Ukisikia wenye fwedha wamekupora mke usilalamike.

Ukisikia wenye fwedha wamekupora mke usilalamike.

Kaka yangu Kigogo, ukiendelea na tamaa za namna hiyo hutaweza kumuona raisi wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Au kwa kuwa siku hizi kuna ARV zakupa matumaini? Samahani kama nimekuumiza!!


Mama mdogo hiyo picha tu inanifurahisha saana, nakumbuka mheshimiwa alivyukuwa anamtetea babu mugabe, ´Post zako zote na Jina lako vinaendana kabisa ABARIKIWE ALIYEKUZAA, PAMOJA NA WALIOKULELEA
 
si huyo mrembo wanaemsifia????
Mimi namuona wa hovyo......

Same here Boss
Hata mie sijaona kitu cha kunitishia sana. I think the kiuono is a bit too rounded up...ndiyo bantu beauty lakini siyo wote zinawakosha.
 
WANAWAKE WENGINE NI WAZURI KIASI KWAMBA AKIWA NA BWANA HOE HAE KAMA MIMI HATA NIKIPORWA NA PEDESHEE, ITABIDI UGUZE MOYO, NA KUSONGA MBELE KUTAFUTA MWINGINE.
HEBU CHEKI KITU HIKI KIMEKAAA KAMA PEARL MAMAA YA THERENGETITHERENGETI..
1202109467_irenefrontwebs.jpg

Hamfikii wa kwangu.....ala,kwani nini bana?

Mtabaki kusifia wa wenzenu tuu hadi muwasahau wenu.Wakipata 'wa kuwasifia' huko barabarani mtamlaumu nani?
 
Kweli mwenye pesa sio mwenzio.
Na pesa ndio sabuni ya roho.....
Ila leo zinakupa mwanamke mzuri kama uwoya.. Kesho zinakupa ukimwi
 
Mbona huku Tanga wapo wengi sana wa design kama hiyo mkuu? Tushawazowea wala moyo haudundi.
 
watafiti wa mambo ya saikolojia wanasema wanaume wanaooa wanawake warembo/wazuri sana wana hatari kubwa ya kupata magonjwa mbalimbali nakufa mapema kwa sababu ya wasiwasi wa kunyang'anywa au kuzungukwa na watu wengine; sababu ya wivu, na hofu katika moyo. Daima wanakuwa na mawazo na tension kubwa. Hvyo ni hatari kuuugua. Ndo hayo ya kuoa mwanamke mrembo kama huyo wa hapo kwenye picha. Ukimwoa huyo jiandae kupata presha, kisukari,ugonjwa wa moyo na siku ya masiku moyo unapasuka. Kwe heri mwalimu!


Hii kweli kabisaaaa.......!
 
Aaa wapi! Nikiporwa kifaa kama hicho hapo, lazima nife na mtu, hata kama sina pesa.
 
Jamani huyu dada ni mzuri au alivyovaa anavutia? maana sijui ni dada gani apige picha ya namna hiyo na aonekane mbaya
...Mkuu mbona wapo wadada akivaa kama alivyovaa huyo Ireen huwezi kuangalia mara 2?? Huyu demu yuko bomba sana ukiondoa dosari zingine zinazomzonga.
 
Maumbo hayo nayazimia, sijui itakuaje wakinipora?
Lakini si watampora na kisha anarudi kwangu? atazeeka tu atanikuta!
Mliwahi kufikiri, mrembo kama huyo nae anazeeka na sura yake inakuwa na mikunjo,makunyanzi kama mfuko wa malboro?
 
Bujubuj kweli wewe balaa.bado unatamani tu kuturusha roho wenzio!!. make duh balaa.
 
na kujiua vilevile umesahau.

Babu Kijana ni kweli usemayo, soma hii hapa chini toka Mwananchi ya leo. Kazi kweli kweli

===========================================

Mahakama yasomewa waraka kesi ya mauaji

James Magai

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imepokea waraka ambao inadaiwa uliandikwa na Benson Urio kabla ya kutenda kosa baada ya kushtakiwa kwa jaribio la mauaji.


Katika kesi hiyo namba moja ya mwaka 2008, Benson anadaiwa kujaribu kumuua aliyekuwa mpenzi wake, Omega Leweta ambaye ni mkazi wa Kimara jijini Dar es Salaam baada ya kumvizia akiwa usingizini na kuanza kumkatakata kwa mapanga sehemu mbalimbali za mwili.


Pia mshtakiwa huyo anadaiwa kuwa baada ya kumkatakata mpenzi wake, Benson pia anadaiwa kujikatakata shingoni kwa panga kwa lengo la kujiua sambamba na mpenzi wake huyo.


Waraka huo ambao unadaiwa kuandikwa na mshtakiwa huyo kwenda kwa mama yake mzazi, Felister Urio ulisomwa juzi mahakamani hapo na shahidi wa tano katika kesi hiyo D/Sgt. Gotard Ipande wakati akitoa ushahidi katika kesi hiyo.


Waraka huo unaonyesha dhamira ya mshtakiwa huyo kumuua mpenzi wake na baadaye kujiua.


Katika waraka huo, Benson anaeleza jinsi mama yake alivyomlea na kumtakia maisha mema, lakini baadaye anaanza kueleza jinsi alivyopendana na mpenzi wake hadi wakati anaondoka kwenda Ulaya.


Anaeleza jinsi alivyokatisha maisha yake ya barani Ulaya na jinsi ambavyo mpenzi wake hakufurahia kurejea kwake mapema na baadaye kueleza jinsi mpenzi huyo alivyobadilika baada ya kurejea.


"Hali niliyokukuta nayo haikuwa nzuri kama nilivyokuzoea. Nilikuuliza una tatizo gani ukajibu hakuna tatizo. Nilikuuliza au umepata mpenzi mwingine ukasema hakuna. Nilivyokufahamu siyo ulivyokuwa na siku zilivyozidi kwenda nilikuuliza kila tulivyozoeana," anasema katika waraka huo.


“Hadi leo uhusiano wangu kwake hauko, hata ya kusema anachonisemesha ni salamu tu, habari za asubuhi na za saa hizi atokapo kazini. Hata wakati wa kula ni mende tu ndio wanamfukuza chumbani na kumwambia nenda kakae na mwenzako umemwacha;


Hata nikimsemesha anaitikia tu ‘mhu’ sasa jamani naomba kuuliza, ni mapenzi gani haya? Je ni kwa sababu ya kusafiri kwangu? Je, ni kwa sababu ya umaskini wangu jamani kwa vile sina pesa,” anahoji.


"Uhusiano kwangu si mzuri, isitoshe kashfa na dharau na kejeli zimezidi;Nimegundua Omega ana kiburi kwa sababu ana pesa, siku hizi anajuana na watu wengi, lakini kazi anayofanya katafutiwa na dada yangu Happy lakini leo hata Happy hamthamini."


Anaendelea kueleza katika waraka huo kuwa anahisi mpenzi wake alipata bwana wakati akiwa Ulaya na anamshangaa kwa jinsi asivyojielewa kwa kuwa alikuwa mpishi wa chakula, maarufu kama "Mama Ntilie". Anaeleza jinsi alivyomsomesha mwanae Grace tangu darasa la nne hadi sekondari.


Anaeleza jinsi alivyotuma dola za Kimarekani 250 na baadaye Sh5.5 milioni kwa ajili ya ubarikio wa Grace na zawadi nyingi zenye thamani ya dola 300 za Kimarekani wakati aliporejea nchini, lakini bado anadharaulika na anamaliza waraka wake kwa kueleza kuwa hana deni bali yeye ndiye anayewadai watu aliowataja na kwamba vitu vyote apewe mama yake.
 
lakini nyie wanaume mnafurahisha sana uzuri wa mkakasi ......
 
Back
Top Bottom