tanzania na DRC.

Lakini kwa Tshisekedi, hali inaonekana tofauti. Serikali ya Tanzania inaonekana kumsaidia kwa "machale machale"—yaani, si kwa nguvu kama ilivyokuwa kwa Kabila na Kabila. Kwa nini?


  • Je, ni kwa sababu hakuwa sehemu ya mfumo wa ushawishi wa Tanzania?
  • Au ni kwa sababu alipotwaa madaraka, alikimbilia kushirikiana zaidi na Kenya badala ya Tanzania?
  • Au alidhani waasi wa M23 wangebakia kule kule Goma, bila kujua kuwa nguvu zao zinatoka Kigali na Kampala?

Tanzania inajua kinachoendelea. Watu wetu wa intelligentsia wamekusanya taarifa zote. Lakini inaonekana Tanzania imeamua kuwapotezea kwa sasa—kwa sababu nzuri tu.


Je, JWTZ Itaendelea Kukaushia au Itaingilia Kati?


Historia inaonesha kuwa Tanzania si nchi inayopenda kuona mataifa jirani yanameguka vipande vipande. Tuliwaunga mkono sana Wacongo bila masharti, tukiwapa muda wa kujijenga. Lakini wao wakaleta dharau.


Sasa swali kubwa ni: Tshisekedi atajinasua vipi?


  • Atapiga magoti kwa Tanzania na kuomba msaada?
  • Atazidi kung’ang’ania kwa Kenya na wengine, huku waasi wakiendelea kuikata DRC vipande vipande?

Muda utaamua. Lakini kwa sasa, JWTZ linaendelea na "hamsini zake", likiwa linajua vizuri kwanini halijarudi vitani kama ilivyofanya mwaka 2012-2013. Sababu tunayo, tena inajitosheleza!
Kila kitu kimeelezwa hapa
 

Attachments

  • Screenshot_20250130-184353.png
    Screenshot_20250130-184353.png
    163.2 KB · Views: 4
  • Screenshot_20250130-184546.png
    Screenshot_20250130-184546.png
    196.1 KB · Views: 4
Bi Tozo hana uelewa wowote na masuala ya geo-politics, waziri wa ulinzi mwenyewe hajui lolote kuhusu masuala ya kivita ma usalama. Siku ile kathibitisha baada ya kubadili darubini mbele nyuma na nyuma mbele halafu yupo busy utasema yupo serious, sasa sijui alikuwa anaona nini, kwa maana darubini ukiigeuza pa kuangalizia unaona taswira ya kitu ipo mbali zaidi...

We imagine mtu darubini hajui kutumia, hivi atakuwa ana uelewa hata na kinachoendelea DRC?

Haya mambo yanahitaji kiongozi mwenye uelewa kwa upana kuhusu migogoro hii na historia zake, tena uelewa kwa undani zaidi, haya masuala yanahitaji intel.

Inahitajika kiongozi mwenye kujua historia za undani kuhusu majirani zake.

Mtu anasikiliza taarabu atajuaje hayo masuala?
Si kweli magenerali wetu wanamsaidia mama kwa kribu sana tena sana kuliko wakati wowote na naamini ni wao ndio wametoa ushauri kuwa jeshi letu litulie kimya.
Ngoj ruendelee kusubiri kitachojiri.
 
JWTZ ikachukue kandarasi Hilo ipige Pesa
Hizo ndizo Kazi zenyewe.

Ndani ya JWTZ kiundwe kikosi kingine cha kushughulikia mambo ya Nje ya mipaka ya Nchi.

Vijana waajiriwe wakapige Kazi. Hela iletwe nchini.
Hayo Mengine ya sifa za kijinga tuachane nayo
Sahihi kabisa

Mwaka huu nategemea kuajiria vijana zaidi ya 5000 JWTZ

Nategemea kuona sasa tunaanza kuwa Military Base Mashariki mwa Congo ambapo wanajeshi na polisi wetu watakuwa wanakuwa deployed kwa miaka miwili miwili


Nategemea kuona Military Base kubwa za Navy Lake Tanganyika na Lake Victoria zenye equipment za kisasa ikiwemo melivita za kisasa kwa ajili ya kutoa support kwa vikosi vyetu vya Congo where necessary
 
Kinacho shangaza Kagame anamfokea president wa SA anamwacha jirani yake wa Tanzania 😆
Yaani mpaka nahisi na sisi tumejinga na rwanda maana makubaliano ya mwisho kati ya Laurent kabila na museven na kagame yalifanyika hapahapa dar na wapambe ndio sisi jamani.. kwamba yule mzee angewapa kipande rwanda na uganda sasa kabila mkubwa aliwabadilikiaalipofanikiwa jambo lake alafua akaja kulia kwetu tumsaidie tukamsaidia kweli kwa upendo tatizo Congo si watu wa shukrani na ni wajivuni mnomno..
 
Sahihi kabisa

Mwaka huu nategemea kuajiria vijana zaidi ya 5000 JWTZ

Nategemea kuona sasa tunaanza kuwa Military Base Mashariki mwa Congo ambapo wanajeshi na polisi wetu watakuwa wanakuwa deployed kwa miaka miwili miwili


Nategemea kuona Military Base kubwa za Navy Lake Tanganyika na Lake Victoria zenye equipment za kisasa ikiwemo melivita za kisasa kwa ajili ya kutoa support kwa vikosi vyetu vya Congo where necessary
Mwenyekiti wazo lako ni mzuri sana!
 
Sahihi kabisa

Mwaka huu nategemea kuajiria vijana zaidi ya 5000 JWTZ

Nategemea kuona sasa tunaanza kuwa Military Base Mashariki mwa Congo ambapo wanajeshi na polisi wetu watakuwa wanakuwa deployed kwa miaka miwili miwili


Nategemea kuona Military Base kubwa A Navy Lake Tanganyika na Lake Victoria zenye equipment za kisasa ikiwemo melivita za kisasa kwa ajili ya kutoa support kwa vikosi vyetu vya Congo where necessary

Sio kila Jambo tuwaige wazungu.
Mengine tunaweza kujiongeza wenyewe.

Kwa nchi yetu ulinzi na Usalama ni huduma ambayo wananchi lazima wapewe lakini ulinzi na Usalama ni biashara inayolipa kama tukiiuza kwa nchi zingine.

Serikali na vyombo vya kijeshi vinaweza kuundw Kitengo kingine cha kijeshi ambacho kitapewa mafunzo ya kijeshi na kitahusika zaidi na mission za Nje ya Nchi.
Hapa wachukuliwe wale watu ambao wanapenda Michezo Hatari, Dili Hatari na wapiganaji wa Kulipwa lakini Kwa maslahi yao na maslahi ya Nchi.

Kisha Kazi ianze.
Kuliko vijana wawe Panya road au mateja huko mtaani na barabarani na Wana hobby ya mambo kama hayo ni Bora wapelekwe huko

Lakini lazima wapewe mafunzo ya kimedani wawe na uwezo.
Sio waende kuuza roho Zao huko
 
JWTZ hatu wapeleki Congo 2025 tuna uchaguzi na ccm inataka ibakishe walinzi wake. Soma nyakati
Hapa hakuna threat kwamba kutakuwa na machafuko yapi hayo..?

Wananchi wameridhika na maisha yao na wanapilika zao siasa wengi hawapendi kabisa.
 
Back
Top Bottom