Ukiona Kiongozi wa Tanzania anakosa msimamo hadi anafikisha miaka 60 tambua anatafuta ajira za juu na uteuzi wa watoto wake

Ukiona Kiongozi wa Tanzania anakosa msimamo hadi anafikisha miaka 60 tambua anatafuta ajira za juu na uteuzi wa watoto wake

kifupi kirefu

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2018
Posts
539
Reaction score
3,507
Mfumo wetu wa ajira unaeleza kuhusu sifa za mwomba ajira na unafafanua hadi timu ya usahili. Ni mfumo mzuri na Dunia nzima inautumia.

Kilichotokea Tanzania Leo wazazi wamekosa uvumiliv, hauna mzazi mwanasiasa mwenye nafasi za juu anayetaka mtoto wake asote kupanda Madaraja na vyeo kwenye utumishi wa umma. Viongozi wengi wanapigana watoto wao wakitoka shule tu wapate uteuzi Tena uteuzi wa Rais.

Kwanini wamefikia hatua hii? Labda uteuzi wa Rais umeshuka thamani, mwanafunzi anamaliza chuo anakata kuajiriwa anasubiri nafasi za uteuzi zikitoka apewe nafasi ya uteuzi na asipopata uteuzi kwenye chama panawaka moto.

Ipo mifano mingi ya watoto wa viongozi waliomaliza vyuo wakaenda kukaa UVCCM na alipoinga JpM akawateua. Ipo mifano ya viongozi AMBAO watoto wao wametoka home hadi kwenye madaraka ya ukurugenzi na Katibu Tawala awamu ya sita.

Katika mazingira ya kawaida tunaweza dhania teuzi hizi zimelenga vijana, HAPANA.Zingelenga vijana tungeshuhudia hata waliopo mtaani wanaotafuta kazi wangepata uteuzi, hizi teuzi siyo za vijana ni teuzi za watoto wa viongozi.

Hali hii inapelekea Katika Bunge zipo familia Zina wawakiishi wawili, ukifuatilia si kwamba familia hizi zinaweza sana kuhudumia wananch Bali familia hizi zimefikia nafasi wanataka mishahara ya Bunge na mashangingi ya serikali yakakae nyumbani kwao. Furaha Yao nikuona magari ya umma na kodi za umma zinalekezwa nyumbani kwao.

Impact yake ni kwamba, wazee waliopaswa kusmama na kuwa na msimamo wa Taifa wamegeuka wanafiki Kwa sababu ukiwa na msimamo watoto wako watakosa uteuzi.Ukitaka familia Yako iendelee kuletwa nyumbani na mashangingi ya serikali kubali uwe mjinga wa fikra.

Hali hii si salama kwa ustawi wa Taifa letu, tutakuja kutawaliwa na wazungu kwa sababu watawala tulionao wamekalia unafiki na majungu

Niombe viongozi mliopo madarakani ruhusuni nafasi za uteuzi kuombwa kama nafasi nyingine, watu wapate kwa merits siyo kwa hisani. Mkiruhusu comitition wazazi wetu wataacha kujipendekeza kwenye TV na kusema NIMEKOSA SANA.

Hii ni fedhea kwa Taifa, viongozi wamepoteza hadhi, viongozi wamekuwa vinyonga......wanachotamka adharani sicho wanachofanya sirini. Watu wa aina hii wanakisasi kibaya Sana, mfano mzuri fuatilieni nape alivyokwenda kumwomba msamaha JpM na namna alivyotema nyongo baada ya Mzee kutangulia mbele ya HAKI.

Maana yake Nape alikuwa anamchukia JPM kupita maelezo hasa baada yakudhalilishwa Ikulu. Tusimwamini Ndugai Sana, umri wake umeenda, ametenegeneza jina Kwa muda mrefu, alichofanya Leo kiwape viongozi alarm kwamba huyu mtu ana hasira moyoni ila amelazimishwa kufanya alichofanya.

Siku akipata madaraka zaidi ya hayo ataumiza watu, siku Nape akipata madaraka ataumiza wale wote waliomwadhibu. Hivi ni visasi wala tusidanganyane kwamba ni mfumo wa CCM, haya ni matokeo yakulinda familia Yako ipate uteuzi, hii nikulinda mke asitenguliwe nk

VIJANA TAFUTENI BIASHARA NA KAZI MSITAFUTE UTEUZI MTADHALILIKA KAMA WAZEE WANAVYOVULIWA NGUO PAMOJA NA NAFASI ZAO KUBWA.
 
Watu wa aina hii wanakisasi kibaya Sana, mfano mzuri fuatilieni nape alivyokwenda kumwomba msamaha JpM na namna alivyotema nyongo baada ya Mzee kutangulia mbele ya HAKI. Maana yake Nape alikuwa anamchukia JPM kupita maelezo hasa baada yakudhalilishwa Ikulu. Tusimwamini Ndugai Sana, umri wake umeenda, ametenegeneza jina Kwa muda mrefu, alichofanya Leo kiwape viongozi alarm kwamba huyu mtu ana hasira moyoni ila amelazimishwa kufanya alichofanya. Siku akipata madaraka zaidi ya hayo ataumiza watu, siku Nape akipata madaraka ataumiza wale wote waliomwadhibu. Hivi ni visasi wala tusidanganyane kwamba ni mfumo wa CCM, haya ni matokeo yakulinda familia Yako ipate uteuzi, hii nikulinda mke asitenguliwe nk

Nakubaliana na wewe 100% kuwa huyu Ndugai ni mnafiki wala asichukuliwe kuwa kweli ameomba msamaha bali ana ajenda yake ya siri!! Mfano ni wa huyo Nape alipomuangukia JPM na kuomba msamaha mbele ya wananchi lakini nyie wote wananchi ni mashahidi jinsi huyo huyo Nape leo hii anamkashifu mwendazake bila hata aibu!!! Hivyo hivyo Ndugai atafanya kwa Samia mara tu asipokuwa na madaraka. Huyu ni wa kumuondoa mapema iwezekanavyo bila kumuonea aibu. Hivi anavyofanya ni kujikosha tu. Huyu mgogo sio wa kumuamini asilani. Mama Samia ampuuze te huku akiendelea na majukumu yake.
 
Niombe viongozi mliopo madarakani ruhusuni nafasi za uteuzi kuombwa kama nafasi nyingine, watu wapate kwa merits siyo kwa hisani
Katiba mpya inahitajika kubadili hili...kuna vyeo vingi vya uteuzi ni kama vya kupeana ulaji tu...haiwezekani mkoa uteuliwa RC,DC,RAS,DED,DAS wakati raia wa hayo maeneo wangeweza tu kujichagulia viongozi wachache wa kuendesha mikoa kwa njia ya kura huku baadhi ya vyeo vikifutwa.
 
Back
Top Bottom