Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

Ukitaka kuishi vizuri Dar es Salaam ishi Kigamboni

mkadiriajimajenzi

JF-Expert Member
Joined
Dec 31, 2015
Posts
549
Reaction score
614
Kigamboni (sasa ni wilaya) ni sehemu ya jiji la Dar es Salaam ambayo tofauti na maeneo mengine ilichelewa kuendelezwa kimiundombinu mpaka kufika miaka ya 90. Watu walichelea kuishi huko kutokana na kupaona ni maporini palipostahili kuishi wanyama.

Hivi leo, mambo ni tofauti sana, mji unakua kwa kasi ya ajabu, barabara zinajengwa kutangulia makazi ya watu, ni sehemu pekee katika jiji la Dar es Salaam ambako ukiingia unasahau kuhusu foleni za barabarani, hali ya hewa ni nzuri kutokana kutokuwepo kwa ujenzi holela wa nyumba, ni karibu sana na city centre na kuna fursa nyingi za kuanzisha biashara.

Binafsi nilifika kwa mara ya kwanza na kuhamia Kigamboni mwaka 2015 kutoka Survey maeneo ya karibu na Mlimani city nilipoishi kwa takribani miaka minne ila mpaka kufikia leo sijawahi kujutia kuishi huku wala kuwaza kuhamia mahali pengine katika mji huu kutokana na sifa nilizozitaja hapo juu na kwa bahati nzuri Mungu amenijaalia kujenga kakibanda huku huku.

Kwa ambao hawajawahi kufika huku hudhani kwamba Kigamboni ni kisiwa na kwamba usafiri pekee wa kufika huku ni wa kuvuka maji kwa pantoni, la hasha! Kigamboni si kisiwa bali imetenganishwa na sehemu nyingine ya jiji kwa sehemu ya bahari iliyoingia nchi kavu (ghuba) ambayo ni bandari ya Dar es Salaam na Kwa sasa ukiachilia usafiri wa wa pantoni kuna daraja na barabara mbili ambazo unaweza kupita bila hata kuiona hiyo bahari.

Karibuni sana Kigamboni.
 
Ukiwa na gari ndo utaona tabu yake kama huna huwezi ona. Kwanza kigamboni imejitenga na mji wakati wa usiku vivuko vinasumbua sana
Shida kweli kweli na ma gharama yani ina maana wewe kuvuka itakulazimu upoteze 90-100K per months kwenda na kurudi kwako! Huu ujinga ndio unanifanya Kigamboni sitaki hata kupasikia
 
Ukiwa na gari ndo utaona tabu yake kama huna huwezi ona. Kwanza kigamboni imejitenga na mji wakati wa usiku vivuko vinasumbua sana
Kwahili nakupinga mkuu, kivuko kinafanya kazi masaa 24. Labda siku ulio pita palikuwa na hitilafu. Ila hata upite tisa usiku huduma ipo tena kina vusha hata watu 15 na gari 2[emoji2369][emoji2369][emoji2369][emoji2369]
 
Tuwaombe mamlaka husika wapunguze bei ya kivuko cha daraja, haiwezekani bei iwe sawa na bantoni. Bei ikipungua, wengi tutashawishika kuja kuishi huko
Bei itapungua au tozo kitolewa kabisa. Fedha ya ujenzi wa mradi ikirudi. Be patient
 
Back
Top Bottom