Ukitaka Kufanikiwa kwenye haya maisha achana na matumizi ya Smartphone

Smartphone inategemea wewe mtumiajia unaitumiaje, kumbuka wewe unapolalamika kwamba inakurudisha nyuma wakati huohuo kuna mwingine kafanikiwa kupitia smartphone. Ni chaguo lako tu
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Biashara zote sikuhizi zinategemea social networks thru smartfones kukuza wigo wa wateja. Wewe bladfaken mmoja kutoka sweken huko unakuja kusema chimatifoni bla bla bla...shwain kabisa.
Mada kama hizi ukiwapelekea wafanyabiashara wakariakoo sijui kama watakuelewa eti smartphone inachelewesha maendeleo?
 
Simu 200 mpaka 300 na kuendelea walio wengi wako na kazi zao labda unaongelea wanao kula nyumbani watoto wa mama
 
Kila kitu/jambo kwa kiasi...uraibu kwenye jambo lolote ni hatari sana!
Kwa maisha ya sasa, ni ngumu sana kuachana na mitandao ya kijamii...maofisini siku hizi watu wameunda Makundi ya WhatsApp wanawasiliana kwa urahisi sana...kuna Makundi hayana tija, kuna mitandao yenye tija kidogo...nadhani hiyo ndiyo yakuachana nayo.
Simu janja zimerahisisha mambo mengi sana kupitia Application programs, badala ya kuwa na computer, unakuwa na simu janja, ni ndogo, inabebeka kiurahisi, inatunza chaji kwa muda mrefu...n.k. Smart phone ni PC ndogo.
Mtoa mada, nakushauri, chagua mitandao yenye tija, binafsi situmii Facebook(not interested), Instagram(inakula sana bandle), Telegram(not interested), TikTok(not interested), ila natumia WhatsApp(kiofisi zaidi), Twitter(maarifa ya maisha) na Jamiiforums(nimepata maarifa mengi sana hapa).
 
Wewe ulitakiwa uulize, uitumiaje smartphone yako kwa faida kuliko unavyopata hasara!

Smartphone zinafaida sana. Hata maarifa tu nayo ni faida pia. Binafsi nimejifunza maarifa mbalimbali kupitia smartphone. Kwa mfao, zile platforms za upatu za kutapeli watu nimezisoma sana humu JF hivyo huwa nakuwa balozi kwa ndugu na jamaa ambao hawana exposure ya hizo kampuni, wenyewe wapo bize na vitochi au Facebook sana.

Binafsi bando haliishi sana kwangu kwa sababu nina simu mbili smartphone na ndogo. Smartphone naitumia kwa ajili ya mtandao tu, na mara nyingi huwa naiacha nyumbani, ni mara chache sana kutembea nayo. Ikifika jioni au usiku au wikendi nikiwa home ninaingia zaidi JF tena mara moja au mbili kwa siku, nasoma habari kwenye vyombo vya habari vya kitaifa na kimataifa, natazama FB kidogo, makundi ya Whatsapp bila kudownload video. Mwisho nazima smartphone naiweka kwenye droo, naendelea kutumia simu ndogo. Kwangu MB 450 zinamaliza wiki kabisa.

Usiwe unapenda kuwa online muda wote huku ukidownload kila video inayopostiwa, bando zinakula hela. Unaweza kujikuta kwa mwezi unatumia hadi laki moja bila kujua.
 
Kama ndo una miaka 21,na unatumia muda wako mwingi kwenye smartphone.Uza hiyo simu haraka sana.Ninawaza utakuwa Baba wa aina gani wa familia sasa.Bora kama umejitambua.
 
Siwezi kuunga mkono sana hoja hii
Mimi sifanyi biashara ya mtandao lakini pamoja na elimu yangu ya darasani najifunza pia mengi kupitia mitandao ya kijamii na nimekuwa mwerevu na kuonekana mwenye ufahamu mpana.
Matumizi ya smartphone yanaweza kukubadilisha kwa upande chanya ama hasi ni vile mtumiaji atakavyokuwa analenga
 
Inaonesha una control ndogo sana ,kuna watu smartphones zi.ewafanikishia mambo mengi mnoo na wamejifunza meengi kupitia smartphones ninachoamini ni kwamba kama una uwezo mzuri wa kuji limit basi mambo yako meengi sana yatanyooka
 
Ungeacha kutumia kwanza Alfu ndo ukaja na ushuhuda,Tatzo umeshaur kuacha matumiz kabla ya kupata faida zake
 
Nyie mnaosema smartphone ni office zenu za kutangaza bidhaa zenu sio??? Ona wenzenu wanavyopoteza hela kwenye vitu visivyo wasaidia, wanatangaza biashara zao ila no reaction on their post hakuna likes wala comments, sasa hapo smartphone kukuongezea wigo wa wateja uko wapi zaidi ya kupoteza muda wako na pesa zako #kijana acha ubishi hakuna biashara mtandaoni yenye uaminifu nyingi ni utapeli ingia mtaani imeshaandikwa tuta kula kwa jasho hakuna kitu chepesi
 
Samrtphone ni kama ulimi unaamua mwenyewe uutumie Namna gani
Kuharibu au kujenga
 
Kumbuka kuna watu wanatumia hizo smartphone kutengeneza kipato lakini.

Kikubwa ujue unataka au unatafuta nini na kwa malengo gani hapo hutochukia smartphone na uhakika.
 
tunatuma picha, tunapokea picha za kufanyia kazi. Mteja anatuma picha ya kitu fulani anataka atengenezewe bidhaa kama hiyo. Sasa smartphone tukiziacha huoni kama tutakuwa gizani? Tatizo vijana wasio na kazi na wasio na cha kujifunza mambo humo wanaperuzi tu bila kupata faida kwao ni hasara
 
Huwezi kuikimbia technologia ukafanikiwa
 
Kwa taarifa yako kuchoma mkaa ni dili nowadays watu wamejenga majumba kupitia biashara hiyo unayoidharau, kwakuwa wewe ni msomi unaona biashara ya mkaa ni ya kudharirisha ok endelea kupoteza muda huko kwenye hizo mnazoziita digital marketing, trade forex, betting nk, ili upige dollars ukiwa umekaa tu kwenye kiti bossy
 
Reactions: CGE
Na mteja akitaka umtumie picha je
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…