Ukiona adui anakubembelezea chakula, chukua tahadhari!

Ukiona adui anakubembelezea chakula, chukua tahadhari!

Mikono yenye Sugu

Senior Member
Joined
Jul 1, 2020
Posts
133
Reaction score
215
Ghafla umezuka wema kutoka kusikojulikana kuwaomba CHADEMA wawasilishe majina ya wabunge wa viti maalum ili wajumuishwe kwenye mchakato wa uapishaji.

Hii inaogopesha! Ni wiki moja tu imepita tokea wafuasi na viongozi wa CHADEMA kufanyiwa kila aina ya unyama na mwisho kupokwa kila walichostahili kwenye zoezi la uchaguzi.

Cha ajabu kuna jitihada kubwa sasa za kuwabembeleza wachukue nafasi ya viti maalum "vya kugawiwa" na waliopora kila kitu.

Tahadhari kwa CHADEMA; ukiona adui anakubembelezea chakula au maji, chukua tahadhari. Huenda chakula hicho kimetiwa sumu, ama ya kukuua ghafla au ya kukumaliza polepole.

Msishiriki haramu iliyotendeka kwa ahadi ya peremende, matajimaliza wenyewe.
 
CCM NA NEC wanateseka kuwaomba CHADEMA WAPELEKE MAJINA YA VITI MAALUM.

Wakati mwenyekiti wao ana umri wa miaka 60 ambao ndio umri wa hii nchi ILIYOTAWALIWA NA CCM YEYE KWA UONGO ANASEMA WAPINZANI WAMECHELEWESHA MAENDELEO.

Mzee kinana aliwahi kumwita mwenyekiti wake JPM KUWA NI MSHAMBA SANA.
 
Kamati inayopitisha hayo majina ina member 15
Kati ya hao watatu wanazuiliwa kushiriki kikao
Wengne walipigwa marufuku kwenda Dar hivyo tusilaumiane majina hatupeleki
Kama vipi wampe hizo nafasi bibi Queen
 
Back
Top Bottom